Wanjamvi,
Hii mada ina maana sana. Kwa bahati mbaya sana wachangiaji wameongozwa na jazba na kuigeuza kama sehemu ya kashfa, kejeli na hata matusi. Tuache hayo tuijadili yenyewe
Kwanza,majina ya vitu, mitaa n.k. ni sehemu ya historia na utambulisho (Land Mark) na hivyo yanapaswa kupewa heshima.
Mtaa wa Aggrey ukitajwa fikra za msikilizaji zinaenda Dar es salaam na kuuhusisha na siasa za nchi hii.
Ngamiani ni landlmark ya Tanga kama ilivyo Mikindani Mtwara, Mukendo Musoma au Isevya Tabora.
Kwa nchi za wenzetu ni nadra kuondoa majina au alama za utambulisho au historia.
Wana utaratibu wa kutoa majina kwa maeneo mapya unaoongozwa na bodi maalumu ya wataalam.
Kuna nchi yenye sheria kiongozi hapewi alama hadi miaka 5 ipite tangu uongozi wake kwsababu maalum
Pili,utaratibu wa nchi yetu serikali za mitaa ndizo zenye wajibu wa kupanga miji yao yakiwemo majina ya mitaa,siyo jukumu la serikali kuu unless utaratibu huo umebadilika mwaka huu.
Kwa mintaarafu hiyo siyo sahihi kumlaumu JK. Watu wa kwanza kulaumiwa ni baraza la madiwani la jiji la Dar es Salaam.Meya wa jiji la Dar es Salaam ndiye 'mtuhumiwa nambari moja''
Meya, mameya, madiwani na wabunge wanapaswa kuja hapa na kutueleza utaratibu wa kubadilisha majina umetumia vigezo gani na nafasi ya historia ya nchi hii itazibwa na kitu gani.
Barabara ya Ocean road imekuwepo enzi na Ocean road ni hospitali ya matibabu ya kansa.
Hospitali inadhaminiwa na serikali ya ujerumani.
Moja ya umuhimu wa Ocean road ni kuwa hospitali ambayo mtaalam maarufu wa tiba (Dr Robert Koch) aliwahi kufanya utafiti wa maradhi ya malaria, black water fever,na homa ya malale.
Kupitia tafiti hizo Dr Koch alitunukiwa medali ya Nobel. Hospitali ya ocean rd ina historia pia kati ya umishenari(Lutheran), ujerumani, Zanzibar na Uingereza.
Yapo mahusiano kituo cha NIMR. Ni kwa maana hiyo German cancer research ina udau mkubwa sana na Ocean road.Kubadili jina la barabara inayokwenda katika eneo hili maarufu ni kuipoteza kabisa historia.
Kama ambavyo barabara ya Bagamoyo ilivyopoteza kiunganisho chake na jiji la mzizima, tunaendelea kuona sehemu ya Ocean rd nazo zinapoteza maana ya historia, utafiti na mengineyo.
Kama walitaka kumtunuku Obama bado walikuwa na nafasi ya kujenga barabara kwasababu walijua ujio huu muda mrefu.Au basi wangeweza hata kuita uwanja mpya 'Obama stadium' n.k
Lakini pia kuna jambo zuri linalotokana na hoja hii. Kuna wanahistoria feki hapa jamvini wanaoeneza uongo kuwa majina ya wazee wao yanafuta katika mitaa kwa chuki za Nyerere dhidi ya jamii fulani.
Barabara ya Bagamoyo imebadilishwa wapo kimya, sasa ocean road wapo kimya.
Miaka miwili au mitatu ijayo watakuja na paper na vitabu kulaani Nyerere kwa kubadili Ocean rd.
kwa hili lazima nafsi zao ziwasute na ni ushahidi tusisikilize tungo zao zilizodhamiria kueneza chuki na fitna.
Naomba tujikite katika mada tuachane na hoja ya aya ya mwisho