Nyuma yako - Riwaya ya SteveMollel

*NYUMA YAKO --- 02*

*Simulizi za series*


ILIPOISHIA

Na kwasababu haujayapa kipaumbele kama yale ya mbele, mambo haya ya nyuma huwa ya ghafla na hatarishi zaidi, yakikuacha ukiwa umelala chini hujiwezi, damu zakububujika.

Tazama nyuma yako. Huenda kuna mchezo unaendelea ambao hauuoni.

ENDELEA

SURA YA PILI …

Ni kwa muda mfupi kwa kadiri tulivyoweza tukawa tumefika Marekani, New York. Safari hiyo ni ya umbali wa masaa kumi na tano na dakika thelathini na tatu. Lakini kwasababu ya mambo ya masaa, kijografia Hong Kong ipo mbele kimajira kuliko Marekani hivyo tukafika siku hiyo hiyo tuliyotokea Hongkong, Jumatano, huku Marekani yakiwa ni majira ya mchana.

Ni ajabu enh? Basi ili tusipotazane hapa, maana kuna mikanganyiko zaidi huko mbele, acha tueleweshane kwa ufupi. Dunia huzunguka toka Magharibi kuelekea Mashariki, kwahiyo basi upande wa Mashariki huwai kuliona Jua kuliko ule wa Magharibi. Tupo pamoja?

Kwahivyo basi, ukiwa Hong Kong unatangulia kuliona na kulichoka jua kabla hata Marekani hawajaliona. Na wakuta Hong Kong ikiwa ni Jumatano, bado Marekani ni Jumanne au Jumatatu usiku baadhi ya maeneo machache ya Magharibi ya mbali. Kwahiyo kusafiri kutoka Hongkong kwenda Marekani, ni safari unayopoteza muda, yaani badala ya muda kuongezeka, unakuwa unapungua maana umetoka Mashariki kurudi Magharibi ambapo kupo nyuma kimasaa.

Natumai umenielewa.

Lakini hapa New York si ambapo tulikuwa tunaelekea. Makao makuu ya CIA yapo Virginia, umbali wa maili mia nne na nane toka jiji la New York. Kwa mwendo wa basi ingetugharimu masaa saba kasoro, hatukuwa na muda huo wa kupoteza kwahiyo ikatulazimu kuchukua ndege ili angalau tutumie lisaa limoja na robo hivi kufika Virginia.

Tukafanya hivyo, pasipo kupumzika, tukafika Virginia majira ya saa tisa alasiri. Nikamwacha Jack Pyong na mpenzi wake mie nikienda mpaka makao makuu kukutana na Inspector General, bwana Ethan Benjamin, mwanaume wa makadirio ya miaka hamsini kasoro haba.

“Karibu, Marshall,” akanikaribisha akinionyeshea kiti. Nikaketi na kumtazama. Alikuwa tayari ananitazama kwa umakini kana kwamba mwalimu wa usafi akitafuta kasoro kwenye sare ya mwanafunzi.

Bwana Ethan ni mtu mmoja mpole sana. Ni mara chache sana utamsikia akipaza sauti yake. Hupenda kutumia macho na maneno machache tu haswa akikukumbusha juu ya uwepo wako kwenye taasisi nyeti kama hiyo, CIA.

Mara kadhaa amekuwa akisema kabla ya kuwaruhusu maajenti wakafanye kazi zao, CIA ni moyo wa Marekani, hivyo msifanye taifa kuwa mfu.

Ni ngumu sana kumjua kama yupo kwenye msongo wa mawazo ama furaha. Uso wake ni mfichavi mzuri sana wa hisia. Najaribu sana kuwa kama yeye, lakini naishia kushindwa. Haswa nikiwa na mpumbavu Jack Pyong.

Akasafisha koo lake na kuniambia, “Marshall, nina kazi kubwa sana ya kukupatia. Najua hautaniangusha.” Akili yangu ikaanza kuwaza itakuwa kazi gani hiyo ya kunitoa kwenye likizo yangu na kuitwa moja kwa moja na Inspector General? Ndivyo tulivyofundishwa. Yakupasa kuwaza ya mbele, hata kubashiri kwa mantiki pale unapoona kuna haja ya kufanya hivyo. Halikuwa kosa.

Ila sikuweza kuwaza sana kwa maana nilipaswa pia kuweka akili na masikio yangu kwenye kinywa cha mkuu wangu wa kazi.

“Hapa tuongeapo, Raisi amepotea,” akasema kisha akanyamaza akin’tazama kwa kunisoma. “Alikuwa njiani akielekea Berlin, Ujerumani, kwenye mkutano wa mataifa makubwa kiuchumi, lakini mpaka sasa tuongeapo hajulikani alipo, na inasemekana ndege yake imeanguka huko mbali ya bahari ya Pasifiki.”

Kauli hiyo ikatosha kunitoa macho kwa mshangao. Nikajitengenezea vema kitini na kumtazama Mkuu akinena.

“Taarifa haijatangazwa rasmi, lakini haiwezi kukaa kabatini kwa muda. Hili laweza kuwa shambulizi la kigaidi, nina mashaka nalo. Na mpaka kukuita hapa maana yake ni kwamba nina mashaka nalo.”

Akanyamaza na kunitazama kwa sekunde mbili, alafu akaniita, “Marshall.”

“Ndio, Mkuu.”

Akasema, “Nishatoa maelezo haya kwa mkuu wako wa kitengo. Unachotakiwa kukifanya ni kwenda kumtafuta Raisi popote alipo. Kama amekufa, tuletee mwili wake hapa niamini. Na pia … vichwa vya hao waliohusika!” akiwa anasema hayo maneno ya mwishoni alikuwa anaminyia kidole chake juu ya meza, macho akiyakaza.

Kwa kuongezea zaidi akaniambia nitashirikiana na inspekta wa FBI (Federal Bureau of Investigation) Miss Danielle James kuhusiana na chochote kile cha upelelezi ntakachokihitaji ndani ya nchi. Hii ni kwasababu CIA huwa wanahusika zaidi na mambo ya nje, nchi za kigeni, wakati FBI wao wakihusika na intelijensia ya ndani ya nchi, kukusanya taarifa, ushahidi, na kushurutisha sheria.

Hivyo kuna nyakati huwa tunategemeana kutekeleza majukumu yetu.

“Utamkuta hapo nje,” akasema mkuu na kumalizia tena, “Usiniangushe, Marshall. CIA ni --”

“Moyo wa Marekani,” nikamsaidia kumalizia kisha nikatikisa kichwa na kutoka nje ya ofisi. Nikakutana na Danielle, mwanamke mkakamavu mwenye nywele nyekundu akiwa amevalia suti rangi ya kahawia. Akanisalimu nami pia nikamsalimu kisha nikaenda kukaa naye kwa ofisi yangu kwa muda mchache mno, nikionelea ni kheri kwanza niende kwenye eneo la tukio kumtafuta Raisi, alafu nitakuja kurejea kuongea naye zaidi.

“Kwahiyo unaonaje?” akaniuliza. Kwakweli sikuwa najua nini ametoka kuongelea, kwani mawazo yangu yalikuwa mbali kidogo. Nilikuwa najaribu kuwaza ni wakina nani watakuwa na ‘guts’ za kufanya tukio kubwa kama hilo? Na amewezaje kufanya vivyo ingali ulinzi wa Raisi huwa ni wa hali ya juu?

“Daniella, tutaonana. Sawa?” nikamuaga nikinyanyuka kuuendea mlango, nikaufungua na kumtazama. Mwanamke huyo akatikisa kichwa kabla hajanyanyuka na kujiendea zake. Mimi nikarejea pale kitini na kuwaza kwa muda kidogo juu ya namna ya kuenenda. Punde nikatungua koti langu jeusi lililopo ndani ya ofisi, nikaliweka begani na kutoka.


**

Ni hivi, katika oparesheni kama hii, siwezi kwenda mwenyewe. Nahitaji msaada toka kwa watu wengine ambao tutaunda timu ya kufanya kazi. Ndani ya CIA kuna kitengo cha shughuli maalum, kwa jina ‘The Special Activities Centre’, kifupi SAC. Kitengo hichi kimegawanyika kwenye makundi mawili; PAG na SOG.

Oparesheni za kisiasa na kiuchumi huendeshwa na ‘The Political Action Group’, kifupi PAG. Hawa wanahusika na ushawishi wa kisiasa na wa kichumi wa Marekani dunia nzima. Na oparesheni zenye hatari ya juu kijeshi hufanywa na ‘The Special Operation Group’ kifupi SOG.

Wahusika wa SOG huwa hawabebelei nguo au kitu chochote cha kuwaonyesha kuwa wao wametokea Marekani. Na hii ni kwasababu muda wowote ule ambapo mambo yakienda kombo, basi Marekani wanaweza kukana kuhusika nao.

Ndani yake kunakuwa na watu wenye ujuzi wa hali ya juu, ambao wengi wao hutolewa kwenye kitengo cha special force au tuite komando toka jeshini. Na kwakufanya mambo kuwa mepesi na ‘manageable’ huwa wachache tu kwa kila oparesheni.

Hivyo basi kwakuwa kila kitu kilishakuwa bayana, nilipoonana na mhusika wa kitengo cha SAC (The Special Activities Centre), akanikabidhi vijana wanne kwa ajili ya kazi akiwa amefuata maelekezo ya Inspector General. Kwahiyo kutokana na kazi tuliyokuwa tunaelekea kufanya, sisi tukawa ni SOG (The Special Operation Group).

**

Ulikuwa ni usiku sasa wa saa mbili tukiwa angani ndani ya ndege ya mapambano. Tukiwa tumekaa kwa kutazamana, tukamsika rubani akitangaza kusema tunaingia eneo la tukio hivyo basi tuanze kujiandaa kwa ajili ya kuchumpa.

Tukaweka kila kitu sawa; begi la parachuti na miwani ya kutusaidia kuona usiku. Tulikuwa tumevalia nguo nyeusi za kombati zisizo na bendera, pia tumebebelea vifaa kadhaa vya kutusaidia kimapambano na kuzamia. Punde rubani aliposema tumefika, mkia wa ndege ukafunguka nasi tukarukia nje pasipo kujiuliza.

Tukachukua kama dakika sita tukiwa hewani tukibebwa na maparachuti tunasukumwa na upepo. Tulipotua, ilikuwa ni kisiwani, tukiwa tunafuata ramani, tukatembea upesi mpaka kufika eneo la ufukweni. Palikuwa kimya haswa. Nikatazama tena kwenye ramani yangu kuhakikisha. Ni kweli nilikuwa mahali ninapostahili.

Hapakuwa na alama ya kitu chochote hapo. Maji yalikuwa yanasukumwa na upepo kutengeneza mawimbi, na miti inatikisika kutengeneza muziki.

Hapa ndiyo nikajua ya kuwa sisi ni watu wa kwanza kufika hapo. Ina maana tangu Raisi aangukie maeneo hayo, hakuna mtu aliyewahi kukanyaga hapo.

**
Tivuu kwenye muda nimekuelewa sana. Marshall ni mtz au mzungu?
 
*NYUMA YAKO – 15*
*Simulizi za series*

ILIPOISHIA
Nilipotua upande wa pili, nikaanza kukimbia kuufuata ukuta mwingine wa nyumba niliyozamia. Kidogo, nikasikia watu wengine wakitua, walikuwa ni wanaume wawili ambao wananifukuzia! Wakaanza kurusha risasi kwa fujo! Kwa pupa!
ENDELEA
Basi haraka nikachumpa kuuvuka ukuta mwingine, hapa hata sikuushika ukuta huu bali kuruka kama samaki. Nikatua kwa ustadi na kisha kukimbia upesi kwanguvu zote kuufuata ukuta mwingine, nao nikiwa nimeukaribia, wanaonikimbiza wakawa wametua. Wakaendelea kufyatua risasi kama njugu!
Hapa moja ikanipunyua mkono na kunisababishia jeraha. Ila sikukoma kukimbia kuokoa nafsi yangu. Nikaruka tena kwenye ukuta mwingine na mwingine na mwingine, alafu nikajificha pahala.
Wale watesi wangu wakasonga wakiwa wameduwaa. Wakatazama kushoto na kulia mimi nikiwa nawachora toka kwenye ua kubwa. Hawakuwa wananiona. Ila kama sijakosea, mmoja wao akahisi huenda naweza nikawa nimejibana nyuma ya ua. Nikaona akimshtua mwenzake akitazama eneo nililopo.
Kuona hivyo, basi upesi nikachomoka na kuwafyatulia risasi. Wote wakalala chini na kunipa amani kwa muda. Nikatoka hapo nyuma ya ua na kukimbia upesi. Nikaruka ukuta mwingine na kuzama barabarani, sikuona mtu nyuma, nilikuwaa mwenyewe sasa. Kidogo nikakutana na gari, nikasimamisha na kumwamuru dereva atoke ndani, alipotii nikazama ndani ya gari na kutimka.
Ila sikufika mbali sana na hilo gari, nikaliacha na kudaka lingine. Nalo liliponisogeza umbali kidogo, nikaliacha na kupanda basi la uma. Nikaenda kabisa nyuma ya basi na kusimama huko. Nilijihisi salama sasa.
Nikafika hotelini na nikiwa naelekea chumbani mwangu, dada wa mapokezi akaniita. Mwanamke mwenye sura pole na mashavu mapana ndani ya sare. Nikamjongea taratibu nikiwa najiuliza nini shida? Akanitazama na kisha akaangalia tarakilishi yake na kuniuliza, “Kuna mgeni wako ulimtuma?”
“Mgeni?”
“Ndio! Kuna mwanaume alikuja hapa kukuulizia.”
“Aliniuliziaje?” nikatahamaki. Basi yule mhudumu akanambia kuwa alitumia maelezo ya mwonekano wangu, na hivyo alivyoniona tu akapata kujua kuwa ndiye mimi. Nami nikamuuliza mtu huyo aonekanaje? Akanieleza.
Maelezo yake yakajenga picha kichwani mwangu kuwa mtu huyo atakuwa ni miongoni mwa wale wajamaa ambao nilipanda nao basi kabla sijawapotea.
Ina maana wameshajua makazi yangu mapya? Nikaona hapa si mahali pa kukaa tena. Nikanyookea chumbani mwangu na kuanza kukusanya vitu muhimu kutoka kwenye begi, haswa pesa na kadi. Lakini kabla sijatoka, nikasikia hodi mlangoni! Nikatulia tuli nikipepesapepesa macho yangu. Kidogo sauti ya kiume ikasema, “mhudumu!” kisha kugonga tena mlango.
Sikusema kitu. Nikaweka silaha yangu mkononi na kujongea mlango. Sijaufikia, nikastaajabu mlango umekumbwa na teke! Ukang’oka na kunivamia na kunidondosha chini!
Kutazama, nikamwona mwanaume akiwa amevalia nguo nyeusi. Sura yake haikuwa ngeni. Alikuwa ni miongoni mwa wale wanaume niliopanda nao basi kabla sijawapotea. Mkononi mwake alikuwa amebebelea bunduki!
Basi haraka nikaunyanyua mlango na kujikinga nao. Bwana yule akatupa risasi kama tano vile pasipo kupumzika, zote zikaishia mlangoni. Mimi nilipochomoza na kumtwanga yangu moja, akawa amekwisha! Alidondoka chini kama mzigo akiwa ameachama mdomo.
Upesi nikanyanyuka na kumtazama. Punde nikasikia sauti kali ya mwanamke ikipiga yowe huko mbali. Hapa nikahisi hamna tena usalama, huenda kuna wavamizi wengine! Nikatoka ndani kushika korido, ila uso kwa uso, umbali wa kama hatua kumi na nane, nikaonana na wanaume wawili wakiwa wanakuja wamebebelea bunduki!
Upesi nikarudi ndani. Nikasikia vishindo vya watu vikikimbia kuja. Nikavunja dirisha na kutokea nje. Chumba changu kilikuwa ghorofa ya kwanza, nikarukia huko chini nikitulia pazia lililokuwa limefunikia magari yaliyoegeshwa, kisha nikajitupia chini na kukimbia!

**

“Kama nisipofanya mambo haya upesi, nadhani yatazidi kuniwia vigumu zaidi na zaidi!” niliteta na Jack nikiwa nimeketi kwenye kiti ndani ya nyumba ya kupumzikia. Niliongea naye kwa muda sana na mwishowe alipokata simu nikajilaza kitandani na kuwaza mambo kadha wa kadha.
Kwa maelezo ambayo nilimpatia Jack, aliniambia yanasawiri na namna alivyokuwa anawaza lakini asiniweke bayana kipi ambacho kipo kichwani mwake, akataka ningoje kwa muda kidogo. Hivyo hapo nilipokuwa nimejilaza nilikuwa namngoja.
Zikapita kama dakika sita, usingizi ukaanza kuninyemelea. Nilisinzia nikipambana na macho yangu mazito. Ikiwa kama dakika ya nane kama niko sahihi, simu yangu ndiyo ikaita Jack akirudi tena hewani.
“Sasa sikia …” akaanza kwa kauli hiyo kisha akanambia kuhusu yule mtoto ambaye alikuwa anakaa na mama yake kwenye nyumba yenye anwani 2345. Kumbe alishamtambua mtoto huyo na kunituma kwenda kumuulizia mwonnekano wake ilikuwa ni kwa ajili ya kuthibitisha tu.
Lakini mtoto huyo ni nani haswa? Hakuwa anafahamu japo nishamwambia kuwa ni Mmarekani. Na kuhusu mama yake, Jack hakuwa na taarifa naye hata kidogo!
Ilikuwa ni ajabu kidogo kwani Jack aliniambia alifanikiwa kum – trace mtoto huyo kupitia game la ‘Subway Surfers’ ambalo humo ndani, kwa ridhaa, wachezaji huweza kuunganisha na mtandao wao wa Facebook ili washindane na marafiki zao.
Lakini zaidi, unaweza ukatazama kuona wachezaji gani wana points nyingi ulimwengu mzima. Basi kwa kupitia huko, Jack Pyong akakuta jina la MUNICH 2345. Na aliposaka jina hilo mtandaoni akitumia picha aliyoiona humo mchezoni, akafanikiwa kulipata. Kwa ufupi, jina la mtoto huyo huitwa Brussels, lakini jina lake la mchezoni hutumia MUNICH 2345, yaani jina la anwani ya nyumba alokuwa anakaa.
“Sasa tunaweza tukampata wapi yeye na mama yake?” nikamuuliza Jack.
“Usijali,” Jack akan’toa hofu. “Mpaka kufikia kesho n’takuwa nishapata!” tukamaliza maongezi na mie nikajilaza sasa.
Nikiwa usingizini, nadhani kwasababu ya kupitia purukushani hapa karibuni za mara kwa mara, nikaota ndoto ya kunishtua. Nilijikuta nikinyanyuka upesi na kushikilia bunduki yangu lakini nilipotazama huku na kule sikuona kitu. Nilikuwa mwenyewe!
Kidogo usingizi ukawa umenitoka. Nikashika simu yangu na kuperuzi, nikaukuta ujumbe toka kwa Daniele. Alikuwa akinijulia hali na kuniuliza wapi nilipofikia. Ujumbe huo ulikuwa umetumwa dakika tisa nyuma.
Nikaujibu kisha nikaweka simu pembeni. Sikutarajia kama Daniele angeujibu kwani ilipita muda kidogo tangu autume lakini kinyume na matarajio yangu, akajibu punde tu. Na hapo ndipo nilipoingia naye kwenye uwanja wa kuchat kw muda kidogo akinieleza mambo kadha wa kadha.
Lakini zaidi lililokamata hisia zangu ni mashambulio mawili ambayo Daniele na timu yake waliyapitia ingali wakiwa kazini. Kwa mujibu wa Daniele, walishambuliwa na mwanamke mmoja na wanaume watatu. Ingawa walikuwa wameficha nyuso zao lakini waliwatambua kutokana na maumbo yao ya mwili.
Shambulio la kwanza lilitokea wakiwa wametoka kwenye nyumba ya Makamu wa Raisi na ya pili wakitoka kwenye ofisi ya Wizara ya usalama wa ndani!
“Watu wangu wawili wameuawa kwasababu ya mashambulizi hayo, na hata kupotea kwa baadhi ya nyaraka. Nimepeleka taarifa kwenye uongozi, wakaniongezea ulinzi.”
Nami nikamshauri kushirikiana na Jack Pyong kwenye mambo kadhaa haswa ya kiteknolojia kwani anaweza kumsaidia. Kwa mawasiliano zaidi nikampatia namba za Jack na hata kumtaarifu Jack juu ya swala hilo.
Baada ya hapo, nikalala.

**

Saa kumi na moja asubuhi…

Nina uhakika simu ilinguruma mara moja tu kabla sijaamka. Niliitazama nikiwa nimekunja uso wa usingizi, kwenye kioo nikaona nimetumiwa na Jack ‘location’ ya eneo ambalo naweza kumpata yule mtoto ambaye tulimjadili.
Basi usingizi ukanikata papo hapo, nikanyanyuka nikaoga na kuvaa kisha kushika barabara kwenda huko ambako Jack alikuwa amenielekeza. Mahali mbali kabisa na jiji la Munich. Tena msituni. Ulikuwa ni kama mwendo wa masaa matano kasoro kwa basi mpaka kufika huko. Huko wenye msitu huo wa ‘Black forest’ ambapo ndipo location ilipoongoza.
Mpaka kupata na kupanda basi ikawa tayari ni saa moja asubuhi, safari ikaanza. Kama kawaida nilikuwa nimekaa nyuma ili nipate nafasi ya kutazama abiria wote ndani ya basi, watakaoshuka na wale watakaoingia.
Nikiwa nimekaa huko nikawa nawaza sana kichwani mwangu, mtoto huyo atakuwa anafanya nini huko Black Forest?
Yupo mwenyewe au na mama yake?
Je wapo wenyewe au na watu wengine?
 
*NYUMA YAKO – 15*
*Simulizi za series*

ILIPOISHIA
Nilipotua upande wa pili, nikaanza kukimbia kuufuata ukuta mwingine wa nyumba niliyozamia. Kidogo, nikasikia watu wengine wakitua, walikuwa ni wanaume wawili ambao wananifukuzia! Wakaanza kurusha risasi kwa fujo! Kwa pupa!
ENDELEA
Basi haraka nikachumpa kuuvuka ukuta mwingine, hapa hata sikuushika ukuta huu bali kuruka kama samaki. Nikatua kwa ustadi na kisha kukimbia upesi kwanguvu zote kuufuata ukuta mwingine, nao nikiwa nimeukaribia, wanaonikimbiza wakawa wametua. Wakaendelea kufyatua risasi kama njugu!
Hapa moja ikanipunyua mkono na kunisababishia jeraha. Ila sikukoma kukimbia kuokoa nafsi yangu. Nikaruka tena kwenye ukuta mwingine na mwingine na mwingine, alafu nikajificha pahala.
Wale watesi wangu wakasonga wakiwa wameduwaa. Wakatazama kushoto na kulia mimi nikiwa nawachora toka kwenye ua kubwa. Hawakuwa wananiona. Ila kama sijakosea, mmoja wao akahisi huenda naweza nikawa nimejibana nyuma ya ua. Nikaona akimshtua mwenzake akitazama eneo nililopo.
Kuona hivyo, basi upesi nikachomoka na kuwafyatulia risasi. Wote wakalala chini na kunipa amani kwa muda. Nikatoka hapo nyuma ya ua na kukimbia upesi. Nikaruka ukuta mwingine na kuzama barabarani, sikuona mtu nyuma, nilikuwaa mwenyewe sasa. Kidogo nikakutana na gari, nikasimamisha na kumwamuru dereva atoke ndani, alipotii nikazama ndani ya gari na kutimka.
Ila sikufika mbali sana na hilo gari, nikaliacha na kudaka lingine. Nalo liliponisogeza umbali kidogo, nikaliacha na kupanda basi la uma. Nikaenda kabisa nyuma ya basi na kusimama huko. Nilijihisi salama sasa.
Nikafika hotelini na nikiwa naelekea chumbani mwangu, dada wa mapokezi akaniita. Mwanamke mwenye sura pole na mashavu mapana ndani ya sare. Nikamjongea taratibu nikiwa najiuliza nini shida? Akanitazama na kisha akaangalia tarakilishi yake na kuniuliza, “Kuna mgeni wako ulimtuma?”
“Mgeni?”
“Ndio! Kuna mwanaume alikuja hapa kukuulizia.”
“Aliniuliziaje?” nikatahamaki. Basi yule mhudumu akanambia kuwa alitumia maelezo ya mwonekano wangu, na hivyo alivyoniona tu akapata kujua kuwa ndiye mimi. Nami nikamuuliza mtu huyo aonekanaje? Akanieleza.
Maelezo yake yakajenga picha kichwani mwangu kuwa mtu huyo atakuwa ni miongoni mwa wale wajamaa ambao nilipanda nao basi kabla sijawapotea.
Ina maana wameshajua makazi yangu mapya? Nikaona hapa si mahali pa kukaa tena. Nikanyookea chumbani mwangu na kuanza kukusanya vitu muhimu kutoka kwenye begi, haswa pesa na kadi. Lakini kabla sijatoka, nikasikia hodi mlangoni! Nikatulia tuli nikipepesapepesa macho yangu. Kidogo sauti ya kiume ikasema, “mhudumu!” kisha kugonga tena mlango.
Sikusema kitu. Nikaweka silaha yangu mkononi na kujongea mlango. Sijaufikia, nikastaajabu mlango umekumbwa na teke! Ukang’oka na kunivamia na kunidondosha chini!
Kutazama, nikamwona mwanaume akiwa amevalia nguo nyeusi. Sura yake haikuwa ngeni. Alikuwa ni miongoni mwa wale wanaume niliopanda nao basi kabla sijawapotea. Mkononi mwake alikuwa amebebelea bunduki!
Basi haraka nikaunyanyua mlango na kujikinga nao. Bwana yule akatupa risasi kama tano vile pasipo kupumzika, zote zikaishia mlangoni. Mimi nilipochomoza na kumtwanga yangu moja, akawa amekwisha! Alidondoka chini kama mzigo akiwa ameachama mdomo.
Upesi nikanyanyuka na kumtazama. Punde nikasikia sauti kali ya mwanamke ikipiga yowe huko mbali. Hapa nikahisi hamna tena usalama, huenda kuna wavamizi wengine! Nikatoka ndani kushika korido, ila uso kwa uso, umbali wa kama hatua kumi na nane, nikaonana na wanaume wawili wakiwa wanakuja wamebebelea bunduki!
Upesi nikarudi ndani. Nikasikia vishindo vya watu vikikimbia kuja. Nikavunja dirisha na kutokea nje. Chumba changu kilikuwa ghorofa ya kwanza, nikarukia huko chini nikitulia pazia lililokuwa limefunikia magari yaliyoegeshwa, kisha nikajitupia chini na kukimbia!

**

“Kama nisipofanya mambo haya upesi, nadhani yatazidi kuniwia vigumu zaidi na zaidi!” niliteta na Jack nikiwa nimeketi kwenye kiti ndani ya nyumba ya kupumzikia. Niliongea naye kwa muda sana na mwishowe alipokata simu nikajilaza kitandani na kuwaza mambo kadha wa kadha.
Kwa maelezo ambayo nilimpatia Jack, aliniambia yanasawiri na namna alivyokuwa anawaza lakini asiniweke bayana kipi ambacho kipo kichwani mwake, akataka ningoje kwa muda kidogo. Hivyo hapo nilipokuwa nimejilaza nilikuwa namngoja.
Zikapita kama dakika sita, usingizi ukaanza kuninyemelea. Nilisinzia nikipambana na macho yangu mazito. Ikiwa kama dakika ya nane kama niko sahihi, simu yangu ndiyo ikaita Jack akirudi tena hewani.
“Sasa sikia …” akaanza kwa kauli hiyo kisha akanambia kuhusu yule mtoto ambaye alikuwa anakaa na mama yake kwenye nyumba yenye anwani 2345. Kumbe alishamtambua mtoto huyo na kunituma kwenda kumuulizia mwonnekano wake ilikuwa ni kwa ajili ya kuthibitisha tu.
Lakini mtoto huyo ni nani haswa? Hakuwa anafahamu japo nishamwambia kuwa ni Mmarekani. Na kuhusu mama yake, Jack hakuwa na taarifa naye hata kidogo!
Ilikuwa ni ajabu kidogo kwani Jack aliniambia alifanikiwa kum – trace mtoto huyo kupitia game la ‘Subway Surfers’ ambalo humo ndani, kwa ridhaa, wachezaji huweza kuunganisha na mtandao wao wa Facebook ili washindane na marafiki zao.
Lakini zaidi, unaweza ukatazama kuona wachezaji gani wana points nyingi ulimwengu mzima. Basi kwa kupitia huko, Jack Pyong akakuta jina la MUNICH 2345. Na aliposaka jina hilo mtandaoni akitumia picha aliyoiona humo mchezoni, akafanikiwa kulipata. Kwa ufupi, jina la mtoto huyo huitwa Brussels, lakini jina lake la mchezoni hutumia MUNICH 2345, yaani jina la anwani ya nyumba alokuwa anakaa.
“Sasa tunaweza tukampata wapi yeye na mama yake?” nikamuuliza Jack.
“Usijali,” Jack akan’toa hofu. “Mpaka kufikia kesho n’takuwa nishapata!” tukamaliza maongezi na mie nikajilaza sasa.
Nikiwa usingizini, nadhani kwasababu ya kupitia purukushani hapa karibuni za mara kwa mara, nikaota ndoto ya kunishtua. Nilijikuta nikinyanyuka upesi na kushikilia bunduki yangu lakini nilipotazama huku na kule sikuona kitu. Nilikuwa mwenyewe!
Kidogo usingizi ukawa umenitoka. Nikashika simu yangu na kuperuzi, nikaukuta ujumbe toka kwa Daniele. Alikuwa akinijulia hali na kuniuliza wapi nilipofikia. Ujumbe huo ulikuwa umetumwa dakika tisa nyuma.
Nikaujibu kisha nikaweka simu pembeni. Sikutarajia kama Daniele angeujibu kwani ilipita muda kidogo tangu autume lakini kinyume na matarajio yangu, akajibu punde tu. Na hapo ndipo nilipoingia naye kwenye uwanja wa kuchat kw muda kidogo akinieleza mambo kadha wa kadha.
Lakini zaidi lililokamata hisia zangu ni mashambulio mawili ambayo Daniele na timu yake waliyapitia ingali wakiwa kazini. Kwa mujibu wa Daniele, walishambuliwa na mwanamke mmoja na wanaume watatu. Ingawa walikuwa wameficha nyuso zao lakini waliwatambua kutokana na maumbo yao ya mwili.
Shambulio la kwanza lilitokea wakiwa wametoka kwenye nyumba ya Makamu wa Raisi na ya pili wakitoka kwenye ofisi ya Wizara ya usalama wa ndani!
“Watu wangu wawili wameuawa kwasababu ya mashambulizi hayo, na hata kupotea kwa baadhi ya nyaraka. Nimepeleka taarifa kwenye uongozi, wakaniongezea ulinzi.”
Nami nikamshauri kushirikiana na Jack Pyong kwenye mambo kadhaa haswa ya kiteknolojia kwani anaweza kumsaidia. Kwa mawasiliano zaidi nikampatia namba za Jack na hata kumtaarifu Jack juu ya swala hilo.
Baada ya hapo, nikalala.

**

Saa kumi na moja asubuhi…

Nina uhakika simu ilinguruma mara moja tu kabla sijaamka. Niliitazama nikiwa nimekunja uso wa usingizi, kwenye kioo nikaona nimetumiwa na Jack ‘location’ ya eneo ambalo naweza kumpata yule mtoto ambaye tulimjadili.
Basi usingizi ukanikata papo hapo, nikanyanyuka nikaoga na kuvaa kisha kushika barabara kwenda huko ambako Jack alikuwa amenielekeza. Mahali mbali kabisa na jiji la Munich. Tena msituni. Ulikuwa ni kama mwendo wa masaa matano kasoro kwa basi mpaka kufika huko. Huko wenye msitu huo wa ‘Black forest’ ambapo ndipo location ilipoongoza.
Mpaka kupata na kupanda basi ikawa tayari ni saa moja asubuhi, safari ikaanza. Kama kawaida nilikuwa nimekaa nyuma ili nipate nafasi ya kutazama abiria wote ndani ya basi, watakaoshuka na wale watakaoingia.
Nikiwa nimekaa huko nikawa nawaza sana kichwani mwangu, mtoto huyo atakuwa anafanya nini huko Black Forest?
Yupo mwenyewe au na mama yake?
Je wapo wenyewe au na watu wengine?
Mbona kidogo kidogo
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom