chief kamchicha
Member
- Jan 22, 2014
- 29
- 56
Mwaka 1978/79 Mwl Nyerere katika uongozi wake aliamua kuingiza nchi vitani kupambana na nduli Idd Amin Dada wa Uganda, ilikua vita ngumu sana, na ilikua ni lazima kumpiga idiamin Ili tanzania iwe salama. Wapo waliomlaumu kwa uamuzi wake wa kwenda vitani, na wapo waliompongeza na kumuunga mkono. Kubwa ilikua ni umuhimu wa vita ile ndani na nje ya Tanzania.
Madhara ya vita ile yalikua ni makubwa na hayaelezeki lakini ilikua ni kheri kuvipiga vita kuliko kukaa na kusubiri kudhihakiwa na idiamini na kuendelea kuua watu wetu maeneo ya kagera.
Vita ni vita huo ndio msemo uliozoeleka kwa ndugu zangu wakurya. Nyakati hizi magufuri anavipiga vita, vita ngumu ya nyakati hizi, vita inayopiganwa na dunia nzima, vita ambayo bado mshindi anaendelea kuwa corona na mshindwa akiendelea kupoteza wapiganaji mahiri wa upande wake. Mheshimiwa anavipiga vita katika mstari wa mbele kabisa pamoja na mataifa tajiri ilimwenguni, hakika historia Inawaandika viongozi wote wa nyakati hizi maana kipimo cha uongozi wao.
Historia itawaandika kwa uwezo wao wa kufanya maamuzi katika hali ngumu. Bila kujari uamuzi waufanyao ni mzuri au mbaya.
Magufuli ataandikwa kama kiongozi shupavu na imara aliyekataa kuburuzwa na sera za kimataifa juu ya ugonjwa wa corona, kwanza kuukataa ugonjwa, kuvikataa vipimo vyao na sasa anazikataa chanjo zao.
Uamuzi wowote uliofanywa si kwa nia mbaya kwa jamii, ila ni katika kutapatapa kuwaokoa na kuwanusuru watu wake.
Vita ni vigumu ila ushindi ni lazima, tuendelee kumuombea kiongozi huyu maana najaribu kuvuta picha kwasasa anajisikiaje, anahuzuni kiasi gani na anamawazo kiasi gani. Japo si mkubari magufuri kwa baadhi ya maswala ila sichoki kumuombea katika wakati huu mgumu.
Chief kamchicha
Madhara ya vita ile yalikua ni makubwa na hayaelezeki lakini ilikua ni kheri kuvipiga vita kuliko kukaa na kusubiri kudhihakiwa na idiamini na kuendelea kuua watu wetu maeneo ya kagera.
Vita ni vita huo ndio msemo uliozoeleka kwa ndugu zangu wakurya. Nyakati hizi magufuri anavipiga vita, vita ngumu ya nyakati hizi, vita inayopiganwa na dunia nzima, vita ambayo bado mshindi anaendelea kuwa corona na mshindwa akiendelea kupoteza wapiganaji mahiri wa upande wake. Mheshimiwa anavipiga vita katika mstari wa mbele kabisa pamoja na mataifa tajiri ilimwenguni, hakika historia Inawaandika viongozi wote wa nyakati hizi maana kipimo cha uongozi wao.
Historia itawaandika kwa uwezo wao wa kufanya maamuzi katika hali ngumu. Bila kujari uamuzi waufanyao ni mzuri au mbaya.
Magufuli ataandikwa kama kiongozi shupavu na imara aliyekataa kuburuzwa na sera za kimataifa juu ya ugonjwa wa corona, kwanza kuukataa ugonjwa, kuvikataa vipimo vyao na sasa anazikataa chanjo zao.
Uamuzi wowote uliofanywa si kwa nia mbaya kwa jamii, ila ni katika kutapatapa kuwaokoa na kuwanusuru watu wake.
Vita ni vigumu ila ushindi ni lazima, tuendelee kumuombea kiongozi huyu maana najaribu kuvuta picha kwasasa anajisikiaje, anahuzuni kiasi gani na anamawazo kiasi gani. Japo si mkubari magufuri kwa baadhi ya maswala ila sichoki kumuombea katika wakati huu mgumu.
Chief kamchicha