Sera zake mbovu alizo siasisi ndio zimeimaliza nchi hii. Aliposhindwa baada ya kutawala zaidi ya miaka ishirini na kushuhudia kila kitu kikishindwa na maji yapo shingoni, yanakaribia kuingia mdomoni, kiujanja ujanja na kiutu uzima akaamua kutoroka uongozi, ndio akamtupia Mwinyi kwa kusingizia kuwa anan'gatuka mapema...!
Ndugu yangu X-PASTER unajua sisi ndiyo nchi pekee East Africa kujega university yetu. Hiyo university of Nairobi na Makere walijenga wazungu. Sasa uliza nani alijenga UDSM? Leo hii wewe umefaidika na matunda ya Nyerere kwa kusoma hadi chuo kikuu halafu unasema sera zake mbovu? Kweli shukurani za punda ni mateke.
Sasa ngoja turudi kwenye historia ya Tanganyika ili uelewe kwanini mwalimu alianzisha hizo sera zake. kumbuka Tanganyika ilikuwa ni koloni la wajerumani, Kama unavyojua koloni ni kama kuwa na mtoto wa kumzaa inabidi umlee. Uthibitisho huu upe hadi leo jinsi wajerumani walivyowekeza Tanganyika (hapa ieleweke sitetei unyonya wao) kama reli, Boma, shule, barabara, mashamba ya mkonge na miji mbalimbali.
Baada ya vita kuu ya kwanza Muingereza, alituchukua kama yatima, na utaona hakuwekeza zaidi ya kujenga vijumba vya uzunguni, hakufanya kitu cha maana kama ujenzi wa reli ya kati ya Mjerumani.
kwa hiyo nchi yetu haikuwa na kitu wakati Mwalimu anaichukua, ilibidi aijenge upya, ndiyo maana alianzisha sera zake za watu, siasa safi na uongozi bora. Katika watu aliwekeza kwenye elimu. Mimi sikubahatika kusoma kipindi hicho cha elimu bure kwasabau sikuwa nimezaliwa lakini wazazi wangu na ndugu zangu wengi walisoma bure.
Kwasababu ya elimu bure waliweza kusoma na hatimaye hata watoto wao (sisi) tumeweza kufika hapa tulipo kwasababu ya mbegu aliyoipanda Mwalimu miaka hiyo ambayo tulikuwa hatujazaliwa. Hiyo ndiyo dira au sera za mtu mwenye uelewa kama wa Mwalimu kuweka msingi ambao matokeo yake yanasaidia kizazi hata cha tatu na cha nne.
Sasa X-PASTER labda sema tuu unataka kuchokoza watu hapa lakini najua unaelewa nichokisema hapa.
Tanzania ni kubwa kulinganisha majirani zetu. Ili kujenga nchi kubwa kama yetu ilibidi mwalimu aondoe ukabila, sasa najua hili hatulioni kama ni faida lakini mimi nimewaona wakenya wengi ambao badala ya kuongea vizuri kama Wakenya wao wanaangaliana kwa makabila. Yaani unakuta Mkenya yuko radhi aongee na Mtanzania kuliko Mkenya mwenzake eti kwasababu anatoka kabila tofauti. Sasa utaniambiaje sera zake zilikuwa mbovu? Wewe hapo unabonga kiswahili kama huna akilia nzuri sasa unafikiri isingekuwa Mwalimu ungeweza kujidai hivyo?
Mi nafikiri wewe na wengi mnaomponda Mwalimu hamuelewe kitu kidogo kinachoitwa msingi. Nyerere aweka msingi mkubwa ila hao waliomfuata waliharibu kila kitu.
Hayo mambo ya kupanga foleni ni kutokana na njaa iliyokumba ukanda wetu (1975) na matatizo ya mafuta yaliyosababishwa na kutokuelewana kati ya waisraeli na warabu. kabla ya hapo uchumi wetu ulikuwa mzuri tuu na madini yetu yalikuwa salama.
Pia kumbuka kuwa wamagharibi walihakikisha ujamaa haufanikiwi (vita vya baridi) kwasababu kufanikiwa kwake kungeleta ushawishi mkubwa katika bara letu kwa hiyo walihakikisha kiuchumi hatufanikiwi. Hata hivyo tulikuwa na viwanda vyetu kama bora, na bidhaa nyingi za made in Tanzania. Chakushangaza sasa hivi watu wanaona ufahari kuvaa Gucci feki eti ruksa aaaaH inakera.
Nchi haipimwi maendeleo kwa watu kumiliki vigari vya mkopo kutoka dubai kama tunavyo danganywa na viongozi wetu bali itaendelea kama itazalisha; iwe tekinolojia, mawazo, bidhaa, nishati n.k na kuuza nchi nyingine na hapo itaweza ingiza fedha za kigeni ambazo zikaingia kwenye mzunguko na kuleta maendeleo. Sio kuchapisha mapesa yasiyo na thamani, yanayo jaa bila ya kuzalisha kitu. Upo mkuu?
Nitaishia hapa kwa leo.