Tumpara Dudu
JF-Expert Member
- Nov 15, 2016
- 617
- 487
Kaka mkubwa,muendelezo lini?
Nashukuru sana ndugu yangu kwa kuniunga mkono
Nashukuru sana ndugu yangu kwa kuniunga mkono
Nyuma ni nyuma eenh.*NYUMA YAKO – 24*
*Simulizi za series*
ILIPOISHIA
Nikatembea kuvuka barabara. Ila hamaki, gari likaja kwa upesi mno likilenga kunizoa! Nikalikwepa upesi ila likanisukumia kando kwanguvu mno! Sijajikusanya, risasi zikatupwa kwa fujo kunifuata! Moja ikajeruhi paja langu la kushoto!
Nikajitahidi kunyanyuka, nikipuuzia maumivu, nikakimbia kidogo, ila napo kabla sijafika popote, nikadungwa risasi ya mgongo. Nikapoteza nguvu na kuanguka.
ENDELEA
Sikufahamu nini kiliendelea baada ya hapo, wala sikujua nilikuwa siko fahamuni kwa muda gani, nilikuja kuamka nikiwa eneo la giza! Sikuwa naona mbele wala nyuma yangu, kushoto wala kulia!
Nikiwa nahema kwanguvu, nikakodoa lakini haikusaidia. Nilikuwa nimefungiwa kitini nisiweze kunyanyuka wala kujitetea. Na kiti chenyewe kilikuwa kimesimikwa chini kiasi cha kutoweza kukinyanyua!
Nikajaribu kukumbuka nini kilitokea mara ya mwisho, sikuambulia kitu bali maumivu ya kichwa. Sikuwa nakumbuka jambo lolote. Kitu pekee nilichoambulia ni kuhisi maumivu kwenye paja langu la kushoto. Nilikuwa na jeraha hapo, nilihisi hilo, lakini sikuweza kugusa sababu ya mikono yangu kufungwa. Na pia, nilikuwa nahisi maumivu mgongoni.
Mengine hayo sikuwa naweza ku … mara mlango ukafunguliwa na kusababisha mwanga mkali kuzama ndani na kunichapa usoni. Haraka nikafunga macho yangu na kuyaminya kwanguvu kujitetea na mwanga ule mkali hivyo sikupata kumwona aliyeingia. Lakini nikajua muda ule ulikuwa ni mchana.
Mlango ulipofungwa, taa zikawashwa kufukuza kiza kile ndani. Hapo ndipo nikamwona mtu yule aliyekuja kunisabahi. Alikuwa mwanaume mrefu mwenye mwili mpana. Alivalia suruali ya jeans, koti la ngozi jeusi, na tisheti ya bluu kwa ndani ikiwa imeandikwa maneno ya njano – “GO **** YOURSELF!”
Mwanaume huyo akasonga karibu yangu akivuta kiti alichokitwaa konani. Akakigeuza kiti hicho na kuketi akin’tazama. Alikuwa ni mwanaume mwenye miba ya ndevu mashavuni na kidevuni. Nyusi zake pana na lips zake nyembamba, kidogo zikiwa zimemezwa na hii miba ya ndevu.
Hapa kabla mwanaume huyo hajasema jambo, nikafahamu kinachoenda kutokea. Mazingira haya hayakuwa mageni kwangu. Nimeshapitia mazingira kama haya maishani mwangu, kama si mara nne basi tano. Angalau nikaanza kuvuta kumbukumbu. Na kumbukumbu zangu hizo zikanambia kuwa mazingira hayo huwa hatarishi.
Huwa yanaambatana na maumivu ya mateso kumlazimisha mtu kuongea kitu ambacho aidha anakijua ama hakijui. Anachohusika nacho ama lah! Lakini sasa mimi nitaeleza nini na kumbukumbu zangu bado hazikuwa zimenijia kichwani?
Si hicho kilichokuwa kinanipa hofu, bali pia hali ile nlokuwamo ilikuwa ni tishio kwa usalama wangu kwani naweza jikuta nikitoa taarifa ambazo hazitakiwi kutolewa kwa adui!
Unajua kabla ya kutumia ujuzi wa kudanganya na kulaghai lazima kwanza uwe unaujua ukweli ili ufahamu namna gani ya kuumba katika njia nyingine ya tofauti ambayo inafanana nayo. Sasa mimi sikuwa naujua huo ukweli. Nilitaraji bwana huyu angenitesa sana kuutoa mwilini mwangu, lakini angeambulia damu tu.
Ila … mawazo haya yalikuwa kinyume. Bwana yule baada ya kunitazama, akaniuliza, “Unanikumbuka?”
Nikatikisa kichwa, “Hapana.” Akatabasamu kisha akapitisha ulimi wake kusafisha meno. Ungepata kuuona ulimi huo kwenye lips zake ukiwa unatembea.
Akaniuliza tena, “Unakumbuka mara yako ya mwisho ulikuwa wapi?”
“Hapana,” nikamjibu.
“Nini unakumbuka?” akaniuliza.
“Mazingira haya,” nikamjibu. “Nadhani sio mageni.”
“Yapi?”
“Haya ya kufungwa kamba kitini, na mtu kukaa mbele yangu.”
Akan’tazama kidogo alafu akanyanyuka aende zake. Nikamwita, “Tafadhali niambie hapa nipo wapi na nafanya nini?”
Akan’tazama asiseme kitu alafu akaenda zake. Akaufungua ule mlango na kupotea ila saa hii akiwa ameacha taa zinawaka. Nikaangaza huku na huko ndani ya mahali nilipo. Hakukuwa na kitu isipokuwa meza na kiti upande wangu wa kulia, tena kwa mbali.
Chumba kilikuwa cheusi na kisicho na dirisha. Ila kulikuwa na na viyoyozi ambavyo vilikuwa vinamwaga kipupwe cha baridi. Nikajiuliza hapa ni wapi? Kabla sijapata majibu, tena hata sijachukua sekunde tano, mlango ukafunguliwa akaingia mwanaume mwenye kimo cha kati akiwa anaongozana na mijibaba miwili kwa nyuma.
Mwanaume huyo alikuwa na mustachi mweupe kama nywele zake za kichwani. Amevalia miwani ya jua na mkononi mwake ameshikilia sigara kubwa. Suruali nyeusi na buti kubwa huko chini.
Akasimama karibu yangu, kiti na ile meza vikasogezwa karibu naye. Hapa ndiyo nikajua kumbe vitu vile vilikuwa vimetengwa kwa ajili yake. Lakini mbona hakuja yeye mwanzoni na badala yake akaja yule mwanaume mwingine?
Akili yangu ikaniaminisha kuwa bwana yule alikuwa ametumwa aje kun’tazama kwanza kama najua jambo lolote, kama nakumbuka kitu, na alipoona hilo limefaulu ndipo akaja huyu.
Kwahiyo hawa ndiyo watakuwa wanahusika na kupotea kwangu kwa kumbukunbu, nikaamini hilo. Nikamtazama bwana yule, naye akintazama akaketi. Akanyonya sigara yake kubwa alafu akantemea moshi pasipo adabu!
Akaita, “Kijana!” nami nikamtazama pasipo kumsemesha.
“Najua haukumbuki jambo, nami nipo hapa kukupatia machaguzi mawili ambayo ni juu yako kuchagua.” Aliposema hayo akavuta tena sigara, na tena pasipo adabu, akanipulizia usoni mwangu. Nilimtazama kwa hasira sana na kama ningekuwa na uwezo ningemdaka na kumfunda nidhamu!
“Moja, ufanye kazi na sisi ukapate nyumba ya kukaa, ama mbili, tukuache ukarande mtaani ukiwindwa kama swala!”
Nikashangazwa na hiyo kauli. Kwani wanadhani sina pa kwenda? Nikajiuliza. Wanadhani mimi ni mzururaji au? Wanadhani sina makazi wala kazi ya kufanya?
Nikawauliza, “ninyi ni wakina nani na kwanini mmenikamata?”
Bwana yule akaniambia, “Sipo hapa kwa ajili ya kuulizwa maswali na wewe. Nipo hapa kukupatia nafasi ya pili, kama uko tayari, sema, na pia kama haupo tayari.”
“Nitakubalije kitu nisichokifahamu?” nikawauliza. Yule bwana hakujali swali langu, akanyanyuka na kwenda zake kuufuata mlango. Nikapaza sauti, “Ngoja!” akasimama pasipo kunitazama akiendelea kuvuta sigara yake.
“Nimekubali,” nikamjibu. “Nimekubali kufanya kazi nanyi!” basi bwana huyo akarejea pale kitini kisha akazamisha mkono wake ndani ya mfuko wa koti na kutoa kikopo kidogo chenye tembe nyeupe, akasema, “Unaona hiki?” akitikisa hiko kikopo. “Ni dawa ya kurejesha kumbukumbu zako, na ukifanya kazi yetu kwa takribani juma moja tu, kazi moja tu, utapewa tembe hizi ukaendelee na maisha yako na pesa nyingi mkononi.”
Aliposema hayo akavua miwani yake, hapo ndipo N jicho moja lililobovu, la kulia, na pia tattoo ya chozi jicho la kushoto.
“Deal?” akaniuliza.
Mimi nikamjibu kwa kumtikisia kichwa.
**
Leo nilikuwa najua ni siku gani na muda gani tofauti na ile jana yake. Nilipewa chai nzuri na muda wa kupumzika kwenye chumba ambacho ni ‘luxury’ chenye kila kitu akitakacho binadamu. Na pia jeraha langu lilipewa dawa na kufungwa bandeji.
Sasa ningeweza kutembea, na nadhani hata kukimbia, kwani nilihisi maumivu kwa mbali, na nilitambua kuwa jeraha hilo halikuwa lililonichimba sana. Kama ndani ya majuma mawili ama matatu laweza likawa limepona kabisa.
Nikiwa hapa sebuleni, baada ya kunywa chai, nikaendelea kuwazia kitu ambacho bado sikuwa nakipatia majibu. Hapa nipo wapi? Hawa watu ni wakina nani? Wanataka nini kwangu?
Na kubwa zaidi MIMI NI NANI?
Nikaja tu kuamini kuwa kujiuliza maswali hayo ni kupoteza muda tu maana nisingepata majibu abadani. Inabidi nipate zile tembe. Tembe za kumbukumbu. Lakini sasa nita ….
Ngo! Ngo! Ngo! Sijajibu, mlango ukafunguliwa, akaingia yule mwanaume aliyekuja kunipa chaguzi jana yake kwenye kile chumba. Kama kawaida alikuwa anaongozana na wanaume wawili waliojaza misuli, akaketi kwenye kochi litazamanalo na langu kisha akaniuliza, “Unaendeleaje?”
“Naendelea vizuri,” nikamjibu pasipo kutia neno lingine.
“Sasa upo tayari kwa kazi yetu?” akaniuliza.
“Kazi gani hiyo?” nami nikamuuliza. Akan’tazama kwanza kabla hajavua miwani yake.
***
na hana kumbukumbuSimulizi iko poa. Kasheshe ni pale Stering anapokamatwa huku hana watu wa kumsaidia.
KuuuuuuumbeeeeeeeeStory hii ipo mpaka mwisho. Kama waihitaji tuma 2000 tu kwenda 0685 758 123 kwa story nzima
Karibu sana mkuu. Nitafurahi ukiniunga mkono.Kuuuuuuumbeeeeeeee
Poa mkuu
Kesho nakutafuta
Habari,hii story naweza kuipata yote nikikutumia hiyo 2,000/=?It's been a while hatujaonana wakuu. Najua 'tumemissiana' sana au sio wandugu? Haya sasa nimerudi tena na Riwaya ya NYUMA YAKO yenye mahadhu ya Kijasusi na kiitelijensia kama tulivyofanya kwenye riwaya kadhaa zilizopita.
Riwaya hii mpaka sasa inakaribia ukingoni hivyo kwa mtu atakeyihitaji basi asisite kunijuza kwa namba 0685 758 123 - whatsapp.
Unapewa mkuu, me nimelipa nimepewa mzigo wote tayari.Habari,hii story naweza kuipata yote nikikutumia hiyo 2,000/=?
Bila shakaHabari,hii story naweza kuipata yote nikikutumia hiyo 2,000/=?
Sawa Tevie...nitakuja..huko huko mkuu...Story hii ipo mpaka mwisho. Kama waihitaji tuma 2000 tu kwenda 0685 758 123 kwa story nzima
Asante mkuuSawa Tevie...nitakuja..huko huko mkuu...
Story hii ipo mpaka mwisho. Kama waihitaji tuma 2000 tu kwenda 0685 758 123 kwa story nzima