bampami
JF-Expert Member
- Nov 5, 2011
- 5,697
- 4,107
Ni jana tu tulikuwa tunasherekea krisimass karibu wakristo wote duniani, ni sikukuu ya kumshukuru Mungu kwa kumleta mwanae wa pekee ambaye alikuja kutuokoa na dhambi zetu, kwa ujmla tunaoaswa kusherekea kwa furaha na amani, lakini si wote ambao hutumia sherehe hizo kwa kumheshimu Mungu, wengi wetu hujikuta tukifanya dhambi kama uzinzi, kunywa pombe kwa kupindukia, kudanganya (hasa katika mawasiliano ya simu n.k) n.kHapa UDSM kwa jana wanachuo wengi hawakuwepo maeneo ya chuo, karibu mchana wote mpaka mida ya usiku kama saa nane saa tisa n.k, nlijaribu kutoka nje kidogo ya campus nami nikaenjoy sikukuu, cha ajabu ndugu zanguni karibu maeneo mengi ukianzia survey , mwenge, sinza n.k wanachuo wengi walikuwa po huko. SI MBAYA KUWAPO HUKO KWANI SOTE TUNASHEREKEA.Ilipofika mida ya saa saba, ndipo ndugu zangu a.k.a watoto wa wakulima wakaanza kuingia chuo na bajaji pia bodaboda wamelewa vibaya huzani kama ni wasomi, na boom tulilopewa hili ni baya kuliko yote kwani kuna sikukuu ya xmass na mwaka mpya hivyo ukitumia vibaya boom hilo yamkini hata MTIHANI WA MWISHO HAPO JANUARY 2012 usifanye vizuri kwa kukosa pes, isitoshe sisi tukaao mbali tunahitaji nauli za kurudia huko na hali boom hilohilo ndo tunalitegemea.NDUGU zanguni, mi hatutakubaliana na mgomo wowote utajitokeza semister hii, eti kwasababu boom limeisha unless otherwise.