Hahahahaha! Nitalala usingizi saafi mkuu maana watu pasua kichwa kwelikweli humu!Unazungumzia nguvu ya umeme ama nguvu ya umma?
Of course lazima NSSF isimamiwe na kuna vyombo vinawasimamia, je SSRA wameshasema kitu, BOT wameshasema kitu? Sasa mnapiga kelele za nini JF pipili ya shamba inawawashia nini nyie?
Vile vile nachoshangaa pia wachangiaji wengi wameshawatuhumu NSSF mafisadi wakati hakuna hata mmoja wenu ambaye na vithibitisho juu ya hilo kama sio chuki nini hizo? Na JK ameingia wapi hapo mkuu.
Of course lazima NSSF isimamiwe na kuna vyombo vinawasimamia, je SSRA wameshasema kitu, BOT wameshasema kitu? Sasa mnapiga kelele za nini JF pipili ya shamba inawawashia nini nyie?
Vile vile nachoshangaa pia wachangiaji wengi wameshawatuhumu NSSF mafisadi wakati hakuna hata mmoja wenu ambaye na vithibitisho juu ya hilo kama sio chuki nini hizo? Na JK ameingia wapi hapo mkuu.
Mkuu usimamizi wa SSRA unaingia mambo yakishakuwa yameborongeka kama sikosei .... ... hao ni regulator au sio? Sasa kazi yao sio kupanga projects and then why now hawa NSSR wanaibuka Je walihusika vipi katika projects zilizotangulia za NSSF? Pili labda nikukumbushe kuna issue ya Daraja la kigamboni natumaini umeona TIC wanawapigia kelele, vile vile kuna swala la watoto waliokufa Tabora ambapo NSSF walihusika na vifo vile kwenye one of their Investment. Bila kusahau jinsi NSSF kwa kushirikiana na Manji kwenye biashara za kitapeli natumaini hilo unalifahamu. Sasa basi katika mazingira kama hayo kwa nini sisi watu wazima na akili zetu timamu tuwakubalie kwenye mradi huu wa umeme wakati mosi tunafahamu hawana uwezo, wamekwisha kushindwa sehemu nyingine. Ooops nimesahau walikuwa na issue nyingine ya kujenga kule Nairobi etc.
Sasa hawa ambao wanashindwa hata kuweka website yao Live kweli tunawahitaji kwenye swala la nishati? Labda utusaidie tuone accounts zao kwa kipindi cha miaka mitano ... ... ... .... ili wachangiaji wa NSSF na walipa kodi wa Tanzania wajiridhishe kama wewe.
Guys
Naomba bora tuliangalie hili suala kwa marefu na Mapana maybe for once tungeacha ushabiki na kuwa walau objective kwenye kujibu au kuchangia hii mada. One would have thought kuwa kijireserach kidogo na hasa from someone who post ina forum that prides it members as GREAT THINKERS angeweza kuliangalia hili kwaupana zaidi. Issues za kutazama hapa ni zi fuatazo:
-Current state ya Umeme Tanzania
-Makosa yaliyofanyika wakati wa liberalisation ya sekta ya Umeme
-Role ya NSSF kwenye hili itakuwa ni ipi?
-Je NSSF wanaruhusiwa na stakeholders wao kuingia kwenye hii biashara yak u generate umeme?
-Je kuna faida yoyote itapatikana kwenda NSSF?
-Je wenzetu wan je wanafanya vipi?
Sasa majibu ya hapa yanaweza yakatoa mwanga walau kiasi mkaelewa why I support hawa jamaa kufanya mambo kama haya.
Umeme Tanzania:
Tanzania mwenye jukumu la generate, transmit and distribution ya umeme zamani ilikuwa exclusively TANESCO ambayo kama mjuavyo ni shirika la umma kwa asilimia 100 na wako responsible kupply asilimia 98 ya umeme Tanzania
Statistics zinasema hivi:
- Megawati 381 za umeme ambao tunatumia sasa hivi unatokana na vyanzo vya maji
-Tanzania tuna uwezo wa kuzalisha mpaka Megawatt 5,000 ya umeme
- Per capita electricity consumption yetu ni 46/KWh per annum, ambayo inakuwa kwa asilimia 11-13 au zaidi
Hiyo ni moja kati ya sababu serikali inataka sana secta binafsi ziingie kwenye haya mambo ya kugenerate umeme. Mind you nchi ina watu milioni 40 na ni LESS THAN 10 % wako connected kwenye umeme. Serikali yetu pamoja na madudu mengi yanayotokea huwa ni competent kwa kujua matatizo ila tatizo huwa ni kwenye namna na njia ya kuyatatua hayo matatizo.
Ndio maana kama mnakumbuka miaka ya 90's waliamua kulegeza masharti na kufanya reform kwenye hii sekta ya nishati na kuruhusu wazalishaji binafsi na hapo ndipo walipoingia the Songas na IPTL kwa nia ya kupunguza shedding, Of course it was not without controversy za akina RUGEMALILA (the same dude aliyeingia ubia na TRITEL) na mwishowe wakapelekana mahakamani, yaani IPTL na TANESCO lakini kujua haya yote inabidi uelewe connection kati ya EastCoast Energy v/s Independent Power Tanzania Limited (IPTL) v/s Songas v/s Ministry of Energy and Minerals (Wizara ya Nishati) v/s Parastatal Sector Reform Commission (PSRC) v/s Tanzania Petroleum Development Corporation (TPDC) v/s VIP Engineering Limited (VIP), v/s (TANESCO) v/s NETGroup Solutions vs SIDASida) na bila kuwasahau waheshimiwa wa pale World Bank.
Lakini ukiachilia hao wauzaji wakubwa kulikuwa na wauzaji wengine wadogo kwa TANESCO, kama vile Tanwat (2.5 MW), Kiwira Coal Mine (6.0 MW) na bila kuwasahau Kilombero Sugar (2.5 MW) Mindhali humu kuna GREAT THINKERS nashauri mtafute Economic Recovery Program (ERP) ya 1986-1989 kati yetu na jamaa wa World Bank na IMF ndio mtaelewa kiini cha yoote haya ya reform kwenye sekta hiina zinginezo
MAKOSA TULIYOYAFANYA:
1. POOR COORDINATION: Victim mkubwa hapa alikuwa ni ESI nah ii ilisababishwa na poor coordination. Kupitia wizara mabali mbali (jambo ambalo mpaka leo linaendelea) bilakusahau wadau na wahisani wakati uleee wa kujadili mikataba ya Songas na IPTL. Kama taifa we PAID A HEAVY PRICE. Of course itakuwa ni jambo rahisi sana kukaa hapa na kuanza mambo ya finger pointing lakini haya ndio yale yale kuwa hatutaki kutatua mambo madogo madogo kama ya COORDINATION imagine HAZINA vs NISHATI vs TANESCO vs DONORS vs EVERYONE !!!
2.POOR PRIORITIZATION: Tusijindanganye, evitable consequence of poor coordination is that power sector reforms have been neither clearly prioritized nor implemented na Serikali yetu. Mfano mdogo hatuna clear policy framework for private sector investment katika secta hii, issue skama target percentage of private generation, standard investment incentives and contractual norms kwa jili ya PPA. Bila kusahau kuwa hatuna clear and feasible roadmap for how to make the main off-taker financially and technically viable. Matokeo yake Sekta hii ya Nishati Tanzana in the last 20 years has the sector has gone from dealing with crisis after crisis (kwanza kiangazi cha miaka ya 90 then issue ya high capacity charges, na mengineyo), hii yote imepelekea kudelay of the planning and execution of fundamental reforms necessary for the long-term sustainability of power supply and expansion kwenye nchi yetu na mbaya zaidi hatujui hata priority zetu ziko wapi when it comes to alternative energy!!!! Yaani tumekuwa kama motto mkiwa asiye na baba wala mama wala ndugu wa kumtazama.
3. FAIR AND INDEPENDENT REGULATION: Bila hii hatutofika na hakuna investor atakaye taka kuja kuinvest kwenye hiii sektaka kama hatuna transparency . Imagine kama regulator angekuwepo enzi zile IPTL na Songas wameanza it means akina Mhavile and Co wangekuwa wako bize kuzalisha umeme badala ya kushinda Mahakamani na kwingineko. Sasa hivi tunao EWURA lakini hao wamekuwa kama vile PPRA hawana nguvu zozote zile na sote tunajua no one knows or lets just say its unclear when truly independent oversight will commence. This fact may have cost the country past and present investments and may ultimately impact on future investments.
Sababu zingine ni kutokuwepo kwa uwazi kwenye UNFAIR BIDDING PROCESS, ARBITRATION , CURRENCY DEVALUATION na mengineyo bilakusahau kuwa tunashindwa kua attract makampuni ya uhakika kama TATA kwa kuwa we are not interested na pili hawa washazowe mambo ya transparency sie hayo hatutaki...!
ROLE YA NSSF
Kwenye hili as far as I know NSSF itakuwa ni IPP yaani independent power Producer kama walivyokuwa wengine ila kazi ya distribution ni ya Tanesco hivyo kama wataleta ma generator yao au watatengeza wa Jua au upepo au Gesi toka songo songo thats up to them
JE SHERIA INAWARUHUSU NSSF KUFANYA HIVI:
I would imagine NSSF sio PPF so I cant see them getting involved na jambo ambalo liko kinyume au sheria haiwaruhusu kulifanya. Sina sheria Mama ya ambayo naweza ku quote lakini kama kuna IPP zaidi ya 10 Tanzania sidhani kama wameenda kinyume na sheria. Nadhani hii ipo kwenye investment policy yao so this shouldn't be an issue. Pia si vibaya mkajua kuwa shirika hili lina BOARD ambayo wao ndio wenye maamuzi ya mwisho kwenye mambo kama haya na ndani ya bodi wapo wawakilishi wa wafanyakazi sasa sidhani kama maamuzi yanaweza kufanywa na mtu mmoja
RETURNS:
Kama watu wa investment as far as I know ni kuwa kwa Tanzania inasemekana return ya investment kwenye umeme ni 300% sasa surely hapa naona ni win win situation kwa NSSF
WENZETU NJE WANAFANYAJE?
Malaysia, Philipines,Brazil,Vietnam,India, Jordan, Egypt na kwingineko Pension Funds zao wameinvest kwenye umeme na wanapata returns kubwa sana
Btw TANESCO washankatia umeme ntarudi baadae.
Nadhani mkuu,
Hujanifahamu ni hivi ikiwa NSSF wana matatizo BOT wako wapi au SSRA au Wizara husika? Kama wako kimya inamaana hawana matatizo mkuu.
Nadhani mkuu,
Hujanifahamu ni hivi ikiwa NSSF wana matatizo BOT wako wapi au SSRA au Wizara husika? Kama wako kimya inamaana hawana matatizo mkuu. Kuhusu miradi kama organisation yeyote miradi ni kitu kinakuwa plan ila kama kikiwa kimeonekana hakina faida au natija kwa shirika kinaweza kubakia katika makaratasi tu kama plans za serikali. Umezungumzia utapeli wa Manji huo umebakia ni myth still mpaka leo hakuna kithibitisho kizito kuweka kesi mahakamani. Miradi ya Kigamboni kama umesoma gazeti leo au Jana Dr Dau ametangaza kuwa ujenzi unaanza mwaka huu (sasa sijui kama wameshindwa au ni mipangilio tu kumbuka huu ni uwekezaji mkubwa hawawezi kukurupuka tu kama unavyotaka mtu kujenga nyumba yako).
Kuhusu aacounts zao kweli hilo linatia shaka but katika nchi yetu ambayo hata website ya Wizara ya fedha ina taarifa za mwaka 2005 sishangai NSSF kuwa na website iliyobora ila si uende pale NSSF kuomba financial reports zao (Annual reports). Ikishindikana mnaweza kuwatumia akina Mgaya maana wao si ndio wahudhuriaji wa vikao vya bodi za wadhamini wa NSSF watakuwa nazo tu. Teknolojia Tanzania bado tuko nyuma sana.
Katika haya sihitaji kuyajibu kwani post zako zinaonyesha hoja zimetawaliwa na ubaguzi mwanakijiji. Kwanini kuna sababu mbili naweza kukupa ambazo hazihitaji mwanasayansi wa upasuaji au PhD kufahamu unalenga wapi?
Mosi umeshindwa kutushawishi kwanini tuhofie NSSF zaidi ya PPF au PSPF, LAPF. Hoja kubwa unayoileta jamvini ni ukubwa wa uwekezaji but unasahau kama pension na financial institution inatakiwa kukua kimtaji na kiundeshaji. Hivyo basi kutokana na hilo unasema NSSF inatumika kama mrija wa serikali kukamilisha mipango yao (even though huna ushahidi yakinifu kwa haya uyasemayo).
Pili mashambulizi yako yamelenga mifuko miwili kama ukisoma post zako za nyuma a. NSSF, b. PSPF but mashambulizi katika mifuko mengine umekuwa mchache mno kama sio hakuna kabisa. What do these financial institutions have in common? Wakurugenzi wakuu wote hapa ni waislamu (NSSF ni Dr Dau, PSPF ni Dr Mmanga).
Kama nilivyosema mwanzoni haihitajiki uwe na PhD au kuwa a nuclear scientist kufahamu unalenga wapi. Mifuko mengine je iko hali gani? Vp kule CRDB kwa Dr Kimei? Tushawishi zaidi NSSF wamekosea wapi nitabidili kauli yangu kwasababu awe muislamu au mkristo kama ni fisadi ni vema akemewe na kwa faida ya shirika na tanzania kwa ujumla.
Niliuliza huko Nyuma Dr. Dau aliteuliwa na nani kushika nafasi ya Ukurugenzi NSSF na lini? Maana naona tunazungushana tu hapa.
well.. ushahidi uko katika hoja.
Jamani,
Ukisema wanasiasa wameiharibu TANESCO,una maana gani?...maana yake ni kuwa TANESCO ni shirka la serikali.Historia inaonyesha kuwa serikali ina maamuzi ya kisiasa mno!
So,why do we want to give kiwira back to the government?...so they can have their cadres make decisions for it?...nah,I dont think it's a good idea.
TANESCO's failure is TANESCO's failure,and if you say politicians ruined TANESCO,thats even worse because we don't want politicians hands in kiwira again....so rule TANESCO out,unless they completely overhaul it!
Hoja? "Mamamia". Pumba, ufataani, roho korosho, unaziita hoja? Unashangaza sana.
Hivi hujuwi kuwa mifuko ya pensheni ndio moja katika wawekezaji wakubwa duniani? Tena katika nyanja mbalimbali, mojawapo hii ya "energy"?
Kama hilo hulijuwi, naona sasa unalijuwa. Na kama hilo unalijuwa, jibu lako ni hiyo "para 1".