Mzee Mwanakijiji,
Nimezisoma zote hizo mbili za mwanzo kwakweli hakuna cha muhimu kilichozungumziwa zaidi ya siasa tu. Kama alivyosema Gurudumu at least hii ya mwisho ya Pension Watch imezungumzia zaidi but haijachambua vya kutosha kwani Pension funds and Other thrift institutions zimekuwa zikijiingiza si tu katika infrastructure bali hata kwenye financial markets particularly kuwekeza katika makampuni makubwa kwa kununua shares na kukopesha kwenye bond markets.
Tuje katika madai ya kwamba hakuna misingi ya kuregulate hizi thrift institution hilo sio kweli na infact mnaosema hili hamjafanya your homework vizuri. Banking and Financial Institution Act ya mwaka 1991 ilikuja kufungua mianja ya sekta ya fedha na ikaweka misingi ya vp hiyo sekta iendeshwe. Vile vile Bank of Tanzania Act ya mwaka 1995 iliweka misingi ya vipi hizi sekta za fedha ziwe zinasimamiwa. Pia katika industry husika (social security) kuna Act mbali mbali zilianisha utaratibu wa kuendeshwa kwa hizo sekta. National Provident Fund of 1964 amended in by the Nationa Social Security Act of 1997, Parastatal Pension Fund of 1978 , Public Services Retirement Benefit Act of 1999 and National Health Insurance Act of 1999 na LAPF Act of 2000. Hivyo wanandugu framework zipo na zimekaa vizuri kwani mfumo wake hauna tofauti sana na uliopo katika nchi za Marekani na UK.
Kuhusu lack of regulator of these pension funds and insurance companies at the moment Bank of Tanzania ndio msimamizi wao mkuu but serikali iko katika mchakato wa kuanzisha hilo nadhani walianzisha Social Security Regulatory Authority Act 2008 . Nadhani mwaka jana walikuwa wako mbioni kwani walikuwa wanatafuta Director General wa Regulator. Nakumbuka tarehe 2 January 2011 walitangaza kuwa itakuwa operational this September 2011. Kwahivyo serikali inajiandaa kulitekeleza hilo but Bank of Tanzania still ina perform function ya kuregulate.
Ijapokuwa hiyo Authority haijawa operational hakumaanishi ya kwamba hizi Thrift institutions zisijipanue. Basle 2 ilipokuja iliweka kiwango cha mwisho hizi financial institutions zinatakiwa ziwe na pesa katika balance sheet zao ili kuziwezesha ziweze kuwekeza katika sekta mbali mbali. Hili lilifanywa kwasababu ilionekana hizi institutions zinahela nyingi but zimebanwa mno na usimamizi. Ndio maana ukaona PPF, NSSF zikaanza kujitanua kuwekeza katika majengo na sekta zenginezo. Nia na madhumuni kwanza kupunguza hizi institutions kukaa na pesa nyingi katika mifuko yao (kitu kinachoweza kuchochea ufisadi na mifano ipo kuna thread humu DG wa PPF anatuhumiwa kuiba milioni 500 unadhani chanzo kikuu nini?) , Pili hizi sekta zikikaa na pesa nyingi zinakuwa hazitanuki kimaendeleo na matokeo ni kuwa poor services na kadhalika. Tatu zikitanuka zinachochea maendeleo katika jamii.
Sio kila kitu waungwana muweke conspiracy theory kuna vitu vengine acheni taaluma za watu zifanye kazi zao kwani wanajua wanachokifanya. Moja ya watu wanaojua nini wanafanya ni Dr Dau and I support him kwani it makes sense anachokifanya sio yule anayepita akihonga akina mama na kuzila pesa hovyo!!!!