Habari wana JF, nimejiunga na hii Forums siku si nyingi, ila nimependa sana comment zenu , na ushauri mnaotoa kwa watu mbali mbali pale wanapoomba msaada wa mawazo, nami nikavutiwa nikaona bora nijiunge nanyi labda nitapata mawazo mazuri ambayo yatanifanya niendelee kuishi.
Mimi ni mtoto wa pili katika familia yetu, tulizaliwa wasichana wote 4, tulilelewa vizuri na kusomeshwa pia, bahati nzuri tulipata kazi na Mungu akabariki tuliolewa wote, ila katika maisha Mungu huwa na mipango yake, ndugu zangu wawili wakafariki dunia na kutuachia watoto ambao tunawalea mm na mdogo wangu.Katika kuishi huko mm ndoa ikanishinda ikabidi niachike, nikaenda kujenga kwenye kiwanja cha wazazi wangu, nashukuru Mungu maisha yakaanza kuwa mazuri, nikawa naweza kulea watoto wangu wawili pamoja na wandugu yangu wawili umla nilikuwa na watoto 4.
Katika kuishi huko nikaweza kuongeza nyumba ya pili ambayo nimepangisha napata pesa za kusomeshea watoto. Lakini linalonitatiza ni Mama yangu Mazazi simuelewi kabisa, kwamba anataka mm nitafute sehemu nihame pale kwa sababu anahitaji hizo nyumba kupangisha , anasema nimeshakaa sana inatosha, sasa nikamuuliza kuwa mm si ndiyo nimejibana nikajenga, ananiambia nitoe tofari zangu.
Imefikia steg ya kubagua hata wanangu, kwa kweli inaniuma sana, kwa sababu yeye ni mama yangu, anatakiwa aniunge mkono aslimia 100, lakini yeye ndiyo anakuwa kikwazo kwangu , sifahamu ni kwa nn, na kama nimemkosea kwa nn asiniambie?, najiuliza nimemchukiza nn, sipati jibu.Kama matumizi nampa, au anaona hazitoshi?
Sipendi kuandika hapa , ila imenibidi, naona sina faida ya kuendelea kuishi, maana mume kanishinda
na ninayemtegemea kunisupport kanigeuka, naona bora nife mm na wanangu nimuachie hizo nyumba.
naombeni ushauri nifanyeje?