Ogopa sana watu wa karibu yako, ni hatari

Ambakucha

JF-Expert Member
Aug 16, 2019
277
445
Habari wadau? Sikumbuki kama mada ya aina hii imewahi kutoka. Ila Kama Bado, nataka kuchangia na wadau kwamba, historia ya dunia tangu kuumbwa kwa ulimwengu, mtu wa karibu amekuwa akitajwa sana katika kuua, kukwamisha mambo, kusaliti, kulipa kisasi n.k.

Mifano; Adamu alisalitiwa na mkewe, Hawa. Samsoni aliingizwa chaka na demu wake, Delila. Yuda 'alimuuza' Yesu. Kaini alimuua Abeli. Lusifa alitaka kumpindua Mungu wake. Yakobo alimzunguka kaka yake, Esau kuhusu mbaraka wa baba yao, Isaka.

Marehemu Indira Gandi (alikuwa waziri mkuu wa India), aliuawa na walinzi wake. Laurent Kabila (alikuwa Rais wa DR Congo), aliuawa na walinzi wake. Wajane wengi wanadhulumiwa mali na mashemeji zao. Wanaofukuzwa makazini wanachongewa na watu wa karibu yao.

Kikubwa, historia inaonesha kwamba mtu wa karibu yako ni wa kuchukua tahadhari sana. Hata mke au mume husalitiwa na wa ubavuni mwake. Weka mifano mingine ya wazi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sasa kama kanuni ni kwamba kila mtu wa karibu ni adui utaishi na nani? Utaishi maisha gani? Kama unaona vipi basi jiongeze upate hekima na busara ya kuishi nao!

Hakuna mtu anaweza kuishi peke yake lazima atakuwa na mwenza, watoto, wazazi, majirani, wateja katika shughuri unazozifanya. sasa ukiwaona wote maadui basi wewe ndo tatizo
 
Ulichosema ni kweli na hata maandiko Matakatifu yanashuhudia hayo kwamba adui wa mtu ni wa nyumbani mwake mwenyewe yaani mtu wa karibu yako.

Hata kama atakuwepo mtu mbaya wa mbali lakini lazima apate wa karibu yako aweze kushirikiana nae kukudhuru au kukuharibia mambo yako .

Sasa nini kifanyike?

Ni kujifunza na kushika maagizo ya Mwenyezi Mungu kupitia maandiko Matakatifu.

Ukiishi kwa kumtegemea Mungu na kuwatendea mema watu wote kila mahali kwa kadri uwezavyo nakwambia ajapoinuka mtu kutaka uadui na wewe na kutaka kukudhuru Mungu atanuumbua mapema kabla hajakudhuru au kukuharibia

Mengineyo labda iwe ni mitihani tu ya Mwenyezi Mungu ambayo saingine anaruhusu yatupate mabaya ili kutupima imani .

Na mitihani itokayo kwa Mungu huwa na mwisho mzuri sana!


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Habari wadau? Sikumbuki kama mada ya aina hii imewahi kutoka. Ila Kama Bado, nataka kuchangia na wadau kwamba, historia ya dunia tangu kuumbwa kwa ulimwengu, mtu wa karibu amekuwa akitajwa sana katika kuua, kukwamisha mambo, kusaliti, kulipa kisasi n.k.
Mifano; Adamu alisalitiwa na mkewe, Hawa. Samsoni aliingizwa chaka na demu wake, Delila. Yuda 'alimuuza' Yesu. Kaini alimuua Abeli. Lusifa alitaka kumpindua Mungu wake. Yakobo alimzunguka kaka yake, Esau kuhusu mbaraka wa baba yao, Isaka.
Marehemu Indira Gandi (alikuwa waziri mkuu wa India), aliuawa na walinzi wake. Laurent Kabila (alikuwa Rais wa DR Congo), aliuawa na walinzi wake. Wajane wengi wanadhulumiwa mali na mashemeji zao. Wanaofukuzwa makazini wanachongewa na watu wa karibu yao.
Kikubwa, historia inaonesha kwamba mtu wa karibu yako ni wa kuchukua tahadhari sana. Hata mke au mume husalitiwa na wa ubavuni mwake. Weka mifano mingine ya wazi.

Sent using Jamii Forums mobile app
Aisee kweli kabisa ! Mke wangu kanisaliti penzi kwa mtu (watu) nimemgundua, sasa anataka talaka na machumo ! Du ! Kweli kikulacho...
 
Neno la Mungu linasema usiogope kila iitwapo leo!

Kichwa chako cha Habari ungeandika “kuwa na tahadhari kubwa kwa watu wa karibu yako waweza kuwa hatari”

Maisha ya kuwa na hofu siyo !




Sent using Jamii Forums mobile app
 
Imeandikwa : “mpende adui yako”

Tukitii hilo Neno tukajitahidi kuwapenda maadui zetu kwa mioyo yetu yote kwa uaminifu kabisa nakwambia tutakuwa salama kabisa siku zote.

Adui ukimpenda kwa dhati na kumtendea mema utakuwa umejitengenezea ngao kubwa sana!

Hataweza kusimama mbele zako

Mungu alivyoagiza hivyo ana maana yake nzuri tu kwakuwa yeye ndiyo aliyetufinyanga!

Tatizo letu sisi badala ya kuwapenda maadui na kuwatendea mema kama alivyoagiza Mungu sisi tunawahi kuwachukia.

Tunafanya kinyume na kule alichotuagiza Mungu!

Kumbuka hadithi ya mfano wa Daudi na Mfalme Sauli.

Utaelewa


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sasa kama kanuni ni kwamba kila mtu wa karibu ni adui utaishi na nani? Utaishi maisha gani? Kama unaona vipi basi jiongeze upate hekima na busara ya kuishi nao! Hakuna mtu anaweza kuishi peke yake lazima atakuwa na mwenza, watoto, wazazi, majirani, wateja katika shughuri unazozifanya. sasa ukiwaona wote maadui basi wewe ndo tatizo
Nimemalizia kwa kusema mtu wa karibu yako ni kuchukua tahadhari sana, sijasema usiishi nao. Usikurupuke kisa una bando

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kweli mkuu! na mashangazi ni wachawi sana kwa watoto wa kaka zao hasa akiwa na pesa. wanaona wifi yao anawalingishia

Lumumba aliuawa na plan ya Mobutu,akisaidiwa na CIA

Obote kapigwa Beat na dogo aliye mpatia kazi, akamuonya ukija nakuua.

Kambona alimgeuka Nyerere, akamjua,akampa kibano..

Kenyatta alimuua Thom mboya, mchana kweupee!

Moi akamuua Robert Ouko

Buhari alimkosa kosa Shehu Shaghali.

Murtala mohamad alimuua Buka Suka Dimuka,

Fishes alikoswa kuuawa na Rushdie kwa kuvamia Usiku.

Mugabe kapinduliwa na mnangawa.

Babangida alimgeuka Buhari

Jiwe kawageuzia kibao madogo waliomuweka madarakani kwa kuchezea computer.kiwizi mpaka wakapinda mikono ni vilema leo!

Jiwe huyohuyo kanigeuka leo kwa kumpa kura yangu tena waziwazi; tuishije sasa tuwasuse au..

kimke changu kilinigeuka kwa boss kabila lake nifukuzwe kazi halafu kinaomba hela ya kumpeleka mtoto shule!.
.
 
Neno tukajitahidi kuwapenda maadui zetu kwa mioyo yetu yote kwa uaminifu kabisa nakwambia tutakuwa salama kabisa siku zote.
Hapa mimi ndiyo napapendaga hapa, kauli ya Mungu hakumaanisha ivo, Samson mnadhiri wa Mungu alimpenda adui Delila! mnajua yaliyompata!

Hawa alimpenda Shetani, kisasi chake tuna hangaika mpaka leo!

Ma- Rais wa Africa wanampenda Mzungu tuko wapi leo?

Wayahudi hao mnaoamini ni taifa teule mbona hawapendi waarabu? wana MOSSAD ya kulipa kisasi

Nyerere alikuwa anasali sana, mpaka kukaribia kuitwa mtakatifu mbona hakumpenda Idd Amini dada?



Mimi kajamba nani ndo mnataka nimpende adui ili mnitawale kiu bwete? ndiyo maana ya Dini na Siasa vinaendana! unatulisha matango pori mchana kweupe

Gwajima Mlokole wa juu mbona hajamsamehe Bashite mpaka akafikia hatua ya kumlaani hadharani kuwa atashuka kisiasa, mungu gani huyo anawatakiwa watu mabaya, Mungu alisema ananyeshea mvua wabaya na wazuri, akasisitiza kuwa utavuna ulicho panda yaani Gwajima akipanda laana atavuna laana.

Adui lazima awajibike kwa matendo yake, siyo km wewe unavyo tupiga changa la macho! nimpende adui animalize?/?! kama Mkoloni alivotumaliza kwa vifungu km hivi. vya kizamani, wewe bado unavitumia. sali sana upate ufunuo!
 
Back
Top Bottom