plagiarism
Senior Member
- Jul 14, 2021
- 133
- 295
Rushwa ni mwenendo usio faa anao ufanya mtu kwa manufaa yake binafsi. Kuna Aina nyinginza rushwa Kama rushwa ya fedha, ngono, Mali n.k
Sababu za kuongezeka kwa rushwa nchini.
Ongezeko la umaskini nchini hupelekea kutoa rushwa kwa lengo la kujipatia kitu flani mfano kazi.
Ubinafsishaji hii hulenga wale waliopo serikalini na binafsi kwa kutumia Mali za umma na kujibinafsisha kuwa ni zao. Usimamiaji mbovu, mfano kwenye ujenzi, huduma za kijamii huwa kuna matumizi makubwa ya rushwa.
Hizi Ni baadhi ya sababu zinazo pelekea ongezeko la rushwa, lakini pia kuna njia ambayo itapunguza rushwa nchini Kama ifuatavyo.
Usimamizi mzuri wa Mali, fedha n.k, hii itasaidia watu kupunguza matumizi ya rushwa kwa kuhofia kujulikana.
Kuweka sheria Kali itakayo wabana watu wote kuto kutoa rushwa Wala kupokea.
Elimu kwa wananchi ili waweze jua haki zao za msingi na kupunguza adha ya kuibiwa fedha na Mali zao.
Kupunguza umaskini kwa kutoa ajira kila mwaka lakini pia kuweka njia wezeshi za kujiajiri kwa watu itafanya rushwa kupungua na kuleta maendeleo yenye tija nchini.
Hitimisho. Rushwa haikubaliki usikubali kutoa Wala kupokea rushwa na kila mmoja awe mlinzi wa mwenzie kutokomeza janga hili.
Sababu za kuongezeka kwa rushwa nchini.
Ongezeko la umaskini nchini hupelekea kutoa rushwa kwa lengo la kujipatia kitu flani mfano kazi.
Ubinafsishaji hii hulenga wale waliopo serikalini na binafsi kwa kutumia Mali za umma na kujibinafsisha kuwa ni zao. Usimamiaji mbovu, mfano kwenye ujenzi, huduma za kijamii huwa kuna matumizi makubwa ya rushwa.
Hizi Ni baadhi ya sababu zinazo pelekea ongezeko la rushwa, lakini pia kuna njia ambayo itapunguza rushwa nchini Kama ifuatavyo.
Usimamizi mzuri wa Mali, fedha n.k, hii itasaidia watu kupunguza matumizi ya rushwa kwa kuhofia kujulikana.
Kuweka sheria Kali itakayo wabana watu wote kuto kutoa rushwa Wala kupokea.
Elimu kwa wananchi ili waweze jua haki zao za msingi na kupunguza adha ya kuibiwa fedha na Mali zao.
Kupunguza umaskini kwa kutoa ajira kila mwaka lakini pia kuweka njia wezeshi za kujiajiri kwa watu itafanya rushwa kupungua na kuleta maendeleo yenye tija nchini.
Hitimisho. Rushwa haikubaliki usikubali kutoa Wala kupokea rushwa na kila mmoja awe mlinzi wa mwenzie kutokomeza janga hili.