Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,470
- 911,174
Nyerere asimamisha ujenzi wa shule
na Mwandishi wetu, Musoma
MBUNGE wa Musoma Mjini, Vincent Nyerere, amesimamisha ujenzi wa shule ya sekondari ya Nyasho baada ya ujenzi huo kuendeshwa bila mtaalamu anayetambulika kisheria.
Akiwa katika shule hiyo, Nyerere alisema kuendelea kuruhusu kujengwa kwa darasa hilo ni kukaribisha maafa ambayo yanaweza kutokea kwa wanafunzi watakaolitumia jengo hilo huku watu wachache wakiendelea kunufaika kwa udanganyifu wanaoufanya katika ujenzi, ili kutumia fedha za umma vibaya.
Nyerere ambaye alikuwa amefuatana na kamati yake ya kutembelea shule mbalimbali za jimbo hilo, alisema ana taarifa kuwa shule hiyo imepewa sh milioni nne kwa majengo mawili, lakini katika shule hiyo ni jengo moja linaloonekana.
Ninachokielewa katika ujenzi wa majengo ya shule hii yanatakiwa kuwa mawili sasa jengo lingine liko wapi mbona linaonekana moja? Je fedha za jengo lingine zipo? aliuliza mbunge huyo.
Kutokana na hali hiyo, Nyerere alimwagiza Mtendaji wa Kata ya Nyasho, Everist Tiginga, kuhakikisha sh milioni mbili zilizosalia zinapatikana, ili zitumike katika kutengeneza madawati ambayo yatasaidia wanafunzi watakaojiunga katika shule hiyo.
na Mwandishi wetu, Musoma
Akiwa katika shule hiyo, Nyerere alisema kuendelea kuruhusu kujengwa kwa darasa hilo ni kukaribisha maafa ambayo yanaweza kutokea kwa wanafunzi watakaolitumia jengo hilo huku watu wachache wakiendelea kunufaika kwa udanganyifu wanaoufanya katika ujenzi, ili kutumia fedha za umma vibaya.
Nyerere ambaye alikuwa amefuatana na kamati yake ya kutembelea shule mbalimbali za jimbo hilo, alisema ana taarifa kuwa shule hiyo imepewa sh milioni nne kwa majengo mawili, lakini katika shule hiyo ni jengo moja linaloonekana.
Ninachokielewa katika ujenzi wa majengo ya shule hii yanatakiwa kuwa mawili sasa jengo lingine liko wapi mbona linaonekana moja? Je fedha za jengo lingine zipo? aliuliza mbunge huyo.
Kutokana na hali hiyo, Nyerere alimwagiza Mtendaji wa Kata ya Nyasho, Everist Tiginga, kuhakikisha sh milioni mbili zilizosalia zinapatikana, ili zitumike katika kutengeneza madawati ambayo yatasaidia wanafunzi watakaojiunga katika shule hiyo.