Nyoka kuingia ndani ya nyumba na kutoonekana

Nyoka kuingia ndani ya nyumba na kutoonekana

Imeshawahi kumtokea rafiki yangu pia,nyoka aliingia chumbani na hakutoka,walifunga mlango wakwaga mafuta ya taa hakutoka na walipomsaka hakupatikana,mimi pia Panya aliingia chumabni kwangu,na tulimsikia akitusumbua usiku mzima, tulipoamka asubuhi kabla ya kufungua mlanguo tulimsaka chumba kizima hakuonekana.Mimi kwa imani yangu naamini kuwa inawezekana ni nguvu za giza ,nilichofanya nimepiga maombi na sijaona huyo panya mpaka leo.
Usiku panya huwa anapenya kwenye mlango chumbani kwangu na nimekariri kila saa NNE au tano usiku sasa akiingia nikianza kumsaka simuoni halafu chumbani hamna mavitu kweupe kila nikimsaka simuoni na kweupe sasa nikirudi kwenye kiti itapita muda kidogo namuona ananyata na kupenya kwenye mlango na kusepa nilikuwa najiuliza huwa anajificha wapi wakati kote kweupe na huwa namvizia daily akiingia ninaye lkn sekunde kayayuka simuoni nikawa nastaajabu daily ila kuna siku nikaona kitobo kidogo huwezi kugundua pembezoni ya ukuta nikajua hapo huwa anayayukia

Hamna uchawi mkuu kuna mmoja kitambo alikuwa akijificha kwenye system unit CPU huwezi kudhani kabisa chini ya CD ROM ,sema wana akili ya fasta

Nikagundua pembeni ya ukuta kwenye sakafu kuna tobo huwezi kuliona ndio huwa akiona anatafutwa huingia kule

Panya wajanja lazima kuna sehemu hapo anajificha
 
Usijipe bure ' presha ' Mkuu ukitaka kujiridhisha kabisa kama yupo au hayupo tafuta mafuta ya Taa hapo ulipo ingia nayo humo ' stoo ' yamwage kisha toka zako nje nakuhakikishia ndani ya ama Sekunde 30 au dakika 1 huyo Nyoka atakufuata ulipo na kukuomba radhi / msamaha kwani hakuna kitu ambacho kinawamudu Nyoka kama ' Kerosene ' ( mafuta ya Taa ). Hapo huwa hawana ' ujanja ' Mkuu. Hilo la kwamba sijui Nyoka huwa anapotea naomba niwe wa mwisho kuliamini kwani sijazoea kulishwa tango pori / kudanganywa na hizi ' stori ' zetu za Vijiweni na Vibarazani kwani hata Mimi nakumbuka tokea nikiwa mdogo nilikuwa nikiambiwa kuwa ukiwaona Paka Dume na Jike ' wanabanduana / wanatinduana / wanangonoka ' mubashara eti utakufa ila GENTAMYCINE nimekuwa ni ' Mdau 'mkubwa wa kuwaangalia Paka wakifanya hako ' kamchezo ' katamu tokea udogo wangu hadi sasa nawalia tu ' chabo ' nikiwafumania na nipo hai hivi.
Nitaleta mrejesho baada ya kumwaga mafuta ya taa ila tulitoa vitu vyote stoo kukawa patupu
 
Mafuta ya taa na mwaga chumvi ya kutosha nyoka atatoka.sasa ujue inawezekana amehamia chumba kingine au darini au kwenye viatu aubox uwe mwangalifu usikazanie stoo.fanya usafi ikiwa ni pamoja na kumwaga mafuta yataa na chumvi eneo lote lilinalozunguka nyumba..usisahau aliingia bila kuonekana na pia anaweza kutoka bila kuonekana.
 
Wakizaliwa huwa wanauwawa na ndiyo maana huwezi kumkuta mmasai kilema
walemavu wapo mkuu,nishawahi kuwaona,mmoja yupo pale iringa mjini anauza shanga maeneo ya posta...
 
chukua pilipili mbuzi iliyokauka kisha chomeni, manina, atatoka mwenyewe au mtamkuta keshakauka
 
ukideal na nyoka huku umetanguliza imani potofu utaishia kuamini mengi. maana nyoka hata akitoka haagi au hapigi kelele na hatoki kama bibi harusi wa zamani (hawa wa sikuhizi wanarukaruka utadhani wao ndio wameoa) ni spidi. kwa sababu ni usiku lolote linaweza kuwa lilitokea. hapa kuna ng'e amepotea kwenye mazingira ya kutatanisha namlia timing daily ipo siku ataangukia kwenye mikono yangu.
atakuwa alitoka au kahama location. Mtafute kibailojia mkuu usichanganye na imani za jadi za majirani
 
Usijipe bure ' presha ' Mkuu ukitaka kujiridhisha kabisa kama yupo au hayupo tafuta mafuta ya Taa hapo ulipo ingia nayo humo ' stoo ' yamwage kisha toka zako nje nakuhakikishia ndani ya ama Sekunde 30 au dakika 1 huyo Nyoka atakufuata ulipo na kukuomba radhi / msamaha kwani hakuna kitu ambacho kinawamudu Nyoka kama ' Kerosene ' ( mafuta ya Taa ). Hapo huwa hawana ' ujanja ' Mkuu. Hilo la kwamba sijui Nyoka huwa anapotea naomba niwe wa mwisho kuliamini kwani sijazoea kulishwa tango pori / kudanganywa na hizi ' stori ' zetu za Vijiweni na Vibarazani kwani hata Mimi nakumbuka tokea nikiwa mdogo nilikuwa nikiambiwa kuwa ukiwaona Paka Dume na Jike ' wanabanduana / wanatinduana / wanangonoka ' mubashara eti utakufa ila GENTAMYCINE nimekuwa ni ' Mdau 'mkubwa wa kuwaangalia Paka wakifanya hako ' kamchezo ' katamu tokea udogo wangu hadi sasa nawalia tu ' chabo ' nikiwafumania na nipo hai hivi.
maneno mbofu mbofu tu
 
Nitaleta mrejesho baada ya kumwaga mafuta ya taa ila tulitoa vitu vyote stoo kukawa patupu

Weka mafuta ya Taa hayo Mkuu hiyo ndiyo ' jeuri ' ya Nyoka yoyote mengineyo wanakudanganya tu. Ila kwa maelezo yako tu nadhani huyo Nyoka si kwamba ametoweka kama hao ' Waswahili ' walivyokudanganya ila yawezekana ile jana alijificha mahala na hamkumuona ila mlivyompa tu ' Visogo ' vyenu nae baade akatiririka na kuserereka zake ' kusikojulikana '.
 
Wakizaliwa huwa wanauwawa na ndiyo maana huwezi kumkuta mmasai kilema
Hapana siyo kweli, nimeshuhudia mmasai kilema miaka ya 2008 kuna shule maeneo ya mbagala alikua mlinzi
 
mimi naomba mnifafanulie kwanini hakuna masai albino?
Kwa mila na desturi za Masai, yeyote aliyezaa mlemavu alihusishwa na laana hiyo na kuonekana alifanya jambo baya katika jamii. Hivyo, ili kuipoteza laana na kuondoa mkosi huo, mtoto akibainika kuwa mlemavu, alikuwa akiuawa kwa kunyongwa, au kutupwa porini ajifie au aliwe na wanyama.

Mwanamke akijifungua Ormaima (mlemavu/albino) familia hufanya mikakati kumkabidhi kwa “Orkirkoi” yaani mtu anayetumika kunyonga Ormaima au kuwatelekeza porini. Orkirkoi hufanya kazi hiyo kwa ujira wa ng’ombe. Analipwa na ndugu wa mtoto mlemavu anayenyongwa au kutelekezwa afie porini na hukubaliana kuitunza siri hiyo mpaka kufa.
 
Kama ni nyumba ya nyasi amechill anasikia mwekee kioo mwite kwa kisukuma utamwona anakuja anacheza
 
Doh, Nyoka amepotea kusikojulikana,aaah, kumbe haya mambo yanawezekana?
 
mimi naomba mnifafanulie kwanini hakuna masai albino?
Kwa sababu tuu wewe hujawahi kutana nao husigeneralise kwamba hakuna, mimi nimeenda nao shule na kijijini kwetu walikuwepo mpaka wazazi albino.
 
Back
Top Bottom