Waufukweni
JF-Expert Member
- May 16, 2024
- 4,393
- 14,499
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Profesa Palamagamba Kabudi amesema Rais Samia ameweka mazingira wezeshi kwa Wasanii nchini kwa kuwapa mitaji ya kuboresha kazi zao ambapo katika uongozi wake amefufua mfuko wa Utamaduni na Sanaa uliokuwa umekufa kwa zaidi ya miaka 10 na kipindi kifupi jumla ya miradi 359 ya Utamaduni na Sanaa imepatiwa mikopo yenye jumla ya thamani ya TSh. Bilioni 5.250.