Oh, weekend imeshawaendea vibaya!

Oh, weekend imeshawaendea vibaya!

Hata hawakutarajia ingekuwa hivi!

Wengine hata najua wazi hawana taarifa na kinachoendelea juu yao. Lakini kaamua, liwalo na liwe.

Mmefanya vema mliofanikisha juhudi za kumpa majina ya ziada; atakuwa aliudhika kukuta aliowaamini nao ni nyoka.

Kafanya jambo jema; lakini kama atafanya hivi bado wale jamaa watalegeza kamba? Kuongezeka kwa watuhumiwa kutaleta neema kwetu kama nyumba?

Naam, weekend imewaendea vibaya; ambao hawakutarajiwa ndo watalia na kusaga meno. Mwaka unaisha vibaya kwao!

Lakini, kilio chao ni kicheko cha wengine! Wenye macho wameona... Wengine vaeni miwani mtaweza soma!
swali la kizushi Invisible kwa nini mara nyingi sana mada nyeti kama hizi huwa una penda kupost usiku?
 
Last edited by a moderator:
...hizi wishful thinking za Watanzania nategemea JK na genge lake la wezi wangekua wanapita humu JF kusoma wishes za watanzania dhidi ya wezi wanaomzunguka JK...Wakati huu pia tusisahau kundelea kuhoji na kutafta ukweli juu ya wamiliki wa Simba Trust yenye 50% shares kule PAP....pia waliopokea zile fedha za stanbic kupitia accounts zisizo na majina..Nakumbusha juu ya hili maama ni kawaida ya watanzania kusahau yote mara baada ya JK kuwapumbaza na hatua zake za Zima moto kila mara ....wakati wa mabadiliko TZ ni huu....
 
sisi kina gogo la shamba mwisho wa siku tulizompa Kikwete ni leo,asipotoa maamuzi leo ajue kilichompata Zitto ndicho kitakachompata atachukiwa katika maisha yake yote yeye na familia yake na asahau kutokea ndani ya familia yake kuwe na mwana siasa wa kueshimika na mwisho wao lazima kuwe na majuto
 
leo ni siku ya mwisho tuliompa Kikwete asipotoa uamuzi,ajue yeye na familia yake mwisho wake ni majuto, asije kulaumu kwamba sisi kina gogo la shamba hatukumshauri
 
Kha kweli Obama raisi wa dunia,bila ya Obama Escrow ingejiescrow yenyewe,tukisema wananchi hatusikilizwi pamoja na kuwa sisi ndio tuliowachagua watutumikie lakini akisema bwana mkubwa anayetusaidia kujaza vibaba vyetu mara moja tunaufyata,Watanzania hadi lini tutabaki kusubiri Obama awashikie bango wahuni ndio waondolewe?
 
Invisible fumbo umewafumbia wajinga( chi chi em) werevu tumekusoma,acha watapetape na pesa zetu warudishe haraka sio mpaka wahisani waseme!!!!!
 
siyo kumu-underestmate jk ni dhaifu tena mwandamizi kabsaaa, hatua atakazo chukua ni kwa hisani ya watu wa marekani.

I have a very strong feeling kuna warning ya ban, hakuna kubarizi states. Akaona nani anataka kukosa mitoko. Kwa ubinafsi hawa viongozi wetu walio nao wako tayari kabisa kukosa hizo fedha za donors, hawajali shida za wabongo hata.
 
Hatuwezi kushangilia kuanguka kwa watu fulani fulani, ikiwa mhimili wa uovu bado umesimama! Ni afadhali kisifanyike kitu ili hatimaye watu wagutuke!
 
nchi yetu ni kama nyumba chafu na ccm ni kama tambara la deki ambalo nalo ni chafu tena kuzidi nyumba yenyewe. Ni upunguani uliokidhiri kuendelea kudhani kuwa tutaisafisha nyumba kwa kutumia tambara hili lilioza. Kadri tutakavyoendelea kulitumia ndivyo tutakavyozidi kuichafua hii nyumba.
 
Ya CAG ipo JF kitambo; sema watu waliisoma bila miwani. Iangalie upya thread yangu utaona kuwa ipo kitambo hapa!

Ndugu Usiyeonekana, siuoni ukurasa wa 14 wa ripoti ya CAG katika ambato ulilotuwekea humu JF, nauomba haraka sana (dharura) - kama huwezi kuuweka humu nitumie kwa barua pepe sasa hivi tafadhali!
 
nchi yetu ni kama nyumba chafu na ccm ni kama tambara la deki ambalo nalo ni chafu tena kuzidi nyumba yenyewe. Ni upunguani uliokidhiri kuendelea kudhani kuwa tutaisafisha nyumba kwa kutumia tambara hili lilioza. Kadri tutakavyoendelea kulitumia ndivyo tutakavyozidi kuichafua hii nyumba.

Heri tambara chafu maana unaweza kulifua na kuendelea kulitumia kuliko jipya lenye kunguni
 
inchi ya matukio hii...kukikaa bila tukio hapanogi

leta vitu Invisible
 
Last edited by a moderator:
Watu washerehekea nini ? Hata akichukua hatua (too late), nchi imeshakufa. Hatua ilikuwa pale alipoingia madarakani. Tena hatua gani basi? Ataweza kuwafunga, kuwayang'anya mali zao zote? Mwizi hawezi kumfanyia mwizi mwenziwe hivyo isipokuwa katika hali moja tu: wanapogombania mgao.
Kumfukuza kazi mtu kama Chenge, au yeyote katika kundi, ni kumtaka tu aende kustaafu ale pesa zake vizuri!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom