Nyuma yako - Riwaya ya SteveMollel

*NYUMA YAKO – 18*
*Simulizi za series*

ILIPOISHIA
Tulipofika pakavu, nikamtazama mtoto na kubaini alikuwa amejigonga kwenye jiwe ingali tu mtoni. Na kwa namna alivyokuwa anatoka damu, inabidi ifanyike namna upesi ya kumsaidia, la sivyo alikuwa anatuacha!
Nikamwambia mama yake, “gandamizia mahali pa jeraha, nakuja!” mimi nikaenda kutafuta majani yatakayoweza kumsaidia jerahani.
ENDELEA
Nilifahamu ndani ya msitu ule sitakosa ninachotaka. Nikakimbia upesi na kufanya jitihada za kuangaza macho yangu nikitumia stadi niliyonayo juu ya madawa ya asili. Tulifunzwa hii. Tulifunzwa namna ya kudumu na kumudu kwenye hali mbalimbali kama hizi.
Ndani ya muda mfupi, nikapata kuona kichaka chenye majani membamba na ncha kana kwamba sindano. Nikajongea hapo na kuchuma majani kadhaa na kuyatia mdomoni kutafuna alafu nikaanza kurudi upesi kule kwa yule mwanamama na mwanaye.
Nilipofika majani mdomoni mwangu yalikuwa tayari yashalainika vya kutosha. Nilikunja sura kwa uchungu wake mithili ya shubiri. Nikayatema na kumpachika yule mtoto eneo lake la jeraha alafu nikachana sehemu ya shati langu kutengeneza bandeji, nikamfungia hapo kichwani na kumweka mtoto huyo begani tuendelee na safari.
Tukiwa tunatembea, nikapata sasa wasaa wa kumuuliza maswali kadhaa. Niliona huu ni muda muhimu wa kufanya hivyo maana lolote linaweza kutokea muda wowote. Basi likitokea, angalau niwe nimetimiza robo ya haja yangu.
“Wewe ni nani? Kwanini watu hawa wamekuteka?” Niliuliza nikimtazama mwanamke huyo ambaye alikuwa akitembea kwa ukakamavu. Alikuwa na ushupavu ndani yake.
Akanitazama na kunyamaza kwanza akipiga hatua. Alipovuta pumzi ndefu ndipo akanijibu pasipo kunitazama, “Nilidhani utakuwa unanijua ndo’ maana ukaja kuntafuta.” Kisha akaniuliza, “Ajenti, umekujaje kumtafuta mtu ambaye humjui?”
“Umejuaje kama mimi ni ajenti?”
Akatabasamu. “Anayeweza kuyafanya yote haya, ni raia wa kawaida?” kabla sijanena akaendelea kunena, “Umefanya kazi kweli kujua wapi nilipo. Hata sasa kuwa hai unastahili pongezi.”
Nikamtazama na pasipo kuongea nikarudisha macho yangu mbele tuendako nikitarajia mwanamke huyo ataendelea kunena.
“Mimi ni raia wa kawaida kabisa. Ni mmarekani ninayeishi Ujerumani pamoja na mwanangu. Sina shida nyingine na mtu!”
“Huku Ujerumani unafanya nini? Na kwanini Ujerumani?”
“Una maswali mengi sana. Sidhani kama nipo kwenye mood ya kukata kiu chako. Pengine baadae nikiwa nimetulia.”
“Wamekufanya lolote ulipokuwa chini yao?”
Akatikisa kichwa. “wasingeweza kunifanya kitu.”
Nikamtazama kwa maulizo pasipo kusema kitu. Nadhani yeye mwenyewe akajiongeza na kunijibu swali langu la kimya. “Bado wananihitaji. Mimi ni asset kwao. Hawawezi kunidhuru.”
“Unamaanisha nini wewe ni asset?”
“Nimekuambia una maswali mengi. Najua. Tutakapotulia nitakuambia, pengine nitakata kiu chako.”
“Hauwezi ukanambia hata machache?”
“Naitwa Britney. Ni raia wa Marekani. Nadhani hayo yanakutosha.”
Sikutaka kusumbuana naye. Niliona ninyamaze kimya, kweli hayupo kwenye mood, japo kifuani mwangu nilikuwa nalaumu sana kutokujua kinachoendelea ingali tulipokuwa kitu chochote kingeweza kujiri.
Tukatembea kwa kama dakika kumi, akantazama kisha asiseme kitu akatazama zake mbele. Nadhani alikuwa anajiuliza maswali kichwani. Baada ya sekunde kadhaa, akasema, “Naomba umtazame mwanangu. Yeye ndo’ kitu pekee nilichonacho kwa sasa.” Kisha akasimama na kun’tazama. Nami nikasimama. Akaniambia, “Niahidi hilo … niahidi mtoto wangu atakuwa salama.”
“Nakuahidi,” nikasema kwa sauti ya kutikisika. Akaniuliza, “Unaniahidi?”
“Ndio, nakuahidi,” saa hii nikasema kwa kujiamini. Basi akaridhika tukaendelea na safari. Akaniambia kama tukitembea kwa takribani robo saa tutakuwa tumefika barabarani.
Tukatembea kwa kama dakika sita, yeye mwenyewe akaanza kuongea. “Nimemkumbuka sana mama yangu,” sauti yake ilikuwa ya mtu anayekaribia kulia.
“Kama ningalifuata alichonambia, nisingalikuwa hapa.”
Nikamtazama nisimsemeshe kitu. Nilihofia maneno yangu yangeweza kumkatiza. Nilimwacha afanye vile alivyokuwa anataka.
Akavuta makamasi mepesi kisha akaendelea, “Sasa nimekuwa mkimbizi nisiye na makazi. Toka kwenye kamera za mwanga mpaka kujificha chini ya uvungu na nyuma ya milango. Ama kweli maisha huweza badilika ndani ya sekunde moja tu!
Ndani ya sekunde moja mtu akawa kilema. Akapoteza alivyovipata kwa masaa. Ndani ya muda huo mchache akawa amebadili mwelekeo wa maisha yake.”
Nikaendelea kumtazama pasipo kutia neno. Niliona uso wake ukiwa umebadilika rangi kuwa mwekundu. Alikifikicha pua yake na kumwaga tena maneno, “Hakuna anayejua kesho yake, sio? … mimi sikudhani kama siku moja ntakuja kuwa na familia. Sikuwa nawaza hilo jambo kabisa, labda kwasababu ya aina ya maisha niliyoyachagua.
Maisha yalonifanya ninyooshewe kidole kila nilipopita nikionekana laana, mchafu na niliyelaaniwa. Sikutaka mwanangu aje kushea laana yangu. Ashindwe kupita mtaani kwasababu ya mama yake. Ni adhabu. Najua ukubwa wa adhabu hiyo maana nimeibeba mgongoni kwa muda mrefu. Inachosha na kuumiza.
Watamani kukaa mbali na walimwengu ambao ni wepesi wa kuhukumu na wachoyo wa fadhila. Lakini ajenti, wawezaa kukaa mbali na dunia?”
Aliniuliza akintazama. Nikamtikisa kichwa kukataa pasipo kutia neno. Basi akatabasamu kwa mbali na kisha akakaa kimya kidogo. Tukatembea kwa kama dakika moja asinene jambo ila nikiamini ataendelea tu kusema.
Nilihisi ana kitu kifuani. Atajihisi mwepesi endapo atakitoa.
Akajifuta machozi na mikono ya sweta lake alafu akatazama juu kwenye matawi ya miti, pembeni na kisha mbele.
“Hata kama niki –”
“Shhh!” nikamzuia upesi nikimwonyeshea ishara ya kidole mdomoni. Kuna kitu nilihisi. Tulisimama tukatulia tuli na kutazama kushoto na kulia. Masikio yangu yalinambia nimesikia sauti ya watu wakiteta. Na sikuwa nimekosea, lah! Nyuma yetu kwa umbali, tukawaona wanaume wawili waliokuwa wamevalia nguo nyeusi na mikononi mwao wana bunduki ndefu!
Wanaume hawa hawakuwa na usafiri, bali wakitumia miguu yao.
Haraka nikamtaka Britney akimbie na mie kabla sijafungua miguu yangu nikafyatua risasi kuwalenga wanaume wale kuwapumbazisha kwa muda kidogo.
Tukakimbia na kukimbia. Nao wale wanaume wakawa wanaendelea kutukimbiza, wakawa pia wanatupa risasi wakijaribu kunilenga.
Nikiwa nimembebelea mtoto, nikakimbia kwa kasi na kwanguvu mpaka kumwacha Britney nyuma. Si kwamba alikuwa anakimbia taratibu, hapana! Na wala hakuonekana mtu anayehitaji msaada. Alikuwa anajimudu kukimbia.
Hatukudumu muda mrefu mbioni, nikasikia risasi ya karibu zaidi na kisha sauti ya kike ikilalama! Kutazama, nikamwona Britney akidondoka chini!
“Shit!” nikamsikia mmoja wale wajamaa wanaotukimbiza akilaani, kisha kwa punde akamlaumu mwenzake kwa kumfyatulia risasi Britney. Hapa nikatumia nafasi hiyo upesi kuwamiminia risasi na kuwalaza chini.
Nikamtazama Britney. Alikuwa amelengwa kwenye shina la nyuma la shingo. Risasi ilivunja uti wake wa mgongo! Ilikuwa ngumu kwake kupona. Damu zilimtiririka. Macho yake yalimwaga machozi akinishika kwanguvu na kung’ata meno yake.
“Ajenti, mtazame vema mwanangu,” akasema akikwamakwama. Kisha akaninong’oneza, “Naitwa Juliette Simpson. Natumai utakuwa unanijua.” Alafu akajifia.
Akafa mbele ya macho yangu. Akafa mwanaye akiwa bado hajitambui.
Nikawaendea wale wanaume niliowaua na kuwapekua. Sikuwakuta na kitu zaidi ya bunduki na risasi kadhaa. Nikazichukua. Nilipomrudia Britney ambaye kabla hajafa alinipa jina lingine, naye nikampekua kama ana kitu. Alikuwa mtupu.
Nikapata maswali juu ya nini cha kufanya. Haraka nikatoa simu yangu na kumchukua picha kadhaa, nashukuru simu yangu haikuwa simu inayoingiza maji.
Nikiwa nimempiga picha mbili tu, nikasikia tena sauti ya watu, hiyo ikawa ishara kuwa sitakiwi kukaa hapo tena. Nikaanza kukimbia. Huko nyuma nikasikia, “Yule!” na vishindo vya watu vikinifuata kwa kasi!
Nikakimbia sana lakini nguvu zangu hazikuwa kama za hapo awali, nilichoka mno. Kumbeba mtu kwa muda wote ule huku nikikimbia na kutembea haikuwa jambo jepesi. Hivyo basi nikaanza kupunguza kasi ya mwendo wangu na kupelekea wale maadui wanikaribie zaidi!
Wakatupa risasi kadhaa. Nashukuru miti ilinikinga. Nilisikia zikipasua na kugotea mitini. Nilipoona maji yanazidi kupiku unga, nazidi kukaribiwa na hali ni mbaya, nikakimbilia mtoni na kujitosea humo!
Nilizama maana kina kilikuwa kirefu. Risasi zikatumwa kunifuata ndani ya maji, zikanipitia kupunyua, lakini kwakuwa maji yalikuwa na nguvu na mengi ya kutosha kunipeleka, yakaniepushia na balaa!
Yakanisomba kunisafirisha.

***
Barikiwa sana
 
*NYUMA YAKO – 19*
*Simulizi za series*

ILIPOISHIA
Nilizama maana kina kilikuwa kirefu. Risasi zikatumwa kunifuata ndani ya maji, zikanipitia kupunyua, lakini kwakuwa maji yalikuwa na nguvu na mengi ya kutosha kunipeleka, yakaniepushia na balaa!
Yakanisomba kunisafirisha.
ENDELEA
Maji yalipotuama, tukiwa tumesafiri kwa kama robo saa, nikachoropoka toka mtoni kuitafuta barabara.
Haikuwa safari ndefu sana. Sidhani kama nilichukua zaidi ya dakika kumi, nikawa tayari nimefika kwenye lami ambapo niliomba msaada na upesi nikapatiwa. Nadhani ilikuwa ni sababu ya mtoto niliyekuwa nimembeba. Mama mmoja ambaye alikuwa anasafiri na mbwa wake, alisimamisha akiwa ananitazama kwa huruma kisha akaniuliza naelekea wapi kabla hajaniruhusu niingie ndani na kuendelea na safari.
Nikiwa ndani akawa ananidadisi nini kimenitokea, na kwasababu sikutaka kumsababishia taharuki, nikamlaghai kuwa tumepata ajali. Akanipeleka mpaka mjini kabisa na kuniacha hospitalini. Mtoto akatazamwa jeraha na kupatiwa dawa za kumsaidia dhidi ya maumivu na kumkausha jeraha.
Baada ya hapo nikatafuta mahali pa kupumzikia. Nikamlaza mtoto na mimi kufanya utaratibu wa chakula maana njaa nayo ilikuwa inauma. Kila kitu kilipokuwa sawa, nikajilaza kitandani nikiwa nawaza.
Mwanamke yule aliyefia mikononi mwangu, mtoto huyu ambaye yupo pembeni, watu wale waliokuwa wanatufukuza na mahusiano yao na Raisi! Nilihisi mambo yamechangamanaa sana.
Sikudhani kama msako wangu wa Raisi ungenisafirisha ukubwa huo. Nikanyanyua simu na kumpigia Jack Pyong kumweleza yote yaliyojiri. Naye akashangaa sana lakini lile la Britney likamshangaza zaidi. Akanisihi nimtumie picha za mwanamke huyo na kisha jina lake hilo la mwisho ambalo alilisema kabla hajafariki, yaani Juliette Simpson.
Nikafanya hivyo, akaniambia nimpatie muda kidog basi atanirejeshea majibu. Nikaendelea kujilaza kitandani. Kama baada ya dakika tano, mtoto yule akaamka akilalamikia maumivu makali kichwani.
Nikampatia dawa na kumhasa apumzike zaidi. Lakini kabla hajafanya hivyo, akaniuliza mama yake yupo wapi? Hapa nikapata kigugumizi.
“Unaitwa nani?”
“Henessy,” akanijibu akiwa ananitazama kwa kufinya macho.
“Henessy, Mama ametangulia Marekani. Marekani si ndo’ nyumbani?”
Akasita kisha akaniuliza, “Kwanini ameenda mwenyewe?” kisha macho yake yakalowana machozi. “Kwanini ameniacha?’
“Hajakuacha,” nikasema nikimkodolea macho. Nikamfuta machozi na kumpoza, “ilibidi atangulie kwenda huko maana ndege ilijaa. Nasi tutamfuata, usijali.”
Akan’tazama kwa maulizo. Akafuta machozi kwa mgongo wa kiganja chake kisha akaniuliza kwa sauti ya kubashiri, “Tutaenda lini?”
“Usijali, tutaenda. Kuna mambo kadhaa namalizia kama kesho ama keshokutwa. Sawa?” akatikisa kichwa kuafiki lakini kishingo upande. Kidogo simu yangu ikaita, alikuwa ni Jack Pyong, nikapokea akaanza kunambia nini amepata.
“Tony,” akaanza kwa kuniita jina. Sauti yake ilikuwa ya chini na msisitizo. Akanambia, “Huyo mdada ni mwigiza picha za ngono!”
“Yupi?”
“Huyo Juliette! Namaanisha Juliette Simpson!”
“Huyo niliyekutumia picha?”
“Acha basi kuniuliza maswali ya kijinga. Kwani tumetoka kuongelea nini hapa muda si mrefu?”
“Kuna mtu mwenye maujinga kama wewe?”
“Nitaacha kukwambia! Ohoo!”
“Sema basi. Unajua credit inaenda!”
“Sasa nikitaka kusema wewe unaanza mambo yako. Tulia kama unanyolewa.”
“Sawa, nimetulia. Kwahiyo unanambia—” kabla sijamalizia nikamtazama yule mtoto, sikutaka asikie. Nikasonga kando kidogo.
“…kwahiyo Juliette huyo ni pornstar?” Pornstar maanaye mcheza sinema za ngono.
“Ndio. Ni maarufu tu. Sikuwa najua hilo mpaka nilipoingia mtandaoni!”
“Sasa Jack, mcheza sinema za ngono atakuwa ana mahusiano gani na kupotea kwa Raisi?”
“Tony, hiyo ni kazi yako. Unanipachikia mimi sasa?”
“Sasa we fala, huko mtandaoni ulikuwa unafanya nini?”
“Nakutafutia huyo mtu wako. Ebu sikia, kesho kama nikipata muda nitaenda kwenye kampuni aliyokuwa anafanyia kazi. Pengine nitapata baadhi ya majibu. Baadae!”
Akakata simu na kuniachia maswali lukuki kichwani. Niliona mambo yanazidi kuwa magumu. Nikazama mtandaoni na kuandika jina la yule mwanamke, punde nikaona majibu ya ajabu. Kweli mwanamke yule alikuwa mcheza sinema za ngono.
Lakini kwa taarifa zaidi, alikuwa mstaafu! Lakini kwa kazi hii kuna mstaafu kweli ilhali video zake bado zipo hewani na watu wanaweza kuzipakua na kuzitazama?
Nilipofuatilia zaidi nikabaini na hiyo kampuni aliyokuwa akifanyia kazi. Kwa jina, LEXANDER PLEASURE ikiwa inasimamiwa na mwongozaji mwenye asili ya kilatini aitwaye jina la utani, Bomboclat!
Hapa sasa nikapata kujua kwanini mwanamke yule alishangaa nilipomwambia simfahamu. Huenda alidhani umaarufu wake kwenye michezo hiyo ungelinigusa hata mimi. Lakini pia nikafahamu kwanini alinipatia majina mawili, mosi Britney, pili Juliette. Ina maana Britney lilikuwa ni jina lake la uhalisia wakati Juliette Simpson likiwa ni la ‘kazini’.
Nikashusha pumzi ndefu nikimtazama yule mtoto. Nilikuwa nawaza kama atakuwa anajua kuwa mama yake huko mtandaoni yupo uchi. Nikajikuta natikisa kichwa kisha nikaanza kusuka tu mipango ya kurudi Marekani maana sikuwa na cha ziada cha kukifanya tena hapa Ujerumani.
Hivyo nikaona ni stara kufunga safari, kesho asubuhi na mapema, kwenda jiji la Berlin ambapo ndipo kuna ubalozi wa Marekani.
Siku hiyo nipumzike tu kwakweli. Nilikuwa nimechoka mno. Shurba nilizopitia zilikuwa zatosha kunifanya nijilaze.

**

Kesho yake …

Berlin, Ujerumani.

Nilitoka ndani ya balozi nikiwa na uhakika wa safari yangu jioni. Na kwakuwa nilijitambulisha na kuthibitisha humo ndani kuwa mimi ni ajenti wa CIA, basi mambo hayakuniwia sana ‘ugumu’.
Nikaongozana na Henessy mpaka mgahawani kujipatia chakula. Hapo tukakaa kwa muda wa kama nusu saa kabla hatujajiweka kwenye basi na kwenda mpaka beach. Nilitaka angalau nifurahie ujio wangu hapo Ujerumani japo ulikuwa ni wa kikazi.
Walau nipate muda wa ‘kuenjoy’ kabla sijaacha ardhi hiyo kurejea nyumbani. Nikiwa hapo nikapata nafasi ya kuzoezana na Henessy ambapo tulicheza na kufukuzana pamoja tukiwa tunapigwa na pepo ya bahari.
Tukiwa tumechoka, tukawa tunatembeatembea tu fukweni. Lakini kama baada ya hatua zetu kadhaa, paliongokea mwanamke mmoja ambaye amevalia ‘casual’. Uso wake ulikuwa umefichwa na miwani meusi na miguu yake imebanwa na jeans iliyopauka. Begani ananing’iniza mkoba mdogo uliobana kwapa lake.
Mwanamke huyo akiwa anapunga mkono wake na kutabasamu, aliita, “Heneessyy!” tukageuka wote kutazama. Alikuwa anatokea upande ilipo barabara kuu.
Nikamuuliza Henessy, “Unamjua huyo mwanamke?”
Henessy hakunijibu, badala yake akawa anamtazama kwa umakini mwanamke huyo pengine akumbuke kama alishawahi kumwona mahali. Hivyo kabla hajanipa majibu, mwanamke huyo, kwakuwa alikuwa anakimbia na kutembea kwa kasi, akawa ametufikia.
Akan’salimu kwa upesi, akitumia kiingereza, kisha akainama kumtazama Henessy akitabasamu. “Hujambo Henessy? … unaendeleaje muda wote huo?”
Henessy akamjibu lakini bado akiwa anamtazama kwa macho yaliyokaza. Nikamuuliza mwanamke huyo, “Tafadhali unaweza kujitambulisha?”
“Oow!” akasema akivua miwani yake. Macho yake yalikuwa ya paka yakiwa na uchangamfu ndani yake. Akatabasamu na kunipatia mkono, “Naitwa Jolene! Ni rafiki yake na Britney.”
“Oooh! Nimefurahi kukujua,” nikamjibu nisiongezee mengi. Akaniuliza, “na wewe? Wewe ni nani?”
“Naitwa Rodney. Ni rafiki pia wa Britney!”
Akaangaza kushoto na kulia. “Britney yupo wapi?”
“Hayupo. Hatujaja naye hapa!”
“Ooh! Yupo wapi kwa sasa. Ni muda sijawasiliana naye. Hata sasa imenichukua muda sana kumtambua Henessy!”
“Ni simulizi ndefu kidogo,” nikamjibu na kumwomba, “tunaweza tukapata dakika kadhaa za kuongea?”
Akaridhia baada ya kutazama saa yake ya mkononi. Tukasonga kwenda mahali fulani tulivu kwenye eneo hilohilo la ufukweni, hapo tukapata vinywaji laini na kupiga soga nikitaka kufahamu machache juu ya Britney lakini nikiwa nimemlaghai kuwa mimi na Britney ni mtu na mchumba wake. Tumekutana na akanieleza mambo kadhaa, ikiwamo kujihusisha na kucheza sinema za ngono.
Kwa kufanya hivyo nilitarajia kumpa mwanya mwanamke huyo wa kutonificha kitu. Kumtengenezea mazingira ya yeye kuwa huru kunielekza lolote maana hata lile ambalo lingeweza kuwa siri, mimi tayari nalifahamu.
“Umemjua Britney kwa muda gani?”
“Miaka mingi tu. Alikuwa ni rafiki yangu toka High school!”
“Kwahiyo ulikuwa unafahamu juu ya yeye kujihusisha na ile kazi?”
“Yah! Ni rafiki yangu, nitashindwaje kujua hilo?”
“Mlikuja kupotezana naye muda gani?”
“Aaahmm kama mwaka mmoja na nusu hivi uliopita.”
“Kwanini mkapotezana? Hakukuaga kama anakuja Ujerumani?”
“Hakunambia! Nilistaajabu amepotea. Simu yake nayo haikuwa inapatikana.”
“Lakini ulikuwa unajua kuwa ameenda Ujerumani?”
Akabinua mdomo. “Napo nilikuwa sijui.”
“Kwahiyo huku Ujerumani umekuja kufanya nini, Jolene?”
“Kwenye matembezi yangu tu. In fact, kuna ndugu yangu anaishi huku. Nimekuja kumsalimu.”
Akanywa juisi na kisha akaniuliza, “Vipi na wewe? Ni Mmarekani, sio?”
“Ndio.”
“Kwahiyo ndiyo uko na Britney huku?”
“Ndio. Nipo naye.”
“Unatokea wapi Marekani na unajihusisha na nini?”
“Mimi ni mwalimu High school! Natokea California.”
“Ulikutanaje na Britney? Hakuwahi kunambia kuhusu wewe.”
Nikatabasamu. “Nadhani kwasababu ulipotezana naye.”
Akapandisha mabega. “Labda!” kisha akaniuliza, “So mtakuwa huku kwa muda gani?”
“Si muda mrefu sana, tutarudi Marekani.”
“Ooh! Basi si mbaya kesho mkaja nyumbani kwetu. Kuna tafrija ya siku yangu ya kuzaliwa. Nadhani Britney atakuwa anakumbuka hilo.”
“Samahani, hatutaweza kuja.”
“Kwanini?”
“Kuna mahali tutaenda. Sidhani kama tutapata muda.”
Akamtazama Henessy kisha akarudisha uso wake kwangu. “Mnaenda Marekani, sio?”
“Hapana, si Marekani,” nikamjibu. “Ni hapahapa ndani ya Ujerumani.”
“Ndiyo mkose muda wa kuja kuniona? Kweli? Sidhani kama Britney atakuwa amenisahau na kutonijali kiasi hiko!”
Nikanyamaza nikikosa cha kumjibu. Nikanyanyua glasi ya juisi na kunywa fundo moja. Nikamwona yule mwanamke akifungua mkoba wake na kutoa simu. Akabonyeza kidogo na kuweka sikioni, “Njoo unichukue!” kisha akarejesha simu mkobani na kutoa bunduki! Akaninyooshea na kuniambia, “Ukifanya lolote la kipumbavu ntakugeuza mzoga!”

**
 
*NYUMA YAKO – 20*
*Simulizi za series*

ILIPOISHIA
Nikanyamaza nikikosa cha kumjibu. Nikanyanyua glasi ya juisi na kunywa fundo moja. Nikamwona yule mwanamke akifungua mkoba wake na kutoa simu. Akabonyeza kidogo na kuweka sikioni, “Njoo unichukue!” kisha akarejesha simu mkobani na kutoa bunduki! Akaninyooshea na kuniambia, “Ukifanya lolote la kipumbavu ntakugeuza mzoga!”
ENDELEA
“Nyoosha mikono juu!” akaniamuru. Nami nikatii ikiwemo pia na Henessy naye akanyoosha mikono yake juu. Na mwanamke huyo akiwa ameiminyia silaha mbavuni mwangu katika namna ambayo haionekani na mtu mwingine, akaniamuru nielekee nje ya eneo hilo kuelekea moja kwa moja kule lami.
Nikatii, tukatoka tukitembea kwa ukakamavu kuelekea huko. Tukiwa njiani mwanamke yule akawa anaangazaangaza huku na kule kuhakikisha usalama wake, nami kichwani mwangu nikifikiria namna gani ya kujichoropoa.
Tukasonga mpaka mahali ambapo kwa mahesabu tulikuwa tumebakiza umbali mfupi kufikia ule usafiri ambao mwanamke yule anatupelekea. Ghafla, nikiwa hata sijui kinachoelekea kutokea, Henessy akachoropoka toka kwenye mikono ya mwanamke yule mtekaji na kukimbilia miongoni mwa watu waliokuwa wamejaa huko ufukweni!!
Mwanamke yule, akiwa amechanganyikiwa, akamnyooshea bunduki Henessy, mara akapata fahamu kuwa hawezi kumfyatulia risasi hapo, basi akataka kurejesha bunduki kwangu, hapo nikakataa kwa kuudaka mkono wake kisha kuutegua kistadi, akaachia bunduki!
Nikamnyooshea na kumwamuru atulie kama maji mtungini. Nikamtaka anyooshe mikono yake juu na kisha twende kule alipokuwa anataka kunipeleka. Akatii.
Nikamwita Henessy na kumtaka akae mahali kuningojea, naja muda si mrefu. Naye akatii. Nikaongozana na mwanamke yule mpaka garini, Van nyeupe yenye vioo vyeusi. Hapo nikagonga mlango, punde ukafunguliwa na mwanaume mwenye kuvalia kapelo.
Nikamkaba vema mwanamke yule niliyekuja naye kisha bunduki nikamwelekezea yule jamaa mwenye kapelo. Tukazama ndani ya gari.
Swali la kwanza nikawauliza wametumwa na nani. Hapo nikiwa nimehakikisha kuwa uso wangu unaogofya.
“Hamna mtu aliyetutuma,” akasema yule jamaa. “Ni sisi wenyewe ndiyo tumekuja hapa.”
“Kufuata nini?”
Kabla jamaa hajanijibu akamtazama kwanza mwenzake. Hapo nikaongezea nguvu kwenye kumkaba mwanamke huyo mpaka kusikia akikoroma.
“Tulikuwa tumemfuata Henessy!” akaropoka jamaa. Nikamuuliza, “Mnamtakia nini na mumpeleke wapi?
Jamaa yule akanyamaza akiwa anantazama. Nikarudia kumuuliza swali langu, hakunijibu, badala yake akaniuliza, “Wewe ni ajenti wa CIA, sio?”
“Jibu nilichokuuliza!” nikamwamuru. Lakini hakuonyesha sura ya hofu, hata akatabasamu na kuendelea na maneno yake, “Hautafanikiwa kwenye hili,” akasema. “Una kazi ngumu sana, ajenti.”
“Nami ndizo hizo ngumu napenda!” nikamjibu kisha nikamfyatulia risasi kuparaza sikio lake la kushoto. Haraka akalidaka sikio lake hilo akilalama kwa maumivu makali! Yule mwanamke nikamgonga na kitako cha bunduki chini ya kisogo chake, akazirai!
Nikamfuata yule mwanaume na kumkwida shati, bado akiwa analalama kwa maumivu makali sikioni, nikamwamuru anijibu maswali yangu!
“Ajenti!” akaniita. “hata kama nikijibu maswali yako haitasaidia kitu.”
“Mambo ya kunisaidia au kutonisaidia nayajua mwenyewe. Nijibu kabla sijazibua sikio lako jingine!”
Bado akawa mgumu. Nikageuza kitako cha bunduki na kumtwanga nacho kwanguvu kwenye shina la pua. Akapiga kelele za maumivu akidaka pua yake ambayo ilikuwa inachuruza damu.
“Mmetumwa na nani?” nikafoka kumuuliza. Alikuwa analalama kwa maumivu mikono yake iliyoziba pua ikijawa na damu lakini bado akawa mbishi! Hakutaka kusema.
Nikabana mikono yake na kumkandika tena kitajo cha bunduki kwenye pua yake yenye maumivu. Damu zikamruka akilalamika kwa maumivu makali. Akalia sasa kama mtoto uso wake ukiwa umefunikwa na damu nyingi.
Nikarudia kumuuliza, “Mmetumwa na nani!”
Bado akawa hasemi. Akalia na kulia tu kwa maumivu anayoyapata. Basi nikamkamata tena mikono yake ili nikamndike tena pua. Hapa akapiga kelele kali, “nasema! Nasema!”
“Sema!” nikamkaripia.
“Tumetumwa na Adolfo!”
Hapa nikamkumbuka yule jamaa niliyemkamata na kumtesea kule hotelini. Kabla hajazirai alisema jina la Rodolfo. Ina maana ndiye huyu Adolfo? Nilipomuuliza huyu jamaa zaidi akasema ni Adolfo. Basi nilikuwa nimesikia vibaya toka kwa jamaa yule siku ile.
Ila Adolfo ni nani haswa? Na kwanini anatufuatilia? Nilipomuuliza hilo, akashindwa kujibu. Nadhani nilikuwa nimemkandika sana. Nilimwona amelegea. Na hatimaye akazirai macho yakiwa hayajafumba vema.
“Shit!” nikapiga dashboard. “Sasa nitapata wapi taarifa za Alfonso?”
Kwa muda kidogo nikapata kufikiri. Nilihitaji sana kumjua huyu Alfonso.

**

Nadhani ilikuwa imepita lisaa tangu tutoke ufukweni mimi na Henessy kwa kutumia van ya wale wavamizi waliokuja kututeka.
Tulipoenda ilikuwa mbali na mji, mbali na purukushani za watu, na huko nyuma ya gari tulikuwa tumewabebelea wale watu wawili, mwanamke na yule mwanaume ambao bado hawakuwa wamepata fahamu.
Basi tukiwa hapo, nikawa nateta na Henessy nikimdadisi kwa maswali kadhaa kadhaa juu yake na mama yake. Hapo ndiyo nikapata kujua kuwa hata alipokuwa kwenye mikono ya watekaji, yeye pamoja na mama yake, alikuwa akipewa simu acheze ‘game’ lakini kwa uangalizi maalumu.
Game alipendalo, Subway Surfers. Hata hapo aliniuliza kama simu yangu ina credit apate kulipakua toka mtandaoni.
Laiti kama wale watekaji wale wangelijua kuwa game hilo ndilo lilikuwa njia ya kuwapata, wasimgeruhusu Henessy ashike simu yao.
“Kuna muda nilikuwa naboreka sana,” alisema Henessy. “Ningekaa kwenye kona nikiwa sina raha, basi angekuja mmoja wao na kuniambia shika ucheze!”
Nikatabasamu nikimwangalia. Alikuwa mtoto mchangamfu na mwenye akili. Hakustahili kupitia yote haya. Kweli dunia haina usawa. Nilimfinya shavu lake nikimchekea kisha nikampatia simu yangu acheze game lake.
“Baba yako yuko wapi, Henessy?”
“Hayupo!” akanijibu akibofyabofya simu.
“Yuko wapi?”
Akapandisha mabega pasipo kunena jambo.
“Henessy, unamjua baba yako?”
“Ndio. Mama aliwahi kunionyesha picha zake.”
“Hujawahi kumwona kwa macho?”
“Aaahm!” akatulia kidogo. Kuna kitu kilikamata macho yake kwenye simu. Alipotulia akaendelea kunena, “Baba yangu ni mtu wa kusafiri sana. Anashinda muda mrefu akiwa kwenye ndege na kwenye mabasi, hivyo amekuwa akija nyakati za usiku nikiwa nimelala tayari. Mama huwa ananiambia.”
“Mara yako ya mwisho kumwona ilikuwa lini?” Akatulia kama hajanisikia. Alikuwa akitazama simu kwa umakini. Punde akanionyeshea kioo cha simu akiniambia, “ona alama zangu!” kisha akacheka. Nikamtazama nikitabasamu. Alikuwa anafurahia sana kile anachokitazama na kukicheza simuni, nikaona maongezi yetu hayatafika popote pale. Acha nimwache acheze baadae tutaongea.
Kidogo, nikasikia mtu akijigeuza garini. Kutazama nikamwona yule mwanamke akirejea fahamuni. Alipotazama vema akanikuta ni mbele yake nikimnyooshea mdomo wa bunduki. Sura nimekunja kibabe, na nikasema maneno machache kwa kumaanisha,
“Umeona kilichomtokea mwenzako?” akageuza shingo kutazama mwili wa mwenzake kando. “kitakutokea na wewe endapo utaleta ujuaji.”
Akakunja uso wake kwa hofu akisema, “mimi sijui kitu!”
Nikatabasamu kikebehi, “acha kunifanya mjinga. Kwahiyo ulitufuata kwa bahati?”
Nikamdaka mkono na kumvuta kumketisha kitako. Nikamwambia, “Mwanamke, sina mzaha na wewe. Ni aidha unambie ama nikulaze hoi. Chaguo ni lako!”
Macho yake yakajawa na machozi. “Nini unataka kufahamu toka kwangu?” akaniuliza.
“Kila kitu unachodhani nastahili kujua!”
“Mimi si rafiki yake Britney. Nilikuongopea tu.”
“Kwanini uliniongopea? Nani alikutuma?”
Akanionyeshea yule mwanaume aliyelala hajitambui pale kando.
“Kwanini alikutuma?”
“Sijui! Alinambie nimteke huyo mtoto.”
“Alafu?”
“Nimpatie!”
“Mlijuaje kama tupo pale ufukweni?”
“Tulikuona ukitokea ubalozini. Walikuwepo hapo wakijua utafika tu.”
“Wakina nani hao?”
“Huyu jamaa na wenzake! … mimi sihusiki. Kweli nakwambia!”
Nikamtazama kwa macho makali kwa sekunde tatu alafu nikamuuliza, “Alfonso ni nani?”
Alipotaka kusema hajui, kabla hajamalizia kauli yake, nikamkita na kitako cha bunduki pembeni ya jicho lake la kushoto, “Shenzi!”
Akalia kwa maumivu. Alivuja damu. Nikamdaka nywele zake kwanguvu na kumuuliza tena, “Alfonso ni nani?”

***
 
*NYUMA YAKO – 19*
*Simulizi za series*

ILIPOISHIA
Nilizama maana kina kilikuwa kirefu. Risasi zikatumwa kunifuata ndani ya maji, zikanipitia kupunyua, lakini kwakuwa maji yalikuwa na nguvu na mengi ya kutosha kunipeleka, yakaniepushia na balaa!
Yakanisomba kunisafirisha.
ENDELEA
Maji yalipotuama, tukiwa tumesafiri kwa kama robo saa, nikachoropoka toka mtoni kuitafuta barabara.
Haikuwa safari ndefu sana. Sidhani kama nilichukua zaidi ya dakika kumi, nikawa tayari nimefika kwenye lami ambapo niliomba msaada na upesi nikapatiwa. Nadhani ilikuwa ni sababu ya mtoto niliyekuwa nimembeba. Mama mmoja ambaye alikuwa anasafiri na mbwa wake, alisimamisha akiwa ananitazama kwa huruma kisha akaniuliza naelekea wapi kabla hajaniruhusu niingie ndani na kuendelea na safari.
Nikiwa ndani akawa ananidadisi nini kimenitokea, na kwasababu sikutaka kumsababishia taharuki, nikamlaghai kuwa tumepata ajali. Akanipeleka mpaka mjini kabisa na kuniacha hospitalini. Mtoto akatazamwa jeraha na kupatiwa dawa za kumsaidia dhidi ya maumivu na kumkausha jeraha.
Baada ya hapo nikatafuta mahali pa kupumzikia. Nikamlaza mtoto na mimi kufanya utaratibu wa chakula maana njaa nayo ilikuwa inauma. Kila kitu kilipokuwa sawa, nikajilaza kitandani nikiwa nawaza.
Mwanamke yule aliyefia mikononi mwangu, mtoto huyu ambaye yupo pembeni, watu wale waliokuwa wanatufukuza na mahusiano yao na Raisi! Nilihisi mambo yamechangamanaa sana.
Sikudhani kama msako wangu wa Raisi ungenisafirisha ukubwa huo. Nikanyanyua simu na kumpigia Jack Pyong kumweleza yote yaliyojiri. Naye akashangaa sana lakini lile la Britney likamshangaza zaidi. Akanisihi nimtumie picha za mwanamke huyo na kisha jina lake hilo la mwisho ambalo alilisema kabla hajafariki, yaani Juliette Simpson.
Nikafanya hivyo, akaniambia nimpatie muda kidog basi atanirejeshea majibu. Nikaendelea kujilaza kitandani. Kama baada ya dakika tano, mtoto yule akaamka akilalamikia maumivu makali kichwani.
Nikampatia dawa na kumhasa apumzike zaidi. Lakini kabla hajafanya hivyo, akaniuliza mama yake yupo wapi? Hapa nikapata kigugumizi.
“Unaitwa nani?”
“Henessy,” akanijibu akiwa ananitazama kwa kufinya macho.
“Henessy, Mama ametangulia Marekani. Marekani si ndo’ nyumbani?”
Akasita kisha akaniuliza, “Kwanini ameenda mwenyewe?” kisha macho yake yakalowana machozi. “Kwanini ameniacha?’
“Hajakuacha,” nikasema nikimkodolea macho. Nikamfuta machozi na kumpoza, “ilibidi atangulie kwenda huko maana ndege ilijaa. Nasi tutamfuata, usijali.”
Akan’tazama kwa maulizo. Akafuta machozi kwa mgongo wa kiganja chake kisha akaniuliza kwa sauti ya kubashiri, “Tutaenda lini?”
“Usijali, tutaenda. Kuna mambo kadhaa namalizia kama kesho ama keshokutwa. Sawa?” akatikisa kichwa kuafiki lakini kishingo upande. Kidogo simu yangu ikaita, alikuwa ni Jack Pyong, nikapokea akaanza kunambia nini amepata.
“Tony,” akaanza kwa kuniita jina. Sauti yake ilikuwa ya chini na msisitizo. Akanambia, “Huyo mdada ni mwigiza picha za ngono!”
“Yupi?”
“Huyo Juliette! Namaanisha Juliette Simpson!”
“Huyo niliyekutumia picha?”
“Acha basi kuniuliza maswali ya kijinga. Kwani tumetoka kuongelea nini hapa muda si mrefu?”
“Kuna mtu mwenye maujinga kama wewe?”
“Nitaacha kukwambia! Ohoo!”
“Sema basi. Unajua credit inaenda!”
“Sasa nikitaka kusema wewe unaanza mambo yako. Tulia kama unanyolewa.”
“Sawa, nimetulia. Kwahiyo unanambia—” kabla sijamalizia nikamtazama yule mtoto, sikutaka asikie. Nikasonga kando kidogo.
“…kwahiyo Juliette huyo ni pornstar?” Pornstar maanaye mcheza sinema za ngono.
“Ndio. Ni maarufu tu. Sikuwa najua hilo mpaka nilipoingia mtandaoni!”
“Sasa Jack, mcheza sinema za ngono atakuwa ana mahusiano gani na kupotea kwa Raisi?”
“Tony, hiyo ni kazi yako. Unanipachikia mimi sasa?”
“Sasa we fala, huko mtandaoni ulikuwa unafanya nini?”
“Nakutafutia huyo mtu wako. Ebu sikia, kesho kama nikipata muda nitaenda kwenye kampuni aliyokuwa anafanyia kazi. Pengine nitapata baadhi ya majibu. Baadae!”
Akakata simu na kuniachia maswali lukuki kichwani. Niliona mambo yanazidi kuwa magumu. Nikazama mtandaoni na kuandika jina la yule mwanamke, punde nikaona majibu ya ajabu. Kweli mwanamke yule alikuwa mcheza sinema za ngono.
Lakini kwa taarifa zaidi, alikuwa mstaafu! Lakini kwa kazi hii kuna mstaafu kweli ilhali video zake bado zipo hewani na watu wanaweza kuzipakua na kuzitazama?
Nilipofuatilia zaidi nikabaini na hiyo kampuni aliyokuwa akifanyia kazi. Kwa jina, LEXANDER PLEASURE ikiwa inasimamiwa na mwongozaji mwenye asili ya kilatini aitwaye jina la utani, Bomboclat!
Hapa sasa nikapata kujua kwanini mwanamke yule alishangaa nilipomwambia simfahamu. Huenda alidhani umaarufu wake kwenye michezo hiyo ungelinigusa hata mimi. Lakini pia nikafahamu kwanini alinipatia majina mawili, mosi Britney, pili Juliette. Ina maana Britney lilikuwa ni jina lake la uhalisia wakati Juliette Simpson likiwa ni la ‘kazini’.
Nikashusha pumzi ndefu nikimtazama yule mtoto. Nilikuwa nawaza kama atakuwa anajua kuwa mama yake huko mtandaoni yupo uchi. Nikajikuta natikisa kichwa kisha nikaanza kusuka tu mipango ya kurudi Marekani maana sikuwa na cha ziada cha kukifanya tena hapa Ujerumani.
Hivyo nikaona ni stara kufunga safari, kesho asubuhi na mapema, kwenda jiji la Berlin ambapo ndipo kuna ubalozi wa Marekani.
Siku hiyo nipumzike tu kwakweli. Nilikuwa nimechoka mno. Shurba nilizopitia zilikuwa zatosha kunifanya nijilaze.

**

Kesho yake …

Berlin, Ujerumani.

Nilitoka ndani ya balozi nikiwa na uhakika wa safari yangu jioni. Na kwakuwa nilijitambulisha na kuthibitisha humo ndani kuwa mimi ni ajenti wa CIA, basi mambo hayakuniwia sana ‘ugumu’.
Nikaongozana na Henessy mpaka mgahawani kujipatia chakula. Hapo tukakaa kwa muda wa kama nusu saa kabla hatujajiweka kwenye basi na kwenda mpaka beach. Nilitaka angalau nifurahie ujio wangu hapo Ujerumani japo ulikuwa ni wa kikazi.
Walau nipate muda wa ‘kuenjoy’ kabla sijaacha ardhi hiyo kurejea nyumbani. Nikiwa hapo nikapata nafasi ya kuzoezana na Henessy ambapo tulicheza na kufukuzana pamoja tukiwa tunapigwa na pepo ya bahari.
Tukiwa tumechoka, tukawa tunatembeatembea tu fukweni. Lakini kama baada ya hatua zetu kadhaa, paliongokea mwanamke mmoja ambaye amevalia ‘casual’. Uso wake ulikuwa umefichwa na miwani meusi na miguu yake imebanwa na jeans iliyopauka. Begani ananing’iniza mkoba mdogo uliobana kwapa lake.
Mwanamke huyo akiwa anapunga mkono wake na kutabasamu, aliita, “Heneessyy!” tukageuka wote kutazama. Alikuwa anatokea upande ilipo barabara kuu.
Nikamuuliza Henessy, “Unamjua huyo mwanamke?”
Henessy hakunijibu, badala yake akawa anamtazama kwa umakini mwanamke huyo pengine akumbuke kama alishawahi kumwona mahali. Hivyo kabla hajanipa majibu, mwanamke huyo, kwakuwa alikuwa anakimbia na kutembea kwa kasi, akawa ametufikia.
Akan’salimu kwa upesi, akitumia kiingereza, kisha akainama kumtazama Henessy akitabasamu. “Hujambo Henessy? … unaendeleaje muda wote huo?”
Henessy akamjibu lakini bado akiwa anamtazama kwa macho yaliyokaza. Nikamuuliza mwanamke huyo, “Tafadhali unaweza kujitambulisha?”
“Oow!” akasema akivua miwani yake. Macho yake yalikuwa ya paka yakiwa na uchangamfu ndani yake. Akatabasamu na kunipatia mkono, “Naitwa Jolene! Ni rafiki yake na Britney.”
“Oooh! Nimefurahi kukujua,” nikamjibu nisiongezee mengi. Akaniuliza, “na wewe? Wewe ni nani?”
“Naitwa Rodney. Ni rafiki pia wa Britney!”
Akaangaza kushoto na kulia. “Britney yupo wapi?”
“Hayupo. Hatujaja naye hapa!”
“Ooh! Yupo wapi kwa sasa. Ni muda sijawasiliana naye. Hata sasa imenichukua muda sana kumtambua Henessy!”
“Ni simulizi ndefu kidogo,” nikamjibu na kumwomba, “tunaweza tukapata dakika kadhaa za kuongea?”
Akaridhia baada ya kutazama saa yake ya mkononi. Tukasonga kwenda mahali fulani tulivu kwenye eneo hilohilo la ufukweni, hapo tukapata vinywaji laini na kupiga soga nikitaka kufahamu machache juu ya Britney lakini nikiwa nimemlaghai kuwa mimi na Britney ni mtu na mchumba wake. Tumekutana na akanieleza mambo kadhaa, ikiwamo kujihusisha na kucheza sinema za ngono.
Kwa kufanya hivyo nilitarajia kumpa mwanya mwanamke huyo wa kutonificha kitu. Kumtengenezea mazingira ya yeye kuwa huru kunielekza lolote maana hata lile ambalo lingeweza kuwa siri, mimi tayari nalifahamu.
“Umemjua Britney kwa muda gani?”
“Miaka mingi tu. Alikuwa ni rafiki yangu toka High school!”
“Kwahiyo ulikuwa unafahamu juu ya yeye kujihusisha na ile kazi?”
“Yah! Ni rafiki yangu, nitashindwaje kujua hilo?”
“Mlikuja kupotezana naye muda gani?”
“Aaahmm kama mwaka mmoja na nusu hivi uliopita.”
“Kwanini mkapotezana? Hakukuaga kama anakuja Ujerumani?”
“Hakunambia! Nilistaajabu amepotea. Simu yake nayo haikuwa inapatikana.”
“Lakini ulikuwa unajua kuwa ameenda Ujerumani?”
Akabinua mdomo. “Napo nilikuwa sijui.”
“Kwahiyo huku Ujerumani umekuja kufanya nini, Jolene?”
“Kwenye matembezi yangu tu. In fact, kuna ndugu yangu anaishi huku. Nimekuja kumsalimu.”
Akanywa juisi na kisha akaniuliza, “Vipi na wewe? Ni Mmarekani, sio?”
“Ndio.”
“Kwahiyo ndiyo uko na Britney huku?”
“Ndio. Nipo naye.”
“Unatokea wapi Marekani na unajihusisha na nini?”
“Mimi ni mwalimu High school! Natokea California.”
“Ulikutanaje na Britney? Hakuwahi kunambia kuhusu wewe.”
Nikatabasamu. “Nadhani kwasababu ulipotezana naye.”
Akapandisha mabega. “Labda!” kisha akaniuliza, “So mtakuwa huku kwa muda gani?”
“Si muda mrefu sana, tutarudi Marekani.”
“Ooh! Basi si mbaya kesho mkaja nyumbani kwetu. Kuna tafrija ya siku yangu ya kuzaliwa. Nadhani Britney atakuwa anakumbuka hilo.”
“Samahani, hatutaweza kuja.”
“Kwanini?”
“Kuna mahali tutaenda. Sidhani kama tutapata muda.”
Akamtazama Henessy kisha akarudisha uso wake kwangu. “Mnaenda Marekani, sio?”
“Hapana, si Marekani,” nikamjibu. “Ni hapahapa ndani ya Ujerumani.”
“Ndiyo mkose muda wa kuja kuniona? Kweli? Sidhani kama Britney atakuwa amenisahau na kutonijali kiasi hiko!”
Nikanyamaza nikikosa cha kumjibu. Nikanyanyua glasi ya juisi na kunywa fundo moja. Nikamwona yule mwanamke akifungua mkoba wake na kutoa simu. Akabonyeza kidogo na kuweka sikioni, “Njoo unichukue!” kisha akarejesha simu mkobani na kutoa bunduki! Akaninyooshea na kuniambia, “Ukifanya lolote la kipumbavu ntakugeuza mzoga!”

**
Oohoo nilihisi tu huyu sio mtu mzuri
 
*NYUMA YAKO – 20*
*Simulizi za series*

ILIPOISHIA
Nikanyamaza nikikosa cha kumjibu. Nikanyanyua glasi ya juisi na kunywa fundo moja. Nikamwona yule mwanamke akifungua mkoba wake na kutoa simu. Akabonyeza kidogo na kuweka sikioni, “Njoo unichukue!” kisha akarejesha simu mkobani na kutoa bunduki! Akaninyooshea na kuniambia, “Ukifanya lolote la kipumbavu ntakugeuza mzoga!”
ENDELEA
“Nyoosha mikono juu!” akaniamuru. Nami nikatii ikiwemo pia na Henessy naye akanyoosha mikono yake juu. Na mwanamke huyo akiwa ameiminyia silaha mbavuni mwangu katika namna ambayo haionekani na mtu mwingine, akaniamuru nielekee nje ya eneo hilo kuelekea moja kwa moja kule lami.
Nikatii, tukatoka tukitembea kwa ukakamavu kuelekea huko. Tukiwa njiani mwanamke yule akawa anaangazaangaza huku na kule kuhakikisha usalama wake, nami kichwani mwangu nikifikiria namna gani ya kujichoropoa.
Tukasonga mpaka mahali ambapo kwa mahesabu tulikuwa tumebakiza umbali mfupi kufikia ule usafiri ambao mwanamke yule anatupelekea. Ghafla, nikiwa hata sijui kinachoelekea kutokea, Henessy akachoropoka toka kwenye mikono ya mwanamke yule mtekaji na kukimbilia miongoni mwa watu waliokuwa wamejaa huko ufukweni!!
Mwanamke yule, akiwa amechanganyikiwa, akamnyooshea bunduki Henessy, mara akapata fahamu kuwa hawezi kumfyatulia risasi hapo, basi akataka kurejesha bunduki kwangu, hapo nikakataa kwa kuudaka mkono wake kisha kuutegua kistadi, akaachia bunduki!
Nikamnyooshea na kumwamuru atulie kama maji mtungini. Nikamtaka anyooshe mikono yake juu na kisha twende kule alipokuwa anataka kunipeleka. Akatii.
Nikamwita Henessy na kumtaka akae mahali kuningojea, naja muda si mrefu. Naye akatii. Nikaongozana na mwanamke yule mpaka garini, Van nyeupe yenye vioo vyeusi. Hapo nikagonga mlango, punde ukafunguliwa na mwanaume mwenye kuvalia kapelo.
Nikamkaba vema mwanamke yule niliyekuja naye kisha bunduki nikamwelekezea yule jamaa mwenye kapelo. Tukazama ndani ya gari.
Swali la kwanza nikawauliza wametumwa na nani. Hapo nikiwa nimehakikisha kuwa uso wangu unaogofya.
“Hamna mtu aliyetutuma,” akasema yule jamaa. “Ni sisi wenyewe ndiyo tumekuja hapa.”
“Kufuata nini?”
Kabla jamaa hajanijibu akamtazama kwanza mwenzake. Hapo nikaongezea nguvu kwenye kumkaba mwanamke huyo mpaka kusikia akikoroma.
“Tulikuwa tumemfuata Henessy!” akaropoka jamaa. Nikamuuliza, “Mnamtakia nini na mumpeleke wapi?
Jamaa yule akanyamaza akiwa anantazama. Nikarudia kumuuliza swali langu, hakunijibu, badala yake akaniuliza, “Wewe ni ajenti wa CIA, sio?”
“Jibu nilichokuuliza!” nikamwamuru. Lakini hakuonyesha sura ya hofu, hata akatabasamu na kuendelea na maneno yake, “Hautafanikiwa kwenye hili,” akasema. “Una kazi ngumu sana, ajenti.”
“Nami ndizo hizo ngumu napenda!” nikamjibu kisha nikamfyatulia risasi kuparaza sikio lake la kushoto. Haraka akalidaka sikio lake hilo akilalama kwa maumivu makali! Yule mwanamke nikamgonga na kitako cha bunduki chini ya kisogo chake, akazirai!
Nikamfuata yule mwanaume na kumkwida shati, bado akiwa analalama kwa maumivu makali sikioni, nikamwamuru anijibu maswali yangu!
“Ajenti!” akaniita. “hata kama nikijibu maswali yako haitasaidia kitu.”
“Mambo ya kunisaidia au kutonisaidia nayajua mwenyewe. Nijibu kabla sijazibua sikio lako jingine!”
Bado akawa mgumu. Nikageuza kitako cha bunduki na kumtwanga nacho kwanguvu kwenye shina la pua. Akapiga kelele za maumivu akidaka pua yake ambayo ilikuwa inachuruza damu.
“Mmetumwa na nani?” nikafoka kumuuliza. Alikuwa analalama kwa maumivu mikono yake iliyoziba pua ikijawa na damu lakini bado akawa mbishi! Hakutaka kusema.
Nikabana mikono yake na kumkandika tena kitajo cha bunduki kwenye pua yake yenye maumivu. Damu zikamruka akilalamika kwa maumivu makali. Akalia sasa kama mtoto uso wake ukiwa umefunikwa na damu nyingi.
Nikarudia kumuuliza, “Mmetumwa na nani!”
Bado akawa hasemi. Akalia na kulia tu kwa maumivu anayoyapata. Basi nikamkamata tena mikono yake ili nikamndike tena pua. Hapa akapiga kelele kali, “nasema! Nasema!”
“Sema!” nikamkaripia.
“Tumetumwa na Adolfo!”
Hapa nikamkumbuka yule jamaa niliyemkamata na kumtesea kule hotelini. Kabla hajazirai alisema jina la Rodolfo. Ina maana ndiye huyu Adolfo? Nilipomuuliza huyu jamaa zaidi akasema ni Adolfo. Basi nilikuwa nimesikia vibaya toka kwa jamaa yule siku ile.
Ila Adolfo ni nani haswa? Na kwanini anatufuatilia? Nilipomuuliza hilo, akashindwa kujibu. Nadhani nilikuwa nimemkandika sana. Nilimwona amelegea. Na hatimaye akazirai macho yakiwa hayajafumba vema.
“Shit!” nikapiga dashboard. “Sasa nitapata wapi taarifa za Alfonso?”
Kwa muda kidogo nikapata kufikiri. Nilihitaji sana kumjua huyu Alfonso.

**

Nadhani ilikuwa imepita lisaa tangu tutoke ufukweni mimi na Henessy kwa kutumia van ya wale wavamizi waliokuja kututeka.
Tulipoenda ilikuwa mbali na mji, mbali na purukushani za watu, na huko nyuma ya gari tulikuwa tumewabebelea wale watu wawili, mwanamke na yule mwanaume ambao bado hawakuwa wamepata fahamu.
Basi tukiwa hapo, nikawa nateta na Henessy nikimdadisi kwa maswali kadhaa kadhaa juu yake na mama yake. Hapo ndiyo nikapata kujua kuwa hata alipokuwa kwenye mikono ya watekaji, yeye pamoja na mama yake, alikuwa akipewa simu acheze ‘game’ lakini kwa uangalizi maalumu.
Game alipendalo, Subway Surfers. Hata hapo aliniuliza kama simu yangu ina credit apate kulipakua toka mtandaoni.
Laiti kama wale watekaji wale wangelijua kuwa game hilo ndilo lilikuwa njia ya kuwapata, wasimgeruhusu Henessy ashike simu yao.
“Kuna muda nilikuwa naboreka sana,” alisema Henessy. “Ningekaa kwenye kona nikiwa sina raha, basi angekuja mmoja wao na kuniambia shika ucheze!”
Nikatabasamu nikimwangalia. Alikuwa mtoto mchangamfu na mwenye akili. Hakustahili kupitia yote haya. Kweli dunia haina usawa. Nilimfinya shavu lake nikimchekea kisha nikampatia simu yangu acheze game lake.
“Baba yako yuko wapi, Henessy?”
“Hayupo!” akanijibu akibofyabofya simu.
“Yuko wapi?”
Akapandisha mabega pasipo kunena jambo.
“Henessy, unamjua baba yako?”
“Ndio. Mama aliwahi kunionyesha picha zake.”
“Hujawahi kumwona kwa macho?”
“Aaahm!” akatulia kidogo. Kuna kitu kilikamata macho yake kwenye simu. Alipotulia akaendelea kunena, “Baba yangu ni mtu wa kusafiri sana. Anashinda muda mrefu akiwa kwenye ndege na kwenye mabasi, hivyo amekuwa akija nyakati za usiku nikiwa nimelala tayari. Mama huwa ananiambia.”
“Mara yako ya mwisho kumwona ilikuwa lini?” Akatulia kama hajanisikia. Alikuwa akitazama simu kwa umakini. Punde akanionyeshea kioo cha simu akiniambia, “ona alama zangu!” kisha akacheka. Nikamtazama nikitabasamu. Alikuwa anafurahia sana kile anachokitazama na kukicheza simuni, nikaona maongezi yetu hayatafika popote pale. Acha nimwache acheze baadae tutaongea.
Kidogo, nikasikia mtu akijigeuza garini. Kutazama nikamwona yule mwanamke akirejea fahamuni. Alipotazama vema akanikuta ni mbele yake nikimnyooshea mdomo wa bunduki. Sura nimekunja kibabe, na nikasema maneno machache kwa kumaanisha,
“Umeona kilichomtokea mwenzako?” akageuza shingo kutazama mwili wa mwenzake kando. “kitakutokea na wewe endapo utaleta ujuaji.”
Akakunja uso wake kwa hofu akisema, “mimi sijui kitu!”
Nikatabasamu kikebehi, “acha kunifanya mjinga. Kwahiyo ulitufuata kwa bahati?”
Nikamdaka mkono na kumvuta kumketisha kitako. Nikamwambia, “Mwanamke, sina mzaha na wewe. Ni aidha unambie ama nikulaze hoi. Chaguo ni lako!”
Macho yake yakajawa na machozi. “Nini unataka kufahamu toka kwangu?” akaniuliza.
“Kila kitu unachodhani nastahili kujua!”
“Mimi si rafiki yake Britney. Nilikuongopea tu.”
“Kwanini uliniongopea? Nani alikutuma?”
Akanionyeshea yule mwanaume aliyelala hajitambui pale kando.
“Kwanini alikutuma?”
“Sijui! Alinambie nimteke huyo mtoto.”
“Alafu?”
“Nimpatie!”
“Mlijuaje kama tupo pale ufukweni?”
“Tulikuona ukitokea ubalozini. Walikuwepo hapo wakijua utafika tu.”
“Wakina nani hao?”
“Huyu jamaa na wenzake! … mimi sihusiki. Kweli nakwambia!”
Nikamtazama kwa macho makali kwa sekunde tatu alafu nikamuuliza, “Alfonso ni nani?”
Alipotaka kusema hajui, kabla hajamalizia kauli yake, nikamkita na kitako cha bunduki pembeni ya jicho lake la kushoto, “Shenzi!”
Akalia kwa maumivu. Alivuja damu. Nikamdaka nywele zake kwanguvu na kumuuliza tena, “Alfonso ni nani?”

***
mdogo mdogo we,, tutaimsliza tu
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom