Oman wanazungumza Kiswahili pia?

Oman wanazungumza Kiswahili pia?

Siyo kiswahili tu , hata Kinyamwezi pia wanazungumza ...!
 
ukipelekwa mahakamani au polisi nchini oman unaulizwa unataka kujibu kwa kiswahili au kiarabu
 
Sio 98%, na ujue Kiswahili kinatofauti na eneo na eneo, ukikisikia kiswahili cha DRC hakina kabisa maneno ya Kiarabu na kama yapo ni kachachesana, kiswahili chao kimejaa Kibantu na maneno ya kifaransa
Ndugu unapoteza nguvu zako bure kumuelimisha huyo mwanafunzi wa sekondari, sijui wanawezaje ku "log in" huku jamiifurums
 
Now I understand why Zanzibaris want to quit...
 
Zaidi ni Tanzania bara,ndio ina idadi kubwa sana ya watu wenye asili ya Oman.Kuanzia Bagamoyo,Tanga,Dar,Mtwara,Tabora,Shinyanga,Mwanza,Sumbawanga nk.

Ni kweli unajua kuna dhana kwamba wa Oman wengi ni kutoka Zanzibar lkn kiuhalisia Zanzibar ni sababu ya mambo ya utawala wa sultan kipindi hicho nachoweza sema wa bara na hasa mikoa ya Tabora , Tanga na shinyanga ndo ina idadi kubwa sana yenye waaarab na machotara wa kiarabu

Na hata Oman yenyewe pia wako waarabu waliokuja Africa kwa maana ya Zanzibar, Mombasa na walio enda Bahrain (hawa walienda fanya kazi kutokana na maisha magumu ya Oman muda huo) pia Iran na India walienda kibiashara na kutawala baadhi ya sehemu

Kwa waliokuja Africa pia walitoka sehem karibu zote za Oman lkn wengi ni kutoka hasa maeneo ya , Centre Oman ' hapa unakutana na makabila kama Aljabri na Alhabisy (hawa wamekaa sana maeneo ya Tanga,Nzega,nata,mwangohe, Tinde , maganzo, choma cha nkola, itobo kwa ufupi Tabora vijijini na shinyanga na wengine Karagwe wa kaenda Rwanda mpaka Burundi

Kwa wapenda soka mtamkumbuka kipa kama sikosei wa Wigan aliitwa Alhabisy ( hili ni jina la kabila bado warabu wanajinasibisha sana kwa makabila yao ) wazazi wake ni kutoka maeneo ya Tabora vijijini wakahamia Oman

Turudi ktk mada hakuna Taifa nje ya Africa wanaongea kiswahili zaidi ya nchi ya Oman ni Taifa pekee ndo Mtanzania au mtu yoyote anaeongea kiswahili hawezi pata shida ya mawasiliano
 
Ili kumaliza utata kwetu tunaofuatilia uzi huu, hebu tuwekee paragraph moja ya kiingereza cha UK na nyingine ya kinaijeria na zote zikiwa na ujumbe mmoja.

Kaka ELI-91 , unajua ni ngumu sana kuelewa ninachokiandika na ninachojaribu kukieleza
Mfano, kwa sisi East Africa tunasema MIMI ambayo ina accent ya Kiarabu lakini Kiswahili cha Congo wanasema MIYE ikiwa ni accent ya Kifaransa
Pesa tunasema Fedha-kiarabu wao Congo wanasema Faranga

Ukiongea siku za juma kama tunavyoongea sisi huku hakuna Mkongo atakayekuelewa, utawachanganya kabisa wao wanatumia namba au maneno ya kifaransa
Jumatatu-Siku ya Kwanza (Lundi)
Jumanne-Siku ya Pili (Mardi)
Jumatano- Siku ya Tatu (Mercredi)
Alhamis-siku ya nne (Jeudi)
ijumaa-siku ya Tano (Verdred)
Jumamosi- siku ya Posho (Samedi)
Jumapili-Siku ya Mungu (Demanche)
 
Nimeona baadhi ya watu waliokuja na Meli ya mfalme wa Oman wakizungumza Kiswahili vizuri. Nilitaka kujua kama kwenye taifa hilo uzungumza Kiswahili
Chukua na hii Mfalme wa Oman, Shekh Kabus ni mzenji.
 
Ni kweli unajua kuna dhana kwamba wa Oman wengi ni kutoka Zanzibar lkn kiuhalisia Zanzibar ni sababu ya mambo ya utawala wa sultan kipindi hicho nachoweza sema wa bara na hasa mikoa ya Tabora , Tanga na shinyanga ndo ina idadi kubwa sana yenye waaarab na machotara wa kiarabu

Na hata Oman yenyewe pia wako waarabu waliokuja Africa kwa maana ya Zanzibar, Mombasa na walio enda Bahrain (hawa walienda fanya kazi kutokana na maisha magumu ya Oman muda huo) pia Iran na India walienda kibiashara na kutawala baadhi ya sehemu

Kwa waliokuja Africa pia walitoka sehem karibu zote za Oman lkn wengi ni kutoka hasa maeneo ya , Centre Oman ' hapa unakutana na makabila kama Aljabri na Alhabisy (hawa wamekaa sana maeneo ya Tanga,Nzega,nata,mwangohe, Tinde , maganzo, choma cha nkola, itobo kwa ufupi Tabora vijijini na shinyanga na wengine Karagwe wa kaenda Rwanda mpaka Burundi

Kwa wapenda soka mtamkumbuka kipa kama sikosei wa Wigan aliitwa Alhabisy ( hili ni jina la kabila bado warabu wanajinasibisha sana kwa makabila yao ) wazazi wake ni kutoka maeneo ya Tabora vijijini wakahamia Oman

Turudi ktk mada hakuna Taifa nje ya Africa wanaongea kiswahili zaidi ya nchi ya Oman ni Taifa pekee ndo Mtanzania au mtu yoyote anaeongea kiswahili hawezi pata shida ya mawasiliano
Ni sawa kabisa mkuu maanake ukiteremka pale airport Muscat,unakutana maafisa forodha,uhamiaji polisi wengi wao wanaongea kiswahili utadhani huko Kariakoo.
Kuna kipindi nilisafiri na mwanajeshi wa jeshi la Oman akiwa anakuja likizo Zanzibar.
 
Ndugu unapoteza nguvu zako bure kumuelimisha huyo mwanafunzi wa sekondari, sijui wanawezaje ku "log in" huku jamiifurums
kiswahili ni kimoja tu..hakuna cha Kongo wala Bujumbura,Kongo wao wanaita kingwana,wataokota-bhatalokota,risasi-masasi,kiswahili cha wapi hicho
 
Nilifika Muscat, sikuwahi kuongea English kwa wiki moja niliyokaa, mwendo ni Swahili tu, nilienjoy Sana, jamaa wanaongea Swahili safi kabisa, lakini lafudhi ya Zanzibar
 
ukifika Tabora pale unawakuta watoto wa kiarabu jaribu kumuuliza jina utaskia naitwa Kashinje Maganga na kinyamwezi anapiga vizuri kabisa
 
Kiingereza ni kimoja pia,hao wengine wameamua kuumiza matamshi ya baadhi ya maneno,ndiyo maana unaambiwa kuna FORMAL ambayo ni ya UINGEREZA hakuna kiingerza cha Naijeria wala kongo,isipokuea INTONATION tu na hiyo inatokana na lugha zao eanazotumia.
Usijifabganye kama kuna kiingereza cha KIHAYA wala KiSUKUMA,ni lafudhi na matamshi tu yaliyoathiriwa na lugha fulani ama za makabila au Mataifa,unawezaje kusema KIINGEREZA cha NAIJERIA wakati umeshasema"KIINGEREZA?"
HII MAANA YAKE NI LUGHA YA UK.
Usiwe mvivu wa kufikiri.
Kama unajua kuanzia advance hukusoma,HGL,HGk napia chuo hukusoma masuala ya lugha basi usitoe maelezo ambayo siyakwe,tuliosoma lugha as professional tunaona unapotosha
 
Kiingereza ni kimoja pia,hao wengine wameamua kuumiza matamshi ya baadhi ya maneno,ndiyo maana unaambiwa kuna FORMAL ambayo ni ya UINGEREZA hakuna kiingerza cha Naijeria wala kongo,isipokuea INTONATION tu na hiyo inatokana na lugha zao eanazotumia.
Usijifabganye kama kuna kiingereza cha KIHAYA wala KiSUKUMA,ni lafudhi na matamshi tu yaliyoathiriwa na lugha fulani ama za makabila au Mataifa,unawezaje kusema KIINGEREZA cha NAIJERIA wakati umeshasema"KIINGEREZA?"
HII MAANA YAKE NI LUGHA YA UK.
Usiwe mvivu wa kufikiri.
Mkuu vipi wale wanazuoni wanaofundisha kwamba kuna American English na British English kwa maelezo yako ina maana hakuna kitu kama hicho? Niongezee uelewa hapo
 
Nimeona baadhi ya watu waliokuja na Meli ya mfalme wa Oman wakizungumza Kiswahili vizuri. Nilitaka kujua kama kwenye taifa hilo uzungumza Kiswahili
Waoman wengi wametokea hapo VISIWANI...kiswahili sio ISSUE kwao
 
Sio 98%, na ujue Kiswahili kinatofauti na eneo na eneo, ukikisikia kiswahili cha DRC hakina kabisa maneno ya Kiarabu na kama yapo ni kachachesana, kiswahili chao kimejaa Kibantu na maneno ya kifaransa
Kiswahili kipo pwani ya Afrika mashariki, kilichopo Kongo ni maigizo yake. Pia kiswahili kimekopy baadhi ya maneno ya kijapani, kihindi, kiarabu na kibantu. Hata hivyo Zanzibar ilikuwa sehemu ya ya nchi Oman kabla Tanganyika haijavinyakuwa visiwa vyake. Hivyo ndani ya Oman kiswahili fasaha kinazungumzwa huko
 
Kaka ELI-91 , unajua ni ngumu sana kuelewa ninachokiandika na ninachojaribu kukieleza
Mfano, kwa sisi East Africa tunasema MIMI ambayo ina accent ya Kiarabu lakini Kiswahili cha Congo wanasema MIYE ikiwa ni accent ya Kifaransa
Pesa tunasema Fedha-kiarabu wao Congo wanasema Faranga

Ukiongea siku za juma kama tunavyoongea sisi huku hakuna Mkongo atakayekuelewa, utawachanganya kabisa wao wanatumia namba au maneno ya kifaransa
Jumatatu-Siku ya Kwanza (Lundi)
Jumanne-Siku ya Pili (Mardi)
Jumatano- Siku ya Tatu (Mercredi)
Alhamis-siku ya nne (Jeudi)
ijumaa-siku ya Tano (Verdred)
Jumamosi- siku ya Posho (Samedi)
Jumapili-Siku ya Mungu (Demanche)
Umeni-quote mimi ilhali ujumbe umemkusudia ELI-91 sio?

Ni hivi nyie mliojifunza kiswahili mkiwa Sekondari endeleeni kuamini kiswahili ni KIBANTU ila sisi tuliozaliwa ndani ya kiswahili na kupitia madrasa, tunajua athari ya lugha ya kiarabu ndani ya kiswahili. Hicho cha Congo ndugu sio kiswahili, ni lugha tu nyingine yenye maneno mengi au kadhaa ya kiswahili.
 
wazanzibar ni wale wale wa Oman kwani jeuri ya kuvunja MUUNGANO unadhani wanaitoa wapi.. na wakijitoa leo kwenye Muungano wanatuacha kiuchumi haki ya Mungu
Ama kweli we mavipunda unajua zanz lazma iwe dubai ikitoka kwenye muungano ndo mana wakulu wanakomaa usivunjwe bara tukaaibika
 
Back
Top Bottom