Nyuma yako - Riwaya ya SteveMollel

*NYUMA YAKO – 16*
*Simulizi za series*

ILIPOISHIA
Nikiwa nimekaa huko nikawa nawaza sana kichwani mwangu, mtoto huyo atakuwa anafanya nini huko Black Forest?
Yupo mwenyewe au na mama yake?
Je wapo wenyewe au na watu wengine?
ENDELEA
Basi mawazo hayo yakanifanya nisisinzie ndani ya basi nikawa natazama dirishani na muda mwingine mlangoni pale ambapo basi lilikuwa linasimama.
Tulipotembea kwa muda wa kama lisaa limoja, basi likasimama nasi, watu ndani ya basi, tukapata wasaa wa kununua vitu vya kuchangamsha kinywa na kujaza matumbo kisha safari ikaendelea.
Hapo tukatembea kwa lisaa limoja tena tukawa tumefika Black Forest. Nikashuka na nikiwa natazama simu yangu nikaanza kusonga.
Haki ulikuwa ni msitu mkubwa sana. Sikujua kwanini uliitwa Black Forest, yaani msitu mweusi, na kwa muda huo bado sikuwa najua kwanini msitu huo ni maarufu nchini Ujerumani.
Ulikuwa umeota mgongoni mwa safu ya milima. Hapa kukiwa kimya na kwa mtu mwenye woga akikaa mbali aogope hata kukatiza.
Basi kwakuwa maelekezo ya kwenye simu nilishayameza, nikaweka simu mfukoni na kuendelea kuzama msituni. Nikatembea kwa kama kilomita moja na nusu, bado milima tu ilikuwa imenizingira, mbele na nyuma yangu kwa sana.
Nilipomaliza kilometa mbili, kwa mahesabu ya harakaharaka, nikaanza kujiuliza kama kweli nitakuwa nimefuata maelekezo ninayotakiwa kwani sikuwa naona alama wala ishara yoyote ya binadamu.
Nikatoa simu yangu mfukoni nitazame. Nilikuwa sahihi. Nikairejesha na kuendelea kukwea. Kidogo kwa umbali, nikaona kijumba cha rangi nyeupe. Kilikuwa ni kijumba pweke maana kikipakana na miti pekee.
Basi nikazidi kusonga na kusonga, nikiwa naamini sasa kile kijumba ndipo mahali ninapotakiwa kufika. Na niliposonga zaidi na zaidi nikagundua kuwa kile hakikuwa kijumba bali nyumba, ni unbali tu ndio ulikuwa unafanya paonekane padogo.
Lakini … nikapata maswali. Mtoto yule atakuwa anafanya nini huku msituni kwenye nyumba ile? Na kama yupo na mama yake, kwanini wanaishi huku? Mbali kabisa na dunia?
Mawazo haya yakanipa hoja niliyotokea kuiamini. Kuna kitu hakipo sawa. Na hivyo natakiwa kubeba kila aina ya tahadhari ninapoelekea kwenye nyumba hiyo.
Niliposonga, nikiwa nimebakiza umbali wa kama robo kilometa kuikuta ile nyumba, nikatulia na kuitazama vema kuikagua. Nilipokuwa nimekaa palikuwa ni eneo la juu kidogo hivyo palinipa fursa ya kutazama vema.
Kwa usalama zaidi nikalala chini na nikatenga dakika kama kumi za kukagua eneo hilo kabla ya kupasogelea zaidi.
Basi nikiwa hapo, nikatulia tuli sana. Palikuwa ni eneo tulivu mno ukiondoa upepo usukumao matawi ya miti.
Ikiwa kama imepita dakika tano tangu nilale hapo, nikastaajabu kichwa changu kikisukumizwa na kitu kigumu kisha sauti ya kijerumani ikaniamuru, “Tulia hivyo hivyo!”
Nami nikatii nikiamini kuwa mtu huyo amenishikia bunduki.
Akaniuliza mimi ni nani na hapo nafanya nini, tena akiwa ananisisitizia nisigeuke kumtazama. Kwa taratibu nikamjibu mimi ni mtalii na nalishangaa kuona nyumba hiyo msituni.
Akaniamuru nisimame nikiwa nimenyoosha mikono juu. Nikatii. Bado nikiwa simtazami. Akanipekua upesi kwa mikono, akahisi nina silaha. Akaichomoa, ilikuwa ni bunduki yangu. Hapo ndiyo nikaona akitupa mti kando na kutumia silaha yangu kuniwekea kichwani!
Kumbe hata silaha hakuwa nayo.
Sasa akaniamuru nigeuke. Nilipofanya hivyo nikakutana na mwanaume aliyevalia hovyo, ndevu nyingi na kofia ya soksi nzito kichwani. Mkononi mwake alikuwa amebebelea tunda, papai, akila kana kwamba sokwe mtu.
Akaniuliza, “unataka kufa?”
Sikumjibu. Akarudia tena swali lake, “Unataka kufa?”
“Hapana!” nikamjibu, asiniongeleshe kitu akashika njia kwenda zake. Alipopiga hatua tatu akanigeukia na kunambia, “kama hutaki kufa, nifuate!”
Basi mimi nikamfuata. Njiani nikamuuliza yeye ni nani na anafanya nini humo msituni. Hakunijibu. Alikuwa kimya akiwa anakula tunda lake ambalo halijamenywa!
Baada ya kama dakika kumi za kutembea, tukafika mbele ya kijumba dhoofu, kimesanifiwa kwa magogo na majani. Humo akazama ndani na kunitaka mimi nikae pale nje. Kidogo akatoka akiwa amebebelea kikombe cha bati ambacho sikujua mule ndani ameweka nini. Akawa anakunywa.
Akanitazama kana kwamba ndo’ mara ya kwanza ananiona alafu akaniuliza, “wewe ni nani?”
“Nishakwambia hapo awali,” nikamjibu. Akakunja uso na kuuliza, “muda gani? Nimekutana na wewe popote pale?”
Nikastaajabu. Nikadhani ananifanyia utani.
“… hata silaha yangu umechukua wewe!” nikamweleza. Akajitazama na kujikuta na bunduki. Haraka akanirushia akinitazama kwa mashaka. Hapa nikafahamu na kuthibitisha kuwa mtu huyu hakuwa sawa.
Nikamweleza mimi naitwa Jerry na nilikuwa nataka kufahamu juu ya nyumba ile iliyopweke msituni!
“Nyumba ipi hiyo?” akaniuliza akiwa ameweka kituo kutafuna.
“Ile ambayo ulinikuta naitazama,” nikamjibu. Akan’tazama kwa mashaka kisha akaniuliza, “ipi hiyo?”
Nikaona isiwe tabu nikamwelekeza. Ajabu alikuwa anaifahamu. Kumbe bwana huyu ana tatizo la kupoteza kumbukumbu za karibu. Alipojua ninachokiongelea, akaendelea kutafuna kisha muda si mrefu akaniuliza, “Una biashara gani hapo?”
“Nataka tu kujua,” nikamjibu na kuongezea, “Ni wakina nani wanaishi hapo?”
“Sijui nani anaishi hapo!” bwana yule akan’jibu. Kabla sijaongea, akaendelea, “Huwa naona watu kadhaa hapo. Sijui nani anapaishi?”
“Unaweza kunambia watu hao ni wa aina gani? Yaani wapoje?”
“Wapo kama wewe!”
“Kivipi? Namaanisha mwonekano wao? …” nikamwona akifikiria pasipo malengo. Nikamkatisha kwa kumuuliza, “Vipi, ushawahi kumwona mtoto hapo? Mvulana mwenye nywel nyekundu?”
Akanitikisia kichwa kukataa.
“Na je mwanamke? Hujawahi mwona mwanamke hapo?”
Akanitikisia tena kichwa akibetua mdomo. Alafu akang’ata tunda lake na kutafuna.

**

Baada ya dakika nane …

“shhhiiii!” nikamwonya yule jamaa yangu mwehu niliyemkuta ndani ya msitu. Alikuwa nyuma yangu wakati mimi nikiwa nimejibanza mtini natazama nyumba ninayotaka kuelekea.
Nilipomwonya hivyo, akafunga mdomo wake, nami nikarusha macho yangu kutazama ile nyumba ambayo kwa muda huo ilikuwa ipo kama hatua kumi na mbili tu tokea tulipo. Bado palikuwa kimya. Ni kama vile hakukuwa na mtu hapo.
Nami nilikuwa nimevalia mavazi ya hovyo sana kama mtu yule niliyeongozana naye. Nilimwomba mavazi yake ili basi yakanisaidie pale mambo yatakapokuwa yamenielemea.
Nilipoona ni kimya tu, nikatoka hapo mtini nikiwa nimemwelekeza yule jamaa wangu abakie hapohapo mtini nami nitarejea. Nikaelekea mbele kabisa ya ile nyumba na kujifanya nikiimba wimbo ambao hata siujui na huku nikitazamatazama huku na huko na kuokotaokota vitu vya ajabu.
Punde akatoka mwanaume mmoja aliyekuwa amevalia sweta nyeusi inayokaba koo na suruali jeans ya bluu mpauko. Mkononi alikuwa na bunduki ndogo. Akan’tazama na kuniuliza kwa amri, “wewe nani?” Alikuwa anatumia lugha ya kijerumani.
“Mimi Jerry!” nikamjibu, kisha nikampuuzia na kuendelea kuokotaokota vitu. Akapaza sauti, “hey! Sikia!” nikamtazana.
“Hapa si mahali pa kuchezeachezea, sawa? … potea!”
Kabla sijasema kitu, yule jamaa wangu niliyemwacha mtini akatoka na kupaza sauti akiuliza, “Ninyi! Mnafanya nini hapo?”
Nikamwona yule jamaa aliyetoka ndani ya nyumba akishikwa na tahadhari. Akaikamata silaha yake vema akiwa amekunja sura. Mara akaninyooshea na kuniuliza. “mnafanya nini hapa?”
Yule jamaa kule pembezoni mwa mti akapaza sauti, “muue huyo! Kwanza amevalia nguo zangu! Sijui kazitoa wapi?”
Yaani alikuwa ameshasahau kuwa yeye ndo’ kanipa!
Nikamtazama kwa kushangaa lakini huku nikijipapasa kufuata silaha yangu. “Phili, unasemaje?” nikamtunga jina upesi. Kabla jamaa yule hajajibu, nikawa nimeshapata silaha yangu kiunoni, nikaichomoa upesi na kumwonyeshea yule jamaa aliyetoka ndani ya nyumba.
“Weka silaha chini!” nikamwamuru. Akawa mbishi. Naye alikuwa ameninyooshea bunduki akiwa amen’tolea macho.
“Siweki, weka wewe!”
Nikamwambia, “unajua sisi tuko wawili. Unadhani yule ni chizi sio?”
Akageuza shingo yake kumtazaama yule jamaa wangu kule pembeni ya mti. Jamaa akatabasamu kama mdoli.
“pale ana silaha, anasubiri nimpe amri tu. Usiwe mjinga, weka silaha chini nyoosha mikono juu!” nikamsihi. Akafikiri kidogo.
“Wewe ni nani?” akaniuliza. “Muamerika?”
Sikumjibu.
“Hautatoka ndani ya msitu huu salama. Hata kama ukiniua.” Akasema akinitikisia kichwa. Mimi nikaendelea kumsihi, “weka silaha chini! Mara hii sitaongea tena, sina muda wa kupoteza!”
Basi akatii amri yangu baada ya kun’tazama kwa sekunde tatu.

***
 
*NYUMA YAKO – 17*
*Simulizi za series*

ILIPOISHIA
Sikumjibu.
“Hautatoka ndani ya msitu huu salama. Hata kama ukiniua.” Akasema akinitikisia kichwa. Mimi nikaendelea kumsihi, “weka silaha chini! Mara hii sitaongea tena, sina muda wa kupoteza!”
Basi akatii amri yangu baada ya kun’tazama kwa sekunde tatu.
ENDELEA
Nikazama naye ndani nikiwa nimemwekea bunduki kichwani. Sebuleni nikawakuta wanaume wawili ambao nikawaamuru waweke silaha chini la sivyo nitammaliza mwenzao. Ajabu wakatii. Nikasonga kidogo na kumwamuru mmoja wao akafungue milango, nipate kuona yaliyondani.
Wakati anafanya hivyo nikawa nawataza kiumakini wasifanye jambo lolote. Ndani ya chumba cha kwanza nikampata mtoto na mama yake. Mtoto yule ambaye nilishaambiwa na Jack Pyong.
Nikawaamuru wasonge mbele na kwa tahadhari nikawafyatulia risasi wale wanaume watatu miguuni washindwe kunifukuza nitakapotoka hapo kisha nikamwamuru yule mtoto ambaye nimemtoa humo ndani aziokote silaha na kunipatia. Baada ya hapo tukatoka ndani na kuzama msituni, hamaki yule bwana mwehu naye akaungana na sisi. Tukawa tunakimbia.
Sikujua tunaelekea wapi, ila nilitaka tu twende mbali na lile eneo kwa usalama wetu. Lakini tukiwa tunasonga, kidogo yule mama, mama ambaye nimetoka kumwokoa kwenye mikono ya wale wadhalimu, akanishauri tuelekee upande wetu wa mashariki.
Nami pasipo kubisha, maana sikuwa na huo muda, tukaongoza kwenda huko tukiwa tunakimbia. Kidogo, tukasikia sauti za pikipiki nyuma yetu. Tulipogeuka na kuangaza hatukuziona. Zilikuwa mbali ila kiuhakika zikija uelekeo wetu.
Tukakazana kukimbia, na kama baada ya dakika mbili, sasa tukaanza kuona pikipiki zikija kwa kasi nyuma yetu. Zilikuwa tatu kwa idadi. Kila moja ikiwa imebebelea watu wawili wawili, wa nyuma akiwa amebebelea bunduki!
Nikapaza sauti, “kimbiaa! Kimbia!” lakini ni wazi tusingeweza kimbia zaidi ya kasi ya pikipiki. Na nilihofia endapo watu wale wangeanza kufyatua risasi ingetuwia vigumu kupona.
Kweli, risasi zikaanza kurushwa kwa fujo! Zikapasua na kutoboa miti huku zikitupunyua na kupita kando za masikio yetu. Kidogo, yule jamaa mwehu tuliyekuwa tunaongozana naye, akabamizwa risasi ya mgongo! Niliona damu zikowa zinaruka kama vumbi, na mara akadondoka chini!
Ulishawahi mwona farasi akidondoka ingali yu kwenye kasi? Namna anavojikita na kujivunjavunja? Naam ndivyo ilivyokuwa kwa bwana huyu. Alidondoka vibaya mno, nahisi alivunjika vibaya sana haswa uti wake wa mgongo na shingo.
Nilitamani sana kumtazama kwa kujali lakini sikuwa naweza maana kufanya hivyo kungekuwa ni kutaka kifo. Nikaendelea kukimbia pamoja na wale niliowaokoa, lakini sasa mambo yakiwa magumu zaidi. Niligundua risasi zote zilikuwa zimenielekea mimi, kuniangusha chini, kwani zilinipita pembeni ama kupasua miti niliyokuwa nayo karibu, na hatimaye moja ikan’tifua begani!
Bahati haikunipasua mfupa, bali ilizama kwenye nyama na kunifanya nivuje damu kwa wingi. Vitu vingine ni kama bahati tu. Muda mwingine Mungu humsaidia mja wake pale anapokuwa anatenda lile lililojema, huwa naamini hivyo. Kuna muda niligeuka kutazama nyuma na kumbe muda huohuo risasi ilitupwa kunipasua kichwa, hivyo kugeuka kwangu kukawa kumeniokoa!
Risasi ikaparasa shavuni kwa upesi na kwenda kukomea mtini! … pah! Hata nikatahamaki.
Ila nilikuja kujifunza kuwa, watu wale waliokuwa wanatukimbiza walikuwa wamedhamiria kunimaliza mimi na si yule mwanamke na mtoto. Niliona wao wakiwa hawalengwi wala kudhamiriwa. Risasi hazikuwa zikiwapunyua na kuwawinda bali mimi na yule jamaa yangu ambaye tayari ameshalambishwa vumbi!
Basi kujua hilo, nikaanza kujisogeza kwa yule mwanamke na mtoto mpaka kujiweka mbele yao ingali sijui wapi tunapoelekea. Kwa kufanya hivyo, ghafla risasi zikakoma kurushwa. Kumbe nilikuwa sahihi!
“Usifyatue! Usifyatue!” nilisikia sauti ikiamuru kwa kijerumani. Hapa ndiyo nikajua na kuthibitisha kumbe wale mateka bado walikuwa wa thamani kwa wale wadhalimu. Bado walikuwa wanawahitaji na hiyo ni kumaanisha bado kuna kazi hawajaimalizia.
Lakini kukaa huku mbele ya mateka kusingelidumu kwa muda! Pikipiki zilikuwa zinakuja kwa kasi nyuma yetu na sasa ungeweza kusema kwamba, baada ya kama dakika moja tu, tutakuwa tumeshafikiwa na kunyakuliwa!
Kwahiyo basi hapa ilinilazimu kutafuta namna ya kutuweka salama. Nikachomoa bunduki mbili toka kiunoni mwangu na kuanza kuwatupia risasi wale waliokuwa wanatukimbiza. Kwa kufanya hivyo wakapunguza kasi na hata kuzubaa kwa kujikinga dhidi ya risasi!
Na kumbuka wao walikuwa hawawezi tena kunitupia risasi kwakuwa najifichia kwa watu wasiotaka kuwaua.
Nikawadungua watatu, wawili walikuwa madereva, mmoja akiwa abiria. Nikawa nimebakiza pikipiki moja. Nayo baada ya kusonga karibu zaidi, nikamfyatulia dereva risasi, akaikwepa na kumpata abiria wake. Akadondoka chini dereva akiendelea kutufuata.
Basi baada ya kuona amebakia mmoja, tena dereva ambaye alikuwa ameweka nguvu zake kwenye usukani, nikasimama na kumweka vema kwenye rada alafu nikamfyatulia risasi mbili kwa wakati moja, nikapasua mabega yake na kumfanya achie usukani! Kabla hajadondoka chini, nikamtupia tena risasi nyingine, ikatoboa kofia yake ngumu na kumpasua kichwa, akajifia.
Basi mimi nikarudi nyuma, nikawamalizia wale wengine walioko chini kwa mbali, kisha nikachukua pikipiki ya yule aliyekuwa mbele kabisa, niliyetoka kumuua punde, kisha nikambeba yule mwanamke na mwanaye na kutimka kwa kasi!
Nikaendesha pikipiki hiyo kana kwamba nacheza mchezo wa kwenye kompyuta ama simu. Nilikwepa miti kama mchezo huku nikisababisha hofu kubwa kwa wale niliowapakia. Walikuwa wakipiga yowe na kunisihi nipunguze kasi lakini sikuwaskiza kwani nilikuwa najua ninachofanya. Nilitaka kuumaliza msitu huu angalau niikute lami na kunyoosha nayo.
Kidogo tena tukasikia sauti za pikipiki zatujia. Nikaongeza kasi zaidi, punde tu, tukafika mpakani! Hapa tulikuwa tumesimama juu ya korongo, na huko chini, kama mita mia tano, kukiwa na mto mkubwa wenye maji ya kasi!
Nikakunja kona na kuanza kuambaa ambaa na hili korongo kwenda upande ambao mto unaelekea. Kama dakika tatu, kwa nyuma, wakatokea watu waliokuwa juu ya pikipiki sita! Wakawa wanatukimbiza kwa kasi sana, kasi zaidi ya pikipiki yetu.
Na kidogo tu, wakaanza kutupa risasi kwa fujo. Hawakuwa wanalenga watu bali pikipiki, nadhani lengo lao lilikuwa ni kupasua matairi ama kutusababishia ajali watukamate. Nilijitahidi kuiyumbisha pikipiki kuwakwepa ila napo nikaona kuna hatari ya kuwabwaga abiria.
Nikaendelea kukazana na mwendokasi. Lakini napo nisifike mbali, mbele yetu tukaona watu wakiwa wamesimama, watano kwa idadi, wakiwa wameziba njia na pikipiki zao. Mikononi wamebebelea bunduki na wamezielekezea upande wetu!
Hapo nikamsikia yule mwanamke niliyembeba akisema, “tunakufa!” naye mtoto wake akadakia kwa kusema vivyo hivyo, “tunakufa!” Mimi nikawaambia, “nishikeni kwanguvu!”
Kisha nikaminya mafuta na kuelekezea pikipiki korongoni! Tukashika ardhi kwa muda mdogo tu kabla pikipiki haijapaa hewani kwa muda wa kama dakika moja na kisha kutumbukia kwenye maji!
Waaah!!

**
Nilipoyazidi nguvu maji, nikatoa kichwa changu na kutafuta watu niliozama nao. Sikuwaona! Si kwamba maji hayakuwa na nguvu, hapana, bali angalau niliweza kuyamudu tofauti na mwanzoni tulipozama, yalikuwa na nguvu mno!
Nilitazama kushoto na kulia, bado tulikuwa ndani ya msitu, na bado sikuwa nawaona ‘watu wangu’. Nilipiga mbizi nikijitahidi kwa nguvu kuelekea maji yanapotokea, ila kidogo nikasikia sauti ya kike toka nyuma yangu, “msaada!”
Nilipopinda shingo kutazama, nikamwona yule mwanamke akipambana kumsaidia mwanaye. Lakini maji yakimzidi nguvu, akizama na kunyanyuka na kunywa maji!
Basi upesi nikarudi na kumfikia. Nikamnyakua mtoto na kumtaka anishike wakati mimi nikiwa natumia mkono wangu mmoja kupiga mbizi twende pakavu. Mtoto hakuwa ana ufahamu. Kichwa chake kilikuwa kinavuja damu.
Tulipofika pakavu, nikamtazama mtoto na kubaini alikuwa amejigonga kwenye jiwe ingali tu mtoni. Na kwa namna alivyokuwa anatoka damu, inabidi ifanyike namna upesi ya kumsaidia, la sivyo alikuwa anatuacha!
Nikamwambia mama yake, “gandamizia mahali pa jeraha, nakuja!” mimi nikaenda kutafuta majani yatakayoweza kumsaidia jerahani.

***
 
*NYUMA YAKO – 18*
*Simulizi za series*

ILIPOISHIA
Tulipofika pakavu, nikamtazama mtoto na kubaini alikuwa amejigonga kwenye jiwe ingali tu mtoni. Na kwa namna alivyokuwa anatoka damu, inabidi ifanyike namna upesi ya kumsaidia, la sivyo alikuwa anatuacha!
Nikamwambia mama yake, “gandamizia mahali pa jeraha, nakuja!” mimi nikaenda kutafuta majani yatakayoweza kumsaidia jerahani.
ENDELEA
Nilifahamu ndani ya msitu ule sitakosa ninachotaka. Nikakimbia upesi na kufanya jitihada za kuangaza macho yangu nikitumia stadi niliyonayo juu ya madawa ya asili. Tulifunzwa hii. Tulifunzwa namna ya kudumu na kumudu kwenye hali mbalimbali kama hizi.
Ndani ya muda mfupi, nikapata kuona kichaka chenye majani membamba na ncha kana kwamba sindano. Nikajongea hapo na kuchuma majani kadhaa na kuyatia mdomoni kutafuna alafu nikaanza kurudi upesi kule kwa yule mwanamama na mwanaye.
Nilipofika majani mdomoni mwangu yalikuwa tayari yashalainika vya kutosha. Nilikunja sura kwa uchungu wake mithili ya shubiri. Nikayatema na kumpachika yule mtoto eneo lake la jeraha alafu nikachana sehemu ya shati langu kutengeneza bandeji, nikamfungia hapo kichwani na kumweka mtoto huyo begani tuendelee na safari.
Tukiwa tunatembea, nikapata sasa wasaa wa kumuuliza maswali kadhaa. Niliona huu ni muda muhimu wa kufanya hivyo maana lolote linaweza kutokea muda wowote. Basi likitokea, angalau niwe nimetimiza robo ya haja yangu.
“Wewe ni nani? Kwanini watu hawa wamekuteka?” Niliuliza nikimtazama mwanamke huyo ambaye alikuwa akitembea kwa ukakamavu. Alikuwa na ushupavu ndani yake.
Akanitazama na kunyamaza kwanza akipiga hatua. Alipovuta pumzi ndefu ndipo akanijibu pasipo kunitazama, “Nilidhani utakuwa unanijua ndo’ maana ukaja kuntafuta.” Kisha akaniuliza, “Ajenti, umekujaje kumtafuta mtu ambaye humjui?”
“Umejuaje kama mimi ni ajenti?”
Akatabasamu. “Anayeweza kuyafanya yote haya, ni raia wa kawaida?” kabla sijanena akaendelea kunena, “Umefanya kazi kweli kujua wapi nilipo. Hata sasa kuwa hai unastahili pongezi.”
Nikamtazama na pasipo kuongea nikarudisha macho yangu mbele tuendako nikitarajia mwanamke huyo ataendelea kunena.
“Mimi ni raia wa kawaida kabisa. Ni mmarekani ninayeishi Ujerumani pamoja na mwanangu. Sina shida nyingine na mtu!”
“Huku Ujerumani unafanya nini? Na kwanini Ujerumani?”
“Una maswali mengi sana. Sidhani kama nipo kwenye mood ya kukata kiu chako. Pengine baadae nikiwa nimetulia.”
“Wamekufanya lolote ulipokuwa chini yao?”
Akatikisa kichwa. “wasingeweza kunifanya kitu.”
Nikamtazama kwa maulizo pasipo kusema kitu. Nadhani yeye mwenyewe akajiongeza na kunijibu swali langu la kimya. “Bado wananihitaji. Mimi ni asset kwao. Hawawezi kunidhuru.”
“Unamaanisha nini wewe ni asset?”
“Nimekuambia una maswali mengi. Najua. Tutakapotulia nitakuambia, pengine nitakata kiu chako.”
“Hauwezi ukanambia hata machache?”
“Naitwa Britney. Ni raia wa Marekani. Nadhani hayo yanakutosha.”
Sikutaka kusumbuana naye. Niliona ninyamaze kimya, kweli hayupo kwenye mood, japo kifuani mwangu nilikuwa nalaumu sana kutokujua kinachoendelea ingali tulipokuwa kitu chochote kingeweza kujiri.
Tukatembea kwa kama dakika kumi, akantazama kisha asiseme kitu akatazama zake mbele. Nadhani alikuwa anajiuliza maswali kichwani. Baada ya sekunde kadhaa, akasema, “Naomba umtazame mwanangu. Yeye ndo’ kitu pekee nilichonacho kwa sasa.” Kisha akasimama na kun’tazama. Nami nikasimama. Akaniambia, “Niahidi hilo … niahidi mtoto wangu atakuwa salama.”
“Nakuahidi,” nikasema kwa sauti ya kutikisika. Akaniuliza, “Unaniahidi?”
“Ndio, nakuahidi,” saa hii nikasema kwa kujiamini. Basi akaridhika tukaendelea na safari. Akaniambia kama tukitembea kwa takribani robo saa tutakuwa tumefika barabarani.
Tukatembea kwa kama dakika sita, yeye mwenyewe akaanza kuongea. “Nimemkumbuka sana mama yangu,” sauti yake ilikuwa ya mtu anayekaribia kulia.
“Kama ningalifuata alichonambia, nisingalikuwa hapa.”
Nikamtazama nisimsemeshe kitu. Nilihofia maneno yangu yangeweza kumkatiza. Nilimwacha afanye vile alivyokuwa anataka.
Akavuta makamasi mepesi kisha akaendelea, “Sasa nimekuwa mkimbizi nisiye na makazi. Toka kwenye kamera za mwanga mpaka kujificha chini ya uvungu na nyuma ya milango. Ama kweli maisha huweza badilika ndani ya sekunde moja tu!
Ndani ya sekunde moja mtu akawa kilema. Akapoteza alivyovipata kwa masaa. Ndani ya muda huo mchache akawa amebadili mwelekeo wa maisha yake.”
Nikaendelea kumtazama pasipo kutia neno. Niliona uso wake ukiwa umebadilika rangi kuwa mwekundu. Alikifikicha pua yake na kumwaga tena maneno, “Hakuna anayejua kesho yake, sio? … mimi sikudhani kama siku moja ntakuja kuwa na familia. Sikuwa nawaza hilo jambo kabisa, labda kwasababu ya aina ya maisha niliyoyachagua.
Maisha yalonifanya ninyooshewe kidole kila nilipopita nikionekana laana, mchafu na niliyelaaniwa. Sikutaka mwanangu aje kushea laana yangu. Ashindwe kupita mtaani kwasababu ya mama yake. Ni adhabu. Najua ukubwa wa adhabu hiyo maana nimeibeba mgongoni kwa muda mrefu. Inachosha na kuumiza.
Watamani kukaa mbali na walimwengu ambao ni wepesi wa kuhukumu na wachoyo wa fadhila. Lakini ajenti, wawezaa kukaa mbali na dunia?”
Aliniuliza akintazama. Nikamtikisa kichwa kukataa pasipo kutia neno. Basi akatabasamu kwa mbali na kisha akakaa kimya kidogo. Tukatembea kwa kama dakika moja asinene jambo ila nikiamini ataendelea tu kusema.
Nilihisi ana kitu kifuani. Atajihisi mwepesi endapo atakitoa.
Akajifuta machozi na mikono ya sweta lake alafu akatazama juu kwenye matawi ya miti, pembeni na kisha mbele.
“Hata kama niki –”
“Shhh!” nikamzuia upesi nikimwonyeshea ishara ya kidole mdomoni. Kuna kitu nilihisi. Tulisimama tukatulia tuli na kutazama kushoto na kulia. Masikio yangu yalinambia nimesikia sauti ya watu wakiteta. Na sikuwa nimekosea, lah! Nyuma yetu kwa umbali, tukawaona wanaume wawili waliokuwa wamevalia nguo nyeusi na mikononi mwao wana bunduki ndefu!
Wanaume hawa hawakuwa na usafiri, bali wakitumia miguu yao.
Haraka nikamtaka Britney akimbie na mie kabla sijafungua miguu yangu nikafyatua risasi kuwalenga wanaume wale kuwapumbazisha kwa muda kidogo.
Tukakimbia na kukimbia. Nao wale wanaume wakawa wanaendelea kutukimbiza, wakawa pia wanatupa risasi wakijaribu kunilenga.
Nikiwa nimembebelea mtoto, nikakimbia kwa kasi na kwanguvu mpaka kumwacha Britney nyuma. Si kwamba alikuwa anakimbia taratibu, hapana! Na wala hakuonekana mtu anayehitaji msaada. Alikuwa anajimudu kukimbia.
Hatukudumu muda mrefu mbioni, nikasikia risasi ya karibu zaidi na kisha sauti ya kike ikilalama! Kutazama, nikamwona Britney akidondoka chini!
“Shit!” nikamsikia mmoja wale wajamaa wanaotukimbiza akilaani, kisha kwa punde akamlaumu mwenzake kwa kumfyatulia risasi Britney. Hapa nikatumia nafasi hiyo upesi kuwamiminia risasi na kuwalaza chini.
Nikamtazama Britney. Alikuwa amelengwa kwenye shina la nyuma la shingo. Risasi ilivunja uti wake wa mgongo! Ilikuwa ngumu kwake kupona. Damu zilimtiririka. Macho yake yalimwaga machozi akinishika kwanguvu na kung’ata meno yake.
“Ajenti, mtazame vema mwanangu,” akasema akikwamakwama. Kisha akaninong’oneza, “Naitwa Juliette Simpson. Natumai utakuwa unanijua.” Alafu akajifia.
Akafa mbele ya macho yangu. Akafa mwanaye akiwa bado hajitambui.
Nikawaendea wale wanaume niliowaua na kuwapekua. Sikuwakuta na kitu zaidi ya bunduki na risasi kadhaa. Nikazichukua. Nilipomrudia Britney ambaye kabla hajafa alinipa jina lingine, naye nikampekua kama ana kitu. Alikuwa mtupu.
Nikapata maswali juu ya nini cha kufanya. Haraka nikatoa simu yangu na kumchukua picha kadhaa, nashukuru simu yangu haikuwa simu inayoingiza maji.
Nikiwa nimempiga picha mbili tu, nikasikia tena sauti ya watu, hiyo ikawa ishara kuwa sitakiwi kukaa hapo tena. Nikaanza kukimbia. Huko nyuma nikasikia, “Yule!” na vishindo vya watu vikinifuata kwa kasi!
Nikakimbia sana lakini nguvu zangu hazikuwa kama za hapo awali, nilichoka mno. Kumbeba mtu kwa muda wote ule huku nikikimbia na kutembea haikuwa jambo jepesi. Hivyo basi nikaanza kupunguza kasi ya mwendo wangu na kupelekea wale maadui wanikaribie zaidi!
Wakatupa risasi kadhaa. Nashukuru miti ilinikinga. Nilisikia zikipasua na kugotea mitini. Nilipoona maji yanazidi kupiku unga, nazidi kukaribiwa na hali ni mbaya, nikakimbilia mtoni na kujitosea humo!
Nilizama maana kina kilikuwa kirefu. Risasi zikatumwa kunifuata ndani ya maji, zikanipitia kupunyua, lakini kwakuwa maji yalikuwa na nguvu na mengi ya kutosha kunipeleka, yakaniepushia na balaa!
Yakanisomba kunisafirisha.

***
 
Naam mkuu
Kumekucha na makucha yake
Huku hakupoi wala .......
Yaani mwanzo mwisho
 
*NYUMA YAKO – 18*
*Simulizi za series*

ILIPOISHIA
Tulipofika pakavu, nikamtazama mtoto na kubaini alikuwa amejigonga kwenye jiwe ingali tu mtoni. Na kwa namna alivyokuwa anatoka damu, inabidi ifanyike namna upesi ya kumsaidia, la sivyo alikuwa anatuacha!
Nikamwambia mama yake, “gandamizia mahali pa jeraha, nakuja!” mimi nikaenda kutafuta majani yatakayoweza kumsaidia jerahani.
ENDELEA
Nilifahamu ndani ya msitu ule sitakosa ninachotaka. Nikakimbia upesi na kufanya jitihada za kuangaza macho yangu nikitumia stadi niliyonayo juu ya madawa ya asili. Tulifunzwa hii. Tulifunzwa namna ya kudumu na kumudu kwenye hali mbalimbali kama hizi.
Ndani ya muda mfupi, nikapata kuona kichaka chenye majani membamba na ncha kana kwamba sindano. Nikajongea hapo na kuchuma majani kadhaa na kuyatia mdomoni kutafuna alafu nikaanza kurudi upesi kule kwa yule mwanamama na mwanaye.
Nilipofika majani mdomoni mwangu yalikuwa tayari yashalainika vya kutosha. Nilikunja sura kwa uchungu wake mithili ya shubiri. Nikayatema na kumpachika yule mtoto eneo lake la jeraha alafu nikachana sehemu ya shati langu kutengeneza bandeji, nikamfungia hapo kichwani na kumweka mtoto huyo begani tuendelee na safari.
Tukiwa tunatembea, nikapata sasa wasaa wa kumuuliza maswali kadhaa. Niliona huu ni muda muhimu wa kufanya hivyo maana lolote linaweza kutokea muda wowote. Basi likitokea, angalau niwe nimetimiza robo ya haja yangu.
“Wewe ni nani? Kwanini watu hawa wamekuteka?” Niliuliza nikimtazama mwanamke huyo ambaye alikuwa akitembea kwa ukakamavu. Alikuwa na ushupavu ndani yake.
Akanitazama na kunyamaza kwanza akipiga hatua. Alipovuta pumzi ndefu ndipo akanijibu pasipo kunitazama, “Nilidhani utakuwa unanijua ndo’ maana ukaja kuntafuta.” Kisha akaniuliza, “Ajenti, umekujaje kumtafuta mtu ambaye humjui?”
“Umejuaje kama mimi ni ajenti?”
Akatabasamu. “Anayeweza kuyafanya yote haya, ni raia wa kawaida?” kabla sijanena akaendelea kunena, “Umefanya kazi kweli kujua wapi nilipo. Hata sasa kuwa hai unastahili pongezi.”
Nikamtazama na pasipo kuongea nikarudisha macho yangu mbele tuendako nikitarajia mwanamke huyo ataendelea kunena.
“Mimi ni raia wa kawaida kabisa. Ni mmarekani ninayeishi Ujerumani pamoja na mwanangu. Sina shida nyingine na mtu!”
“Huku Ujerumani unafanya nini? Na kwanini Ujerumani?”
“Una maswali mengi sana. Sidhani kama nipo kwenye mood ya kukata kiu chako. Pengine baadae nikiwa nimetulia.”
“Wamekufanya lolote ulipokuwa chini yao?”
Akatikisa kichwa. “wasingeweza kunifanya kitu.”
Nikamtazama kwa maulizo pasipo kusema kitu. Nadhani yeye mwenyewe akajiongeza na kunijibu swali langu la kimya. “Bado wananihitaji. Mimi ni asset kwao. Hawawezi kunidhuru.”
“Unamaanisha nini wewe ni asset?”
“Nimekuambia una maswali mengi. Najua. Tutakapotulia nitakuambia, pengine nitakata kiu chako.”
“Hauwezi ukanambia hata machache?”
“Naitwa Britney. Ni raia wa Marekani. Nadhani hayo yanakutosha.”
Sikutaka kusumbuana naye. Niliona ninyamaze kimya, kweli hayupo kwenye mood, japo kifuani mwangu nilikuwa nalaumu sana kutokujua kinachoendelea ingali tulipokuwa kitu chochote kingeweza kujiri.
Tukatembea kwa kama dakika kumi, akantazama kisha asiseme kitu akatazama zake mbele. Nadhani alikuwa anajiuliza maswali kichwani. Baada ya sekunde kadhaa, akasema, “Naomba umtazame mwanangu. Yeye ndo’ kitu pekee nilichonacho kwa sasa.” Kisha akasimama na kun’tazama. Nami nikasimama. Akaniambia, “Niahidi hilo … niahidi mtoto wangu atakuwa salama.”
“Nakuahidi,” nikasema kwa sauti ya kutikisika. Akaniuliza, “Unaniahidi?”
“Ndio, nakuahidi,” saa hii nikasema kwa kujiamini. Basi akaridhika tukaendelea na safari. Akaniambia kama tukitembea kwa takribani robo saa tutakuwa tumefika barabarani.
Tukatembea kwa kama dakika sita, yeye mwenyewe akaanza kuongea. “Nimemkumbuka sana mama yangu,” sauti yake ilikuwa ya mtu anayekaribia kulia.
“Kama ningalifuata alichonambia, nisingalikuwa hapa.”
Nikamtazama nisimsemeshe kitu. Nilihofia maneno yangu yangeweza kumkatiza. Nilimwacha afanye vile alivyokuwa anataka.
Akavuta makamasi mepesi kisha akaendelea, “Sasa nimekuwa mkimbizi nisiye na makazi. Toka kwenye kamera za mwanga mpaka kujificha chini ya uvungu na nyuma ya milango. Ama kweli maisha huweza badilika ndani ya sekunde moja tu!
Ndani ya sekunde moja mtu akawa kilema. Akapoteza alivyovipata kwa masaa. Ndani ya muda huo mchache akawa amebadili mwelekeo wa maisha yake.”
Nikaendelea kumtazama pasipo kutia neno. Niliona uso wake ukiwa umebadilika rangi kuwa mwekundu. Alikifikicha pua yake na kumwaga tena maneno, “Hakuna anayejua kesho yake, sio? … mimi sikudhani kama siku moja ntakuja kuwa na familia. Sikuwa nawaza hilo jambo kabisa, labda kwasababu ya aina ya maisha niliyoyachagua.
Maisha yalonifanya ninyooshewe kidole kila nilipopita nikionekana laana, mchafu na niliyelaaniwa. Sikutaka mwanangu aje kushea laana yangu. Ashindwe kupita mtaani kwasababu ya mama yake. Ni adhabu. Najua ukubwa wa adhabu hiyo maana nimeibeba mgongoni kwa muda mrefu. Inachosha na kuumiza.
Watamani kukaa mbali na walimwengu ambao ni wepesi wa kuhukumu na wachoyo wa fadhila. Lakini ajenti, wawezaa kukaa mbali na dunia?”
Aliniuliza akintazama. Nikamtikisa kichwa kukataa pasipo kutia neno. Basi akatabasamu kwa mbali na kisha akakaa kimya kidogo. Tukatembea kwa kama dakika moja asinene jambo ila nikiamini ataendelea tu kusema.
Nilihisi ana kitu kifuani. Atajihisi mwepesi endapo atakitoa.
Akajifuta machozi na mikono ya sweta lake alafu akatazama juu kwenye matawi ya miti, pembeni na kisha mbele.
“Hata kama niki –”
“Shhh!” nikamzuia upesi nikimwonyeshea ishara ya kidole mdomoni. Kuna kitu nilihisi. Tulisimama tukatulia tuli na kutazama kushoto na kulia. Masikio yangu yalinambia nimesikia sauti ya watu wakiteta. Na sikuwa nimekosea, lah! Nyuma yetu kwa umbali, tukawaona wanaume wawili waliokuwa wamevalia nguo nyeusi na mikononi mwao wana bunduki ndefu!
Wanaume hawa hawakuwa na usafiri, bali wakitumia miguu yao.
Haraka nikamtaka Britney akimbie na mie kabla sijafungua miguu yangu nikafyatua risasi kuwalenga wanaume wale kuwapumbazisha kwa muda kidogo.
Tukakimbia na kukimbia. Nao wale wanaume wakawa wanaendelea kutukimbiza, wakawa pia wanatupa risasi wakijaribu kunilenga.
Nikiwa nimembebelea mtoto, nikakimbia kwa kasi na kwanguvu mpaka kumwacha Britney nyuma. Si kwamba alikuwa anakimbia taratibu, hapana! Na wala hakuonekana mtu anayehitaji msaada. Alikuwa anajimudu kukimbia.
Hatukudumu muda mrefu mbioni, nikasikia risasi ya karibu zaidi na kisha sauti ya kike ikilalama! Kutazama, nikamwona Britney akidondoka chini!
“Shit!” nikamsikia mmoja wale wajamaa wanaotukimbiza akilaani, kisha kwa punde akamlaumu mwenzake kwa kumfyatulia risasi Britney. Hapa nikatumia nafasi hiyo upesi kuwamiminia risasi na kuwalaza chini.
Nikamtazama Britney. Alikuwa amelengwa kwenye shina la nyuma la shingo. Risasi ilivunja uti wake wa mgongo! Ilikuwa ngumu kwake kupona. Damu zilimtiririka. Macho yake yalimwaga machozi akinishika kwanguvu na kung’ata meno yake.
“Ajenti, mtazame vema mwanangu,” akasema akikwamakwama. Kisha akaninong’oneza, “Naitwa Juliette Simpson. Natumai utakuwa unanijua.” Alafu akajifia.
Akafa mbele ya macho yangu. Akafa mwanaye akiwa bado hajitambui.
Nikawaendea wale wanaume niliowaua na kuwapekua. Sikuwakuta na kitu zaidi ya bunduki na risasi kadhaa. Nikazichukua. Nilipomrudia Britney ambaye kabla hajafa alinipa jina lingine, naye nikampekua kama ana kitu. Alikuwa mtupu.
Nikapata maswali juu ya nini cha kufanya. Haraka nikatoa simu yangu na kumchukua picha kadhaa, nashukuru simu yangu haikuwa simu inayoingiza maji.
Nikiwa nimempiga picha mbili tu, nikasikia tena sauti ya watu, hiyo ikawa ishara kuwa sitakiwi kukaa hapo tena. Nikaanza kukimbia. Huko nyuma nikasikia, “Yule!” na vishindo vya watu vikinifuata kwa kasi!
Nikakimbia sana lakini nguvu zangu hazikuwa kama za hapo awali, nilichoka mno. Kumbeba mtu kwa muda wote ule huku nikikimbia na kutembea haikuwa jambo jepesi. Hivyo basi nikaanza kupunguza kasi ya mwendo wangu na kupelekea wale maadui wanikaribie zaidi!
Wakatupa risasi kadhaa. Nashukuru miti ilinikinga. Nilisikia zikipasua na kugotea mitini. Nilipoona maji yanazidi kupiku unga, nazidi kukaribiwa na hali ni mbaya, nikakimbilia mtoni na kujitosea humo!
Nilizama maana kina kilikuwa kirefu. Risasi zikatumwa kunifuata ndani ya maji, zikanipitia kupunyua, lakini kwakuwa maji yalikuwa na nguvu na mengi ya kutosha kunipeleka, yakaniepushia na balaa!
Yakanisomba kunisafirisha.

***
shukrani mkuu
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom