Nyumba ndogo jamani


...Mkuu, pole sana ndugu yangu, ...sina la kukusaidia zaidi ya kukuelewesha utambue mkeo yumo naye katika msongo mkubwa wa mawazo. Inahitaji busara kubwa kum handle mkeo katika hali hiyo, kum support hizo phase za mid-life crisis anazopitia kwa sasa.

Kusoma ni kuelimika, nimejaribu ku summarize few quotes (na rangi za kukutahadharisha) kwa nini wanawake wana cheat, huenda nawe ikakupa picha kinachoweza kuja tokea;

source; Infidelity, Cheating Wives - Women's Infidelity
 
Nyumba kubwa thamani yake iko katika ubora mkubwa baba anapo zeeka au kuugua. Pia linapotokea tatizo lolote, ni kinga kubwa kuliko nyumba ndogo.
 
Mbuu mid-life crisis, what does it mean in swahili au nifafanulie zaidi maana nalionaona sana. asante sana
 
Mbuu mid-life crisis, what does it mean in swahili au nifafanulie zaidi maana nalionaona sana. asante sana

...ule msongo wa mawazo, halafu unakuta mtu mzima anafanya mambo kinyume na umri wake, "mtu mzima hovyo!", ...hali ya kukata tamaa inakopelekea mtu kumfanya mkiwa, kujisikia mpweke, kukata tamaa ya maisha, kutaka kujiua,...

Mid-life kwa maana, umri wa ujana ushaaga (asilimia kubwa, umri kati ya miaka 40-45 kwa wanaume, na 35-40 kwa wanawake), utu uzima unakuingia, ilhali akili haitaki kukubaliana na ukweli huo... hali ya kuwa na mashaka na kujishuku uwezo wako wa kila jambo, kuanzia kazini, kumtosheleza kitandani mwenza, uwezo wa kuisaidia familia,...muonekano 'hasi' wa kimaumbile (kuchusha, nk)...

hali hii hupelekea mtu kufanya mambo kinyume na tabia zake za kawaida, mfano; ulevi, ugomvi, kujichanganya na watu chini ya umri wake, kutafuta dogo dogo... nk....

umepata picha japo kidogo sasa? Kiswahili fasaha cha mid-life crisis sijui, kwa wengine watajidai ni western cultures, ilhali hata hapa Bongo wengi tu utasikia wamejitia kitanzi maisha 'yakiwashinda!' kiuchumi, kiunyumba, na hata kwa kero kazini.
 
Kuna idadi kubwa sana ya wanawake kuliko mimi na wewe tunavyoweza kufikiri, wanaoamini kwamba wanaume wote wana nyumba ndogo. Je wewe mwanamke ndivyo unavyoamini? Je wewe mwanaume umeshawahi kuambiwa hivyo na mkeo au mpenzi wako? Kama bado basi wewe una bahati.

Kwa nini wanawake hawa wanaamini hivyo? Kuna sababu kubwa moja tu ambayo ndiyo yenye kufanya imani hii kushika mizizi, nayo ni malezi. Wanawake kama ilivyo wanaume wamelelewa kwa kuamini kwamba wao ni dhaifu na wanaume ni imara. Wamelelewa kwa kufundishwa kwamba wao hawana haki zote ndani ya nyumba kama ilivyo kwa wanaume.

Katika kuamini huku wanawake wamejikuta wakiwa ni aina ya watumishi ndani ya ndoa na wamejikuta wakiwa ni watu wa jikoni ndani ya ndoa na waamejikuta wakiwa watu wa kupewa amri na kuzipokea ndani ya ndoa. Katika mkabala huo wanawake wamejikuta wakiwa hawana kauli wala sauti hata katika maswala ya kimaumbile.Kwa mfano ni mwanamume ndiye anayetakiwa kusema ‘leo sijisikii’ na siyo mwanamke na ni mwanaume anayetakiwa kusema ‘leo nahitaji’ na siyo mwanamke.

Mwanamke anapokua na mahusiano na mwanaume mwingine nje, anapewa haraka jina la ‘Malaya sana’ wakati mwanaume anaweza kupewa jina la sifa “mkali” au “mtu wa watoto” hata kama ana mahusiano na wanawake kumi. Hii sio nasibu ya mambo bali matokeo ya malezi yetu.

Kwa kupewa nafasi kama hii mwanaume amekua huru kushiriki tendo la ndoa kwa kadri atakavyo kwenye familia zetu. Nyumbani hua tunaona jinsi watoto wakiume wanapokua na marafiki wa kike lisivyo jambo la ajabu , bali tu pale watoto wa kike wanapo jaribu kuwa na marafiki wa kiume hata wale makaka ambao wao huwachezea madada wa wengine huko nje huwa wakali sana kwa madada zao.

Kwa mkabala kama huo, kwenye jamii yetu mwanamke kua mcheshi, mzungumzaji huru na mkaribishaji mzuri kuna maana moja tu kwamba huyu ni malaya, bali kwa mwanaume sifa hizo hubaki hivyohivyo na pengine kuongezewa uzito. Hata kama ndani ya sifa hizo kumejificha ufuska ulio kubuhu, hakuna atakayejali sana.

Kuna ukweli kiasi fulani kwamba, wanaume wengi huwa wana ‘nyumba ndogo’ au zaidi ya rafiki mmoja wa kike. Hali hii imepelekea hata watu kuamini kwamba wanaume wana hamu kubwa na tendo la ndoa kuliko wanawake, jambo ambalo limekanushwa na tafiti nyingi zilizofanywa kuhusiana nalo.

Wanaume kwa sababu za kamalezi na ubabe ulio katika mazoea ya kimapokezi tangu kale, wanaamini kwamba wao ndio wenye uhuru wakuchagua kama waendelee kua na mmoja au hapana. Kwa hiyo,kwa sababu wao ndiyo ambao wamejipa funguo ya maamuzi hufanya uharibifu mwingi.

Kwa kuwa wanaume wanaamini kwamba wanapaswa kuabudiwa na wanawake, linapotokea tatizo dogo tu la kindoa huamua kutoka nje, kwa sababu wanawake kwao ni vyombo vya starehe vinavyoweza kununuliwa mwanamume anapojisikia. Lakini pia hii ni kwa sababu, kutoka nje kwao ni aina ya sifa wakati mwingine.

Kutokana na malezi haya ambayo yanahalalisha mwanaume kuwa “kijogoo” wanaume wengi wamekua na urahisi wakutokua waaminifu . Lakini hata hivyo,hakuna ukweli kwamba wanaume wote wana nyumba ndogo. Nadhani unajua tofauti kati “wote” na “wengi”

Ni vigumu kusema idadi halisi kwa maana asilimia, kwani hakuna utafiti rasmi ambao umefanywa, lakini kwa utafiti usio rasmi imethibitika kwamba kwa hapa Jijini Dar es salaam, kuna uwezekano mkubwa kwamba katika kila wanaume kumi, saba wana ‘nyumba ndogo’ au rafiki wa kike zaidi ya mmoja.

Idadi hii ni kubwa sana na kuna haki kwa watu kuamini kwamba kila mwanamume ana ‘nyumba ndogo’. Lakini bila shaka umefika wakati kwa wanaume kujiuliza kama tabia hiyo ina manufaa yoyote kwao na kama huko sio kuwazalilisha wake au wapenzi wao. Je, wake zao wangekua wanafanya hivyo wao wangejisikia vipi,au wanadhani wanawake hawana hisia kama binadamu?
 
bado siamini kama tigo ni kinga muhimu ya ndoa.

hiyo ni kweli kabisa! hata ukimpa tigo mwingine haridhiki tabia ya wanaume wengi ni kutaka kujaribu hiki na kile kwa wanawake tofauti!
 

Mkubwa Mbu umenimaliza kabisa na hii post, yaani ni kama umenitangazia msiba kabisa! Sasa mke wa hivi ni wakuwacha kabisa au siyo, maana naogopa kupata kichaa na watoto wetu ni wadogo. Nadhani tuachane wote tukiwa bado na akili timamu itakuwa nafuu kwetu na watoto.
 
Siku hizi hata wanawake wanatengeneza nyumba ndogo, hili ni tatizo!!!
 
hata umfanye nini mwaume hatosheki,kama ameamua kwenda nyumba ndogo ataenda tuu maana ameshaamini akilini mwake kuwa numba ndogo ni tamu but ukmwi tu wanaume wanatafuta,unaweza kaa na mkeo vizuri na akakupa yote utakayo ukawa mwenye furaha kwenye ndoa yako kuliko nyumba ndogo lakini kwa vile wanaume wamezoe akitaka kufarijika ni nyumba ndogo basi akili yake imemtuma hivyo na ndo maana anaona ni nzuri kumbe anazidi kuwasha moto na kuteketea kwa ndoa yake,tupo wanawake wengine tunajitahidi kufanya yoote yatakiwanya na bado waume zetu wanatoka nje na unajitahidi hata ukijua ana nyumba ndogo unajikaza ili usimuudhi unaongeza mapenzi aa wapi wala haoni wala hathamini,wanawake tuna tabu!!!!!!
 
mbu hapo juu nimesoma post yangu very interesting sijui umeoa umeyajua yote hayo?au upo kwenye ndoa muda gani bla shaka utakuwa mwenye furaha kwenye ndoa yako maana post zako zinaonekana za kikubwa.haswa ile ya dizaini ya kulala kwenye ndoa baada ya miaka kadhaa,bila shaka ukishayajua ote hayo basi utakuwa na mkeo kwa furaha,natamani na mimi mume wangu angeyajua yote hayo nitamshauri aingie humu asome japo wengine wanayoandika huku si wayafanyayo wazuri kushauri lakini ndoa zao sinawaka moto,namjua kaka mmoja ni rafiki yangu sana sitamtaja humu ndo alinionyesha jamii forum lakini yeye yote ayasemayo na kutushauri hatekelezi kwa mkewe,bila shaka wana jamii sio mlivyo,tushaurini lakini na ndoa zenu mfanya mnavyofanya muwe mfano
 
mbu hapo juu nimesoma post yangu very interesting sijui umeoa umeyajua yote hayo?

...🙄

...au upo kwenye ndoa muda gani

...😱

bla shaka utakuwa mwenye furaha kwenye ndoa yako maana post zako zinaonekana za kikubwa.

...😕

haswa ile ya dizaini ya kulala kwenye ndoa baada ya miaka kadhaa,

...🙂

bila shaka ukishayajua ote hayo basi utakuwa na mkeo kwa furaha,

...😳

natamani na mimi mume wangu angeyajua yote hayo nitamshauri aingie humu asome

...😎

japo wengine wanayoandika huku si wayafanyayo wazuri kushauri lakini ndoa zao sinawaka moto,

...🙁

namjua kaka mmoja ni rafiki yangu sana sitamtaja humu ndo alinionyesha jamii forum

...:evil:

lakini yeye yote ayasemayo na kutushauri hatekelezi kwa mkewe,

...😱

bila shaka wana jamii sio mlivyo,tushaurini lakini na ndoa zenu mfanya mnavyofanya muwe mfano

...Kima, Kima, Kima! ...hebu soma posting yako toka chini kwenda juu;



...umeelewa ewe Kima?
 
nimesoma ila fafanua,

*bila shaka wana jamii sio mlivyo,tushaurini lakini na ndoa zenu mfanya mnavyofanya muwe mfano*basi nataka japo niongee na mkeo nimulize kama uyasemayo ndo unayoandika hapa labda na mimi ndoa yangu itakuwa na furaha nikipata ushauri unaosema,nikisoma coments zako naona kama sahamani kama nakufikiria vibaya ni mtu unaendaika lakini si mtekelezaji naona muda mwingi unatumia kwenye net badala ya kuwa na moeo muda wa kumfanyia mkeo yote hayo mwaupata wapi jamani?naona wengine wakirudi makazini naona kwa huyo rafiki yangu moja kwa moja kwa computer hata muda wa kupeana na mkewe hana yeye anawaza jamii forum tuu mapenzi yatatoka wapi?
 
Nyumba ndogo taaaaaaaaaaaaaaaaamu jamani zinajua kubembeleza jamani.
 
Mkuu nadhani kwenye nyumba ndogo kuna faida sana alafu pale inakuwa mashindano kati ya mke mkubwa na mke mdogo sasa wewe unakuwa unapagawa unakuwa huna la kufanya so hapo mambo yanakuwa yanakwenda sawa!!
 

not good
 
Wake ndo wana jukumu la kuwafundisha waume zao mbinu za kuepukana na hawa predators wanaoiba waume za watu!

Mme pia ana nafasi kubwa sana ya kumfundisha mke kwenye mambo husika. Kumbuka wanaume wanavyivitafuta nje ni vitu ambavyo unavyoweza kujifunza na mwenzi wako kupitia vitabu, magazeti, majarida, mikanda, n.k. Taarifa zipo nyingi sana ni wewe tu kama unaitafuta hiyo furaha kuileta ndani ya ndoa badala ya kwenda kuitafuta nje na kuhatarisha maisha yako na ya familia kwa ujumla. Unaweza kujifanya hujui pamoja na kuwa unajua, ukanunua kitabu au mkanda na kusoma au kuangalia kwa pamoja na mwenzi wako na huku mkijadiliana ni style zipi zitawafaa. Mnaweza kuchagua mitindo ambayo mnaona haitawaumiza na taratibu mnaijongea ile migumu. Tukiwe sehemu ya kutatua matatizo ya ndoa, nyumba ndogo zitakwisha. Na hili linawezekana kama utaweka mbele long term stability kwa ajili ya ndoa yako na mwelekeo wa maisha ya watoto wako hapo baadaye. Kumbuka mwenendo wa maisha utakaouchukuwa katika maisha ya ndoa yana impact kubwa sana katika maisha ya baadaye ya watoto wako.
 
pole na ukome.......

......unashindwaje kumwambie mkeo kuwa unahitaji patanisho la ndoa.....
......nikushauri kitu nimekusoma unaonekana kweli yemekukuta na ingekuwa mie mwenyewe angesalenda...sasa kwa kuwa unampeleka kiseminari nakupa sahuri za kimishionari

........mtoe out onyesha unamjali sana na kumpenda....msiagize chakula wanawake wakishakula wanakuwa wavivu hatakuskiliza sana sana ataomba mrudhishe nyumbani akalale....kwenye mazungumzo mwambie bayana....

why she doin ugaidi wa namna hio....msikilize atakavyojibu akionekana kuwa mgumu kubali mpe siku zingine 2 kila siku mpe somo bado akiwa mgumu basi m treat kama dada yako hakuan kumuita dear muite jia lake.....kuwa busy sana na kazi....usiku angalia movie hata katuni kama una access na net kata ishu JF mpaka liamba...kisha lala sebuleni mara moja moja....

.....Hg usimguse utanogewa hao HG wana skills za kufa m2.....suuza rungu kwa kupiga mgalala.....usimuombe penzi...after 1month njoo utaniambia.....TGNP an TAMWA inawadanganya wana visheria vyao eti ubakaji ndani ya ndoa....
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…