Mheshimiwa JK,
Wewe ni mtu mkubwa sana na kila unaloongea linapewa uzito unaostahili! Jana umedai kuwa "Mwanasheria maarufu, Tundu Lissu anachanganya Sheria na anawachanganya na wengina nao wanamwamini!"
Ombi: naomba Mhashimiwa JK utuambie ni Sheria ipi ambayo TL alichanganya na kuwachanganya wengine!
Nahofia kwamba inawezekana uliyejichanganya ni wewe kwa kutokujua Sheria!
Au unaposikia akina Jaji Werema anaporusha madongo huko Bungeni unaamini kuwa madongo hayo yana ukweli wowote! Hata hivyo ulituambia kuwa akili za kuambiwa changanya na za kwako! Kwa hiyo nilikuwa natarajia kuwa angalau za kuambiwa/kusikia ungechanganya na za kwako! Otherwise unajidhalilisha sana kuponda mtu ambaye ana-Practice fani ambayo hujui lolote au unajua kidogo kuhusu fani hiyo!