Mr George Francis
Senior Member
- Jun 27, 2022
- 186
- 212
PAKA WAKO UKIMNYIMA CHAKULA
ATAENDA KULA KWA JIRANI.
Sina shaka kuwa unawafahamu PAKA, kama hujawai kufuga, basi hata kwa jirani zako ushawahi kuwaona.
PAKA ni miongoni mwa wanyama wa kufugwa wanaoishi vizuri na binadamu, lakini pia wana tabia ya kubadilika na kuwa moja ya viumbe hatari kwa binadamu.
Moja ya tabia nzuri za PAKA ni kupenda anapopendwa.
PAKA ana uwezo wa kuwajua watu wote wa ndani anapofugwa ni nani ana upendo na yeye na ni nani ambaye hampendi.
PAKA ukimpenda na kumthamini atajua na atatulia ndani ya nyumba na kutelekeza majukumu yake.
PAKA ukimyima chakula, ataenda kula kwa jirani.
PAKA ni mpambanaji sana na anajua kujitafutia. Kamwe hawezi kufa kwasababu ya njaa.
PAKA ukimyima chakula, anaweza pia kuwa mwizi.
PAKA anahitaji mapenzi, PAKA anahitaji mahaba, PAKA anahitaji michezo, PAKA anahitaji furaha.
Kama utamnyima PAKA wako mapenzi, mahaba, michezo au furaha basi usije kumpa lawama siku ukimkuta kwa jirani yako au kwa moja ya mafiki zako au kwa mtu mwingine yeyote anayetambua thamani yake.
Sijui unanielewa lakini!!? Hahahaha!!! Basi hicho ndicho ninachokimaanisha.
Mtunze PAKA wako vizuri, mpe kile anachokihitaji kwa wakati. Njaa ni mbaya sana, kiu inaumiza.
Kamwe! Hakuna PAKA anayeweza kuvumilia njaa. Hakuna PAKA anayeweza kuvumilia mateso.
PAKA ukimyima chakula, ataenda kula kwa jirani na akirudi kwako yeye ni kulala tu, wala hana time na wewe. Yani kwa kifupi, atakuwa yupo kama vile hayupo.
Ukitaka akukamatie panya atakwambia sina uwezo wa kukamata panya. Ni vile tu na yeye anafanya kusudi.
Yani wewe unamyima hiki na yeye anakunyima kile. Hahaha!! Hii ni hatari sana!!
Tambua duniani hauko pekeyako, watu wanaomtamani PAKA wako ni wengi sana na wanaendelea kumshawishi kila siku ili wampate.
Usipokuwa makini, utampoteza kirahisi sana, ukija kushtuka keshaondoka na si wako tena. Bahati hairudi malambili.
Thamini sana ulichonacho, kiheshimu, kitunze na ukilinde.
PAKA wa watu unaowatamani, kuna wenyewe wanaowafanya wawe vile walivyo, hata wako ni mzuri kuliko wako lakini ni vile tu wewe umeamua kumchukulia poa PAKA wako.
Ujumbe huu ni kwako baba, kwako mama, kwako kaka, kwako dada. Neema ya Mungu na iwe juu yako katika kujifunza.
#No_Learning_No_Earning
So we have to Learn.
Prepared By
Mr George Francis
Email: mr.georgefrancis21@gmail.com
ATAENDA KULA KWA JIRANI.
Sina shaka kuwa unawafahamu PAKA, kama hujawai kufuga, basi hata kwa jirani zako ushawahi kuwaona.
PAKA ni miongoni mwa wanyama wa kufugwa wanaoishi vizuri na binadamu, lakini pia wana tabia ya kubadilika na kuwa moja ya viumbe hatari kwa binadamu.
Moja ya tabia nzuri za PAKA ni kupenda anapopendwa.
PAKA ana uwezo wa kuwajua watu wote wa ndani anapofugwa ni nani ana upendo na yeye na ni nani ambaye hampendi.
PAKA ukimpenda na kumthamini atajua na atatulia ndani ya nyumba na kutelekeza majukumu yake.
PAKA ukimyima chakula, ataenda kula kwa jirani.
PAKA ni mpambanaji sana na anajua kujitafutia. Kamwe hawezi kufa kwasababu ya njaa.
PAKA ukimyima chakula, anaweza pia kuwa mwizi.
PAKA anahitaji mapenzi, PAKA anahitaji mahaba, PAKA anahitaji michezo, PAKA anahitaji furaha.
Kama utamnyima PAKA wako mapenzi, mahaba, michezo au furaha basi usije kumpa lawama siku ukimkuta kwa jirani yako au kwa moja ya mafiki zako au kwa mtu mwingine yeyote anayetambua thamani yake.
Sijui unanielewa lakini!!? Hahahaha!!! Basi hicho ndicho ninachokimaanisha.
Mtunze PAKA wako vizuri, mpe kile anachokihitaji kwa wakati. Njaa ni mbaya sana, kiu inaumiza.
Kamwe! Hakuna PAKA anayeweza kuvumilia njaa. Hakuna PAKA anayeweza kuvumilia mateso.
PAKA ukimyima chakula, ataenda kula kwa jirani na akirudi kwako yeye ni kulala tu, wala hana time na wewe. Yani kwa kifupi, atakuwa yupo kama vile hayupo.
Ukitaka akukamatie panya atakwambia sina uwezo wa kukamata panya. Ni vile tu na yeye anafanya kusudi.
Yani wewe unamyima hiki na yeye anakunyima kile. Hahaha!! Hii ni hatari sana!!
Tambua duniani hauko pekeyako, watu wanaomtamani PAKA wako ni wengi sana na wanaendelea kumshawishi kila siku ili wampate.
Usipokuwa makini, utampoteza kirahisi sana, ukija kushtuka keshaondoka na si wako tena. Bahati hairudi malambili.
Thamini sana ulichonacho, kiheshimu, kitunze na ukilinde.
PAKA wa watu unaowatamani, kuna wenyewe wanaowafanya wawe vile walivyo, hata wako ni mzuri kuliko wako lakini ni vile tu wewe umeamua kumchukulia poa PAKA wako.
Ujumbe huu ni kwako baba, kwako mama, kwako kaka, kwako dada. Neema ya Mungu na iwe juu yako katika kujifunza.
#No_Learning_No_Earning
So we have to Learn.
Prepared By
Mr George Francis
Email: mr.georgefrancis21@gmail.com