Ogopa hizi shuhuda

Kuhusu Rupia, umegeneralise sana, Nikupe tu hili, Babu yangu Mimi, mzaa mama, alikuwa mganga wa tiba za Asili, Alikuwaga na kopo zima Zimejaa Rupia, alipofariki mwaka 1990, vifaa vyote vya uganga alikabidhiwa Babu mdogo, alivyofariki 1997, akawa Hakuna wa kurithi vile vitu, kila mtoto hakuwa tayari kurithi, labda pia kwakuwa dini ya ukristo ilikuwa imetawala,

Utaratibu ukafanyika kwenda kurudishwa vilikotolewa pamoja na kopo la Rupia Zimejaa, ili yasiwepo madhara, kwa Yale maagano ya wazee/ mababu, kwa sisi tulioko.

Yule aliyezirudisha msituni nae alifariki kwasababu ya umri maana ndiye aliyekuwa amesalia. Na taratibu za kurudishwa alikuwa anazijua yeye. Sasa hizi Rupia Kama zinachukuliwa zinaweza kuwa na kazi, au Ni Makapi tu.

Nilipopata akili iliniuma Sana kuwa kumbe tulikuwa na utajiri mkubwa hivi alafu tumeutupa porini.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu, hizi siyo njia ya mkato, Ni sawa na wale wanaoiba huko serikalini si wanapata hela. Huku mtaani na kwenyewe Kuna miundo tofauti ya utafutaji, wapambanaji wanatumia miguu yote miwili, hujui mpira utatokea upande upi ili ufunge goli.

Watu wanatafuta namna ya kutoka kimaisha, na hizi shughuli zinahitaji resources, money. Maskini hawezi kutafuta hivi vitu Ni gharama.

Kama wewe una njia Moja ya utafutaji sawa hakuna wa kukulaumu umechagua mfumo huo, wengine wanaenda na all approach.





Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hayo marupia hata sisi tulikuwa nayo na bado mpaka leo kuna wazee vijijini ndani huko wanayo.. Na mengine sio rupiah (rupee) bali ni coins za zamani tuu... Rupiah halisi zimeandikwa neno rupee na mwaka na picha.. Si rupiah zote zenye nguvu bali ni za miaka fulani
Hizo zenu za urithi zilifanyiwa featuring ya ushirikina
Thamani halisi ya rupiah ni kwa ajili ya kuuzwa ulaya na kuwekwa kwenye majumba ya makumbusho kisha zinaandikiwa historia na watu wakiingia humo wanalipa kiingilio
Matumizi mengine ni souvenir na watu wenye pesa na wale wanaopenda kufanya collection ya vitu vya kale ndio hununua..
Rupiah zenye nguvu ya miujiza ni kama hazipo tena huko zilikokuwa zimefichwa.. Watu walishatembea nazo kitambo tuu..
Vijijini kuna story za kudanganyana sana.. Ukimpa mtu wa Kijijini laki moja kwa kitu cha kawaida kabisa hizo habari zitavumishwa mpaka basi
Jr
 
Acknowledgement
 
Aisee
Niendelee kutafuta Ngekewa itanipa tu hela.
Utajiri wa free masson- utapeli
Rupia - utapeli
Mercury- utapeli
Forex - utapeli
Hazina za mjerumani - utapeli

Nyoka mwenye vichwa 12 - utapeli

Niendelee kulima, kuvua, biashara, kuchoma dhahabu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Only hard work pays... Successful life has no short cut... Wako wapi mapapaa waliotamba mjini?
Jr
 
Mkuu usimlaumu huyo kilimo Ni karata as long naye aliingia kwenye kilimo.Ingeweza kukulipa au isikulipe.Kilimo kina pande mbili Tena unapoingia ukae ukijua Hilo.

Kuna mwaka nyanya zililipa balaaa mwaka unaofuata kila mtu akaingia shambani,kilichotokea Mungu anajua.Ndo ilikuwa inauzwa jero

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Password walipata wapi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wanakurudisha kwenye zero

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…