Oman wanazungumza Kiswahili pia?

Oman wanazungumza Kiswahili pia?

Idadi kubwa ya wenye asili ya Oman,waliishi Tanganyika(Tanzania bara).Kuanzia Mtwara,Tanga,Tabora,Shinyanga,Mwanza,Sumbawanga,nk.Na mpaka leo vizazi vya hao watu wapo,japo wengi wemchanganyika na makabila ya asili kwa kuoana.
Nakubaliana na wewe mkuu.
Kuna waarab wengi waishio mwanza wana ndugu wa damu huko Oman.

Nilisoma na mwarab mmoja ambaye hivi sasa ni mwanajeshi wa rank ya juu huko oman.
Mzee wao alikuwa mbaguzi sana, hakupenda watoto wake kuchangamana na ngozi nyeusi hasa ktk mahusiano ya mapenzi, ilikuwa kijana akifika umri wa barehe anamhamishia oman ili akaoe au kuolewa na waarab wa kwao.
 
Ndugu unapoteza nguvu zako bure kumuelimisha huyo mwanafunzi wa sekondari, sijui wanawezaje ku "log in" huku jamiifurums
Kiswahili si kiarabu ila kimekopa baadhi ya maneno kutoka katika kiarabu kama vile kilivyokopa pia maneno mengine ya lugha nyingine kama kiingereza, kireno, kijerumani nk.

Binafsi naona kiswahili kama kimeegamia katika lugha za kibantu zaidi mfano,

Kuuma-kuluma, kuona-kulola, maji-manji, jiwe-liwe, nyumba-numba, Mungu-Murungu, mwanamke-ng'wanike, mwanaume-mlume, mwanz-ng'wanzo, kula- kulya.

Maneno ya kibantu ni mengi sana kwenye kiswahili kuliko kiarabu.
 
Kuna mwilingiliano mkubwa sana kati yetu na ndugu zao wengi mnoo wapo Zanzibar hapo

Kwa kifupi sema Oman lilikuwa koloni la (The Zenj Empire) Zanzibar, Hii ni kwa sababu mtawala wa Oman alikuwa anaishi Zanzibar The Sultan administered Oman from Zanzibar which was his headquarters ila wenzetu hawakupenda kuweka historia sawa. I stand to be corrected.
 
Kilichowaleta zaidi waomani ni kukuza biashara baina ya Oman na East Africa. Kwa upande wa Oman nchi yao sehemu kubwa ni jangwa na mvua chache mno. Ili kujiimarisha (Food reserve) wanaweza kuwa wawekezaji wakubwa katika kilimo ndani ya East Africa. Oman ina mafuta (oil) na gesi na wana ujuzi katika haya kwa miaka mingi na wanaweza kushirikiana na TZ katika kuendeleza gesi.
 
Umeni-quote mimi ilhali ujumbe umemkusudia ELI-91 sio?

Ni hivi nyie mliojifunza kiswahili mkiwa Sekondari endeleeni kuamini kiswahili ni KIBANTU ila sisi tuliozaliwa ndani ya kiswahili na kupitia madrasa, tunajua athari ya lugha ya kiarabu ndani ya kiswahili. Hicho cha Congo ndugu sio kiswahili, ni lugha tu nyingine yenye maneno mengi au kadhaa ya kiswahili.

Nimekuquote kwa sababu uliniquote sehemu ulitaka kuona tofauti ya lugha hizo

Siku zote mi huwa najua vizuri sana, mtoto wa Kiislam hawezi kukubali kuwa Kiswahili sio Kiarabu, ndugu yangu kujua kiswahili sio kupitia Chuo, kwa taarifa yako wako wengi waliozaliwa sehemu ya Waswahili na wala sio Waislam na wanakijua Kiswahili vizuri tu

Ngoja nikufahamishe kitu
Lugha hii inayoitwa Kiswahili ilikuwepo kwa Karne na Karne ikiitwa KINGOZI , na Wafanyabiashara wa zamani waliokuwa wakitoka Congo kuleta mizigo Pwani walikuwa wakiongea hiyo lugha, na Mizigo iliyokuwa ikifika pwani ilisafirishwa kwenda Uarabuni na hao Wabantu,

Waarabu walipofika hapa Tanganyika waliwakuta watu wa eneo lote la Pwani ya Tanganyika, Kenya wakiongea hiyo lugha na ndio wakaiita lugha ya watu wa Pwani,
Na Waarabu walioanza kufuata njia ya Wafanya biashara ya kwenda Congo, waliwakuta watu njiani wakiongea hiyo Lugha Hiyohiyo (maeneo kama Bagamoyo, Morogoro, Dodoma, Singida, Tabora, Shinyanga, Kahama, Kigoma mpaka DRC) Usifikiri Waarabu ndio waliovumbua hiyo njia, hiyo njia ilikiwepo miaka na miaka na Waarabu waliifata tu wakiongozwa na Wafanya biashara wa Kibantu

Baada ya Wafanyabiashara wa Kiarabu kudominate hiyo njia taratibu wakaanza kuingiza maneno yao ya kiarabu na yakawa comon kwenye hicho KINGOZI, na kwa sababu walikaa muda mrefu athari yao kwenye hiyo lugha ni kubwa zaidi, mfano waarabu waliwakuta WANGOZI wanajua kuhesabu vizuri tu na wao Waarabu wakaongeza au kubadirisha matamshi ya namba tatu katika mtiririko wa kuhesabu mfano moja, mbili, tatu, nne, tano, "nane na kumi vyote ni Kibantu lakini Sita, Saba na Tisa ni Kiarabu, so sio kama hiyo Lugha walioikuta haina hizo namba, bali wao waarabu walizitumia sana hizo namba tatu kwa lugha yao na ndio zikatoholewa kuwa lugha rasmi, lakini mpaka leo ukisema Kenda watu wanajua ni Tisa

Pia kuna Maneno ya kutoka Persia yaliyoletwa na wachuhuzi wa kutoka huko, maneno kama chai, achari=pickle, Serikali, Diwani, Sheha nk,
kuna maneno pia ya KiPortuguese pia yapo ndani ya Kiswahili mfano leso" (handkerchief), "meza" (table), "gereza" (prison), "pesa" ('peso', money), nk.
Pia yapo maneno mengi tu ya Kiingereza, Kijerumani nk, japokuwa maneno hayo yameingizwa kwenye Kiswahili lakini sio kweli kwamba tulikuwa hatuna maneno ya Kiswahili yenye maana hizo, maneno machache sana ya Kisayansi na kitechnolojia ndio huwezi kuyakuta kwenye KINGOZI
 
Kiswahili sio kimoja kaka, Ni kama kiingereza tu, Uk wana Chao, USA wana chao, Jamaica wana Chao, Nigeria wana Chao,

Shelisheli wana Kiswahili chao, kuna sehemu ya Madagascar pia wana chao, Kenya Nairobi na Mombasa kuna tofauti, DRC wana chao, tembea uone kaka, acha kubisha uko nyuma ya QWERTY

Hizo ni lahaja. Zipo karibu 10 ama zaidi. Kimvita, kimtangata, kiamu, kingazija, Kimzizima, kitumbatu, kipemba, kiadimu, kiunguja, kimwani,
 
Ao mawaziri wote watatu ambao ndio viongozi wa msafara ni wazaliwa wa hapa uswahilini na jamaa zao wapo Wengi tu hapa hapa
 
Muungano ukivunjika Zenji itakuwa kama Dubai, tumeishikilia Zenji kuiendeleza hatutaki nin sasa hiki

Wakipewa nchi yao huku bara mtaenda kuomba msaada huko Zanzibar
 
Ama kweli we mavipunda unajua zanz lazma iwe dubai ikitoka kwenye muungano ndo mana wakulu wanakomaa usivunjwe bara tukaaibika
Hapo ndio unapima IQ ya ki Africa ipo vipi. maendeleo ni ku kumbatia mawazo ya kimaskini.
 
98% na ndiyo maana tunaambiwa÷
kiswahili ni lugha nasibu iliyoanzia pwani ya Afrika mashariki ambapo wenyeji wa UPWA huo uliitwa "aswahili" au "sawahili".
Thibitisha hilo kwa hoja kuntu mkuu
 
Kiingereza ni kimoja pia,hao wengine wameamua kuumiza matamshi ya baadhi ya maneno,ndiyo maana unaambiwa kuna FORMAL ambayo ni ya UINGEREZA hakuna kiingerza cha Naijeria wala kongo,isipokuea INTONATION tu na hiyo inatokana na lugha zao eanazotumia.
Usijifabganye kama kuna kiingereza cha KIHAYA wala KiSUKUMA,ni lafudhi na matamshi tu yaliyoathiriwa na lugha fulani ama za makabila au Mataifa,unawezaje kusema KIINGEREZA cha NAIJERIA wakati umeshasema"KIINGEREZA?"
HII MAANA YAKE NI LUGHA YA UK.
Usiwe mvivu wa kufikiri.
Utofauti wa kiingereza cha Marekani na uingereza.

waingereza- maize.
wamarekani- corn.

Waingereza - dustbin
Wamarekani-gabage can.

Waingereza-biscuit
Wamarekani-cookies.

Waingereza- mobile/cell phone
Wamarekani-payphone.

Waingereza-Father
Wamarekani-Daddy

Waingereza-you and me
Wamarekani-you and I

Waingereza- colour
Wamarekani-color

Mifano mingi sana
 
Jamani Mmetufumbua machon sisi tusojua ....
kumbe ndio maana waTz wengi wenye asili ya Pwani wanapataja sana Oman......
mnatutamanisha tusio hata na passport
 
Sio 98%, na ujue Kiswahili kinatofauti na eneo na eneo, ukikisikia kiswahili cha DRC hakina kabisa maneno ya Kiarabu na kama yapo ni kachachesana, kiswahili chao kimejaa Kibantu na maneno ya kifaransa
Mfano umekwisha kutumika
 
We ushamba umeacha lini?, hivi hata hujui Kiswahili kilivyogawanyika?, Kiswahili kina matabaka kaka, ngoja basi nikufahamishe na uelewe tofauti ya kiswahili cha Tanzania na Kikongo
Cha Tanzania kina mchanganyiko wa Kiarabu, Kibantu, Kiingereza nk, Lakini kiuhalisia maneno Mengi ya Kiarabu yana Kibantu chake, kwa sisi huku Tanzania maneno ya kiarabu bado mengi yanasimama kwenye lugha yetu, lakini kwa Congo maneno almost yote ya Kiarabu hayatumiki na mbadala wake wanatumia maneno ya Kibantu na Kifaransa,
Sasa basi kwa Mkongo akiongea Kiswahili cha kwao kwa sisi Watanzania tunaelewa anachokiongea, lakini sisi tukiongea Kiswahili chetu chenye Kiarabu wanapata shida san kujua tunachoongea
Na hata Congo yenyewe Kiswahili pia kina tofauti, East Congo angalau tunaweza kuongea vizuri, lakini Katanga ni shida kabisa, na Kinshansa almost hakuna Kiswahili

Acha ushamba wewe
Hiyo migawanyiko inaitwa lahaja(dialect) lugha ni moja inaitwa kiswahili ila lahaja ndo zipo nyingi
 
Nadhani asilimia 50 ya maneno ya kiswahili ni kiarabu. Iliyobaki ni mchanganyiko wa lugha za kibantu.
 
Nadhani asilimia 50 ya maneno ya kiswahili ni kiarabu. Iliyobaki ni mchanganyiko wa lugha za kibantu.

Ni kweli kwa Kiswahili kinachotumika Pwani ya East Africa (Tanganyika, Zanzibar, Mombasa nk) lakini si kweli kwa Kiswahili cha DRC, cha DRC labda kila only 10%ya Kiarabu, lakini Asilimia kubwa ni Kibantu kisha Kifaransa
 
Hiyo migawanyiko inaitwa lahaja(dialect) lugha ni moja inaitwa kiswahili ila lahaja ndo zipo nyingi

Kaka mimi wala sipingi hilo, na hilo linajulikana na liko wazi na ndio maana chote kitaitwa kiswahili, tofauti ninayoisema mimi ni kuwa, Kiswahili chetu ndio kina Kiarabu, Kibantu, Kiingereza nk, lakini sehemu zingine Kiswahili hakina kabisa maneno ya Kiingereza unakuta Kifaransa, pia kina asilimia chache sana ya maneno ya Kiarabu na sehemu kubwa ni Kibantu
 
Back
Top Bottom