Pamoja na yote nampenda mume wangu

Pamoja na yote nampenda mume wangu

Yamkini wakati wa kufunga ndoa uliapa "kumpenda ktk raha,shida na ktk uchepukaji wake!"
 
Vizuri endelea kumpenda maana kuachana haitatui tatizo
 
Mtu akikupenda kweli huwa anakuheshimu! Sasa ukiona mpk unajua tabia zake chafu na amezionyesha kwako jiulize kweli anakupenda au ameamua akuweke mlinzi wa nyumba yake na ya status yake.
 
Mungu aendelee kukupa moyo huo wa uvumilivu. Maana bado una umri mdogo pia inaonyesha bando ndoa yako haina muda mrefu (changa) Hakuna anayeingia kwenye ndoa ili aachike baada ya muda si mrefu ila ni Makwazo tena mengine hayavumiliki kabisa.

Mimi ni mrembo sana tena bint mdogo,ndiyo nafikisha miaka 25 nimekuwa nasumbuliwa na wanaume wengi wenye sifa zote lakn leo mpaka kesho pamoja na mapungu ya mume wangu sijaona wa kumfananisha nae

Nimeshika sitetereki,siyumbishwi,nimesima imara!

Ndoa ni msamiati,,

Aliekuoa ni accountancy wa bank au? He he he he
umechelewa kudelete nshaziquote sorry
 
Nakuunga mkono ananivumilia kwa mengi namvumilia pia jaman
 
Mtu akikupenda kweli huwa anakuheshimu! Sasa ukiona mpk unajua tabia zake chafu na amezionyesha kwako jiulize kweli anakupenda au ameamua akuweke mlinzi wa nyumba yake na ya status yake.

hapo na mimi nilikuwa najiuliza, anasema pamoja na mabaya yote lakini anajua anapendwa, sasa kupendwa na kufanyiwa mabaya sijui kunaingiliana vipi?
 
hapo na mimi nilikuwa najiuliza, anasema pamoja na mabaya yote lakini anajua anapendwa, sasa kupendwa na kufanyiwa mabaya sijui kunaingiliana vipi?

nadhani kwake kupendwa ni kule kutimiziwa mahitaji muhimu, amesema kila akitakacho mumewe anampa, fuatilia post zake za nyuma utaona
 
Mi boraa nisijuee nikijuaaa tuu upendo kwishaaaaaaaa
 
nadhani kwake kupendwa ni kule kutimiziwa mahitaji muhimu, amesema kila akitakacho mumewe anampa, fuatilia post zake za nyuma utaona

Mahitaji muhimu ndo yepi hayo hebu nijuzeni. Ni kununuliwa gari? Kununuliwa nguo na makorokoro mengine? Nijuavyo mimi hakuna hitaji muhimu baina ya wanandoa km uaminifu,heshima na kujali. Unapofanya ujinga inafika kipindi hadi unaleta kondom nyumbani kwa mkeo ndo mapenzi hayoo??? Kama ndoa ndo inataka uvumilivu wa hivi mmmh!! Huko kaeni wenyewe mnaoweza kuvumilia ubaradhuli wa namna hii.
 
Back
Top Bottom