Huo ndio uongo wa shetani. Anawachinja watu halafu anawadanganya kwa kuwaambia: "jirani yako ndio mchawi" Matokeo yake watu badala ya kupambana na shetani wanapambana na majirani zao.
Shetani leo nimekuumbua; ukome kuwadanganya watu.
Usiogope hawezi kukufwata wala kukutesa, umemkosea nini mpaka akufanyie hayo yote
Ni Wachawi wanakutesa
Bado upo kwenye tatizo la kushindwa kutofautisha
Lakini pia unasumbuliwa na changamoto ya kutokutumia madaraja/rank/classification unapokuwa ukilinganisha vitu
Tunapokuwa tunazungumzia vitu tunatumia ranks
Kama ni Tembo basi waweke kwenye kundi lao la Tembo
Kama ni Paka weka kundi la Paka
Unachofanya wewe ni kuweka Paka kundi la Tembo ndio maana classification inakataa
Na hiki ndicho tunachoshindwana hapa sio kingine
Wewe unanieleza kuwa mjusi anaweza kumnyonga Simba ndio maana tunabishana
Waone Mashehe wenye elimu ya Majini wakusaidie kutofautisha kati ya Wachawi, Mizimu, Vibwengo na Majini na hawa ndio wanaokusumbua
Fanya hivyo itakusaidia sana
Huna cha kumshawishi Shetani apoteze muda wake kuja kwako kwasababu wewe sio Malaika wala haupo daraja la Malaika ambalo ndio rank yake
Wewe huwezi kukaa daraja la Malaika bali daraja lako ni la binadamu
Angalao ungekuwa Malaika ndipo angekukumbuka au kukuona lakini wewe ni binadamu, daraja lako ni la binadamu na mara nyingi utapambananishwa na binadamu wenzako pamoja na Wanyama
Hakuna atakae kuandalia shindano la mapigano na Malaika kwasababu utashindwa
Lakini ukiandaliwa shindano na binadamu mwenzako unaweza kushinda
Shikilia kanuni yangu ya Ukuu
Siku zote raisi ataweka miadi na raisi mwenzake
Dollar ya Marekani itakaa kwenye kundi la dollar
Euro itakaa kundi la Euro, Tshillings hali kadhalika
Huwezi kuwambia watu kuwa Tshillings au Kshillings ipo kwenye kundi la Dollar au Euro
Nikieleza watu kuwa raisi wa Marekani alifunga safari kuja mtaani kwangu kuzungumza na mimi kwanza kabisa nitatengeneza taswira ya uenda wazimu mbele za watu, watu watasadiki kuwa nasumbuliwa na matumizi ya mihadarati au kichaa
Kwanini watasema hivi ni kwasababu watatumia formula ya Ukuu
Formula ya Ukuu inasema kuwa Tembo atakaa kundi la Tembo wenzake kwasababu wanaendana lakini Tembo hataweza kukaa kundi la Paka kwasababu ya kupishana kwa madaraja
Nazungumza kwa kutumia Ukuu na Madaraja, sizungumzi kama Chiriku mwenye lengo la kusifia
Nakuacha na swali hili naomba unijibu tafadhali
Swali: Je yupo mbuzi aliyewahi kumnyonga Tembo?
Kama yupo basi thibitisha
Kama hayupo toa sababu kwanini haijawezekana mbuzi kumnyonga tembo!
Setfree