Hebu ngoja niandike -----
Ni kweli kabisa hili gazeti la m a w i o sijui limewakosea nini.
Mwandishi Mahiri wa Makala na Mwanasheria wa Jijini Dar es Salaam Nyaronyo Mwita Kicheere amehamia CCM, kati ya sababu kubwa zilizomhamisha CHADEMA, anasema Viongozi wake hawana sura ya Tabasamu, tofauti na viongozi wa CCM, Kikubwa zaidi anasema ameamua kuipenda CCM kwa kuwa Mwenyekiti wake Jakaya Kikwete ni mtu Rahimu, anayependa watu wake na kuwahurumia kutokana na magumu ya maisha, Juzi juzi ametangaza jinsi alivyopelekewa orodha ya majangili 40 wanaotikisa mbuga zetu lakini hakuwachukulia hatua yeyote kwa kuwa wanafanya ujasiriamali kujikimu na wanaweza kuwekeza. Nyaronyo amesema pia, anahamia CCM kwani kesho au keshokutwa akikamatwa na ngozi ya Chui, ya Mamba, au meno ya Tembo atapata msamaha kama wale 40 waliosamehewa na Kikwete.
Nyaronyo anasema, CHADEMA wangekuwa madarakani leo, ambao viongozi wao hawana tabasamu, akamtaja Mbowe Slaa, Lissu na Lwakatare nchi isingekalika, maana ni wazee wa visasi, maana Wezi wangekamatwa, watekaji wangesakwa, wauza dawa za kulevya wangekuwa wote gerezani.
Tena akaongeza kuwa hii si mara ya kwanza Kikwete kusamehe. Amesamehe Majangili 40, kama alivyosamehe wezi wa EPA, Nyaronyo anasema Tumshukuru Mungu kwa kuwa na Kikwete, Rais anayesamehe. = Chanzo gazeti la -----
Hana akili huyu kama hiyo ndio sababu.wizi na ufisadi ulioko nchini wewe unauunga mkono?kweli akili ni nywele.kila mtu ana zake
Safari,Sijamwelewa hapa?
shule na vyuo vya kata ni janga!
Ni mtu makini sana anajiamini sana, ana watoto wazuri kweli ningekuwa sijaoa ningemuoa RHOBI au Tumaini, makala zake zina fasihi sana na ukiingia kichwakichwa utaweza kumuelewa.......... nakumbuka ndio aliyemtimua nchimbi jangwana.... Ukimuona yupo simple sana, nampenda sanaaaaaaaaaa.
Naam, ngoma inogile, tutampokea tundu lissu na pro.safari na baregu sio mda mrefu
Hana akili huyu kama hiyo ndio sababu.wizi na ufisadi ulioko nchini wewe unauunga mkono?kweli akili ni nywele.kila mtu ana zake
CCM inapendwa jamani, tuache utani
Mkuu soma vizuri, Jamaa amewakilisha kifasihi.
Mkuu umesoma mada kwa umakini kweli?
mwanasheria nguli mkali wa fasihi umefikisha ujumbe kwa mkuu wa kaya.mzee wa tabasamu,mtu wa kusamehe ingawa anawajua majangili,wezi ,wauza poda,.......kweli nyaronyooooo kicheeeeeeere umetisha
wewe ndo hujaelewa chochote katika uzi huuNaam, ngoma inogile, tutampokea tundu lissu na pro.safari na baregu sio mda mrefu
Hana akili huyu kama hiyo ndio sababu.wizi na ufisadi ulioko nchini wewe unauunga mkono?kweli akili ni nywele.kila mtu ana zake