Ongezeko la Posho za Wabunge ni Wizi na Dhulma dhidi ya Wafanyakazi

mwanakijjii makala yako inawauliza wanaccm na rais wao mie ningependa niwaulize makamanda je katika kikao cha ikulu waligusia kusikitishwa kwao na ongezeko hilo au waliuchuna? Mara nyingi nemekuwa nikisoma makala zako naona zinaegemea upande mmoja bila kuangania upande wapi nao wanamsukumo gani katika tatizo husika. Huwa nafurahi kusoma makala za maggid mjengwa jamaa huwa anasimamia ukweli yaani yupo balanced sana.

Kwa sasa Tanzania baada ya miaka 50 ya uhuru tumekuwa na uhaba wa waandishi wa namna ya Maggid Mjengwa wengi wa waandishi ni "maslahi" wanaotetea makundi yanayowashibisha au yenye manufaa nao. Waandishi lazima wajue umuhimu wao wa kupasha habari jamii/hadhira na adhari zake pamoja na faidi katika maendeleo ya jamii kwa ujumla.

Maggid Mjengwa hajawahi kuwa "balanced".... Maggid ni mwanaCCM, uchaguzi wa Rais na Ubunge uliopita alitumia blog yake na aliweka wazi kabisa kwamba yeye ni mwanaCCM na haoni ni nani wa kushindanishwa na JK..... Sema ni muwazi.... sijui km UWAZI na being balanced are synonymous.

Kwenye posho Watanzania ni km tumerogwa. Najiulizaga ni kwanini ni Tanzania tu mtu anaibiwa na serikali, mtu binafsi, kampuni etc lakini tuko kimya tu na tunapiga soga jioni iwe majumbani, vijiweni, bar etc kuhusiana na hilo, ila HATUTHUBUTU kusema basi...... TUtaandika humu, tutasema vijeweni jioni, wengine watalia etc ndo tumemaliza.......... Kwanini hatuna uthubutu wa kusema basi POSHO, BASI MEREMETA, BASI RICHMOND, nilikuwa Mtwara two weeks ago kunawazungu wanajidai wanafanya exploration ya oil, nilishuhudia kwa macho yangu kila lisaa meli nyingi sana zinaondoka zimejaza crude oil.... Wale wazungu wanaishi Dar, wanakula lunch Dar na kulala Dar...... nilishuhudia flight ikiwachukua saa 7 na kuwarudisha saa 9 na jioni saa kumi mbili...... Wadada zetu, watoto wetu wanaosoma SAUT - Mtwara, UTUMISHI ndio viburudisho vyao - wakitoka mle melini wanahongwa 200,000/= kwa udhalilishaji waliofanyiwa - TUTHUBUTU na tuseme BASI........ Its a high time for that..... "We must meet the needs of the present generation without compromising the ability of future generations to meet their own need" WCED: 1987:8)... to realize that TUANZE BASI KUSEMA BASI..............
 
i can't control my temper, nadhani ni busara nijiondoe kwenye hii thread mambo mengine ni zaidi ya maudhi.
mkuu tuendelee kuwepo ndio wawakilishi wetu hawa wanajua wazi hatuwatuma haya .. Ila tunaziona dhamira zao dhati kwenye hili
tujihatidi kuzuia hasira zetu "i choose engineering as my career and i fall in love with it ntapata hela tu huku na taifa litanufaika na mchango wangu"
 
Hakuna nia ya dhati ya kuiboresha Tanzania miongoni mwa wabunge na wanasiasa. Kitu ninachokiona ni kuwa, wanasiasa wanafikiri wao ndio pekee waliopewa urithi wa Tanzania. Wanawasahau watanzania wengine, kama vile hawapo.
 
Hakuna nia ya dhati ya kuiboresha Tanzania miongoni mwa wabunge na wanasiasa. Kitu ninachokiona ni kuwa, wanasiasa wanafikiri wao ndio pekee waliopewa urithi wa Tanzania. Wanawasahau watanzania wengine, kama vile hawapo.

Kibaya zaidi wabunge wa CCM wamekuwa ndo wasemaji wa serikali kwa namna hiyo wapo kwa masrahi ya matumbo yao
 
nid dhulma kubwa sana kwa wananchi ambao ni walalahoi
mkuu kwenye hili hawatoki wala hawaponi hata kwa kikombe cha babu it is unfair .. Wanafunzi wa vyuo vikuu wakigoma wanaitwa wahuni wapenda starehe nk.., wazee wa east african comm. Wakiandamana kudai salio lao wazee wa maji washa wanatumwa kuwatawanya lol
 
Huwa nafurahi kusoma makala za maggid mjengwa jamaa huwa anasimamia ukweli yaani yupo balanced sana.

Kwa sasa Tanzania baada ya miaka 50 ya uhuru tumekuwa na uhaba wa waandishi wa namna ya Maggid Mjengwa wengi wa waandishi ni "maslahi" wanaotetea makundi yanayowashibisha au yenye manufaa nao. Waandishi lazima wajue umuhimu wao wa kupasha habari jamii/hadhira na adhari zake pamoja na faidi katika maendeleo ya jamii kwa ujumla.

Kama mjengwa ndiye unamuona mwandishi aliye balanced sana basi utakuwa na matatizo katika kusoma makala. Lakini inawezekana si matatizo bali ni upande uliouchagua kusimamia, angle unayoitumia kumuangalia mjengwa inakuweka kwenye nafasi ya kumuona yuko balanced sana huku wengine wakiwa wanapendelea.
Mjengwa huyu huyu wa iringa anaye wabeba ccm kwa mbeleko ya chuma? au mjengwa mwingine? mjengwa huyu huyu anayewaponda wapinzani kila siku amekuwa balanced tangu lini?

Kwa taarifa yako tu ni kwamba mjengwa ni miongoni mwa waandishi "maslahi" wanaotetea makundi yanayowashibisha au yenye manufaa nao!! chukua hiyo kama ulikuwa hujui.
 
Zitto kabwe


hii ni kauli ya Mbunge wa kigoma kaskazini ZITTO KABWE kuhusu kupandishwa kwa posho za vikao vya wabunge.
Nimeshtushwa sana na taarifa za kupandishwa kwa posho za vikao kwa Wabunge. Nimeshtushwa zaidi kwamba Posho hizi zimeanza kulipwa katika mkutano wa Bunge uliopita kabla hata Rais hajaamua maana maslahi yote ya Wabunge huamuliwa na Rais Baada ya kupokea mapendekezo ya Bunge kupitia Tume ya Bunge.

Wabunge wote watambue kwamba kuamua kujipandishia posho zao bila kuzingatia Hali ya maisha ya mwananchi wa kawaida ni usaliti usio na mfano. Mbunge yeyote ambaye anabariki Jambo hili au anaishi hewani haoni tabunza wananchi au ni mwizi tu na anaona Ubunge ni Kama nafasi ya kujitajirisha binafsi.
Kwa Wabunge wa Chadema, wajue uamuzi kuhusu posho ni uamuzi wa chama na ni uamuzi wa kisera. Mbunge yeyote wa Chadema anayepokea posho za vikao anakwenda kinyume na maamuzi ya sera za chama tulizoahidi wananchi wakati wa uchaguzi. Nimemwomba Katibu Mkuu wa chama kuitisha kikao maalumu cha Kamati Kuu ya chama kujadili suala hili.
Toka tarehe 8 juni mwaka 2011 nilikataa kupokea posho za vikao. Popote ninapohudhuria vikao huomba Risiti ya fedha ninazokataa. Baadhi ya Wabunge Kama Januari Makamba wamekataa posho na hata kwenye semina ya kamati ya nishati alikataa na tumeona kwenye vyombo vya habari jina lake likiwa limekatwa ilhali viongozi wakubwa kabisa wamechukua posho. Nampongeza kijana mwenzangu kwa uzalendo huu. Nawataka wabunge wengine wenye Moyo wa dhati kukataa sio tu ongezeko hili la posho Bali posho yote ya vikao. Kwa nini mbunge akubali kulipwa kwa kukaa?

Tazama nchi hii, juzi serikali ilipokea Msaada wa tshs 20bn kwa ajili ya Sensa ya mwakani wakati wabunge wanalipwa 28bn Kama posho za kukaa tu.
Tanzania inaagiza gesi ya matumizi ya nyumbani kutoka nje kwa kutumia mamilioni ya dola za kimarekani. Kuwanda cha kutengeneza LPG kinagharimu tshs 35bn tu, Wabunge peek Yao kwa mwaka wanatumia 28bn kwa posho za kukaa tu achilia mbali mishahara na marupurupu mengine.
Ipo siku Watanzania watatupiga mawe kwa usaliti huu dhidi yao.
 
mkuu kwenye hili hawatoki wala hawaponi hata kwa kikombe cha babu it is unfair .. Wanafunzi wa vyuo vikuu wakigoma wanaitwa wahuni wapenda starehe nk.., wazee wa east african comm. Wakiandamana kudai salio lao wazee wa maji washa wanatumwa kuwatawanya lol

Kibaya zaidi hao tunao nyonywa ndo tumesha jilidhikia na hali hii hawa jamaa watakuja na vitenge, viremba na ubwabwa juu kutulaghai warudi tena bungeni waendeleze unyonyaji wao huu.
 
Shosti,nadhan suala la posho halikua ajenda ikulu,
hili ningependa litolewe ufafanuzi na MAKINDA NA KASHILILA
mwanakijjii makala yako inawauliza wanaccm na rais wao mie ningependa niwaulize makamanda je katika kikao cha ikulu waligusia kusikitishwa kwao na ongezeko hilo au waliuchuna? Mara nyingi nemekuwa nikisoma makala zako naona zinaegemea upande mmoja bila kuangania upande wapi nao wanamsukumo gani katika tatizo husika. Huwa nafurahi kusoma makala za maggid mjengwa jamaa huwa anasimamia ukweli yaani yupo balanced sana.

Kwa sasa Tanzania baada ya miaka 50 ya uhuru tumekuwa na uhaba wa waandishi wa namna ya Maggid Mjengwa wengi wa waandishi ni "maslahi" wanaotetea makundi yanayowashibisha au yenye manufaa nao. Waandishi lazima wajue umuhimu wao wa kupasha habari jamii/hadhira na adhari zake pamoja na faidi katika maendeleo ya jamii kwa ujumla.
 
Hii imedhihirisha kwamba Uongozi wa bunge pamoja na wabunge walio wengi ni wanyonyaji, wajinga, wasaliti na walafi kupindukia.
Nyongeza ya posho haikuwa kipaumbele kwa wakati huu ambapo posho zililalamikiwa na serikali ikaahidi kufuatilia ili kuona uwezekano wa kuziondoa.
Ongezeko hili limekuja kinyume na tumaini la walio wengi kuwa posho hizi zingepunguzwa au kufutwa kabisa.

Mambo ya msingi ya kujiuliza, ni kwa nini kuwepo ongezeko la posho wakati ambapo bunge limepitisha muswada unaolalamikiwa?
Je hakuna uhusiano wa kupanda kwa posho na kupitisha maamuzi bila kutafakari kwa kina?

Kuna hoja za kijinga na kipuuzi zinazotolewa na wabunge kwamba wanahitaji posho kwa ajili ya kutoa misaada kwa wapiga kura wao, la kujiuliza;
Je ni mojawapo ya majukumu ya mbunge kutoa misaada? Hii siyo rushwa inayohalalishwa kwa upuuzi na ujinga tu?
Je ni wabunge tu wanaotoa misaada? kama kuna wengine wanapata wapi posho za kutolea misaada?

Ni muhimu ieleweke kwamba wabunge ni watu kama raia na wafanyakazi wengine serikalini na taasisi binafsi, hawaishi katika nchi nyingine na hivyo ugumu wa maisha ni kwa wote.
Kwa bahati mbaya wamechaguliwa wanyonyaji na watu wasiofaa kutetea maslahi ya wote katika jamii na hii ni hatari kubwa. Hawa wanatakiwa wapingwe kwa gharama yoyote. Hakuna uhalali wa nyongeza hiyo.
 
Zitto kabwe


hii ni kauli ya Mbunge wa kigoma kaskazini ZITTO KABWE kuhusu kupandishwa kwa posho za vikao vya wabunge.
Nimeshtushwa sana na taarifa za kupandishwa kwa posho za vikao kwa Wabunge. Nimeshtushwa zaidi kwamba Posho hizi zimeanza kulipwa katika mkutano wa Bunge uliopita kabla hata Rais hajaamua maana maslahi yote ya Wabunge huamuliwa na Rais Baada ya kupokea mapendekezo ya Bunge kupitia Tume ya Bunge.

Wabunge wote watambue kwamba kuamua kujipandishia posho zao bila kuzingatia Hali ya maisha ya mwananchi wa kawaida ni usaliti usio na mfano. Mbunge yeyote ambaye anabariki Jambo hili au anaishi hewani haoni tabunza wananchi au ni mwizi tu na anaona Ubunge ni Kama nafasi ya kujitajirisha binafsi.
Kwa Wabunge wa Chadema, wajue uamuzi kuhusu posho ni uamuzi wa chama na ni uamuzi wa kisera. Mbunge yeyote wa Chadema anayepokea posho za vikao anakwenda kinyume na maamuzi ya sera za chama tulizoahidi wananchi wakati wa uchaguzi. Nimemwomba Katibu Mkuu wa chama kuitisha kikao maalumu cha Kamati Kuu ya chama kujadili suala hili.
Toka tarehe 8 juni mwaka 2011 nilikataa kupokea posho za vikao. Popote ninapohudhuria vikao huomba Risiti ya fedha ninazokataa. Baadhi ya Wabunge Kama Januari Makamba wamekataa posho na hata kwenye semina ya kamati ya nishati alikataa na tumeona kwenye vyombo vya habari jina lake likiwa limekatwa ilhali viongozi wakubwa kabisa wamechukua posho. Nampongeza kijana mwenzangu kwa uzalendo huu. Nawataka wabunge wengine wenye Moyo wa dhati kukataa sio tu ongezeko hili la posho Bali posho yote ya vikao. Kwa nini mbunge akubali kulipwa kwa kukaa?

Tazama nchi hii, juzi serikali ilipokea Msaada wa tshs 20bn kwa ajili ya Sensa ya mwakani wakati wabunge wanalipwa 28bn Kama posho za kukaa tu.
Tanzania inaagiza gesi ya matumizi ya nyumbani kutoka nje kwa kutumia mamilioni ya dola za kimarekani. Kuwanda cha kutengeneza LPG kinagharimu tshs 35bn tu, Wabunge peek Yao kwa mwaka wanatumia 28bn kwa posho za kukaa tu achilia mbali mishahara na marupurupu mengine.
Ipo siku Watanzania watatupiga mawe kwa usaliti huu dhidi yao.

Maneno mazito sana haya kutoka kwa bwana Zitto,
Pamoja na kwamba kuna baadhi ya wabunge wenzako wa chadema hawaonekani kukuelewa katika hili, na kwakuwa Makamba Jr. ameonekana kuungana nawe kivitendo, hapana shaka kwamba kuna kazi moja kubwa sana ya kufanya kwa sisi wananchi. Tukiamua kwa dhati kabisa kuweka pembeni ushabiki wetu wa kisiasa na kuweka mbele maslahi ya taifa kwa ujumla, tutajikuta tumewaunga mkono Zito na Makamba kwa vitendo, tuatapinga kwa kauli moja kitendo cha wabunge kuonyesha dharau ya wazi wazi kwa wananchi na watumishi wengine wa umma.

Kama ni maisha kupanda ni kwa wote, hawa wabunge walitakiwa wasimame kidete kutetea maslahi ya watumishi wengine yapande ili hata wao wakiongezewa basi wanakuwa wamepata wote. Hii inanikumbusha IGP mstaafu Omari Mahita, aliwahi kuwaambia wabunge kwamba posho ya mbunge kwa siku moja ni sawa na mshahara wa askari polisi kwa mwezi mzima wakamjia sana juu. Na huu ni ushahidi tosha jinsi hawa wabunge wasivyokuwa na upendo kwa watanzania wenzao, wala hawana chembe ya uzalendo kwa nchi yao.
 
sie wengine tunapigania income zetu zipande(salary) which means PAYE nayo inakuwa juu watu wengine wasio na huruma wanatafuta namna ya kuzitafuna hizi hela jamani kuweni na huruma hata kidogo sasa mtakata tumuamini nani hapa.. mbona mnaziweka dhamira zenu za ulafi waziwazi agrrrrrrrh ... KIMA CHA CHINI WAMESHINDWA KUKITETEA WAMEWACHIA TUCTA hivi hawa ndio wawakilishi wetu kweli ........WATATUKAMUA SANA MORE TO COME........

Mkuu kwenye red, pamoja na kwamba wafanyakazi, kama yalivyo makundi mengine ya kijamii, wanastahili maisha bora lakini la kusikitisha; na hili limeenea kila mahali - Bungeni, Serikalini, na kwenye taasisi nyingine rasmi; kila linapozungumzwa suala la kupandisha mishahara zaidi wanolengwa ni wafanyakazi walioko kwenye ajira rasmi hasa wa serikali. This is absolutely wrong. Je, na makundi mengine ya walalahoi wa taifa hili? Wakulima, wavuvi, wafugaji, warina asali, wanafunzi, na wajasiriamali wengine?

Mimi nadhani KATIBA MPYA, pamoja na mengine, isimamie moja kwa moja suala la mishahara na mapato mengine ya makundi yote katika jamii. Kwa mfano, endapo itatokea haja ya kupandisha mishahara na/au posho kwa kundi fulani katika jamii kwa mfano, sambamba na hilo, Serikali ieleze kinagaubaga namna ambavyo ime/itaboresha vipato vya makundi mengine vinginevyo hakuna haja ya kupandisha mishahara au posho. Hii ni muhimu kwa sababu ugumu wa maisha hauwaathiri wafanyakazi rasmi, wabunge, n.k tu, bali huathiri makundi yote.
 
Tatizo langu kubwa wala sio posho. Tatizo kubwa zaidi ni UKUBWA wa BUNGE lenyewe:
-VITI MAALUM ni vingi mno.
-Majimbo ya UCHAGUZI ni mengi sana. Dar peke yake ina MAJIMBO 7.
-Tumejenga majengo mawili makubwa ya Bunge pale Dodoma ndani ya miaka 10 tu.
-Kamati za kudumu za Bunge ni nyingi sana. Zinaendesha mambo yake kwa gharama sana.
-Kamati ya maslahi na utumishi ya Bunge ina nguvu nyingi sana. Hata nyongeza hii ya posho wamefanya wao.
 
zitto, i have always been impressed by you despite all that stick you have been up against.
nakiri mahala pengine umekuwa ukiteleza (which is normal kwani kuanguka si kuteleza, au nimekosea?), lakini you have thus far prevailed.

nilikupa moyo wakati fulani (humu humu JF) kuwa wakati ule ulikuwa unapitia kwenye tanuru kali sana lakini ungefanikiwa kutoka salama (which you did), ungekuwa kiongozi wa mfano wa kuigwa (which is what you now seem to be).
 
mwanakijjii makala yako inawauliza wanaccm na rais wao mie ningependa niwaulize makamanda je katika kikao cha ikulu waligusia kusikitishwa kwao na ongezeko hilo au waliuchuna? Mara nyingi nemekuwa nikisoma makala zako naona zinaegemea upande mmoja bila kuangania upande wapi nao wanamsukumo gani katika tatizo husika. Huwa nafurahi kusoma makala za maggid mjengwa jamaa huwa anasimamia ukweli yaani yupo balanced sana.

Kwa sasa Tanzania baada ya miaka 50 ya uhuru tumekuwa na uhaba wa waandishi wa namna ya Maggid Mjengwa wengi wa waandishi ni "maslahi" wanaotetea makundi yanayowashibisha au yenye manufaa nao. Waandishi lazima wajue umuhimu wao wa kupasha habari jamii/hadhira na adhari zake pamoja na faidi katika maendeleo ya jamii kwa ujumla.

Ninasema kweli kuwa sina ushabiki wa kisiasa. Sitaegemea upande wowote!! Mpaka sasa nimesikia Zitto na Makamba wakipinga hili. Lakini sidhani wewe umeonesha neutrality kwa kuhoji Magwanda wanasema nini. Kuna mambo kadhaa hukuyazingatia katika hitaji lako:

a) Si Magwanda wanaongoza nchi. Ongezeko halikufanywa na Magwanda wala serikali yao. Hivo kusema chochote hakutaondoa ongezeko hilo.
b) Tusiwe watu wa kusikia kimesemwa nini na nani halafu tukadhani ndio mwisho. Kama tusivowahoji Magwanda kwa kulea ufisadi katika wizara, kutokuza uchumi au kwa ugumu wa maisha kwa wengi, ndivo tusivoweza kuhoji kauli yao kuhusu ongezeko la posho.
c) Fedha ni jambo gumu kuliko wengi tunavodhani. Kama ambavyo hatuwezi kuona wewe mwenyewe ukifurahia kupunguzwa mshahara ndivo ilivo kwa wenzetu wabunge. Tuna udhaifu sawa katika pesa!! Ingekuwa ni pendekezo la kuongeza, huenda tungesikia Magwanda na hata wengine, wanatoa mawazo. Kwa kuwa ongezeko tayari limefanywa na wengine, si sawa kusikia lolote lisiloweza kubadilisha ongezeko hilo.
d) Nilishani ungehoji ofisi husika na ongezeko hilo. Kuihoji CDM ni kuikosea haki, sawa na ukisema uihoji NCCR, CUF na wengine. Utapata haki kidogo angalau ukitaka kusikia maoni ya CCM kwani wao ndio wanahusika na serikali iliyochukua uamuzi huu wa kisera.

Now that is neutrality!!
 
Back
Top Bottom