Pajue Iringa kwa kupitia picha

Pajue Iringa kwa kupitia picha

Iringa ni moja ya miji yenye hali ya hewa nzuri sana
 
Sehemu nyingine bana ukifika usiku unaweza Dhani uko Beijing subiri kukuche sasa unaweza Dhani uko kivu kaskazini
 
Kwa tako sijapaona nimekula Ice cream pale sana nikiwa mtoto. I wish pia kuiona Tosamaganga kwasasa inafananaje. Huu mkoa nina historia nao sana. Nimesoma na kuishi Iringa. Ahsante Mkuu, vipi na mmea mnalima?
Tosamaganga umeishi au umesoma? Mimi nimesoma lupalama a primary. Nilikua nakaa bweni tosamaganga boys home. Ninazo picha za maeneo yale. Tuliokuwa bweni boys home na waliomaliza kule juu lyalamo primary huwa tunajikusanya tunaendaga kuwatembelea madogo kila tunapopata nafasi
 
Viwanja na Bar kali huo mji hamna au
Kama ni mtu wa bata na ushazoea pilika pilika za dar kule iringa sio sehemu ya kuishi. Eneo la mjini ni dogo viwanja ni vichache halafu ni ijumaa tu ndio huwa club panachangamka.

Hizo picha tofauti tofauti unazoziona unaweza ukafikiri ni maeneo mengi. Ila zimechukuliwa ndani ya mzunguko wa eneo dogo tu mfano sinza peke ake, halafu hapo ndio mjini sasa. Ukitoka hapo makazi ya watu na mashamba tu
 
wanasema iringa imebarikiwa ningependa kuona hizo baraka hata tatu tu itakuwa imekata kiu changu!
Mkuu matangazo ya utalii hayo, hata kigoma utaambiwa imebarikiwa. Nenda sasa, hakuna kitu.

Lakini Iringa kama una kazi nzuri na unapenda utulivu ni sehemu nzuri kuishi. Disadvantages za iringa kama ni mtu wa viwanja deile kule sio sehemu ya kuishi. Pia mzunguko wa biashara sio mkubwa kwa sababu mji ni mdogo.

Nimeishi iringa miaka mitatu nilinunua kiwanja maeneo ya kigonzile nikaanza ujenzi. Kabla ujenzi haujaisha nikarudi dar. Mwakani nataka nimalizie ujenzi halafu nyumba niwe napangisha kwa wanafunzi au lecture wa chuo cha tumaini. Hopeful nitaweka makazi yangu iringa uzeeni nikiwa sina tena nguvu za kuendana na pilikapilika za dar.
 
Back
Top Bottom