Ocean Road kuitwa Barack Obama road

Ocean Road kuitwa Barack Obama road

Hii nayo ni hoja ya kisiasa? jifunzeni kuweka habari zenu mahala panapo stahili! Mods tafadhalini, ipelekeni jukwaa husika nalo ni habari na hoja mchanganyiko.

Na ukiweza ihamishe wewe
 
Hivi hii jadi ya utumwa itaendelea mpaka lini? Kila akija mgeni basi barabara zinabadilishwa majina, kwani JK anapokwenda Marekani na nchi zingine zote ameshawahi kupewa hata kichochoro? Tumezidi kujidhalilisha kila kukicha. Hilo jina lina historia yake likimaanisha barabara inayopakana na Bahari (ya Hindi). Juzi tu jina la barabara ya Bagamoyo ya Zamani (old Bagamoyo Road) lilibadilishwa na kuwa Mwai Kibaki... Kwa nini kama wanampenda sana huyo Obama wasijenge barabara mpya wakaiita Obama Road? Na hospitali ya Ocean Road, hospitali kubwa ya kwanza kujengwa hapa Dar Es Salaam nayo sasa itaiwa Barack Obama Hospital? jk na serikali yako mnatia kichefuchefu... halafu mnatuambia watanzania hatuna uzalendo, uzalendo utoke wapi wakati mnauza mpaka barabara? Shame on you...
 
wanaumwa hao. kwa nini wasiipe jina hilo ile ya Mbagala.
 
Huo ni kukosa uzalendo na kutaka kuiua historia ya nchi. Majina ya barabara yana historia inayoungana na ile ya nchi. huu mchezo wa kugawa majina kila mara inatokana na uzoefu wa kugawa pia raslimali za nchi kiholela.

Rais wangu ana mapungufu makubwa sana,yanaptlza mapungufu ya kibinadamu
 
Hivi hii jadi ya utumwa itaendelea mpaka lini? Kila akija mgeni basi barabara zinabadilishwa majina, kwani JK anapokwenda Marekani na nchi zingine zote ameshawahi kupewa hata kichochoro? Tumezidi kujidhalilisha kila kukicha. Hilo jina lina historia yake likimaanisha barabara inayopakana na Bahari (ya Hindi). Juzi tu jina la barabara ya Bagamoyo ya Zamani (old Bagamoyo Road) lilibadilishwa na kuwa Mwai Kibaki... Kwa nini kama wanampenda sana huyo Obama wasijenge barabara mpya wakaiita Obama Road? Na hospitali ya Ocean Road, hospitali kubwa ya kwanza kujengwa hapa Dar Es Salaam nayo sasa itaiwa Barack Obama Hospital? jk na serikali yako mnatia kichefuchefu... halafu mnatuambia watanzania hatuna uzalendo, uzalendo utoke wapi wakati mnauza mpaka barabara? Shame on you...

Hawa wamezoea kupora rasilimali za taifa na kuzifanya zao. Ni nani aliwapa ruhusa ya kubadilisha hayo majina? Kuna mwananchi yeyote aliulizwa kuhusu jambo hilo? Hapa hakuna tofauti na wale wanyama waliosafirishwa kwenda Qatar. Viongozi wanadhani nchi hii ni yao!
 
Hii inaweza ikavutia kiasi kuliko ile ya Mwai Kibaki Road, lakini hamna cha maana Obama alichofanya mpaka apewe mtaa/barabara kwa Watanzania.
 
Hawa wamezoea kupora rasilimali za taifa na kuzifanya zao. Ni nani aliwapa ruhusa ya kubadilisha hayo majina? Kuna mwananchi yeyote aliulizwa kuhusu jambo hilo? Hapa hakuna tofauti na wale wanyama waliosafirishwa kwenda Qatar. Viongozi wanadhani nchi hii ni yao!

Madiwani wa manispaa ya İlala watakuwa wameamua hlo
 
Hivi mheshimiwa wetu katika nchi zote alizokwenda amewahi kupewa mtaa au hata kiwanja cha mpira? Sasa sisi ni nini tunaweweseka?


Sent from my BlackBerry 9860 using JamiiForums
 
Bora hata wangempa ile Ohio Street, hapo vipi wakuu??
 
Halafu mnatutaka tuwe Wazalendo kwa Taifa hili,You are not serious!
 
Back
Top Bottom