Nguruvi3
Platinum Member
- Jun 21, 2010
- 16,309
- 33,782
Jamani,
Ukisema wanasiasa wameiharibu TANESCO,una maana gani?...maana yake ni kuwa TANESCO ni shirka la serikali.Historia inaonyesha kuwa serikali ina maamuzi ya kisiasa mno!
So,why do we want to give kiwira back to the government?...so they can have their cadres make decisions for it?...nah,I dont think it's a good idea.
TANESCO's failure is TANESCO's failure,and if you say politicians ruined TANESCO,thats even worse because we don't want politicians hands in kiwira again....so rule TANESCO out,unless they completely overhaul it!
Tanesco ni shirikala umma, Mkurugenzi anateuliwa na Rais (hadi mwaka jana, sijui sasa), bodi ya wakurugenzi inateuliwa na waziri.
Maamuzi mengi yanayoidhoofisha Tanesco ni kutokana na mashinikizo ya wanasiasa na si wataalamu wa fani ya energy.
Mkapa aliingiza Net Group kwa nguvu kwa kutumia FFU, ili hali wafanyakazi walijua tatizo ni nini. Labda Kobello utuelimishe Net group ya mkapa ilisaidiaje mafanikio ya Tanesco.
Kuingia kwa IPTL wakati wa Mwinyi ni mkataba wa kisiasa. Ukweli ni kuwa kulikuwa na njia mbadala, lakini kwa kuangalia 10%, wakasaini mkataba mbovu unaoiua tanesco hadi leo. Waliofanya hivyo ni wanasiasa chini ya mhuri wa baraza la mawaziri. Kobello kama IPTL ni mkataba safi tuthibitishie maana tuna ushahidi wa kutosha kuwa ule ulikuwa uchafu wa wanasiasa.
Richmond ya EL na vimemo vya kushinikiza ipewe tenda kimkato mkato ni ushahidi usiohitaji certificate yoyote kuhusu uingiliaji wa wanasiasa, labda tu kwa anayegoma kuelewa.
Dowans ni ushahidi wa jinsi mikataba inavyoandikwa city centre kijiweni kwa jina la Tanesco. Kama umesoma nyaraka za Dowans haitakuchukua hata dakika mbili kujua ukweli, lakini inahitaji ueledi kujua na kama hakuna utashi wa kuelewa ni ngumu sana.
Tanesco wanapodai bilioni 56 kutoka Zanzibar wanakatazwa kwasababu tu za kisiasa, hata idara na mashirika ya umma ni hivyo. Shirika gani litaendeshwa kwa utaalamu wa kisiasa. Wapi ilifanikiwa hiyo.
Hivi ni kwanini akina January watoe maelezo ya kisayansi juu ya 'energy' na si wataalamu wa fani hiyo.?
January, Zitto, Filikunjombe, Ngeleja na kamati zao wanatakiwa wapate maelezo kutoka kwa wataalam wa Tanesco, na si kazi yao kutueleza kina cha maji mtera au megawatt/ hr zinazozalishwa. Kujiingiza kwao kuna maana zaidi ya umeme ambayo ni 'politics'
Tanesco inatumika kama 'conduit' ya miradi ya wazee kwa gharama za asilimia 20 ya watumiaji na 80 wasio na umeme kabisa.
Kama hakuna maboresho kw tanesco kwa kuiacha huru ijiendeshe kama taasisi, sijui NSSF itakwepaje kibano.