Nyoka kuingia ndani ya nyumba na kutoonekana

Nyoka kuingia ndani ya nyumba na kutoonekana

fofre

JF-Expert Member
Joined
Nov 16, 2016
Posts
805
Reaction score
1,307
Habari zenu wana jukwaa,

Kama kichwa cha habari kilivyo jieleza hapo juu,

Ni kwamba siku chache zilizopita nyoka aliingia nyumbani(stoo), kitu cha kwanza tulicho kifanya ni kuchoma mpira (mnati) baada ya muda alitoka, lakini alipotuona akarudi ndani.

Kwakua ilikua ni usiku tukaamua kufunga mlango wa stoo. Kesho yake asubuhi tulimtafuta sana yule nyoka hakuonekana kabisa na hakuna uwezekano wowote wa kutoka kutokana na mazingira yalivyokuwa, baada ya kuwaelezea majirani walisema hiyo hali huwa ni kawaida kutokea na nyoka huwa anapotea.

Wenye ufahamu na hili jambo naomba mnifafanulie nielewe.
 
Atakuwa jirani huyo..upo mkoa gani? Dawa ya nyoka ni nyoka...itakuwa ni ngumu kuelewana hapo Ila dawa ya nyoka wa mazingara ni nyoka wa mazingara...watu wa gairo wanajua hiyo kitu.
 
Labda kuna shimo lake huko stoo kwenu...

Ila hawa viumbe wanaopenda kurandaranda majumbani dawa yao ni kuwageuza vitoweo tu...

Viumbe kama hao huwezi kuwakuta wanarandaranda kwende stoo/nyumba za Wachina...
 
Labda kuna shimo lake huko stoo kwenu...

Ila hawa viumbe wanaopenda kurandaranda majumbani dawa yao ni kuwageuza vitoweo tu...

Viumbe kama hao huwezi kuwakuta wanarandaranda kwende stoo/nyumba za Wachina...
Hakuna shimo kabisa maana sakafu ni cement
 
Nyoka anauwszo wakujiminya sana na akapenya sehemu ambayo hutoamini.....lakini kuna mazingira tata hapo kwamba mlivyochoma mpira then akatoka, lakini alivyowaona akarudi ndani ambako kuna nukia mpira..!!!! Ukute jirani yako huyo.

Anyway kama stoo palikua na vitu ukute kajikunyata humo ndani
 
Nyoka anauwszo wakujiminya sana na akapenya sehemu ambayo hutoamini.....lakini kuna mazingira tata hapo kwamba mlivyochoma mpira then akatoka, lakini alivyowaona akarudi ndani ambako kuna nukia mpira..!!!! Ukute jirani yako huyo.

Anyway kama stoo palikua na vitu ukute kajikunyata humo ndani
Tulitoa vitu vyote kukawa hakuna kitu kabisa
 
Habari zenu wana jukwaa, kama kichwa cha habari kilivyo jieleza hapo juu ni kwamba siku chache zilizopita nyoka aliingia nyumbani(stoo), kitu cha kwanza tulicho kifanya ni kuchoma Mpira (mnati) baada ya muda alitoka, lakini alipo tuona akarudi ndani, kwakua ilikua ni usiku tukaamua kufunga mlango wa stoo. kesho yake asubuhi tulimtafuta sana yule nyoka hakuonekana kabisa na hakuna uwezekano wowote wa kutoka kutokana na mazingira yalivyo kuwa, baada ya kuwaelezea majirani walisema hiyo hali huwa ni kawaida kutokea na nmyoka huwa anapotea. wenye ufahamu na hili jambo naomba mnifafanulie nielewe.
Imeshawahi kumtokea rafiki yangu pia,nyoka aliingia chumbani na hakutoka,walifunga mlango wakamwaga mafuta ya taa hakutoka na walipomsaka hakupatikana,mimi pia Panya aliingia chumabni kwangu,na tulimsikia akitusumbua usiku mzima, tulipoamka asubuhi kabla ya kufungua mlanguo tulimsaka chumba kizima hakuonekana.Mimi kwa imani yangu naamini kuwa inawezekana ni nguvu za giza ,nilichofanya nimepiga maombi na sijaona huyo panya mpaka leo.
 
Imeshawahi kumtokea rafiki yangu pia,nyoka aliingia chumbani na hakutoka,walifunga mlango wakwaga mafuta ya taa hakutoka na walipomsaka hakupatikana,mimi pia Panya aliingia chumabni kwangu,na tulimsikia akitusumbua usiku mzima, tulipoamka asubuhi kabla ya kufungua mlanguo tulimsaka chumba kizima hakuonekana.Mimi kwa imani yangu naamini kuwa inawezekana ni nguvu za giza ,nilichofanya nimepiga maombi na sijaona huyo panya mpaka leo.
Na baadhi ya watu nilivyo waeleza walisema hili jambo hutokea sana
 
Uchawi wa kutumiana nyoka upo sana Morogoro..Tiba yake wanayo wakaguru ndicho ninachomaanisha...dawa ya nyoka ni nyoka...kivipi? Kuna siku utamuona tena tu..
 
Habari zenu wana jukwaa,

Kama kichwa cha habari kilivyo jieleza hapo juu,

Ni kwamba siku chache zilizopita nyoka aliingia nyumbani(stoo), kitu cha kwanza tulicho kifanya ni kuchoma mpira (mnati) baada ya muda alitoka, lakini alipotuona akarudi ndani.

Kwakua ilikua ni usiku tukaamua kufunga mlango wa stoo. Kesho yake asubuhi tulimtafuta sana yule nyoka hakuonekana kabisa na hakuna uwezekano wowote wa kutoka kutokana na mazingira yalivyokuwa, baada ya kuwaelezea majirani walisema hiyo hali huwa ni kawaida kutokea na nyoka huwa anapotea.

Wenye ufahamu na hili jambo naomba mnifafanulie nielewe.

Usijipe bure ' presha ' Mkuu ukitaka kujiridhisha kabisa kama yupo au hayupo tafuta mafuta ya Taa hapo ulipo ingia nayo humo ' stoo ' yamwage kisha toka zako nje nakuhakikishia ndani ya ama Sekunde 30 au dakika 1 huyo Nyoka atakufuata ulipo na kukuomba radhi / msamaha kwani hakuna kitu ambacho kinawamudu Nyoka kama ' Kerosene ' ( mafuta ya Taa ). Hapo huwa hawana ' ujanja ' Mkuu. Hilo la kwamba sijui Nyoka huwa anapotea naomba niwe wa mwisho kuliamini kwani sijazoea kulishwa tango pori / kudanganywa na hizi ' stori ' zetu za Vijiweni na Vibarazani kwani hata Mimi nakumbuka tokea nikiwa mdogo nilikuwa nikiambiwa kuwa ukiwaona Paka Dume na Jike ' wanabanduana / wanatinduana / wanangonoka ' mubashara eti utakufa ila GENTAMYCINE nimekuwa ni ' Mdau 'mkubwa wa kuwaangalia Paka wakifanya hako ' kamchezo ' katamu tokea udogo wangu hadi sasa nawalia tu ' chabo ' nikiwafumania na nipo hai hivi.
 
Back
Top Bottom