Nyaronyo Kicheere 'ahamia CCM'

Nyaronyo Kicheere 'ahamia CCM'

Mkuu New Force, jameni hizi avatar nyingine!, muwe na huruma japo kidogo, wengine wenzenu tuu dhaifu, hivyo avatar kama hizi ni kutiana tuu majaribuni!, badala ya concenrate na suject matter unajikuta unaishia kukodolea macho avatar huku mawazo yakikupeleka kwengine!.

Hebu wewe jifikiriea avatar kama hii halafu msomaji post ni mtu wa Kanda ya Ziwa!.

image.tiff


Pasco.

Mkuu Pasco Lowasa akiwa rais Rais akakukumbuka kwenye ufalme wake watoto wetu weupe watakwisha.
 
Last edited by a moderator:
Kwa hii thread, walofeli "literature" tutawajua tu kwa kuangalia comments zao!
Wako kibao humu. Lakini sio kufeli nadhani ni kutojua. Kwa kuwasaidia ni kuwa makala hii imeandikwa kwa mtindo wa kejeli. Kejeli maana yake huwa ni kinyume na inavyoelezwa. Mfano mtu anafungwa goli tano halafu anaambiwa "wewe ni kipa mzuri sana" Watu wajifunze kutafakari kabla ya kukurupuka kujibu hoja. Na wengi humu Jf huwa wanaangukia katika mtego huo. Ndio maana wengine badala ya kujadili hoja utakuta wanamshambulia mtoa hoja binafsi au mtu anajibu nje kabisa ya kinachojadiliwa. Kwa ufupi ni kwamba anamkandia Kikwete kwa udhaifu wake wa kutochukua hatua kwa wahalifu na kuwasifu viongozi wa CHADEMA kwa kuwa serious!
 
Hii habari ya Nyaronyo Kicheere kuhamia CCM imeadikwa leo kwenye Gazeti la ----- yenye kichwa: NIMEHAMIA CCM,CHADEMA HAKUNIFAI.

Hii habari imeandikwa kwa namna ya kimafumbo sana. Inahitaji ubongo uliokwenda shule kujua au kupata maana ya ujumbe ulioko ndani ya habari hii.Wazungu husema, you have to read between the lines. Hapa ndipo unaweza kujua nani walisoma RIWAYA na TAMTHILIA na kufaulu mitihani ya Kiswahili au LITERATURE IN ENGLISH( Theme:CONFLICT,PROTEST,etc). Nashangazwa na Magamba kushangilia ati kweli Nyarocho kahamia CCM!! Hahami mtu hapa. Ebo!

Hapa Nyaronyo amewapiga chenga ya mwili hasa wale ambao husomaga vitu juu juu! Ukisoma kwa makini hii habari utagundua moja kwa moja kwamba hapa HAHAMI MTU HAPA TOKA CHADEMA! Kwa kifupi ni kwamba amemchanachana Rais Kiwete kwa kumkebehi kuwa ni MTU MWENYE SURA NZURI NA MPOLE SANA anayeishia kuwasamehe WAIZI WA FEDHA YA EPA,PEMBE ZA NDOVU na WAUZA MADAWA YA KULEVYA. Ameendelea kumsifia Kiwete kwa kuwa ni mtu mcheshi mwenye tabasamu wakti wote ilhali Viongozi wa CHADEMA hawana.

Kwamba Viongozi wa CHADEMA WANA SURA MBAYA,WEUSI,WAKALI NA WAKTI WOTE WAMENUNA!Hawa hawana huruma na mtu kwa hiyo Kicheere ameamua kuhama CHADEMA kwa sababu hizi ambazo kiukweli zinanogesha tu hii habari yenyewe ili kujaribu kuonyesha tofauti iliyoko kati ya CCM na CHADEMA!!!

HAHAMI MTU HAPA!
Unakumbuka kuna kipindi flani aliandika kuwa anataka kubadili jina aitwe riziwani na alipamba sana maandishi yake na kutoa sababu kem kem za yeye kubadili jina. Kweli huyu mwandishi ni mahiri , wanaosoma kichwa cha habari na kuchangia lazima waingizwe chaka lol.
 
Mwandishi Mahiri wa Makala na Mwanasheria wa Jijini Dar es Salaam Nyaronyo Mwita Kicheere amehamia CCM, kati ya sababu kubwa zilizomhamisha CHADEMA, anasema Viongozi wake hawana sura ya Tabasamu, tofauti na viongozi wa CCM, Kikubwa zaidi anasema ameamua kuipenda CCM kwa kuwa Mwenyekiti wake Jakaya Kikwete ni mtu Rahimu, anayependa watu wake na kuwahurumia kutokana na magumu ya maisha, Juzi juzi ametangaza jinsi alivyopelekewa orodha ya majangili 40 wanaotikisa mbuga zetu lakini hakuwachukulia hatua yeyote kwa kuwa wanafanya ujasiriamali kujikimu na wanaweza kuwekeza. Nyaronyo amesema pia, anahamia CCM kwani kesho au keshokutwa akikamatwa na ngozi ya Chui, ya Mamba, au meno ya Tembo atapata msamaha kama wale 40 waliosamehewa na Kikwete.

Nyaronyo anasema, CHADEMA wangekuwa madarakani leo, ambao viongozi wao hawana tabasamu, akamtaja Mbowe Slaa, Lissu na Lwakatare nchi isingekalika, maana ni wazee wa visasi, maana Wezi wangekamatwa, watekaji wangesakwa, wauza dawa za kulevya wangekuwa wote gerezani.

Tena akaongeza kuwa hii si mara ya kwanza Kikwete kusamehe. Amesamehe Majangili 40, kama alivyosamehe wezi wa EPA, Nyaronyo anasema Tumshukuru Mungu kwa kuwa na Kikwete, Rais anayesamehe. = Chanzo gazeti la -----

sijakusoma....................
 
Tanzania inahitaji akili kama hizi siyo za kufuata mkondo kama mto.
 
Naam, ngoma inogile, tutampokea tundu lissu na pro.safari na baregu sio mda mrefu

Wewe kweli T2015 CCM maana unachangia bila ya kutambua maudhui ya MADA. Ungemfahamu Nyaronyo Kichere ni nani usingeandika ulichoandika
 
Mbona watu wanamtete sana eti lugha ya kimafumbo hamna kitu kama hiyo hapa bongo.Siasa haina fasihi wewe ipo siku mtasikia mbona Zitto aliposema Atakuwa wa mwisho kuondoka CDM mkasema mnafiki.Mimi simwamini hata siku moja mtu anayeongea kwa jina la Siasa hapa kuna kitu hizi statement hazitoki bure bure.2015 sio mbali just around the corner tutajua watoa statement zakujifanya kama hawataki lakini wanataka.
 
Mwandishi Mahiri wa Makala na Mwanasheria wa Jijini Dar es Salaam Nyaronyo Mwita Kicheere amehamia CCM, kati ya sababu kubwa zilizomhamisha CHADEMA, anasema Viongozi wake hawana sura ya Tabasamu, tofauti na viongozi wa CCM, Kikubwa zaidi anasema ameamua kuipenda CCM kwa kuwa Mwenyekiti wake Jakaya Kikwete ni mtu Rahimu, anayependa watu wake na kuwahurumia kutokana na magumu ya maisha, Juzi juzi ametangaza jinsi alivyopelekewa orodha ya majangili 40 wanaotikisa mbuga zetu lakini hakuwachukulia hatua yeyote kwa kuwa wanafanya ujasiriamali kujikimu na wanaweza kuwekeza. Nyaronyo amesema pia, anahamia CCM kwani kesho au keshokutwa akikamatwa na ngozi ya Chui, ya Mamba, au meno ya Tembo atapata msamaha kama wale 40 waliosamehewa na Kikwete.

Nyaronyo anasema, CHADEMA wangekuwa madarakani leo, ambao viongozi wao hawana tabasamu, akamtaja Mbowe Slaa, Lissu na Lwakatare nchi isingekalika, maana ni wazee wa visasi, maana Wezi wangekamatwa, watekaji wangesakwa, wauza dawa za kulevya wangekuwa wote gerezani.

Tena akaongeza kuwa hii si mara ya kwanza Kikwete kusamehe. Amesamehe Majangili 40, kama alivyosamehe wezi wa EPA, Nyaronyo anasema Tumshukuru Mungu kwa kuwa na Kikwete, Rais anayesamehe. = Chanzo gazeti la -----
hizo ndizo sifa za kuwa kiongozi wa chama cha ccm
 
Back
Top Bottom