Mkuu Shomari
Kwanza kabisa, inaitwa Kurugenzi anayoongoza Kamanda Singo Masalamakali Kigaila Benson, inaitwa Kurugenzi ya Oganaizesheni na Mafunzo.
Juu ya hoja yako;
1. Suala la mafunzo kwa CHADEMA si suala la kufuata tukio au matukio, limefafanuliwa wazi na vyema kabisa kwenye kanuni
za chama.
2. Kurugenzi inafuata programu maalum ya mafunzo iliyopitishwa na Kamati Kuu ya CHADEMA.
3. Tunaweza kukupatia mifano michache hapa, hasa ya hivi karibuni kabisa ili ujue namna ambavyo majukumu ya Kurugenzi
ya Kigaila inafanya kazi, ikizingatiwa umuhimu wake katika suala zima la kufua rasilimali watu.
-Hivi karibuni, Kurugenzi imemaliza mafunzo ya madiwani wote nchi nzima, takriban watu 450, pamoja na viongozi wa chama,
jumla wote karibu watu 1000.
-Hata ukiamua kufanya utafiti kidogo tu hapo ulipo kwa kutumia tu vidole vyako na ku-google, unaweza kuona namna ambavyo kupitia Kurugenzi hiyo ya Benson, Chama kilitoa mafunzo ya nadharia na vitendo kwa wenyeviti na makatibu wa mikoa yote ya kichama nchi nzima.
Mafunzo hayo yalifanyika Kayanga, Karagwe. Ni mafunzo ambayo kwa kweli yataifanya M4C kuendeshwa kwa ufanisi ziadi kuanzia ngazi za chini kabisa mpaka mkoa, badala ya kutegemea ngazi ya taifa pekee.
Kurugenzi hiyo pia imekuwa ikitoa mafunzo kila viongozi wapya wanapochaguliwa. Mfano mzuri ni mafunzo ya viongozi wa ngazi ya kata na majimbo kwa mikoa ya Mtwar na Lindi.
Kwa hakika hii ni mifano michache tu inayoonesha namna ambavyo Kurugenzi ya Oganaizesheni na Mafunzo, inavyotekeleza majukumu yake.
Makene
0688 595831/ 0752 691569