Ocean Road kuitwa Barack Obama road

Ocean Road kuitwa Barack Obama road

Kwanini wasijenge barabara mpya ndio wakajikombea kuuita jina?. Katika hili aibu naiona mimi.
 
nI KWELI WAMEKOSEA OCEAN ROAD kihistoria ni ya wajerumani
Meck sadick kasema hiyo ni kama zawadi ambayo manispaa ya Ilala imeamua kumpa Rais wa Marekani baraka Obama.
Mimi naona wamekosea kufanya hivyo. wangempa kinyago cha samaki sababu samaki ndo ipo kwenye nembo ya Ilala. mia
 
Tunakoelekea University of Dar es salaam itakuja kupewa jina la rais fulani
 
mkuu inaonekana unapenda,watu wapropaganda aina ya akina kagame,na mseveni utawala waku renuew pole sana!maziwa uaminishwa ni maji.
Nimeandika joke mkuu!! Ubongo wangu mzima Sana!! Nawajua Museveni na Kagame vzr!!
 
sasa na hospitali itaitwaje? Ocean road hospital au barak obama road hospital? Poor minded! Akili ndogo kutawala akili kubwa.. Aagh..!
 
Madiwani wa manispaa ya İlala watakuwa wameamua hlo

Hivi hakuna sheria iliyopo ambayo inapaswa kufuatwa kabla ya kuamua kubadili au kuupa mtaa jina? Tunao watu wengi sana watanzania wanaostahili heshima kiasi cha kupewa majina ya mitaa na barabara zetu ili tuwaenzi, hivi hawa viongozi wa Tanzania tumewaokota wapi? Sehemu ninayoishi mimi majina ya mitaa na barabara wamepewa watu mashuhuri kulingana na hisoria ya nchi yao. Kuna waandishi maarufu walioleta sifa kwa nchi, wanamichezo, watu waliopigania uhuru na demokrasia kwa nchi hii, watu ambao hata vizazi vijavyo vitawakumbuka kwa mchango wao kwenye historia ya mahali hapa. Majina mengine ni kama hayo yanayotokana na mahali barabara ilipo, mfano hiyo Ocean Road. Bahari ya Hindi bado ipo na itaendelea kuwepo, ndiyo asili ya jina la barabara hiyo... Hivi ukiwa diwani basi ukiamua hata kumpa mkeo jina la barabara imekuwa ruksa?
 
Hii Serikali inatakiwa ifuate washauri wa Airtel YATOSHA! oi
 
sasa na hospitali itaitwaje? Ocean road hospital au barak obama road hospital? Poor minded! Akili ndogo kutawala akili kubwa.. Aagh..!

Kuna watu mnafikiri, mpaka inatisha. Ndiyo maana huwa tunawangoeni kucha na meno.
 
Kama majina ya viongozi fulani yanaweza kutumiwa kubatiza baadhi ya barabara fulanifulani jijini Dar-es-Salaam kimzahamzaha basi huko ni kukosa muono.

Lakini kama jina la Baraka Obama limeweka historia nchini Tanzania kutokana na ziara zake zake hizi mbili (hii ya sasa ya ile ya 2009) na kwakuwa barabara ya Ocean imekuwa ikiitwa hivyo miaka nendarudi.

Na kwakuwa jina la Baraka Obama linamhusu mtu ambae ni raisi wa kwanza mwenye asili ya Afrika ambae anaongoza nchi yenye nguvu kubwa kuliko zote duniani yaani Marekani.

Na kwakuwa nchini Kenya nchi ambayo Baraka Obama ni asili yake na pengine hawajatumia sana jina lake kubatiza baadhi ya miundo mbinu kadha wa kadha.

Lakini pia kwa kuwa kuna majina kadha wa kadha ambayo yanatumika kuwaenzi baadhi ya viongozi wa nchi yetu na hata wale wa nje kama Jomo Kenyatta, Samora Machel, Edward Sokoine, Shaban Robert, Albert Luthuli , Patrice Lumumba, Nelson Mandela, Sam Nujoma na wengine.

Basi kwa ukarimu wetu tunaweza kubatiza barabara hiyo maarufu ya ufukweni mwa bahari ya Hindi na ikaitwa barabara ya Barack Hussein Obama.

Hakuna anaejali ikiwa serikali imeamua hivyo na haioni sababu ya kuuliza maoni ya wananchi kwani ardhi ni mali ya serikali.

Hiyo ndio nchi yetu tukufu ya Tanzania.
 
MWAI KIBAKI ana barabara imejengwa 4 ways THIKA SUPER-EXPRESS HIGHWAY,wewe unamwita hapa unatafuta kichochoro cha matajiri uchwara wa MBEZI beach kukwepea traffic jam unakiita MWAI KIBAKI ROAD?Ndiyo maana mzee wa watu akashauri WATZ mtembee tembee hata huku EAST AFRICA muone wenzenu wanafanya nini!PITY!

Mkuu nilipita hii Barabara ni Noma, Tanzania tumabakia a siasa, Serekari wako bise kubambikia CHADEMA kesi
 
Wampatie na kipande cha ardhi ama moja ya hifadhi nyingi tulizo nazo...
 
Back
Top Bottom