Nyota ya Magharibi yang'aa, mbegu yachipua, Kitoto Chaanza Tambaa!

Rev. Kishoka

JF-Expert Member
Mar 7, 2006
4,526
1,529
Mzee Kikumbi Mwanza Mpango, maarufu kama King Kiki, ana wimbo wake mmoja maarufu ambao anaimba "fungua njia, kitoto chaanza Tambaa"!

Mchungaji anakuomba Mtanzania fungua moyo na njia, Kitoto kimeanza tambaa!

Kama kuna jambo lililotoa msisimko mkubwa na kujenga hisia mpya za kimapinduzi ndani mwangu kutoka kwa Wanasiasa wa Tanzania katika miaka ya karibuni, ni hotuba ya Ndugu yangu Zitto Kabwe aliyoitoa Busanda, wakati wa kampeni za uchaguzi mdogo wa jimbo kutafuta mbunge.

Hotuba ya Zitto imebeba kilio cha kila Mtanzania anayelilia haki, anayelilia maslahi, anayelilia tumaini, anayelilia ahueni aachane na Umasikini, Ujinga na Maradhi ili Mtanzania huyu aweze kuwa mshiriki kamilifu katika ujenzi wa nchi yake na afaidi matunda ya nchi yake.

Tofauti na hotuba za Wanasiasa wawe wa CCM au Upinzani, Zitto kanivutia kwa kitu kimoja, hakutoa ahadi hewa, bali katoa wito wa kuwaomba Watanzania kama wanajali nchi yao na hawaridhiki na hali halisi iliyoko nchini, basi jimbo la Busanda lisiangukie tena kwa CCM kama mazoea.

Hotuba yake imenikumbusha hotuba zile za Wanamapinduzi wa Afrika waliopigania Uhuru wa Afrika. Nyerere, Kenyatta, Kaunda, Cabral, Balewa, Azikiwe, Ben Bela, Lumumba, Nkrumah, Toure na wengine wengi ambao ndio walikuwa mstari wa mbele katika kuleta ukombozi kwa Afrika kutoka kwa makucha ya Wakoloni.

Hali yetu Tanzania sasa hivi chini ya CCM haina tofauti na msukumo wetu tuliouanza tangu vita vya kina Mtemi Mkwawa, Isike, Mangi Meli, Mirambo, Abushiri, Kinjekitile, mpaka walioanzisha TAA, TANU na hata UMMA, ZNP na hata ASP. Walichokifanya wahenga wetu ni kupigana vita vya nguvu, hoja na itikadi mpaka tukaushinda ukoloni na Mkoloni akakubali kushindwa na kuridhia kutuachia nchi yetu tujiongoze.

Zitto ametusaidia sisi wote Wanaharakati tunaotaka kuleta Mapinduzi mapya Tanzania, iwe tukiwa ni wafuasi wa CCM au vyama vya Upinzani, kwa kutoa hotuba moja iliyoshiba na nono kumuamsha Mtanzania atambue kuwa mazoea ya kuchagua CCM bila kudai uwajibikaji hayafai.

Nasema kuwa Nyota ya Magharibi imeng'aa, mbegu imechipua na kitoto kimeanza kutambaa ni kutokana na furaha niliyonayo kuona kuwa tulichokuwa tukimfunda Zitto kwenye kumbi zetu na kumdai azinduke, kumeleta matunda kwa yeye kuamka wakati muafaka na kutoa hotuba yenye ujumbe mkubwa kama huo.

Sidhani kama wengi wetu, tulikuwa tayari wala kutumaini kuwa kuna siku kilio chetu kitapewa matangazo ya bure na yenye nguvu kama hotuba hii.

CCM kwa muda mrefu wamekuwa wakitufanya sisi Watanzania kuwa ni wajinga, wametunyanyasa na kutunyonya na kutuacha tuwe wanyonge. Sina maana kusema Zitto ni shujaa basi nasi tupumbae kuimba nyimbo kumtukuza kuwa ni shujaa, bali ni kumshukuru Zitto kwa kuwa jasiri na kutoa msimamo uliojaa upendo, umakini na wala si vitisho au ahadi.

Zitto katoa wito kwa Watanzania kuanza kuiambia CCM, hatufurahii inachokifanya.

CCM ni kichwa ngumu, nami pamoja na mapenzi yangu kwa CCM, nimekuwa nikikiri kwa muda mrefu sana kuwa kuna haja ya kufanyika mapinduzi ya kuifanya CCM izaliwe upya.

Mwalimu Nyerere alisema Upinzani makini utatokea CCM. Je hotuba hii ya Zitto itazaa matunda ya kutimilika maneno ya Mwalimu Nyerere? Je wale Wabunge Magwiji wa CCM wanaodai kuwa wao ni Wapiganaji wenzetu, watakuwa tayari kusimama mguu sawa na kwa mwendo mkakamavu kukibadilisha Chama chao kianze kulitumikia Taifa?

Najua wengi wetu tutasema laiti kama Zitto angekuwa na umri sawia ili agombee Urais mwakani wakati wa uchaguzi mkuu, mimi nitasema, Zitto wala hana haja ya kufanya pupa.

Amepanda mbegu bora, kazi inayofuatilia ni kupalilia, kunyeshea, kuwekea mbolea, kuondoa magugu na kuendelea kuulea mmea ili utoe mazao bora.

Safari ya kuiamsha CCM imepata nishati na nguvu mpya, nasi tujiunge pamoja na kumpasha na kumhoji kila Mtanzania awe mkweli kwa nafsi yake kama anaridhika na hali ya Maisha yake na Uongozi wa CCM ambao umekomaa kwa miaka 48 na haujaleta matunda yaliyo bora ya muda mrefu kutuletea neema ambayo itatuondoa kwenye utegemezi na unyonge.
 
Rev.
Amani iwe nawe!

Kweli hapa ametambaa kwa mikiki-mikiki;

"Hotuba ya Zitto imebeba kilio cha kila Mtanzania anayelilia haki, anayelilia maslahi, anayelilia tumaini, anayelilia ahueni aachane na Umasikini, Ujinga na Maradhi ili Mtanzania huyu aweze kuwa mshiriki kamilifu katika ujenzi wa nchi yake na afaidi matunda ya nchi yake."

Maneno mazito kama haya;Good for the 2020 banner!
 
Shalom

Kwa lugha yoyote ile ile hotuba ilikuwa nzuri sana. nashukuru eti listi kwa mara ya kwanza nchini nimeweza kusoma hotuba na kuimaliza huku machozi yakini toka!.
 
yap! kaka hayo yaloandikwa kama kariri ya yale yalosemwa na Ndg. Zito yanaonesha dhahiri kuwa huyu bw. kadhamiria na kajitoa kwa ajili ya kutetea walo wengi, ni kazi inayotaka ukomavu,ushirikiano na msimamo wa hali ya juu kuweza kufikia malengo. kama wana mageuzi wengine Zito keshafanya makubwa na ya kupigia mfano, sie pia tunaweza kufanya vile afanyavyo Zito na hasa ktk kuongeza nguvu, yule anayeumia na kulia kisa hilo neno ataweza vumilia jino
 
Tuwekeeni hiro ri hotuba rizuri turisome, maana jeshi ra porisi rinataka kujiridhisha ikiwa kweri ni rihotuba rizuri isije rikawa rinachochea uvunjifu wa amani ambayo Sisiem imeijenga kwa miakamingi. Jeshi ra porisi rimejipanga vizuri kukabiriana na wachochezi hawa wanajiita wakombozi na kuanza rimepereka ri kikosi la Fanya Fujo Uone
 
Hata kabla sijaisoma, ninafurahi kusikia positive news kuhusu Tanzania na kutoka kwa mtanzania kwa ajili ya tanzania.
ngoja niitafute hiyo posti,
Sisi wenye roho nyepesi huwa tunaogopa posti nyingine ati,
zinaharibu siku kwa maumivu ya roho,
kama hii, nilikuwa naiepuka kwa dhati kabisa!! lakini ngoja nikaicheki sasa!
Asante
 
Nasubiri majibu kutoka kwa Chiligati, Mzee Makamba na Msekwa!

Kishoka ulisha wahi ona tu mzima povu likimtoka?
Ila ninacho shangaa they know deep inside kwamba wanacho kifanya si sawa, kweli chama chao hakina jipya, kimetekwa na mafisadi, kwanini wasiwe waungwana wakasema ukweli?
 
Rev. Kishoka:

Ideologically mpaka sasa sioni mnachopigania ni nini? CHADEMA ambao wanajifanya kuwa ni wa mkondo wa kuria, wafuasi wao mashuhuri hapa JF ni wajamaa wa kutupwa.

Hivi kuna principle gani katika harakati zenu? Hivi CCM wakiweza kuizima au kuifanyika kazi UFISADI, mtakuwa na kitu gani cha kuzungumza?

Let's face it. Critics wengi wa CCM mko brankrupty ki-ideas kama CCM yenyewe. Enlight me if I were wrong.
 
Kwa kweli Mheshimiwa Zito kwa umri wake hawapaswi kuwa CHADEMA wala CCM. Kungekuwepo na chama mbadala na hivyo hata kama ingeendeshwa kama NGO, hata mimi ningeihama CCM. Zito ndiyo aina ya vijana watakaoiongoza Tanzania baada ya 2015. Huyu na wenzie wangemfaa sana JK. JK as a leader nina hakika ndani ya nafsi yake hapendezewi na uoza huo wa CCM leadership. Sasa afanye kama alivyofanya Rais Mbingu wa Mutharika. Aanzishe chama kingine na ajitoe CCM. Ili kiwe na watu safi. Au naota jamani??
 
Ndugu Zakumi,
Kuna ubaya gani kuchukia ufisadi?
hata CCM, wakiweza kuutoa na wakajitoa kuongoza nchi kama watu wenye akili na mapenzi, hakuna mtu ataelalamika. Tatizo tu ni pale ambapo wanapogoma kubadilika, wanapogoma kufanya kazi walioomba wenyewe, walioapa wenyewe, na bado wanataka kuendelea huku wakijua fika kuwa wananchi hawapendi wanachofanya.
hii ni dharau au ujinga uliokithiri. Hakuna apenda, Naweza kukisia kuna watu wameshakula hio hela na sasa wanatamani wairudishe, manake inawatia karaha, aibu nafsi zinawasuta,
Ila sasa wale ambao ni kama nzi aonapo kidonda, anaposhindwa kukiacha, sijui tutawafanyaje, kama hatutaki kuwaua!
 
Huyu na wenzie wangemfaa sana JK. JK as a leader nina hakika ndani ya nafsi yake hapendezewi na uoza huo wa CCM leadership. Sasa afanye kama alivyofanya Rais Mbingu wa Mutharika. Aanzishe chama kingine na ajitoe CCM. Ili kiwe na watu safi. Au naota jamani??

We all wish our president could have been stronger, and do big things, which we all know are possible in Tanzania, But he doesnt!!! Where do put him??
He has his strengths though, we all know his priorities, where he can and does stretch his muscles.
 
Jamani hotuba ya ZITO ina hoja za uhakika, za ukombozi.

Mtu ukiisoma machozi yatiririka...

Hata hivyo ni watu wachache sana wanaipata, sisi tunaoisoma kila tunapotaka tupo asilimia moja.

Hii Hotuba sio kwa Busanda pekee...

Ichapishwe kwenye gazeti tena, irudiwe mara nyingi. Pia sisi wana JF tuanzishe kijarida cha JF ambapo tutachangia kuchapisha na kugawa bure.

Iwe ni vijarida ambavyo vitagawanywa hadi vijijini,

Hapa JF tutasikia,tutajadili hoja nzuri sana sa kuchukia ufisadi lakini hatufaidiki kitu. Hoja zetu zinaishia hapa hapa. Sisi tupo kama mia tano au zaidi???

Nashauri hoja nzuri kama za Zito, Kama za mishahara ya wabunge, na nyingine ziwe zijachapishwa weekly na kugawa Tanzania nzima. Tuamshe wananchi wa vijijini, na hivyo wataelewa na kujua haki zao na ukombozi wa Tanzania.
 
kwa wale tuliokuwapo tz tujitahidi hotuba kama hizi za uhamasishaji ziwafikie wale walengwa wote huko vijijini.maana sie wamijini ndio tushasikia lakini wa vijijini sidhanii kama wamesikia lolote kuhusu yaliyosemwa na mheshimiwa.mapinduzi tuanze sasa kabla ya 2010.
 
yap! kaka hayo yaloandikwa kama kariri ya yale yalosemwa na Ndg. Zito yanaonesha dhahiri kuwa huyu bw. kadhamiria na kajitoa kwa ajili ya kutetea walo wengi, ni kazi inayotaka ukomavu,ushirikiano na msimamo wa hali ya juu kuweza kufikia malengo. kama wana mageuzi wengine Zito keshafanya makubwa na ya kupigia mfano, sie pia tunaweza kufanya vile afanyavyo Zito na hasa ktk kuongeza nguvu, yule anayeumia na kulia kisa hilo neno ataweza vumilia jino

Nilimwamini sana Zitto siku za nyuma ila kitendo chake cha kutetea Dowans bado hakijafutika moyoni mwangu. Maana Dowans ni ya Rostam na kwa maana nyingine inawezekana kabisa akawa na uhusiano wa karibu sana na huyu fisadi papa. Kwa kawaida wanasiasa huwa wataalamu sana wa kutunga hotuba kwa kuangalia mazingira ya wakati husika na mara wakipewa madaraka hubadilika na kusahau ahadi zao.
Tulimwamini sana Kikwete wakati wa kampeni zake na slogan zake ya "Ari mpya, nguvu mpya na kasi mpya", pamoja na "maisha bora kwa kila Mtanzania" hakika zilikonga nyoyo za watanzania wengi mimi nikiwa mmojawao na kura yangu nilimpa. Lakini sasa twajionea wenyewe, yuko mfukoni mwa RA wala hafurukuti. Maisha bora kwa kila Mtanzania yamegeuka kuwa maisha bora kwa kundi la wanamtandao tena kwa wizi.

Kuna mtu hapa JF alishawahi kusema kuwa RA amesikika akilalamika kuwa JK hana msimamo hasa baada ya kutowatetea rafiki zake wa karibu kama EL. Sasa isije ikawa amesoma mwelekeo wa siasa za TZ akaona Zitto anaushawishi mkubwa na anaanza kumwandaa ili aje aendelee kuifisadi nchi yetu iliyobarikiwa kwa kila namna ya utajiri.

Ndugu zangu huu ni mtazamo wangu tu.
 
Nchi yetu ilipopata uhuru tulikuwa na maadui watatu wakubwa:

1. Ujinga 2. Maradhi 3. Umaskini

Leo hii almost 50 yrs down the line maadui hao hatujawakabili na mbaya zaidi wale waliokuwa na jukumu la kuongoza mapambano hayo wametuongezea lijinamizi lingine au adui mkubwa kabisa UFISADI!
 
Back
Top Bottom