Nyuma yako - Riwaya ya SteveMollel

Nyuma yako - Riwaya ya SteveMollel

*NYUMA YAKO – 21*
*Simulizi za series*

ILIPOISHIA
Nikamtazama kwa macho makali kwa sekunde tatu alafu nikamuuliza, “Alfonso ni nani?”
Alipotaka kusema hajui, kabla hajamalizia kauli yake, nikamkita na kitako cha bunduki pembeni ya jicho lake la kushoto, “Shenzi!”
Akalia kwa maumivu. Alivuja damu. Nikamdaka nywele zake kwanguvu na kumuuliza tena, “Alfonso ni nani?”
ENDELEA
Jicho lake la kushoto lilivilia damu. Kweli aliumia. Ila sikumwonyesha uso wa huruma bali ule uonyeshao kuwa mengi yanafuata hapo mbele endapo akiwa mkaidi.
Akalia kwa muda kidogo. Na mafua akapata. Akan’tazama na kunambia kwa uso mtakatifu, “Simjui Alfonso mimi!”
Nikamdaka nywele zake kwanguvu sana kisha nikamuuliza amemjuaje Britney? Na zile soga alizokuwa ananipa je? Akasema alidanganya! Yeye si rafiki wa Britney kama alivyosema. Yote aliyosema alidanganya.
Na vipi kuhusu Henessy? Alimjuaje? Nikapata swali. Nacho akaniambia hakuwa anafahamu lolote lile kumhusu. Yote hayo alipandikiziwa mdomoni akayaseme.
“Nani alikupandikizia hayo?” nikamuuliza.
“Huyu!” akaninyooshea kidole yule jamaa aliyelala kando. “Ni huyu hapaa!”
Lakini hapana! Mimi haikuniingia akilini kuwa mwanamke huyu hajui lolote kumhusu Alfonso. Ni kwamba tu nguvu yangu haikutosha kuondoa gamba lake alimojifichia.
Hivyo nikaona kuna haja ya mimi kuongeza ‘pressure’ kidogo niuone uhalisia. Endapo akifaulu jaribio hilo basi ningemwacha huru.
Nikadaka mkono wake wa kulia na kuvunja kidole chake cha mwisho! Kat! Akapiga yowe kwa maumivu makali. Sikumwonea huruma, nikadaka tena kidole kinachofuata akiwa anajitetea kujikomboa, nacho nikakiminya kukivunja, akapiga kelele, “Najua!”
“Unajua nini?” nikamuuliza nikiendelea kubinya kidole hicho karibu na kukivunja.
“Namjua Alfonso! Tafadhali niachie!” nikamwachia na kumwambia, “Enhe, ni nani na wapi alipo?”
Akatetema kwanza kwa kilio akitazama kidole chake kilichokuwa kimepinda. Akajaribu kukishika, akaishia kulalama kwa maumivu. Akavuta makamasi na kun’tazama kwa hasira na ghadhabu yenye maumivu ndani yake, “wewe ni mnyama!” akasema.
“Mwanamke, sina muda wa kupoteza na wewe,” nikamwonya. “naweza kuwa mnyama wa kupeti ama wa kukutafuna kutokana na mienendo yako. Sasa utasema ama tuendelee kumalizia vidole?”
Akajifuta makamasi na mkono wake wa kushoto kabla hajaanza kusema,
“Alfonso ni bosi wetu, anaishi huku Berlin, Ujerumani. Anatulipa vizuri sana, na ametuahidi kutulipa zaidi tutakapomaliza kazi yetu.”
“Kazi gani hiyo?”
“Sikia, ajenti. Mimi sijui mengi sana, na ukinilazimisha niseme hivyo hivyo nitaishia kukudanganya. Ninachojua ni kwamba, Alfonso anamhitaji huyo mtoto, Henessy. Ndiye pekee aliyebakia baada ya mama yake kufariki.”
“Kwanini anawahitaji hao watu? Wa kitu gani?”
“Kwasababu ya Raisi! Raisi wa Marekani. Hii ni familia yake Raisi. Henessy ni …” nikamsihi apunguze sauti yule mtoto asisikie. “Henessy ni mtoto wa Raisi!”
“Unatania, sio?”
“Unauona huu ni muda wa matani, ajenti? Nikiwa nimevunjwa kidole na kubabuliwa kichwa?”
“Umejuaje kama hii ni familia ya Raisi? Hamna mtu anayelijua hilo!”
“Ndio ujue sasa kuwa ajenti hakumaanishi kujua kila kitu kuhusu Marekani. Hata Secret Service hawaitambui siri hii. Hii ni familia ya siri!”
“Lakini …”
“Sikia, unafahamu kuwa Britney alikuwa ni pornstar, mcheza picha za ngono maarufu, unadhani Raisi gani angebeba sifa hiyo? Tena amezaa naye! Angemwambia nani juu ya hilo? Huoni ni kujichafua, kuchafua chama, kuchafua taifa? … ndiyo maana ni familia ya siri! … Raisi alikuwa ana mahusiano na Britney! Mcheza sinema za ngono!”
Habari hii haikuwa ya kawaida. Lilikuwa ni jambo kubwa tena likisemwa ndani ya van ya kawaida, nchi ngeni! Likikuwa ni jambo nyeti la kuteka vichwa vya habari ulimwengu mzima!
“Una uhakika na unachoongea?”
“Ajenti, kwa akili yako unadhani kuna haja gani ya kusumbuka na mcheza ngono? Sisi si ISIS au Boko Haram useme tunateka raia yeyote wa Marekani!”
“Sasa kwanini Alfonso anataka hii familia? Na Raisi yupo wapi?”
Nilikuambia awali, mimi sijui mengi. Na hata huyu uliyemziraisha hapa, hatokueleza kipya. Wote tunachojua na tulichopewa kufanya ni kutafuta familia hii na kuiweka mikononi mwetu. Hayo mengine, anayajua Alfonso tu!”
“Niambie wapi anapatikana.”
Kabla hajasema akasita kidogo.

***

Basi safari yangu ya kurudi Marekani jioni ya hii siku ilibidi niifute ili nipate kufuatilia haya yaliyojiri.
Nikiwa nimevalia nguo nyeusi ambazo nilizikwapua toka kwa yule jamaa wa kwenye van, nikashuka toka garini na kusonga kuifuata nyumba fulani kubwa inayopatikana upande wa magharibi wa jiji la Berlin.
Nyumba hii ndiyo ambayo nimeelezwa kuwa ya Alfonso kwa mujibu wa mateka wangu. Kwahiyo nilikuwapo hapa nikiwa natarajia kupata majibu ya maswali yangu mawili, mosi, kwanini Alfonso anawinda familia hii ambayo nimeambiwa ni ya Raisi, na pili, Raisi yupo wapi? Niliamini atakuwa ana fahamu!
Nikaudaka ukuta huu mrefu na kuukwea, kisha nikatumbukia ndani. Kwa ufupi, labda tuepushe kupoteza muda, nilitumia kama dakika nane kufika nilipokuwa natakiwa kuwapo. Na huku safari yangu hiyo ikiwa imegharimu maisha ya watu watano.
Ilikuwa ni usiku wa saa tano, na tofauti na nilivyokuwa nawaza, nikamkuta huyu jamaa ambaye niliamini kuwa ni Alfonso, amelala akikoroma!
Nikamuwekea silaha kichwani na kumnong’oneza aamke kwani nina maongezi naye machache. Alipoamka akashtuka kuonana na sura ngeni. Japo sikuwasha taa, tulikuwa tunaonana vizuri kwasababu ya mwanga wa taa za nje.
Mwanaume huyu alikuwa wa makamo ya hamsini kwa umri japo nywele zake hazikuwa na tembe ya mvi. Mnene kwa umbo lakini anayejiweza. Alikuwa anazungumza kiingereza vizuri kwa lafudhi ya kimarekani hivyo nikajua moja kwa moja ni wa nyumbani..
Akajivuta akiketi kitako kisha akan’tazama, pasi na woga, akaniuliza, “Unataka nini kwangu muda huu?”
Kabla sijamjibu, yeye akaendelea kunena, “Sikia, ajenti.” Sijui alijuaje kama mimi ni ajenti. Pengine kwa namna nilivyozama ndani. Akiwa ananinyooshea kidole, akawa anasema, “kama umekuja hapa kwa kudhani nina majibu ya maswali yako na ya nchi yako …” akabinua mdomo, “hesabu umefeli!”
“Maswali gani unayoyaongelea wewe?” nikamuliza. Akagunia kifuani. “Sijui Raisi wa Marekani alipo, sawa?’ akanambia akin’kodolea macho. “Kama wewe tu, sijui Raisi wenu alipo! Kama umekuja hapa kuniuliza hilo, basi umefeli.”
Nikaketi kitandani. Sikuamini anachokisema, najua hata mwizi ni ngumu kukiri alhali umemkamata na ngozi.
“Alfonso, haujui Raisi alipo ila unafahamu familia yake. Sio?”
“Ajenti, nimefanya kazi na namiliki klabu nyingi za usiku jijini Los Angeles na Miami. Huko wanawake wanacheza uchi na wengine kujiuza. Britney alikuwa ni mfanyakazi wangu kwa miaka mitano. Unadhani kipi ambacho nisingekijua?”
“Kwanini ukamteka? Yeye pamoja na mwanae!”
Akatikisa kichwa na kusema, “Ungeniuliza kwanza kwanini nipo Ujerumani?”
Kabla sijamuuliza hicho alichosema nimuulize, akakijibu yeye, “Nipo huku toka Marekani, ajenti. Kwasababu ya sera za mbovu za Raisi wako juu ya wawekezaji. Amenifilisi sana. Ameniangusha kiuchumi na sikudhani kama ningekuja kusimama tena. Kwa miaka yake miwili tu, ilitosha kunidhoofisha haswa. …
Ajenti, unadhani nilikuwa tayari kurudi nilipotokea baada ya miaka mingi ya kujenga mfuko wangu?” akatikisa kichwa. “Hapana, siko tayari kupoteza yote ndani ya mfumbo mmoja wa macho. Kumteka kwangu Britney na mwanaye, ni kutaka pesa yangu irudi! Arudishe yale yote ambayo amenipotezea.”
“Kwahiyo umeshapata baada ya hapo?” nikamuuliza.
“Aaaahmm .. kidogoo!” akanijibu akifumba jicho lake moja. “Ila si kama nilivyokuwa nikitarajia. Kama unavyojua, Raisi amepotea. Wapi nitapata pesa?”
Sikumwamini maelezo yake. Niliona kuna haja ya kumsafirisha nimpeleke Marekani akatoe maelezo zaidi. Lakini akanitahadharisha, “Nikirudi Marekani, kila mtu atajua Raisi alitembea na kuzaa na mcheza sinema za ngono maarufu. Nadhani unajua itakuwa ni aibu kiasi gani!”
Nikamtazama mwanaume huyo kisha nikamuuliza, “Alfonso, Raisi yuko wapi?”
Akanipandishia mabega, “sijui! Ajenti, sifahamu hilo!” akasema akin’tolea macho. “mimi mwenyewe natamani apatikane nipate pesa yangu!”
Hapa nikajikuta nanyong’onya. Nilidhani hatua hii itakuwa ya karibu kufikia lengo, kumbe nalijidanganya. Bado nipo mbali!
Sasa na wale waliokuwa wanawashambulia wakina ajenti Daniele kule Marekani, kumuua pia O’Neil, ni watu wengine? Watu wasiohusiana na Alfonso?
Kwa muda nikajikuta nikisahau kama nipo kwenye nyumba ya maadui.

**
 
*NYUMA YAKO --- 22*
*Simulizi za series*

ILIPOISHIA
Sasa na wale waliokuwa wanawashambulia wakina ajenti Daniele kule Marekani, kumuua pia O’Neil, ni watu wengine? Watu wasiohusiana na Alfonso?
Kwa muda nikajikuta nikisahau kama nipo kwenye nyumba ya maadui.
ENDELEA
Nilipomulikwa usoni ndipo nikagutuka na kurudisha akili tukioni. Nikakuna kichwa. Hapa nikambana Alfonso na kumtumikisha twende naye nje kwa usalama wangu. Lakini bwana huyu hakutaka katu hata kunitaka nimuue lakini hatatii agizo langu!
Akacheka.
“Bwana mdogo, hutoweza kutoka hai hapa. Ni bora uka surrender!” akanambia kwa kebehi. Nami nisitake maneno mengi, nikafyatua risasi mbili za upesi pembeni na kichwa chake. Nikamtengenezea maumivu makali sikioni, na kama haitoshi nikamtwanga risasi ya mguuni kisha nikaketi kando yake.
“Haya sasa tukae, utakufa taratibu kwa kupungukiwa na damu!”
Bwana huyo akawa analalama sana kwa maumivu. Huku masikioni na kule miguuni. Alivumilia sana na hakukuwa na wa kumsaidia kwani walinzi wake wasingeweza kuzama ndani kwa kuhofia nitammaliza kabisa mkuu wao.
Nami nisiwe na habari yoyote, nikatoa risasi zangu toka kwenye bunduki, nikibakisha tatu, kisha nikizirudisha tena ndani ya bunduki. Nilipofanya mchezo huo kwa dakika kama tano, nikasimama na kuanza kupekua chumba cha Alfonso.
Alfonso akaniita na kuniambia, “Ewe ajenti, nipeleke hospitali kabla sijafia hapa. Huoni kitanda changu kimefurika damu?”
Nikamtazama na kisha nikaendelea na msako wa mule chumbani. Nikamjibu pasipo kumtazama, “Ulijifanya mkaidi, endelea kukaa hapo mpaka utakapoona kuna haja hiyo!”
Akanisihi, “sikia, mruhusu mmoja wa vijakazi wangu twende nikuonyeshe njia ya kupita chini kwa chini tuondoke hapa. Nakuhakikishia utakuwa salama. Ila uniahidi kunipeleka hospitali!”
Nikamtikisia kichwa, “Hapana, siwezi fanya hivyo. Hamna mtu mwingine yoyote atakayeongozana na sisi. Ni sisi peke yetu tu!”
Akaleta ubishi kidogo hapa ila alipoona hali inazidi kuwa mbaya, akakubali. Nikamnyanyua na kutoka naye ndani ya chumba kuelekea chumba kinachofuata ndani ya nyumba hiyo, humo tukazama na kuuelekea mlango mdogo wa sakafuni, nikaufungua na kuzama humo.
Ilikuwa ni njia ya kutokea nje kisiri. Na mlango huu unawekwa maalumu kwa ajili ya kipindi cha mashambulizi. Hivyo mkiwa mnashambuliwa inakuwa rahisi kwa mkazi kutoroka.
Tukatembea humo na ndani ya kama dakika nane, tukawa tumefika mahali ambapo niliona kuna mwanga wa kutokea nje. Tukakazana, hapo nikiwa namburuta bwana huyu ambaye hakuwa anajiweza. Alikuwa mdhaifu sana na anayehisi maumivu.
Lakini kwa namna alivyokuwa amechoka, hakuwa analalamika tena. Alikuwa ameachama kinywa wazi, anatokwa na jasho jingi. Kwa namna nilivyomwona hakuwa anaweza kudumu baada ya lisaa. Ilinipasa nikazane zaidi kama ningelitaka awe hai.

**

Nilishamkabidhi mtoto ubalozini na safari yangu nikiwa nimeisogeza mbele kwa siku mbili.
Alfonso alikuwa hospitalini akipata matibabu, lakini chini ya uangalizi wa kiusalama. Na mimi … nilikuwa hapa mgahawani nikipata chakula cha mchana. Niliagiza kuku wa kuchoma na vegies.
Si kwamba napendelea sana aina hiyo ya chakula, hapana, ila ndo’ chakula ambacho niliona naweza nikala hapa na kujihesabia nimekula.
Nilipomaliza, nikaagiza sharubati na kunywa taratibu nikiwa natafakari baadhi ya mambo huku nikitazama picha kadhaa kwenye simu yangu, picha ambazo nilizipiga kwenye baadhi ya vitu vya Alfonso kule kwenye nyumba yake.
Nikiwa nakaguakagua, simu yangu ikapigwa tokea ubalozini. Nilipopokea ilikuwa ni sauti ya kike ambayo iliteta maneno machache, “Fika ubalozini.”
Nikalipia bili yangu ya chakula kisha nikaelekea huko upesi. Nikakutana na ‘director’, bwana Phillip, akaniambia baadhi ya mambo ambayo wameyapata toka kwa Alfonso.
Watu hawa niliwaachia kazi kidogo ya kuulizia na kufuatilia nyaraka halali za bwana Alfonso hapa Ujerumani, ikiwemo pia na akaunti zake ili tuone uingizaji na utokaji wa pesa zake tangu Raisi alipopotea.
Basi bwana huyu, Phillip kwa jina, akanambia kuwa wamefanikiwa kupata taarifa nilizoagiza. Jambo hili lilikuwa jepesi kwakuwa niliwapatia baadhi ya picha za kadi zake za benki ambazo mimi nilizitolea kule kwenye chumba cha Alfonso.
Na kwa mujibu wa maelezo ya bwana Phillip, Alfonso alianza kupokea dola laki nane za kimarekani kila mwezi baada ya Raisi kupotea. Hivyo swala hili likanipa tena nguvu kuwa Alfonso atakuwa anajua wapi Raisi alipo. Au basi kama hajui, atakuwa anamjua mtu ambaye anajua.
Kidogo akili yangu ikaanza kuwandawanda kabla sijaituliza kuskiza maneno ninayopewa.
“Ni nani ambaye anamwingizia pesa hizo Alfonso?’ nikauliza.
Bwana Phillip akakuna kidevu alafu akapekua karatasi zake na kunambia, “Anaitwa Payne! Payne Cluster.”
“Umepata taarifa zake?”
“Hapana! Tumejitahidi lakini swala hilo limekuwa gumu. Bado tunalifanyia kazi.”
“imekuaje limekuwa gumu na jina la mwenye akaunti mnalo?”
“Tatizo hatumii akaunti moja,” akasema Bwana Phillip. “Jina ni moja lakini amekuwa akitumia akaunti tofauti tofauti. Na kunaa …” akachomoa tena karatasi na kuitazama, kisha akanambia, “Ila mara ya mwisho, pesa zilitoka kwenye akaunti yenye jina la Katie Rodwell.”
“Huyo mmepata taarifa zake?” nikawahi kuuliza. Akabinua mdomo na kutikisa kichwa. “Hapana. Tangu alipotuma pesa hiyo akaunti yake ikafa. Haipo tena!”
Basi nikaona nisipoteze muda sana, nikachukua taarifa hizi na za maeneo ya uwekwaji wa hizo pesa kisha nikaondoka zangu.
Kilinichomishangaza ni kwamba, maeneo matatu ya mwisho kwa Alfonso kuwekewa pesa ilikuwa ni Ujerumani! Yaani watu waliomwekea hiyo pesa walitumia benki za hapahapa Ujerumani. Inamaanisha watu hawa wapo hapahapa nchini!
Sasa nitawapatia wapi? Nikajiuliza. Njia nyepesi ilikuwa ni kwa kupitia Alfonso mwenyewe. Hivyo nikapanga kwenda kumwona.
Baadae majira ya jioni nikawa hospitalini pembeni ya kitanda cha Alfonso. Baada ya kumjulia hali, nikamuuliza maswali yangu, ni nani Payne na yule Katie ambaye walikuwa wanamwekea pesa kwenye akaunti yake?
Akakohoa kwanza kisha akaniambia, “ajenti, nikikuambia siwafahamu utaamini?”
Kabla sijasema jambo, akasema, “Siwafahamu hao watu. Na kama nilivyokueleza hapo kabla, nilikuwa napokea pesa kwa kuwa na familia ya Raisi. Mtu anayeniwekea pesa, mimi sijali. Najali pesa kuingia kwenye akaunti tu!”
“Alfonso,” nikaita na kuuliza, “mara mbili za mwisho kuwekewa pesa zilitokea Ujerumani. Unanambiaje huwafahamu? Ina maana haukukutana nao?”
“Sikukutana nao,” akanijibu kwa sauti ya chini. “Siwafahamu kabisa, ajenti. Mimi nalikuwa napokea pesa tu na si kingine.”
Nikanyamaza nikimtazama. Naye akan’tazama kwa sekunde kadhaa kabla hajaniomba simu yangu aongee na mtu aliyemtambulisha kama binti yake wa pekee. Anahitaji kumwambia juu ya hali yake. Anadhani atakuwa amefanya jema kumjuza.
“Yuko wapi huyo binti?” nikamuuliza.
“Marekani,” akanijibu na kuongezea, “Anasoma huko. Yeye hana makosa na sitaki ahusishwe na mambo yangu. Nataka asome na aendelee na maisha yake kwa amani.”
Mimi, pasipo ajizi, nikampatia simu yangu akapiga. Nikiwa nimesimamishaa masikio, nikasikia, “Halo, Perry. Unaendeleaje? … vipi shule? … Kuna shida yoyote? … nimekumiss sana mwanangu, natazamia kukuona karibuni, naona kuna haja hiyo … hamna shida, kuwa salama mpenzi wangu … niko sawa … kweli … nimepata majeraha kidogo, nikaja hospitali, Berlin … nitakuwa sawa, si kitu kikubwa. Kwaheri … nakupenda.”
Akanikabidhi simu yangu akitabasamu kwa mbali. Nami nikamuaga na kwenda zangu nikiwa nimeshapanga kufuatilia namba ile alozungumza nayo kwa kumtumia ajenti Daniele.
Nikiwa njiani, ili nisisahau hilo jambo, nikamtafuta ajenti Daniele na kumjuza juu ya Perry na namba yake. Nikamwamchia kazi hiyo anipatie majibu baadae. Nikaelekea kwenye makazi yangu, kisha nikaanza kujiandaa kwenda kule nyumbani kwa Alfonso. Nilihisi kule kutakuwa na kitu ambacho kitanisaidia kujua wapi pakuanzia kutafuta wale watu ambao walikuwa wanamtumia pesa.
Mule chumbani, hamtakosekana nyaraka elekezi.
Basi nikafika huko baada ya nusu saa tu, na kwasababu nilikuwa najua mlango ule wa siri, nikauzamia na kuibukia ndani kisha moja kwa moja chumbani mwa Alfonso.
Nilifanya kila jambo kwa utulivu na ukimya kweli. Sikutoa hata punje ya sauti. Nikiwa nasakasaka, nikapata baadhi ya makabrasha ambayo niliyapiga picha kwa simu, ila kidogo nikasikia sauti ya gari ikiingia eneoni.
Nikasonga dirishani na kuchungulia nje. Huko nikaoma BMW x6 nyeusi. Toka kwenye gari hiyo, wakashuka wanaume watatu waliovalia suti. Mmoja wao, hakuwa mgeni machoni pangu.
Nilihisi nimeona vibaya, ila nilipozidi kuangaza nikagundua nilikuwa sahihi. Bwana huyo hakuwa mgeni machoni pangu! Bwana huyo alikuwa ni yule ajenti ambaye alikuwa anahusika na kumlinda Raisi kisha akapotea kwa kusemekana amefia ndani ya nyumba yake iliyoungua moto!
Kumbe yu hai!
Kumbe wanajuana na Alfonso!

**
 
*NYUMA YAKO --- 22*
*Simulizi za series*

ILIPOISHIA
Sasa na wale waliokuwa wanawashambulia wakina ajenti Daniele kule Marekani, kumuua pia O’Neil, ni watu wengine? Watu wasiohusiana na Alfonso?
Kwa muda nikajikuta nikisahau kama nipo kwenye nyumba ya maadui.
ENDELEA
Nilipomulikwa usoni ndipo nikagutuka na kurudisha akili tukioni. Nikakuna kichwa. Hapa nikambana Alfonso na kumtumikisha twende naye nje kwa usalama wangu. Lakini bwana huyu hakutaka katu hata kunitaka nimuue lakini hatatii agizo langu!
Akacheka.
“Bwana mdogo, hutoweza kutoka hai hapa. Ni bora uka surrender!” akanambia kwa kebehi. Nami nisitake maneno mengi, nikafyatua risasi mbili za upesi pembeni na kichwa chake. Nikamtengenezea maumivu makali sikioni, na kama haitoshi nikamtwanga risasi ya mguuni kisha nikaketi kando yake.
“Haya sasa tukae, utakufa taratibu kwa kupungukiwa na damu!”
Bwana huyo akawa analalama sana kwa maumivu. Huku masikioni na kule miguuni. Alivumilia sana na hakukuwa na wa kumsaidia kwani walinzi wake wasingeweza kuzama ndani kwa kuhofia nitammaliza kabisa mkuu wao.
Nami nisiwe na habari yoyote, nikatoa risasi zangu toka kwenye bunduki, nikibakisha tatu, kisha nikizirudisha tena ndani ya bunduki. Nilipofanya mchezo huo kwa dakika kama tano, nikasimama na kuanza kupekua chumba cha Alfonso.
Alfonso akaniita na kuniambia, “Ewe ajenti, nipeleke hospitali kabla sijafia hapa. Huoni kitanda changu kimefurika damu?”
Nikamtazama na kisha nikaendelea na msako wa mule chumbani. Nikamjibu pasipo kumtazama, “Ulijifanya mkaidi, endelea kukaa hapo mpaka utakapoona kuna haja hiyo!”
Akanisihi, “sikia, mruhusu mmoja wa vijakazi wangu twende nikuonyeshe njia ya kupita chini kwa chini tuondoke hapa. Nakuhakikishia utakuwa salama. Ila uniahidi kunipeleka hospitali!”
Nikamtikisia kichwa, “Hapana, siwezi fanya hivyo. Hamna mtu mwingine yoyote atakayeongozana na sisi. Ni sisi peke yetu tu!”
Akaleta ubishi kidogo hapa ila alipoona hali inazidi kuwa mbaya, akakubali. Nikamnyanyua na kutoka naye ndani ya chumba kuelekea chumba kinachofuata ndani ya nyumba hiyo, humo tukazama na kuuelekea mlango mdogo wa sakafuni, nikaufungua na kuzama humo.
Ilikuwa ni njia ya kutokea nje kisiri. Na mlango huu unawekwa maalumu kwa ajili ya kipindi cha mashambulizi. Hivyo mkiwa mnashambuliwa inakuwa rahisi kwa mkazi kutoroka.
Tukatembea humo na ndani ya kama dakika nane, tukawa tumefika mahali ambapo niliona kuna mwanga wa kutokea nje. Tukakazana, hapo nikiwa namburuta bwana huyu ambaye hakuwa anajiweza. Alikuwa mdhaifu sana na anayehisi maumivu.
Lakini kwa namna alivyokuwa amechoka, hakuwa analalamika tena. Alikuwa ameachama kinywa wazi, anatokwa na jasho jingi. Kwa namna nilivyomwona hakuwa anaweza kudumu baada ya lisaa. Ilinipasa nikazane zaidi kama ningelitaka awe hai.

**

Nilishamkabidhi mtoto ubalozini na safari yangu nikiwa nimeisogeza mbele kwa siku mbili.
Alfonso alikuwa hospitalini akipata matibabu, lakini chini ya uangalizi wa kiusalama. Na mimi … nilikuwa hapa mgahawani nikipata chakula cha mchana. Niliagiza kuku wa kuchoma na vegies.
Si kwamba napendelea sana aina hiyo ya chakula, hapana, ila ndo’ chakula ambacho niliona naweza nikala hapa na kujihesabia nimekula.
Nilipomaliza, nikaagiza sharubati na kunywa taratibu nikiwa natafakari baadhi ya mambo huku nikitazama picha kadhaa kwenye simu yangu, picha ambazo nilizipiga kwenye baadhi ya vitu vya Alfonso kule kwenye nyumba yake.
Nikiwa nakaguakagua, simu yangu ikapigwa tokea ubalozini. Nilipopokea ilikuwa ni sauti ya kike ambayo iliteta maneno machache, “Fika ubalozini.”
Nikalipia bili yangu ya chakula kisha nikaelekea huko upesi. Nikakutana na ‘director’, bwana Phillip, akaniambia baadhi ya mambo ambayo wameyapata toka kwa Alfonso.
Watu hawa niliwaachia kazi kidogo ya kuulizia na kufuatilia nyaraka halali za bwana Alfonso hapa Ujerumani, ikiwemo pia na akaunti zake ili tuone uingizaji na utokaji wa pesa zake tangu Raisi alipopotea.
Basi bwana huyu, Phillip kwa jina, akanambia kuwa wamefanikiwa kupata taarifa nilizoagiza. Jambo hili lilikuwa jepesi kwakuwa niliwapatia baadhi ya picha za kadi zake za benki ambazo mimi nilizitolea kule kwenye chumba cha Alfonso.
Na kwa mujibu wa maelezo ya bwana Phillip, Alfonso alianza kupokea dola laki nane za kimarekani kila mwezi baada ya Raisi kupotea. Hivyo swala hili likanipa tena nguvu kuwa Alfonso atakuwa anajua wapi Raisi alipo. Au basi kama hajui, atakuwa anamjua mtu ambaye anajua.
Kidogo akili yangu ikaanza kuwandawanda kabla sijaituliza kuskiza maneno ninayopewa.
“Ni nani ambaye anamwingizia pesa hizo Alfonso?’ nikauliza.
Bwana Phillip akakuna kidevu alafu akapekua karatasi zake na kunambia, “Anaitwa Payne! Payne Cluster.”
“Umepata taarifa zake?”
“Hapana! Tumejitahidi lakini swala hilo limekuwa gumu. Bado tunalifanyia kazi.”
“imekuaje limekuwa gumu na jina la mwenye akaunti mnalo?”
“Tatizo hatumii akaunti moja,” akasema Bwana Phillip. “Jina ni moja lakini amekuwa akitumia akaunti tofauti tofauti. Na kunaa …” akachomoa tena karatasi na kuitazama, kisha akanambia, “Ila mara ya mwisho, pesa zilitoka kwenye akaunti yenye jina la Katie Rodwell.”
“Huyo mmepata taarifa zake?” nikawahi kuuliza. Akabinua mdomo na kutikisa kichwa. “Hapana. Tangu alipotuma pesa hiyo akaunti yake ikafa. Haipo tena!”
Basi nikaona nisipoteze muda sana, nikachukua taarifa hizi na za maeneo ya uwekwaji wa hizo pesa kisha nikaondoka zangu.
Kilinichomishangaza ni kwamba, maeneo matatu ya mwisho kwa Alfonso kuwekewa pesa ilikuwa ni Ujerumani! Yaani watu waliomwekea hiyo pesa walitumia benki za hapahapa Ujerumani. Inamaanisha watu hawa wapo hapahapa nchini!
Sasa nitawapatia wapi? Nikajiuliza. Njia nyepesi ilikuwa ni kwa kupitia Alfonso mwenyewe. Hivyo nikapanga kwenda kumwona.
Baadae majira ya jioni nikawa hospitalini pembeni ya kitanda cha Alfonso. Baada ya kumjulia hali, nikamuuliza maswali yangu, ni nani Payne na yule Katie ambaye walikuwa wanamwekea pesa kwenye akaunti yake?
Akakohoa kwanza kisha akaniambia, “ajenti, nikikuambia siwafahamu utaamini?”
Kabla sijasema jambo, akasema, “Siwafahamu hao watu. Na kama nilivyokueleza hapo kabla, nilikuwa napokea pesa kwa kuwa na familia ya Raisi. Mtu anayeniwekea pesa, mimi sijali. Najali pesa kuingia kwenye akaunti tu!”
“Alfonso,” nikaita na kuuliza, “mara mbili za mwisho kuwekewa pesa zilitokea Ujerumani. Unanambiaje huwafahamu? Ina maana haukukutana nao?”
“Sikukutana nao,” akanijibu kwa sauti ya chini. “Siwafahamu kabisa, ajenti. Mimi nalikuwa napokea pesa tu na si kingine.”
Nikanyamaza nikimtazama. Naye akan’tazama kwa sekunde kadhaa kabla hajaniomba simu yangu aongee na mtu aliyemtambulisha kama binti yake wa pekee. Anahitaji kumwambia juu ya hali yake. Anadhani atakuwa amefanya jema kumjuza.
“Yuko wapi huyo binti?” nikamuuliza.
“Marekani,” akanijibu na kuongezea, “Anasoma huko. Yeye hana makosa na sitaki ahusishwe na mambo yangu. Nataka asome na aendelee na maisha yake kwa amani.”
Mimi, pasipo ajizi, nikampatia simu yangu akapiga. Nikiwa nimesimamishaa masikio, nikasikia, “Halo, Perry. Unaendeleaje? … vipi shule? … Kuna shida yoyote? … nimekumiss sana mwanangu, natazamia kukuona karibuni, naona kuna haja hiyo … hamna shida, kuwa salama mpenzi wangu … niko sawa … kweli … nimepata majeraha kidogo, nikaja hospitali, Berlin … nitakuwa sawa, si kitu kikubwa. Kwaheri … nakupenda.”
Akanikabidhi simu yangu akitabasamu kwa mbali. Nami nikamuaga na kwenda zangu nikiwa nimeshapanga kufuatilia namba ile alozungumza nayo kwa kumtumia ajenti Daniele.
Nikiwa njiani, ili nisisahau hilo jambo, nikamtafuta ajenti Daniele na kumjuza juu ya Perry na namba yake. Nikamwamchia kazi hiyo anipatie majibu baadae. Nikaelekea kwenye makazi yangu, kisha nikaanza kujiandaa kwenda kule nyumbani kwa Alfonso. Nilihisi kule kutakuwa na kitu ambacho kitanisaidia kujua wapi pakuanzia kutafuta wale watu ambao walikuwa wanamtumia pesa.
Mule chumbani, hamtakosekana nyaraka elekezi.
Basi nikafika huko baada ya nusu saa tu, na kwasababu nilikuwa najua mlango ule wa siri, nikauzamia na kuibukia ndani kisha moja kwa moja chumbani mwa Alfonso.
Nilifanya kila jambo kwa utulivu na ukimya kweli. Sikutoa hata punje ya sauti. Nikiwa nasakasaka, nikapata baadhi ya makabrasha ambayo niliyapiga picha kwa simu, ila kidogo nikasikia sauti ya gari ikiingia eneoni.
Nikasonga dirishani na kuchungulia nje. Huko nikaoma BMW x6 nyeusi. Toka kwenye gari hiyo, wakashuka wanaume watatu waliovalia suti. Mmoja wao, hakuwa mgeni machoni pangu.
Nilihisi nimeona vibaya, ila nilipozidi kuangaza nikagundua nilikuwa sahihi. Bwana huyo hakuwa mgeni machoni pangu! Bwana huyo alikuwa ni yule ajenti ambaye alikuwa anahusika na kumlinda Raisi kisha akapotea kwa kusemekana amefia ndani ya nyumba yake iliyoungua moto!
Kumbe yu hai!
Kumbe wanajuana na Alfonso!

**
Thanks Steve
 
*NYUMA YAKO – 21*
*Simulizi za series*

ILIPOISHIA
Nikamtazama kwa macho makali kwa sekunde tatu alafu nikamuuliza, “Alfonso ni nani?”
Alipotaka kusema hajui, kabla hajamalizia kauli yake, nikamkita na kitako cha bunduki pembeni ya jicho lake la kushoto, “Shenzi!”
Akalia kwa maumivu. Alivuja damu. Nikamdaka nywele zake kwanguvu na kumuuliza tena, “Alfonso ni nani?”
ENDELEA
Jicho lake la kushoto lilivilia damu. Kweli aliumia. Ila sikumwonyesha uso wa huruma bali ule uonyeshao kuwa mengi yanafuata hapo mbele endapo akiwa mkaidi.
Akalia kwa muda kidogo. Na mafua akapata. Akan’tazama na kunambia kwa uso mtakatifu, “Simjui Alfonso mimi!”
Nikamdaka nywele zake kwanguvu sana kisha nikamuuliza amemjuaje Britney? Na zile soga alizokuwa ananipa je? Akasema alidanganya! Yeye si rafiki wa Britney kama alivyosema. Yote aliyosema alidanganya.
Na vipi kuhusu Henessy? Alimjuaje? Nikapata swali. Nacho akaniambia hakuwa anafahamu lolote lile kumhusu. Yote hayo alipandikiziwa mdomoni akayaseme.
“Nani alikupandikizia hayo?” nikamuuliza.
“Huyu!” akaninyooshea kidole yule jamaa aliyelala kando. “Ni huyu hapaa!”
Lakini hapana! Mimi haikuniingia akilini kuwa mwanamke huyu hajui lolote kumhusu Alfonso. Ni kwamba tu nguvu yangu haikutosha kuondoa gamba lake alimojifichia.
Hivyo nikaona kuna haja ya mimi kuongeza ‘pressure’ kidogo niuone uhalisia. Endapo akifaulu jaribio hilo basi ningemwacha huru.
Nikadaka mkono wake wa kulia na kuvunja kidole chake cha mwisho! Kat! Akapiga yowe kwa maumivu makali. Sikumwonea huruma, nikadaka tena kidole kinachofuata akiwa anajitetea kujikomboa, nacho nikakiminya kukivunja, akapiga kelele, “Najua!”
“Unajua nini?” nikamuuliza nikiendelea kubinya kidole hicho karibu na kukivunja.
“Namjua Alfonso! Tafadhali niachie!” nikamwachia na kumwambia, “Enhe, ni nani na wapi alipo?”
Akatetema kwanza kwa kilio akitazama kidole chake kilichokuwa kimepinda. Akajaribu kukishika, akaishia kulalama kwa maumivu. Akavuta makamasi na kun’tazama kwa hasira na ghadhabu yenye maumivu ndani yake, “wewe ni mnyama!” akasema.
“Mwanamke, sina muda wa kupoteza na wewe,” nikamwonya. “naweza kuwa mnyama wa kupeti ama wa kukutafuna kutokana na mienendo yako. Sasa utasema ama tuendelee kumalizia vidole?”
Akajifuta makamasi na mkono wake wa kushoto kabla hajaanza kusema,
“Alfonso ni bosi wetu, anaishi huku Berlin, Ujerumani. Anatulipa vizuri sana, na ametuahidi kutulipa zaidi tutakapomaliza kazi yetu.”
“Kazi gani hiyo?”
“Sikia, ajenti. Mimi sijui mengi sana, na ukinilazimisha niseme hivyo hivyo nitaishia kukudanganya. Ninachojua ni kwamba, Alfonso anamhitaji huyo mtoto, Henessy. Ndiye pekee aliyebakia baada ya mama yake kufariki.”
“Kwanini anawahitaji hao watu? Wa kitu gani?”
“Kwasababu ya Raisi! Raisi wa Marekani. Hii ni familia yake Raisi. Henessy ni …” nikamsihi apunguze sauti yule mtoto asisikie. “Henessy ni mtoto wa Raisi!”
“Unatania, sio?”
“Unauona huu ni muda wa matani, ajenti? Nikiwa nimevunjwa kidole na kubabuliwa kichwa?”
“Umejuaje kama hii ni familia ya Raisi? Hamna mtu anayelijua hilo!”
“Ndio ujue sasa kuwa ajenti hakumaanishi kujua kila kitu kuhusu Marekani. Hata Secret Service hawaitambui siri hii. Hii ni familia ya siri!”
“Lakini …”
“Sikia, unafahamu kuwa Britney alikuwa ni pornstar, mcheza picha za ngono maarufu, unadhani Raisi gani angebeba sifa hiyo? Tena amezaa naye! Angemwambia nani juu ya hilo? Huoni ni kujichafua, kuchafua chama, kuchafua taifa? … ndiyo maana ni familia ya siri! … Raisi alikuwa ana mahusiano na Britney! Mcheza sinema za ngono!”
Habari hii haikuwa ya kawaida. Lilikuwa ni jambo kubwa tena likisemwa ndani ya van ya kawaida, nchi ngeni! Likikuwa ni jambo nyeti la kuteka vichwa vya habari ulimwengu mzima!
“Una uhakika na unachoongea?”
“Ajenti, kwa akili yako unadhani kuna haja gani ya kusumbuka na mcheza ngono? Sisi si ISIS au Boko Haram useme tunateka raia yeyote wa Marekani!”
“Sasa kwanini Alfonso anataka hii familia? Na Raisi yupo wapi?”
Nilikuambia awali, mimi sijui mengi. Na hata huyu uliyemziraisha hapa, hatokueleza kipya. Wote tunachojua na tulichopewa kufanya ni kutafuta familia hii na kuiweka mikononi mwetu. Hayo mengine, anayajua Alfonso tu!”
“Niambie wapi anapatikana.”
Kabla hajasema akasita kidogo.

***

Basi safari yangu ya kurudi Marekani jioni ya hii siku ilibidi niifute ili nipate kufuatilia haya yaliyojiri.
Nikiwa nimevalia nguo nyeusi ambazo nilizikwapua toka kwa yule jamaa wa kwenye van, nikashuka toka garini na kusonga kuifuata nyumba fulani kubwa inayopatikana upande wa magharibi wa jiji la Berlin.
Nyumba hii ndiyo ambayo nimeelezwa kuwa ya Alfonso kwa mujibu wa mateka wangu. Kwahiyo nilikuwapo hapa nikiwa natarajia kupata majibu ya maswali yangu mawili, mosi, kwanini Alfonso anawinda familia hii ambayo nimeambiwa ni ya Raisi, na pili, Raisi yupo wapi? Niliamini atakuwa ana fahamu!
Nikaudaka ukuta huu mrefu na kuukwea, kisha nikatumbukia ndani. Kwa ufupi, labda tuepushe kupoteza muda, nilitumia kama dakika nane kufika nilipokuwa natakiwa kuwapo. Na huku safari yangu hiyo ikiwa imegharimu maisha ya watu watano.
Ilikuwa ni usiku wa saa tano, na tofauti na nilivyokuwa nawaza, nikamkuta huyu jamaa ambaye niliamini kuwa ni Alfonso, amelala akikoroma!
Nikamuwekea silaha kichwani na kumnong’oneza aamke kwani nina maongezi naye machache. Alipoamka akashtuka kuonana na sura ngeni. Japo sikuwasha taa, tulikuwa tunaonana vizuri kwasababu ya mwanga wa taa za nje.
Mwanaume huyu alikuwa wa makamo ya hamsini kwa umri japo nywele zake hazikuwa na tembe ya mvi. Mnene kwa umbo lakini anayejiweza. Alikuwa anazungumza kiingereza vizuri kwa lafudhi ya kimarekani hivyo nikajua moja kwa moja ni wa nyumbani..
Akajivuta akiketi kitako kisha akan’tazama, pasi na woga, akaniuliza, “Unataka nini kwangu muda huu?”
Kabla sijamjibu, yeye akaendelea kunena, “Sikia, ajenti.” Sijui alijuaje kama mimi ni ajenti. Pengine kwa namna nilivyozama ndani. Akiwa ananinyooshea kidole, akawa anasema, “kama umekuja hapa kwa kudhani nina majibu ya maswali yako na ya nchi yako …” akabinua mdomo, “hesabu umefeli!”
“Maswali gani unayoyaongelea wewe?” nikamuliza. Akagunia kifuani. “Sijui Raisi wa Marekani alipo, sawa?’ akanambia akin’kodolea macho. “Kama wewe tu, sijui Raisi wenu alipo! Kama umekuja hapa kuniuliza hilo, basi umefeli.”
Nikaketi kitandani. Sikuamini anachokisema, najua hata mwizi ni ngumu kukiri alhali umemkamata na ngozi.
“Alfonso, haujui Raisi alipo ila unafahamu familia yake. Sio?”
“Ajenti, nimefanya kazi na namiliki klabu nyingi za usiku jijini Los Angeles na Miami. Huko wanawake wanacheza uchi na wengine kujiuza. Britney alikuwa ni mfanyakazi wangu kwa miaka mitano. Unadhani kipi ambacho nisingekijua?”
“Kwanini ukamteka? Yeye pamoja na mwanae!”
Akatikisa kichwa na kusema, “Ungeniuliza kwanza kwanini nipo Ujerumani?”
Kabla sijamuuliza hicho alichosema nimuulize, akakijibu yeye, “Nipo huku toka Marekani, ajenti. Kwasababu ya sera za mbovu za Raisi wako juu ya wawekezaji. Amenifilisi sana. Ameniangusha kiuchumi na sikudhani kama ningekuja kusimama tena. Kwa miaka yake miwili tu, ilitosha kunidhoofisha haswa. …
Ajenti, unadhani nilikuwa tayari kurudi nilipotokea baada ya miaka mingi ya kujenga mfuko wangu?” akatikisa kichwa. “Hapana, siko tayari kupoteza yote ndani ya mfumbo mmoja wa macho. Kumteka kwangu Britney na mwanaye, ni kutaka pesa yangu irudi! Arudishe yale yote ambayo amenipotezea.”
“Kwahiyo umeshapata baada ya hapo?” nikamuuliza.
“Aaaahmm .. kidogoo!” akanijibu akifumba jicho lake moja. “Ila si kama nilivyokuwa nikitarajia. Kama unavyojua, Raisi amepotea. Wapi nitapata pesa?”
Sikumwamini maelezo yake. Niliona kuna haja ya kumsafirisha nimpeleke Marekani akatoe maelezo zaidi. Lakini akanitahadharisha, “Nikirudi Marekani, kila mtu atajua Raisi alitembea na kuzaa na mcheza sinema za ngono maarufu. Nadhani unajua itakuwa ni aibu kiasi gani!”
Nikamtazama mwanaume huyo kisha nikamuuliza, “Alfonso, Raisi yuko wapi?”
Akanipandishia mabega, “sijui! Ajenti, sifahamu hilo!” akasema akin’tolea macho. “mimi mwenyewe natamani apatikane nipate pesa yangu!”
Hapa nikajikuta nanyong’onya. Nilidhani hatua hii itakuwa ya karibu kufikia lengo, kumbe nalijidanganya. Bado nipo mbali!
Sasa na wale waliokuwa wanawashambulia wakina ajenti Daniele kule Marekani, kumuua pia O’Neil, ni watu wengine? Watu wasiohusiana na Alfonso?
Kwa muda nikajikuta nikisahau kama nipo kwenye nyumba ya maadui.

**
Hii ndio #KAZINABATA
 
*NYUMA YAKO --- 22*
*Simulizi za series*

ILIPOISHIA
Sasa na wale waliokuwa wanawashambulia wakina ajenti Daniele kule Marekani, kumuua pia O’Neil, ni watu wengine? Watu wasiohusiana na Alfonso?
Kwa muda nikajikuta nikisahau kama nipo kwenye nyumba ya maadui.
ENDELEA
Nilipomulikwa usoni ndipo nikagutuka na kurudisha akili tukioni. Nikakuna kichwa. Hapa nikambana Alfonso na kumtumikisha twende naye nje kwa usalama wangu. Lakini bwana huyu hakutaka katu hata kunitaka nimuue lakini hatatii agizo langu!
Akacheka.
“Bwana mdogo, hutoweza kutoka hai hapa. Ni bora uka surrender!” akanambia kwa kebehi. Nami nisitake maneno mengi, nikafyatua risasi mbili za upesi pembeni na kichwa chake. Nikamtengenezea maumivu makali sikioni, na kama haitoshi nikamtwanga risasi ya mguuni kisha nikaketi kando yake.
“Haya sasa tukae, utakufa taratibu kwa kupungukiwa na damu!”
Bwana huyo akawa analalama sana kwa maumivu. Huku masikioni na kule miguuni. Alivumilia sana na hakukuwa na wa kumsaidia kwani walinzi wake wasingeweza kuzama ndani kwa kuhofia nitammaliza kabisa mkuu wao.
Nami nisiwe na habari yoyote, nikatoa risasi zangu toka kwenye bunduki, nikibakisha tatu, kisha nikizirudisha tena ndani ya bunduki. Nilipofanya mchezo huo kwa dakika kama tano, nikasimama na kuanza kupekua chumba cha Alfonso.
Alfonso akaniita na kuniambia, “Ewe ajenti, nipeleke hospitali kabla sijafia hapa. Huoni kitanda changu kimefurika damu?”
Nikamtazama na kisha nikaendelea na msako wa mule chumbani. Nikamjibu pasipo kumtazama, “Ulijifanya mkaidi, endelea kukaa hapo mpaka utakapoona kuna haja hiyo!”
Akanisihi, “sikia, mruhusu mmoja wa vijakazi wangu twende nikuonyeshe njia ya kupita chini kwa chini tuondoke hapa. Nakuhakikishia utakuwa salama. Ila uniahidi kunipeleka hospitali!”
Nikamtikisia kichwa, “Hapana, siwezi fanya hivyo. Hamna mtu mwingine yoyote atakayeongozana na sisi. Ni sisi peke yetu tu!”
Akaleta ubishi kidogo hapa ila alipoona hali inazidi kuwa mbaya, akakubali. Nikamnyanyua na kutoka naye ndani ya chumba kuelekea chumba kinachofuata ndani ya nyumba hiyo, humo tukazama na kuuelekea mlango mdogo wa sakafuni, nikaufungua na kuzama humo.
Ilikuwa ni njia ya kutokea nje kisiri. Na mlango huu unawekwa maalumu kwa ajili ya kipindi cha mashambulizi. Hivyo mkiwa mnashambuliwa inakuwa rahisi kwa mkazi kutoroka.
Tukatembea humo na ndani ya kama dakika nane, tukawa tumefika mahali ambapo niliona kuna mwanga wa kutokea nje. Tukakazana, hapo nikiwa namburuta bwana huyu ambaye hakuwa anajiweza. Alikuwa mdhaifu sana na anayehisi maumivu.
Lakini kwa namna alivyokuwa amechoka, hakuwa analalamika tena. Alikuwa ameachama kinywa wazi, anatokwa na jasho jingi. Kwa namna nilivyomwona hakuwa anaweza kudumu baada ya lisaa. Ilinipasa nikazane zaidi kama ningelitaka awe hai.

**

Nilishamkabidhi mtoto ubalozini na safari yangu nikiwa nimeisogeza mbele kwa siku mbili.
Alfonso alikuwa hospitalini akipata matibabu, lakini chini ya uangalizi wa kiusalama. Na mimi … nilikuwa hapa mgahawani nikipata chakula cha mchana. Niliagiza kuku wa kuchoma na vegies.
Si kwamba napendelea sana aina hiyo ya chakula, hapana, ila ndo’ chakula ambacho niliona naweza nikala hapa na kujihesabia nimekula.
Nilipomaliza, nikaagiza sharubati na kunywa taratibu nikiwa natafakari baadhi ya mambo huku nikitazama picha kadhaa kwenye simu yangu, picha ambazo nilizipiga kwenye baadhi ya vitu vya Alfonso kule kwenye nyumba yake.
Nikiwa nakaguakagua, simu yangu ikapigwa tokea ubalozini. Nilipopokea ilikuwa ni sauti ya kike ambayo iliteta maneno machache, “Fika ubalozini.”
Nikalipia bili yangu ya chakula kisha nikaelekea huko upesi. Nikakutana na ‘director’, bwana Phillip, akaniambia baadhi ya mambo ambayo wameyapata toka kwa Alfonso.
Watu hawa niliwaachia kazi kidogo ya kuulizia na kufuatilia nyaraka halali za bwana Alfonso hapa Ujerumani, ikiwemo pia na akaunti zake ili tuone uingizaji na utokaji wa pesa zake tangu Raisi alipopotea.
Basi bwana huyu, Phillip kwa jina, akanambia kuwa wamefanikiwa kupata taarifa nilizoagiza. Jambo hili lilikuwa jepesi kwakuwa niliwapatia baadhi ya picha za kadi zake za benki ambazo mimi nilizitolea kule kwenye chumba cha Alfonso.
Na kwa mujibu wa maelezo ya bwana Phillip, Alfonso alianza kupokea dola laki nane za kimarekani kila mwezi baada ya Raisi kupotea. Hivyo swala hili likanipa tena nguvu kuwa Alfonso atakuwa anajua wapi Raisi alipo. Au basi kama hajui, atakuwa anamjua mtu ambaye anajua.
Kidogo akili yangu ikaanza kuwandawanda kabla sijaituliza kuskiza maneno ninayopewa.
“Ni nani ambaye anamwingizia pesa hizo Alfonso?’ nikauliza.
Bwana Phillip akakuna kidevu alafu akapekua karatasi zake na kunambia, “Anaitwa Payne! Payne Cluster.”
“Umepata taarifa zake?”
“Hapana! Tumejitahidi lakini swala hilo limekuwa gumu. Bado tunalifanyia kazi.”
“imekuaje limekuwa gumu na jina la mwenye akaunti mnalo?”
“Tatizo hatumii akaunti moja,” akasema Bwana Phillip. “Jina ni moja lakini amekuwa akitumia akaunti tofauti tofauti. Na kunaa …” akachomoa tena karatasi na kuitazama, kisha akanambia, “Ila mara ya mwisho, pesa zilitoka kwenye akaunti yenye jina la Katie Rodwell.”
“Huyo mmepata taarifa zake?” nikawahi kuuliza. Akabinua mdomo na kutikisa kichwa. “Hapana. Tangu alipotuma pesa hiyo akaunti yake ikafa. Haipo tena!”
Basi nikaona nisipoteze muda sana, nikachukua taarifa hizi na za maeneo ya uwekwaji wa hizo pesa kisha nikaondoka zangu.
Kilinichomishangaza ni kwamba, maeneo matatu ya mwisho kwa Alfonso kuwekewa pesa ilikuwa ni Ujerumani! Yaani watu waliomwekea hiyo pesa walitumia benki za hapahapa Ujerumani. Inamaanisha watu hawa wapo hapahapa nchini!
Sasa nitawapatia wapi? Nikajiuliza. Njia nyepesi ilikuwa ni kwa kupitia Alfonso mwenyewe. Hivyo nikapanga kwenda kumwona.
Baadae majira ya jioni nikawa hospitalini pembeni ya kitanda cha Alfonso. Baada ya kumjulia hali, nikamuuliza maswali yangu, ni nani Payne na yule Katie ambaye walikuwa wanamwekea pesa kwenye akaunti yake?
Akakohoa kwanza kisha akaniambia, “ajenti, nikikuambia siwafahamu utaamini?”
Kabla sijasema jambo, akasema, “Siwafahamu hao watu. Na kama nilivyokueleza hapo kabla, nilikuwa napokea pesa kwa kuwa na familia ya Raisi. Mtu anayeniwekea pesa, mimi sijali. Najali pesa kuingia kwenye akaunti tu!”
“Alfonso,” nikaita na kuuliza, “mara mbili za mwisho kuwekewa pesa zilitokea Ujerumani. Unanambiaje huwafahamu? Ina maana haukukutana nao?”
“Sikukutana nao,” akanijibu kwa sauti ya chini. “Siwafahamu kabisa, ajenti. Mimi nalikuwa napokea pesa tu na si kingine.”
Nikanyamaza nikimtazama. Naye akan’tazama kwa sekunde kadhaa kabla hajaniomba simu yangu aongee na mtu aliyemtambulisha kama binti yake wa pekee. Anahitaji kumwambia juu ya hali yake. Anadhani atakuwa amefanya jema kumjuza.
“Yuko wapi huyo binti?” nikamuuliza.
“Marekani,” akanijibu na kuongezea, “Anasoma huko. Yeye hana makosa na sitaki ahusishwe na mambo yangu. Nataka asome na aendelee na maisha yake kwa amani.”
Mimi, pasipo ajizi, nikampatia simu yangu akapiga. Nikiwa nimesimamishaa masikio, nikasikia, “Halo, Perry. Unaendeleaje? … vipi shule? … Kuna shida yoyote? … nimekumiss sana mwanangu, natazamia kukuona karibuni, naona kuna haja hiyo … hamna shida, kuwa salama mpenzi wangu … niko sawa … kweli … nimepata majeraha kidogo, nikaja hospitali, Berlin … nitakuwa sawa, si kitu kikubwa. Kwaheri … nakupenda.”
Akanikabidhi simu yangu akitabasamu kwa mbali. Nami nikamuaga na kwenda zangu nikiwa nimeshapanga kufuatilia namba ile alozungumza nayo kwa kumtumia ajenti Daniele.
Nikiwa njiani, ili nisisahau hilo jambo, nikamtafuta ajenti Daniele na kumjuza juu ya Perry na namba yake. Nikamwamchia kazi hiyo anipatie majibu baadae. Nikaelekea kwenye makazi yangu, kisha nikaanza kujiandaa kwenda kule nyumbani kwa Alfonso. Nilihisi kule kutakuwa na kitu ambacho kitanisaidia kujua wapi pakuanzia kutafuta wale watu ambao walikuwa wanamtumia pesa.
Mule chumbani, hamtakosekana nyaraka elekezi.
Basi nikafika huko baada ya nusu saa tu, na kwasababu nilikuwa najua mlango ule wa siri, nikauzamia na kuibukia ndani kisha moja kwa moja chumbani mwa Alfonso.
Nilifanya kila jambo kwa utulivu na ukimya kweli. Sikutoa hata punje ya sauti. Nikiwa nasakasaka, nikapata baadhi ya makabrasha ambayo niliyapiga picha kwa simu, ila kidogo nikasikia sauti ya gari ikiingia eneoni.
Nikasonga dirishani na kuchungulia nje. Huko nikaoma BMW x6 nyeusi. Toka kwenye gari hiyo, wakashuka wanaume watatu waliovalia suti. Mmoja wao, hakuwa mgeni machoni pangu.
Nilihisi nimeona vibaya, ila nilipozidi kuangaza nikagundua nilikuwa sahihi. Bwana huyo hakuwa mgeni machoni pangu! Bwana huyo alikuwa ni yule ajenti ambaye alikuwa anahusika na kumlinda Raisi kisha akapotea kwa kusemekana amefia ndani ya nyumba yake iliyoungua moto!
Kumbe yu hai!
Kumbe wanajuana na Alfonso!

**
Utamu utamu
 
*NYUMA YAKO 23*
*Simulizi za series*

ILIPOISHIA
Nilihisi nimeona vibaya, ila nilipozidi kuangaza nikagundua nilikuwa sahihi. Bwana huyo hakuwa mgeni machoni pangu! Bwana huyo alikuwa ni yule ajenti ambaye alikuwa anahusika na kumlinda Raisi kisha akapotea kwa kusemekana amefia ndani ya nyumba yake iliyoungua moto!
Kumbe yu hai!
Kumbe wanajuana na Alfonso!
ENDELEA
Nikapata hamu ya kujua zaidi. Nikiwa nimejibana humo ndani watu wale wakaingia ndani ya jengo, na moja kwa moja wakaketi sebuleni huko wakiongea na kupanga mipango yao.
Chumba nilichomo hakikuwa mbali sana na sebule hivyo nikawa nasikia baadhi ya mambo. Na watu hawa walikuwa wakizungumza kwa lugha ya kiingereza, tena kile cha Marekani.
Wakaongea kwa muda mchache sana, kama dakika tano tu, kisha kikao kikakata, nilichokiambulia kikiwa ni haya machache: mosi, kumhusu Alfonso. Hapa waliteta kwa maneno mawili tu, kuwa wamkute, na baada ya hapo wakagusia swala la malipo, pesa itakuja, na mwisho nikiwa nimegundua kuwa bwana yule ambaye ni ajenti wa Secret Service akiitwa jina la PKP.
Kidogo, gari lile BMW x6 likawashwa na watu wale watatu wakajikwea kwenye gari lao ma kuondoka. Hapo ndipo baada ya kama dakika mbili tu, simu yangu ikaita. Sauti ilikuwa kubwa kidogo ukizingatia na ule ukimya uliokuwepo. Nikapokea na kunena kwa kunong’ona. Alikuwa ni bwana wa ubalozini.
Akasema, “Ajenti, Alfonso ametoroshwa hospitalini!”
Sikutaka maelezo zaidi maana sikuwa eneo zuri kuwasiliana hivyo nikapokea habari hiyo na kurudisha simu mfukoni. Kidogo tu, nikasikia mtu akija. Nikahisi mtu huyo atakuwa amesikia ule mlio wa simu yangu. Haraka nikajificha nyuma ya mlango, na punde tu, mlango ukafunguliwa!
Kutazama, bwana huyo hakuingia ndani, aliangaza kwanza kwa kama sekunde nne, na nadhani alipoona cha kutilia shaka, ndipo akazama ndani. Nilipomtazama nikamwona akitazama kule kwenye droo, mojawapo ilikuwa wazi. Akasonga akitupa mlango kwanguvu ujifunge.
Bahati hakutazama nyuma, akasonga kwenda mbele. Hapo ndipo mimi nikatumia hiyo nafasi kumfuata bwana huyo kwa ukimya wa hali ya juu. Nilipomkaribia, akageuka, ila akawa amekawia kwani nilimdaka shingo yake na kumtuliza pia nikambana kinywa.
Alafu kwa usalama wangu zaidi, nikaufunga mlango kwa funguo.
“Nijibu maswali yangu nami nitakubakizia uhai wako,” nikamwambia bwana yule niliyemuweka kwenye himaya yangu. Naye kwasababu alikuwa amebanwa hakuwa na uwezo wa kunena, ikabidi nimwache kidogo.
Akahema kwanguvu sana akitoa macho. Nikampatia kama sekunde nne tu, kisha nikamuuliza, “Yule PKP ni nani yenu?”
Bwana yule akaleta ukaidi. Nami nisifanye ajizi, nikamkaba tena kwanguvu mpaka nilipohisi amepata adabu ndipo nikamwacha na kumuuliza tena, akanijibu ni mshirika mwenzao! Kabla sijapata muda wa kuminya zaidi majibu toka mwilini mwake, huko nje ya chumba nikasikia wakimuulizia bwana huyu. Naye akanambia, “Watakuwapo hapa muda si mrefu na utakuwa mwisho wako!”
Basi nikawa sina muda wa kupoteza tena hapa, nikamziraisha bwana huyu na kutoka humo ndani upesi. Nikaelekea kile chumba kinachofuata ambacho ndipo penye tundu la kuzamia chini kwa chini kutokea nje. Lakini kufika mlangoni hapo, nikaukuta umefungwa! Nilijaribu kuufungua pasipo mafanikio. Sikuelewa nani ameufunga na kwa muda gani! Na wakati huohuo, nikiwa nasikia sauti ya watu wakija huu uelekeo wangu!
Hapa nikaona nichukue maamuzi ya upesi. Nikauvunja mlango huu kwa teke la nguvu kisha nikazama ndani na kuukimbilia mlango ule wa dharura. Nikaufungua na kudumbukia humo alafu upesi nikaanza kukimbia.
Kidogo huko nyuma nikasikia sauti ya watu wakiteta na kufoka, na masikio yangu yakiwa sahihi, watu hao wakazama ndani ya ile chemba ya chini itokayo nje, humo ambapo mimi nilikuwamo!
Nikakimbia sana. Punde sauti za risasi zikaanza kuvuma kuniwinda. Hata niliposhika ngazi kupanda juu, zingine zikagonga ngazi ile ya chuma na kusababisha kelele kali!
Nilipotoka nikaendelea kukimbia, kidogo nikawa nimewahepuka maadui zangu nao hawakunikamata tena!

**

“Hamna mtu huyo!” sauti ya Daniele ilinguruma kwenye simu.
“Una uhakika?” nikamuuliza kwa mashaka. “Jina lake ni Perry!”
“Hayupo huyo mtu!” Daniele akasisitiza. “Tumefuatilia hiyo namba na kubaini haipo huku Marekani ingawa ina ‘code number’ za huku.”
Hapa ndipo nikajiona mjinga. Alfonso alinizidi maarifa. Yule mtu aliyeongea naye hakuwa mwanaye kama alivyosema, bali mtu wake wa kazi. Na kwa kuongea naye akabaini wapi mwanaume huyo alipo na wakaja kumkomboa!
Nikawaza sana. Na hapa ndipo nikajenga hoja kuwa Bwana yule ambaye alikuwa ni ajenti wa Secret Service, ndiye ambaye atakuwa anamtumia pesa huyu Alfonso. Asili ya jina lake hilo, yaani PKP, ni Payne, Katie na Perry! Hayo ni majina yake ya kujificha nyakati za haja.
Hivyo basi, PKP ndiye ‘mastermind’ wa yote haya. Na kwakuwa alikuwaa ajenti anayehusika na kumlinda Raisi basi ni wazi atakuwa anafahamu wapi Raisi alipo!
Ni lazima PKP atafutwe na kukamatwa popote pale kwa gharama yoyote ile. Pengine akiwa mikononi mwangu nitaelewa mtiririko wa yote haya.
Nikafika hospitali na kisha ubalozini, nikapata maelezo juu ya namna ambavyo Alfonso alivyotoroshwa. Watu hao wavamizi walifika hapo hospitali kama majambazi kisha wakawaweka watu chini ya ulinzi na kumkwapua mtu wao!
Hakukuwa na mtu aliyetambulika maana waliziba nyuso zao kwa barakoa. Na tukio hilo lilidumu kwa takribani dakika sita tu, wakawa wameshapotea!
“Sasa tunafanyaje, ajenti?” akaniuliza director. Nikamwomba simu yake na kufanya mawasiliano na Daniele. Nikamjuza mwanamke huyo atafute kila taarifa anayoijua kumhusu ajenti yule wa Secret Service ambaye alipotea kwenye mazingira ya kutatanisha!
Aliponiuliza sababu, nikamwambia kwa ufupi tu, bwana huyo yu hai na yupo Ujerumani.
“Kweli?”
“Ndio, na anashirikiana na Alfonso.”
“Sawa. Nitalifanyia kazi!” akamalizia Daniele kisha akakata simu.

**

Nikiwa nimeamka na kuoga, Daniele akanipigia simu na kunipatia taarifa zote ambazo amezipata toka kwa yule ajenti. Kumbe jina lake ni Ian Livermore. Amefanyia kazi USSS kwa takribani miaka sita.
Kuhusu familia yake, haikuwa inajulikana. Hakuwa na mke wala mtoto, wazazi wake inasemekana walishafariki miaka kadhaa huko nyuma.
Na kuhusu akaunti zake nazo zilishafungwa. Hakuna rekodi yoyote ya kuingia wala kutoka kwa pesa tangu iliposemekana kuwa amekufa!
Mambo hayo kidogo yakanivunja moyo. Sikuona mwanya wa kupata chochote kitu hapo, ila kwa mwishowe Daniele akanipa tumaini. Anamfuatilia rafiki yake na bwana huyo Ian akitarajia kupata kitu toka kwake.
“Mpaka jioni ntakuwa na la kukwambia!” akamalizia vivyo kabla ya kukata simu.
Nami kuendeleza upelelezi wa hilo jambo, nikaanza kutulia kuangaza yale makabrasha ambayo niliyapiga picha kule kwenye nyumba ya Alfonso. Nikitazama na kukagua vema, kuvuta picha kwa ukubwa na kwa udogo.
Mojawapo ya nyaraka hizo nikagundua ni mkataba. Mkataba huu aliusaini ndugu mmoja anayeitwa Bevin Casen na Alfonso Lundergan. Ulikuwa ni mkataba wa mashirikiano kwa makubaliano ya kulipwa ujira wa takribani dola za kimarekani milioni moja kila mwezi!
Huyu Bevin Casen ni nani? Nikapata maswali. Nikaendelea kupekuapekua na kuja kubaini kuwa pia kulikuwa na mawasiliano ya bwana Ian. Hapa nikajikuta natabasamu. Angalau nilipata pa kuanzia kumtafuta mtu yule.

**

“Ndipo hapa!” akasema dereva uber. Nami kabla sijafanya lolote nikatazama eneo hilo kwa wepesi alafu nikalipia na kutoka ndani ya gari.
Nikatembea kuvuka barabara. Ila hamaki, gari likaja kwa upesi mno likilenga kunizoa! Nikalikwepa upesi ila likanisukumia kando kwanguvu mno! Sijajikusanya, risasi zikatupwa kwa fujo kunifuata! Moja ikajeruhi paja langu la kushoto!
Nikajitahidi kunyanyuka, nikipuuzia maumivu, nikakimbia kidogo, ila napo kabla sijafika popote, nikadungwa risasi ya mgongo. Nikapoteza nguvu na kuanguka.

**
 
*NYUMA YAKO – 24*
*Simulizi za series*

ILIPOISHIA
Nikatembea kuvuka barabara. Ila hamaki, gari likaja kwa upesi mno likilenga kunizoa! Nikalikwepa upesi ila likanisukumia kando kwanguvu mno! Sijajikusanya, risasi zikatupwa kwa fujo kunifuata! Moja ikajeruhi paja langu la kushoto!
Nikajitahidi kunyanyuka, nikipuuzia maumivu, nikakimbia kidogo, ila napo kabla sijafika popote, nikadungwa risasi ya mgongo. Nikapoteza nguvu na kuanguka.
ENDELEA
Sikufahamu nini kiliendelea baada ya hapo, wala sikujua nilikuwa siko fahamuni kwa muda gani, nilikuja kuamka nikiwa eneo la giza! Sikuwa naona mbele wala nyuma yangu, kushoto wala kulia!
Nikiwa nahema kwanguvu, nikakodoa lakini haikusaidia. Nilikuwa nimefungiwa kitini nisiweze kunyanyuka wala kujitetea. Na kiti chenyewe kilikuwa kimesimikwa chini kiasi cha kutoweza kukinyanyua!
Nikajaribu kukumbuka nini kilitokea mara ya mwisho, sikuambulia kitu bali maumivu ya kichwa. Sikuwa nakumbuka jambo lolote. Kitu pekee nilichoambulia ni kuhisi maumivu kwenye paja langu la kushoto. Nilikuwa na jeraha hapo, nilihisi hilo, lakini sikuweza kugusa sababu ya mikono yangu kufungwa. Na pia, nilikuwa nahisi maumivu mgongoni.
Mengine hayo sikuwa naweza ku … mara mlango ukafunguliwa na kusababisha mwanga mkali kuzama ndani na kunichapa usoni. Haraka nikafunga macho yangu na kuyaminya kwanguvu kujitetea na mwanga ule mkali hivyo sikupata kumwona aliyeingia. Lakini nikajua muda ule ulikuwa ni mchana.
Mlango ulipofungwa, taa zikawashwa kufukuza kiza kile ndani. Hapo ndipo nikamwona mtu yule aliyekuja kunisabahi. Alikuwa mwanaume mrefu mwenye mwili mpana. Alivalia suruali ya jeans, koti la ngozi jeusi, na tisheti ya bluu kwa ndani ikiwa imeandikwa maneno ya njano – “GO *** YOURSELF!”
Mwanaume huyo akasonga karibu yangu akivuta kiti alichokitwaa konani. Akakigeuza kiti hicho na kuketi akin’tazama. Alikuwa ni mwanaume mwenye miba ya ndevu mashavuni na kidevuni. Nyusi zake pana na lips zake nyembamba, kidogo zikiwa zimemezwa na hii miba ya ndevu.
Hapa kabla mwanaume huyo hajasema jambo, nikafahamu kinachoenda kutokea. Mazingira haya hayakuwa mageni kwangu. Nimeshapitia mazingira kama haya maishani mwangu, kama si mara nne basi tano. Angalau nikaanza kuvuta kumbukumbu. Na kumbukumbu zangu hizo zikanambia kuwa mazingira hayo huwa hatarishi.
Huwa yanaambatana na maumivu ya mateso kumlazimisha mtu kuongea kitu ambacho aidha anakijua ama hakijui. Anachohusika nacho ama lah! Lakini sasa mimi nitaeleza nini na kumbukumbu zangu bado hazikuwa zimenijia kichwani?
Si hicho kilichokuwa kinanipa hofu, bali pia hali ile nlokuwamo ilikuwa ni tishio kwa usalama wangu kwani naweza jikuta nikitoa taarifa ambazo hazitakiwi kutolewa kwa adui!
Unajua kabla ya kutumia ujuzi wa kudanganya na kulaghai lazima kwanza uwe unaujua ukweli ili ufahamu namna gani ya kuumba katika njia nyingine ya tofauti ambayo inafanana nayo. Sasa mimi sikuwa naujua huo ukweli. Nilitaraji bwana huyu angenitesa sana kuutoa mwilini mwangu, lakini angeambulia damu tu.
Ila … mawazo haya yalikuwa kinyume. Bwana yule baada ya kunitazama, akaniuliza, “Unanikumbuka?”
Nikatikisa kichwa, “Hapana.” Akatabasamu kisha akapitisha ulimi wake kusafisha meno. Ungepata kuuona ulimi huo kwenye lips zake ukiwa unatembea.
Akaniuliza tena, “Unakumbuka mara yako ya mwisho ulikuwa wapi?”
“Hapana,” nikamjibu.
“Nini unakumbuka?” akaniuliza.
“Mazingira haya,” nikamjibu. “Nadhani sio mageni.”
“Yapi?”
“Haya ya kufungwa kamba kitini, na mtu kukaa mbele yangu.”
Akan’tazama kidogo alafu akanyanyuka aende zake. Nikamwita, “Tafadhali niambie hapa nipo wapi na nafanya nini?”
Akan’tazama asiseme kitu alafu akaenda zake. Akaufungua ule mlango na kupotea ila saa hii akiwa ameacha taa zinawaka. Nikaangaza huku na huko ndani ya mahali nilipo. Hakukuwa na kitu isipokuwa meza na kiti upande wangu wa kulia, tena kwa mbali.
Chumba kilikuwa cheusi na kisicho na dirisha. Ila kulikuwa na na viyoyozi ambavyo vilikuwa vinamwaga kipupwe cha baridi. Nikajiuliza hapa ni wapi? Kabla sijapata majibu, tena hata sijachukua sekunde tano, mlango ukafunguliwa akaingia mwanaume mwenye kimo cha kati akiwa anaongozana na mijibaba miwili kwa nyuma.
Mwanaume huyo alikuwa na mustachi mweupe kama nywele zake za kichwani. Amevalia miwani ya jua na mkononi mwake ameshikilia sigara kubwa. Suruali nyeusi na buti kubwa huko chini.
Akasimama karibu yangu, kiti na ile meza vikasogezwa karibu naye. Hapa ndiyo nikajua kumbe vitu vile vilikuwa vimetengwa kwa ajili yake. Lakini mbona hakuja yeye mwanzoni na badala yake akaja yule mwanaume mwingine?
Akili yangu ikaniaminisha kuwa bwana yule alikuwa ametumwa aje kun’tazama kwanza kama najua jambo lolote, kama nakumbuka kitu, na alipoona hilo limefaulu ndipo akaja huyu.
Kwahiyo hawa ndiyo watakuwa wanahusika na kupotea kwangu kwa kumbukunbu, nikaamini hilo. Nikamtazama bwana yule, naye akintazama akaketi. Akanyonya sigara yake kubwa alafu akantemea moshi pasipo adabu!
Akaita, “Kijana!” nami nikamtazama pasipo kumsemesha.
“Najua haukumbuki jambo, nami nipo hapa kukupatia machaguzi mawili ambayo ni juu yako kuchagua.” Aliposema hayo akavuta tena sigara, na tena pasipo adabu, akanipulizia usoni mwangu. Nilimtazama kwa hasira sana na kama ningekuwa na uwezo ningemdaka na kumfunda nidhamu!
“Moja, ufanye kazi na sisi ukapate nyumba ya kukaa, ama mbili, tukuache ukarande mtaani ukiwindwa kama swala!”
Nikashangazwa na hiyo kauli. Kwani wanadhani sina pa kwenda? Nikajiuliza. Wanadhani mimi ni mzururaji au? Wanadhani sina makazi wala kazi ya kufanya?
Nikawauliza, “ninyi ni wakina nani na kwanini mmenikamata?”
Bwana yule akaniambia, “Sipo hapa kwa ajili ya kuulizwa maswali na wewe. Nipo hapa kukupatia nafasi ya pili, kama uko tayari, sema, na pia kama haupo tayari.”
“Nitakubalije kitu nisichokifahamu?” nikawauliza. Yule bwana hakujali swali langu, akanyanyuka na kwenda zake kuufuata mlango. Nikapaza sauti, “Ngoja!” akasimama pasipo kunitazama akiendelea kuvuta sigara yake.
“Nimekubali,” nikamjibu. “Nimekubali kufanya kazi nanyi!” basi bwana huyo akarejea pale kitini kisha akazamisha mkono wake ndani ya mfuko wa koti na kutoa kikopo kidogo chenye tembe nyeupe, akasema, “Unaona hiki?” akitikisa hiko kikopo. “Ni dawa ya kurejesha kumbukumbu zako, na ukifanya kazi yetu kwa takribani juma moja tu, kazi moja tu, utapewa tembe hizi ukaendelee na maisha yako na pesa nyingi mkononi.”
Aliposema hayo akavua miwani yake, hapo ndipo N jicho moja lililobovu, la kulia, na pia tattoo ya chozi jicho la kushoto.
“Deal?” akaniuliza.
Mimi nikamjibu kwa kumtikisia kichwa.

**

Leo nilikuwa najua ni siku gani na muda gani tofauti na ile jana yake. Nilipewa chai nzuri na muda wa kupumzika kwenye chumba ambacho ni ‘luxury’ chenye kila kitu akitakacho binadamu. Na pia jeraha langu lilipewa dawa na kufungwa bandeji.
Sasa ningeweza kutembea, na nadhani hata kukimbia, kwani nilihisi maumivu kwa mbali, na nilitambua kuwa jeraha hilo halikuwa lililonichimba sana. Kama ndani ya majuma mawili ama matatu laweza likawa limepona kabisa.
Nikiwa hapa sebuleni, baada ya kunywa chai, nikaendelea kuwazia kitu ambacho bado sikuwa nakipatia majibu. Hapa nipo wapi? Hawa watu ni wakina nani? Wanataka nini kwangu?
Na kubwa zaidi MIMI NI NANI?
Nikaja tu kuamini kuwa kujiuliza maswali hayo ni kupoteza muda tu maana nisingepata majibu abadani. Inabidi nipate zile tembe. Tembe za kumbukumbu. Lakini sasa nita ….
Ngo! Ngo! Ngo! Sijajibu, mlango ukafunguliwa, akaingia yule mwanaume aliyekuja kunipa chaguzi jana yake kwenye kile chumba. Kama kawaida alikuwa anaongozana na wanaume wawili waliojaza misuli, akaketi kwenye kochi litazamanalo na langu kisha akaniuliza, “Unaendeleaje?”
“Naendelea vizuri,” nikamjibu pasipo kutia neno lingine.
“Sasa upo tayari kwa kazi yetu?” akaniuliza.
“Kazi gani hiyo?” nami nikamuuliza. Akan’tazama kwanza kabla hajavua miwani yake.

***
 
shukrani mkuu
*NYUMA YAKO – 24*
*Simulizi za series*

ILIPOISHIA
Nikatembea kuvuka barabara. Ila hamaki, gari likaja kwa upesi mno likilenga kunizoa! Nikalikwepa upesi ila likanisukumia kando kwanguvu mno! Sijajikusanya, risasi zikatupwa kwa fujo kunifuata! Moja ikajeruhi paja langu la kushoto!
Nikajitahidi kunyanyuka, nikipuuzia maumivu, nikakimbia kidogo, ila napo kabla sijafika popote, nikadungwa risasi ya mgongo. Nikapoteza nguvu na kuanguka.
ENDELEA
Sikufahamu nini kiliendelea baada ya hapo, wala sikujua nilikuwa siko fahamuni kwa muda gani, nilikuja kuamka nikiwa eneo la giza! Sikuwa naona mbele wala nyuma yangu, kushoto wala kulia!
Nikiwa nahema kwanguvu, nikakodoa lakini haikusaidia. Nilikuwa nimefungiwa kitini nisiweze kunyanyuka wala kujitetea. Na kiti chenyewe kilikuwa kimesimikwa chini kiasi cha kutoweza kukinyanyua!
Nikajaribu kukumbuka nini kilitokea mara ya mwisho, sikuambulia kitu bali maumivu ya kichwa. Sikuwa nakumbuka jambo lolote. Kitu pekee nilichoambulia ni kuhisi maumivu kwenye paja langu la kushoto. Nilikuwa na jeraha hapo, nilihisi hilo, lakini sikuweza kugusa sababu ya mikono yangu kufungwa. Na pia, nilikuwa nahisi maumivu mgongoni.
Mengine hayo sikuwa naweza ku … mara mlango ukafunguliwa na kusababisha mwanga mkali kuzama ndani na kunichapa usoni. Haraka nikafunga macho yangu na kuyaminya kwanguvu kujitetea na mwanga ule mkali hivyo sikupata kumwona aliyeingia. Lakini nikajua muda ule ulikuwa ni mchana.
Mlango ulipofungwa, taa zikawashwa kufukuza kiza kile ndani. Hapo ndipo nikamwona mtu yule aliyekuja kunisabahi. Alikuwa mwanaume mrefu mwenye mwili mpana. Alivalia suruali ya jeans, koti la ngozi jeusi, na tisheti ya bluu kwa ndani ikiwa imeandikwa maneno ya njano – “GO **** YOURSELF!”
Mwanaume huyo akasonga karibu yangu akivuta kiti alichokitwaa konani. Akakigeuza kiti hicho na kuketi akin’tazama. Alikuwa ni mwanaume mwenye miba ya ndevu mashavuni na kidevuni. Nyusi zake pana na lips zake nyembamba, kidogo zikiwa zimemezwa na hii miba ya ndevu.
Hapa kabla mwanaume huyo hajasema jambo, nikafahamu kinachoenda kutokea. Mazingira haya hayakuwa mageni kwangu. Nimeshapitia mazingira kama haya maishani mwangu, kama si mara nne basi tano. Angalau nikaanza kuvuta kumbukumbu. Na kumbukumbu zangu hizo zikanambia kuwa mazingira hayo huwa hatarishi.
Huwa yanaambatana na maumivu ya mateso kumlazimisha mtu kuongea kitu ambacho aidha anakijua ama hakijui. Anachohusika nacho ama lah! Lakini sasa mimi nitaeleza nini na kumbukumbu zangu bado hazikuwa zimenijia kichwani?
Si hicho kilichokuwa kinanipa hofu, bali pia hali ile nlokuwamo ilikuwa ni tishio kwa usalama wangu kwani naweza jikuta nikitoa taarifa ambazo hazitakiwi kutolewa kwa adui!
Unajua kabla ya kutumia ujuzi wa kudanganya na kulaghai lazima kwanza uwe unaujua ukweli ili ufahamu namna gani ya kuumba katika njia nyingine ya tofauti ambayo inafanana nayo. Sasa mimi sikuwa naujua huo ukweli. Nilitaraji bwana huyu angenitesa sana kuutoa mwilini mwangu, lakini angeambulia damu tu.
Ila … mawazo haya yalikuwa kinyume. Bwana yule baada ya kunitazama, akaniuliza, “Unanikumbuka?”
Nikatikisa kichwa, “Hapana.” Akatabasamu kisha akapitisha ulimi wake kusafisha meno. Ungepata kuuona ulimi huo kwenye lips zake ukiwa unatembea.
Akaniuliza tena, “Unakumbuka mara yako ya mwisho ulikuwa wapi?”
“Hapana,” nikamjibu.
“Nini unakumbuka?” akaniuliza.
“Mazingira haya,” nikamjibu. “Nadhani sio mageni.”
“Yapi?”
“Haya ya kufungwa kamba kitini, na mtu kukaa mbele yangu.”
Akan’tazama kidogo alafu akanyanyuka aende zake. Nikamwita, “Tafadhali niambie hapa nipo wapi na nafanya nini?”
Akan’tazama asiseme kitu alafu akaenda zake. Akaufungua ule mlango na kupotea ila saa hii akiwa ameacha taa zinawaka. Nikaangaza huku na huko ndani ya mahali nilipo. Hakukuwa na kitu isipokuwa meza na kiti upande wangu wa kulia, tena kwa mbali.
Chumba kilikuwa cheusi na kisicho na dirisha. Ila kulikuwa na na viyoyozi ambavyo vilikuwa vinamwaga kipupwe cha baridi. Nikajiuliza hapa ni wapi? Kabla sijapata majibu, tena hata sijachukua sekunde tano, mlango ukafunguliwa akaingia mwanaume mwenye kimo cha kati akiwa anaongozana na mijibaba miwili kwa nyuma.
Mwanaume huyo alikuwa na mustachi mweupe kama nywele zake za kichwani. Amevalia miwani ya jua na mkononi mwake ameshikilia sigara kubwa. Suruali nyeusi na buti kubwa huko chini.
Akasimama karibu yangu, kiti na ile meza vikasogezwa karibu naye. Hapa ndiyo nikajua kumbe vitu vile vilikuwa vimetengwa kwa ajili yake. Lakini mbona hakuja yeye mwanzoni na badala yake akaja yule mwanaume mwingine?
Akili yangu ikaniaminisha kuwa bwana yule alikuwa ametumwa aje kun’tazama kwanza kama najua jambo lolote, kama nakumbuka kitu, na alipoona hilo limefaulu ndipo akaja huyu.
Kwahiyo hawa ndiyo watakuwa wanahusika na kupotea kwangu kwa kumbukunbu, nikaamini hilo. Nikamtazama bwana yule, naye akintazama akaketi. Akanyonya sigara yake kubwa alafu akantemea moshi pasipo adabu!
Akaita, “Kijana!” nami nikamtazama pasipo kumsemesha.
“Najua haukumbuki jambo, nami nipo hapa kukupatia machaguzi mawili ambayo ni juu yako kuchagua.” Aliposema hayo akavuta tena sigara, na tena pasipo adabu, akanipulizia usoni mwangu. Nilimtazama kwa hasira sana na kama ningekuwa na uwezo ningemdaka na kumfunda nidhamu!
“Moja, ufanye kazi na sisi ukapate nyumba ya kukaa, ama mbili, tukuache ukarande mtaani ukiwindwa kama swala!”
Nikashangazwa na hiyo kauli. Kwani wanadhani sina pa kwenda? Nikajiuliza. Wanadhani mimi ni mzururaji au? Wanadhani sina makazi wala kazi ya kufanya?
Nikawauliza, “ninyi ni wakina nani na kwanini mmenikamata?”
Bwana yule akaniambia, “Sipo hapa kwa ajili ya kuulizwa maswali na wewe. Nipo hapa kukupatia nafasi ya pili, kama uko tayari, sema, na pia kama haupo tayari.”
“Nitakubalije kitu nisichokifahamu?” nikawauliza. Yule bwana hakujali swali langu, akanyanyuka na kwenda zake kuufuata mlango. Nikapaza sauti, “Ngoja!” akasimama pasipo kunitazama akiendelea kuvuta sigara yake.
“Nimekubali,” nikamjibu. “Nimekubali kufanya kazi nanyi!” basi bwana huyo akarejea pale kitini kisha akazamisha mkono wake ndani ya mfuko wa koti na kutoa kikopo kidogo chenye tembe nyeupe, akasema, “Unaona hiki?” akitikisa hiko kikopo. “Ni dawa ya kurejesha kumbukumbu zako, na ukifanya kazi yetu kwa takribani juma moja tu, kazi moja tu, utapewa tembe hizi ukaendelee na maisha yako na pesa nyingi mkononi.”
Aliposema hayo akavua miwani yake, hapo ndipo N jicho moja lililobovu, la kulia, na pia tattoo ya chozi jicho la kushoto.
“Deal?” akaniuliza.
Mimi nikamjibu kwa kumtikisia kichwa.

**

Leo nilikuwa najua ni siku gani na muda gani tofauti na ile jana yake. Nilipewa chai nzuri na muda wa kupumzika kwenye chumba ambacho ni ‘luxury’ chenye kila kitu akitakacho binadamu. Na pia jeraha langu lilipewa dawa na kufungwa bandeji.
Sasa ningeweza kutembea, na nadhani hata kukimbia, kwani nilihisi maumivu kwa mbali, na nilitambua kuwa jeraha hilo halikuwa lililonichimba sana. Kama ndani ya majuma mawili ama matatu laweza likawa limepona kabisa.
Nikiwa hapa sebuleni, baada ya kunywa chai, nikaendelea kuwazia kitu ambacho bado sikuwa nakipatia majibu. Hapa nipo wapi? Hawa watu ni wakina nani? Wanataka nini kwangu?
Na kubwa zaidi MIMI NI NANI?
Nikaja tu kuamini kuwa kujiuliza maswali hayo ni kupoteza muda tu maana nisingepata majibu abadani. Inabidi nipate zile tembe. Tembe za kumbukumbu. Lakini sasa nita ….
Ngo! Ngo! Ngo! Sijajibu, mlango ukafunguliwa, akaingia yule mwanaume aliyekuja kunipa chaguzi jana yake kwenye kile chumba. Kama kawaida alikuwa anaongozana na wanaume wawili waliojaza misuli, akaketi kwenye kochi litazamanalo na langu kisha akaniuliza, “Unaendeleaje?”
“Naendelea vizuri,” nikamjibu pasipo kutia neno lingine.
“Sasa upo tayari kwa kazi yetu?” akaniuliza.
“Kazi gani hiyo?” nami nikamuuliza. Akan’tazama kwanza kabla hajavua miwani yake.

***
 
Big up sana
*NYUMA YAKO – 24*
*Simulizi za series*

ILIPOISHIA
Nikatembea kuvuka barabara. Ila hamaki, gari likaja kwa upesi mno likilenga kunizoa! Nikalikwepa upesi ila likanisukumia kando kwanguvu mno! Sijajikusanya, risasi zikatupwa kwa fujo kunifuata! Moja ikajeruhi paja langu la kushoto!
Nikajitahidi kunyanyuka, nikipuuzia maumivu, nikakimbia kidogo, ila napo kabla sijafika popote, nikadungwa risasi ya mgongo. Nikapoteza nguvu na kuanguka.
ENDELEA
Sikufahamu nini kiliendelea baada ya hapo, wala sikujua nilikuwa siko fahamuni kwa muda gani, nilikuja kuamka nikiwa eneo la giza! Sikuwa naona mbele wala nyuma yangu, kushoto wala kulia!
Nikiwa nahema kwanguvu, nikakodoa lakini haikusaidia. Nilikuwa nimefungiwa kitini nisiweze kunyanyuka wala kujitetea. Na kiti chenyewe kilikuwa kimesimikwa chini kiasi cha kutoweza kukinyanyua!
Nikajaribu kukumbuka nini kilitokea mara ya mwisho, sikuambulia kitu bali maumivu ya kichwa. Sikuwa nakumbuka jambo lolote. Kitu pekee nilichoambulia ni kuhisi maumivu kwenye paja langu la kushoto. Nilikuwa na jeraha hapo, nilihisi hilo, lakini sikuweza kugusa sababu ya mikono yangu kufungwa. Na pia, nilikuwa nahisi maumivu mgongoni.
Mengine hayo sikuwa naweza ku … mara mlango ukafunguliwa na kusababisha mwanga mkali kuzama ndani na kunichapa usoni. Haraka nikafunga macho yangu na kuyaminya kwanguvu kujitetea na mwanga ule mkali hivyo sikupata kumwona aliyeingia. Lakini nikajua muda ule ulikuwa ni mchana.
Mlango ulipofungwa, taa zikawashwa kufukuza kiza kile ndani. Hapo ndipo nikamwona mtu yule aliyekuja kunisabahi. Alikuwa mwanaume mrefu mwenye mwili mpana. Alivalia suruali ya jeans, koti la ngozi jeusi, na tisheti ya bluu kwa ndani ikiwa imeandikwa maneno ya njano – “GO **** YOURSELF!”
Mwanaume huyo akasonga karibu yangu akivuta kiti alichokitwaa konani. Akakigeuza kiti hicho na kuketi akin’tazama. Alikuwa ni mwanaume mwenye miba ya ndevu mashavuni na kidevuni. Nyusi zake pana na lips zake nyembamba, kidogo zikiwa zimemezwa na hii miba ya ndevu.
Hapa kabla mwanaume huyo hajasema jambo, nikafahamu kinachoenda kutokea. Mazingira haya hayakuwa mageni kwangu. Nimeshapitia mazingira kama haya maishani mwangu, kama si mara nne basi tano. Angalau nikaanza kuvuta kumbukumbu. Na kumbukumbu zangu hizo zikanambia kuwa mazingira hayo huwa hatarishi.
Huwa yanaambatana na maumivu ya mateso kumlazimisha mtu kuongea kitu ambacho aidha anakijua ama hakijui. Anachohusika nacho ama lah! Lakini sasa mimi nitaeleza nini na kumbukumbu zangu bado hazikuwa zimenijia kichwani?
Si hicho kilichokuwa kinanipa hofu, bali pia hali ile nlokuwamo ilikuwa ni tishio kwa usalama wangu kwani naweza jikuta nikitoa taarifa ambazo hazitakiwi kutolewa kwa adui!
Unajua kabla ya kutumia ujuzi wa kudanganya na kulaghai lazima kwanza uwe unaujua ukweli ili ufahamu namna gani ya kuumba katika njia nyingine ya tofauti ambayo inafanana nayo. Sasa mimi sikuwa naujua huo ukweli. Nilitaraji bwana huyu angenitesa sana kuutoa mwilini mwangu, lakini angeambulia damu tu.
Ila … mawazo haya yalikuwa kinyume. Bwana yule baada ya kunitazama, akaniuliza, “Unanikumbuka?”
Nikatikisa kichwa, “Hapana.” Akatabasamu kisha akapitisha ulimi wake kusafisha meno. Ungepata kuuona ulimi huo kwenye lips zake ukiwa unatembea.
Akaniuliza tena, “Unakumbuka mara yako ya mwisho ulikuwa wapi?”
“Hapana,” nikamjibu.
“Nini unakumbuka?” akaniuliza.
“Mazingira haya,” nikamjibu. “Nadhani sio mageni.”
“Yapi?”
“Haya ya kufungwa kamba kitini, na mtu kukaa mbele yangu.”
Akan’tazama kidogo alafu akanyanyuka aende zake. Nikamwita, “Tafadhali niambie hapa nipo wapi na nafanya nini?”
Akan’tazama asiseme kitu alafu akaenda zake. Akaufungua ule mlango na kupotea ila saa hii akiwa ameacha taa zinawaka. Nikaangaza huku na huko ndani ya mahali nilipo. Hakukuwa na kitu isipokuwa meza na kiti upande wangu wa kulia, tena kwa mbali.
Chumba kilikuwa cheusi na kisicho na dirisha. Ila kulikuwa na na viyoyozi ambavyo vilikuwa vinamwaga kipupwe cha baridi. Nikajiuliza hapa ni wapi? Kabla sijapata majibu, tena hata sijachukua sekunde tano, mlango ukafunguliwa akaingia mwanaume mwenye kimo cha kati akiwa anaongozana na mijibaba miwili kwa nyuma.
Mwanaume huyo alikuwa na mustachi mweupe kama nywele zake za kichwani. Amevalia miwani ya jua na mkononi mwake ameshikilia sigara kubwa. Suruali nyeusi na buti kubwa huko chini.
Akasimama karibu yangu, kiti na ile meza vikasogezwa karibu naye. Hapa ndiyo nikajua kumbe vitu vile vilikuwa vimetengwa kwa ajili yake. Lakini mbona hakuja yeye mwanzoni na badala yake akaja yule mwanaume mwingine?
Akili yangu ikaniaminisha kuwa bwana yule alikuwa ametumwa aje kun’tazama kwanza kama najua jambo lolote, kama nakumbuka kitu, na alipoona hilo limefaulu ndipo akaja huyu.
Kwahiyo hawa ndiyo watakuwa wanahusika na kupotea kwangu kwa kumbukunbu, nikaamini hilo. Nikamtazama bwana yule, naye akintazama akaketi. Akanyonya sigara yake kubwa alafu akantemea moshi pasipo adabu!
Akaita, “Kijana!” nami nikamtazama pasipo kumsemesha.
“Najua haukumbuki jambo, nami nipo hapa kukupatia machaguzi mawili ambayo ni juu yako kuchagua.” Aliposema hayo akavuta tena sigara, na tena pasipo adabu, akanipulizia usoni mwangu. Nilimtazama kwa hasira sana na kama ningekuwa na uwezo ningemdaka na kumfunda nidhamu!
“Moja, ufanye kazi na sisi ukapate nyumba ya kukaa, ama mbili, tukuache ukarande mtaani ukiwindwa kama swala!”
Nikashangazwa na hiyo kauli. Kwani wanadhani sina pa kwenda? Nikajiuliza. Wanadhani mimi ni mzururaji au? Wanadhani sina makazi wala kazi ya kufanya?
Nikawauliza, “ninyi ni wakina nani na kwanini mmenikamata?”
Bwana yule akaniambia, “Sipo hapa kwa ajili ya kuulizwa maswali na wewe. Nipo hapa kukupatia nafasi ya pili, kama uko tayari, sema, na pia kama haupo tayari.”
“Nitakubalije kitu nisichokifahamu?” nikawauliza. Yule bwana hakujali swali langu, akanyanyuka na kwenda zake kuufuata mlango. Nikapaza sauti, “Ngoja!” akasimama pasipo kunitazama akiendelea kuvuta sigara yake.
“Nimekubali,” nikamjibu. “Nimekubali kufanya kazi nanyi!” basi bwana huyo akarejea pale kitini kisha akazamisha mkono wake ndani ya mfuko wa koti na kutoa kikopo kidogo chenye tembe nyeupe, akasema, “Unaona hiki?” akitikisa hiko kikopo. “Ni dawa ya kurejesha kumbukumbu zako, na ukifanya kazi yetu kwa takribani juma moja tu, kazi moja tu, utapewa tembe hizi ukaendelee na maisha yako na pesa nyingi mkononi.”
Aliposema hayo akavua miwani yake, hapo ndipo N jicho moja lililobovu, la kulia, na pia tattoo ya chozi jicho la kushoto.
“Deal?” akaniuliza.
Mimi nikamjibu kwa kumtikisia kichwa.

**

Leo nilikuwa najua ni siku gani na muda gani tofauti na ile jana yake. Nilipewa chai nzuri na muda wa kupumzika kwenye chumba ambacho ni ‘luxury’ chenye kila kitu akitakacho binadamu. Na pia jeraha langu lilipewa dawa na kufungwa bandeji.
Sasa ningeweza kutembea, na nadhani hata kukimbia, kwani nilihisi maumivu kwa mbali, na nilitambua kuwa jeraha hilo halikuwa lililonichimba sana. Kama ndani ya majuma mawili ama matatu laweza likawa limepona kabisa.
Nikiwa hapa sebuleni, baada ya kunywa chai, nikaendelea kuwazia kitu ambacho bado sikuwa nakipatia majibu. Hapa nipo wapi? Hawa watu ni wakina nani? Wanataka nini kwangu?
Na kubwa zaidi MIMI NI NANI?
Nikaja tu kuamini kuwa kujiuliza maswali hayo ni kupoteza muda tu maana nisingepata majibu abadani. Inabidi nipate zile tembe. Tembe za kumbukumbu. Lakini sasa nita ….
Ngo! Ngo! Ngo! Sijajibu, mlango ukafunguliwa, akaingia yule mwanaume aliyekuja kunipa chaguzi jana yake kwenye kile chumba. Kama kawaida alikuwa anaongozana na wanaume wawili waliojaza misuli, akaketi kwenye kochi litazamanalo na langu kisha akaniuliza, “Unaendeleaje?”
“Naendelea vizuri,” nikamjibu pasipo kutia neno lingine.
“Sasa upo tayari kwa kazi yetu?” akaniuliza.
“Kazi gani hiyo?” nami nikamuuliza. Akan’tazama kwanza kabla hajavua miwani yake.

***
 
Man steve hiki chako ni zaidi ya kipaji,kila nikitafakari inakuwaje mpaka unayafanya haya nabaki kukubali tu MUNGU mkubwa.Na binadamu tunatofautiana sana.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom