Panya wavamia mashamba Msata

Panya wavamia mashamba Msata

BABA TUPAC

JF-Expert Member
Joined
Sep 30, 2015
Posts
1,533
Reaction score
3,837
Wakuu,

Kuna panya wasioeleweka wamevamia mashamba ya Msata wanakula mbegu.

Watu wakipanda mbegu mashambani mwao kabla hazijaota panya hao wanakula hizo mbegu kabla hazijaota.

Haijalishi umepanda mbegu za mahindi, choroko, alizeti au zao lolote lile panya wanakula. Hatujui wametokea wapi, kwa maana hiyo mwaka huu hatutapata chakula tunaolima Msata.

Nipo Msata, kijiji cha Mazizi. Tatizo hili lipo vijiji vyote vya jirani pia

Kwakuwa Mshana Jr anaielewa vizuri, tafadhali karibu kwa mjadala.
 
Poleni wakulima wa msata. Hali imekuwa ngumu hadi panya nao wanaingia kwenye kundi la wasiojulikana.

Wizara ya Kilimo ina wataalam wa kutatua hili tatizo lakini mjiandae kisaikolojia maana msishangae mnapewa paka.

Tanzania kilimo kimepigwa teke kabisa sijui kwa nini
 
  • Thanks
Reactions: Auz
Ngoja aje mshana akiwa na jopo la wachawi nadhani ufumbuzi lazima upatikane
 
Kuna uzi unaeleza jinsi ya kuua panya humu kwa kutumia mchanganyiko wa cement
 
Hao panya wamesumbua sana wakulima huko Mlimba, kilombero.Yaani ukipanda mbegu ya mpunga au mahindi wanakula yote,unabidi upande tena.Sijui wameletwa na wazungu hawa panya au vipi
 
Hii ni akili ndogo. Mkishindwa maisha mnawasingizia wazungu badala ya kupambana na hali zenu mtanue akili na kuvumbua utatuzi.

Hao panya wamesumbua sana wakulima huko Mlimba, kilombero.Yaani ukipanda mbegu ya mpunga au mahindi wanakula yote,unabidi upande tena.Sijui wameletwa na wazungu hawa panya au vipi
 
Nyoka ndo ufumbuzi wa tatizo hili. Waletwe nyoka wengi sana wawekwe kwenye mashamba... Kama wanaweza mleta mpiga filimbi wa hamelin yeye agesaidia kwa urahisi zaidi.

Wakuu,

Kuna panya wasioeleweka wamevamia mashamba ya Msata wanakula mbegu.

Watu wakipanda mbegu mashambani mwao kabla hazijaota panya hao wanakula hizo mbegu kabla hazijaota.

Haijalishi umepanda mbegu za mahindi, choroko, alizeti au zao lolote lile panya wanakula. Hatujui wametokea wapi, kwa maana hiyo mwaka huu hatutapata chakula tunaolima Msata.

Nipo Msata, kijiji cha Mazizi. Tatizo hili lipo vijiji vyote vya jirani pia

Kwakuwa Mshana Jr anaielewa vizuri, tafadhali karibu kwa mjadala.
 
Kuna mitego ya iliyotengenezwa na Sua. kwa watu wa Morogoro nadhani waliiona siku ya maonyesho ya kilimo. anaweza tengeneza mtu yoyote shambani, ni vyema watu wa msata mtume mtu akajifunze aje awafundishe, msimu ujao mpate mahindi.
 
Wakuu,

Kuna panya wasioeleweka wamevamia mashamba ya Msata wanakula mbegu.

Watu wakipanda mbegu mashambani mwao kabla hazijaota panya hao wanakula hizo mbegu kabla hazijaota.

Haijalishi umepanda mbegu za mahindi, choroko, alizeti au zao lolote lile panya wanakula. Hatujui wametokea wapi, kwa maana hiyo mwaka huu hatutapata chakula tunaolima Msata.

Nipo Msata, kijiji cha Mazizi. Tatizo hili lipo vijiji vyote vya jirani pia

Kwakuwa Mshana Jr anaielewa vizuri, tafadhali karibu kwa mjadala.
Dawa yao ndogo sana:-
Chimbia chini Madumu na Ndoo zikiwa wazi kwenye maeneo mbalimbali hapo shambani arafu jaza maji.
Arafu eneo lote la jirani hizo Ndoo zungushia pumba za Mahindi.
Utashangaa kila baada ya muda unaenda kutoa mamia ya Mizoga ya Panya kwenye hizo Ndoo.
Hilo zoezi mkifanya wote kwa kushirikiana ndani week tu mtamaliza au kupunguza tatizo.
 
Nyoka ndo ufumbuzi wa tatizo hili. Waletwe nyoka wengi sana wawekwe kwenye mashamba... Kama wanaweza mleta mpiga filimbi wa hamelin yeye agesaidia kwa urahisi zaidi.
Unashauri nini wewe??? Halafu panya wakiisha walete nguchiro kumaliza nyoka ndio waanze kupalilia?
 
Nyoka ndo ufumbuzi wa tatizo hili. Waletwe nyoka wengi sana wawekwe kwenye mashamba... Kama wanaweza mleta mpiga filimbi wa hamelin yeye agesaidia kwa urahisi zaidi.
Kisha mlete nini kuwatoa nyoka?
 
Hao ni wakuwafugia paka tu washinde huko shamban
 
Back
Top Bottom