Njoo uone huyu jamaa anavyomzodoa shetani hadharani

Njoo uone huyu jamaa anavyomzodoa shetani hadharani

Iko hivi sio kwamba ni wasaidizi au labda anawatuma
Hawa mizimu na majini nao wana uroho wa madaraka wanafanya hivyo ili nao waheshimike
Na mara nhingi wanatumia jina lake kuwahadaa watu kwamba wao ndio Shetani lengo lao wapate heshima
Ni sawa na Wachungaji matapeli watakudanganya Mungu amewatuma kwako ila lengo lao wanataka uwaheshimu na uwape fedha zako
Kwahiyo hawa majini na mizimu watakudanganya wao ni Shetani kwasababu wanataka uwaogope Setfree
Wewe kumbe huijui historia ya shetani. Shetani alikuwa malaika mkuu mbinguni, wakati huo alikuwa akiitwa Lucifer. Huyo ndiye aliyeongoza uasi mbinguni kwa kushirikiana na theluthi moja ya malaika waliokuwa chini yake. Alivyotupwa chini hao malaika wadogo wakatupwa pamoja naye. Hao ndio wanaojulikana kama mapepo, na wengine wanawaita majini au vibwengo. Wote wanafanya uovu kwa pamoja na hukumu yao wote imeishatolewa.

Acha kumsifia shetani. Ukiendelea kumsifia na kushirikiana naye utatupwa motoni pamoja naye.
 
Kila mtu awe mdogo awe mkubwa, awe mtume awe layman, maadam amekokoka, amepewa mamlaka ya kumkanyaga shetani (Luka 10:19). Shetani ni muongo, anajimwambafy tu lakini Jina la Yesu likitajwa anatetemeka. Unafikiri hii mada haioni? Anaiona sana tu lakini hana nguvu ya kunizuia kumzodoa!
Nakuelewa lakini sasa huwa hafwati watu kwasababu anatuona ni wadogo kwake sisi tunaishia kupigana na Wachawi, Mizimu na Majini

Na hawa majini wana tabia ya kutumia jina lake watakwambia wao ni Shetani
Sio hivyo tu hata Mizimu wanauwezo wa kutupotosha wao wametumwa

Lengo lao waogopwe
Ndio maana kila kona ya dunia kuna mabango ya kutibu matatizo ya Majini na Mizimu au vinwengo kama Chuma ulete
Hawa ndio wanatusumbua kila siku Setfree
 
Wewe kumbe huijui historia ya shetani. Shetani alikuwa malaika mkuu mbinguni, wakati huo alikuwa akiitwa Lucifer. Huyo ndiye aliyeongoza uasi mbinguni kwa kushirikiana na theluthi moja ya malaika waliokuwa chini yake. Alivyotupwa chini hao malaika wadogo wakatupwa pamoja naye. Hao ndio wanaojulikana kama mapepo, na wengine wanawaita majini au vibwengo. Wote wanafanya uovu kwa pamoja na hukumu yao wote imeishatolewa.

Acha kumsifia shetani. Ukiendelea kumsifia na kushirikiana naye utatupwa motoni pamoja naye.
Yani tunakuelewa
Hatuzungumzi kwa kusifia bali kutaka kuonesha kuwa tutizame tumepishanaje na vitu kuanzia umri ndipo tunyooshe kidole

Swala ni kwamba Shetani hafwati watu kwasababu hatuna cha kumshawishi wanaotufwata ni Mizimu, Vibwengo, Wachawi na Majini
Na hawa wana tabia ya kujifanya ni Shetani kwahiyo wanatuchanganya ila uhalisia ni kuwa sio Shetani

Shetani hana muda wa kupoteza kufwata watu kwasababu hatuna cha kumshawishi sana sana ataenda kuzungumza na Malaika
 
Nakuelewa lakini sasa huwa hafwati watu kwasababu anatuona ni wadogo kwake sisi tunaishia kupigana na Wachawi, Mizimu na Majini
Wewe unaongea bila ushahidi wowote. Ushahidi huu hapa unaoonesha kuwa shetani anawafuata watu lakini tumepewa mamlaka ya kumpinga.
1 Pet 5:8
Mwe na kiasi na kukesha; kwa kuwa mshitaki wenu Ibilisi, kama simba angurumaye, huzunguka-zunguka, akitafuta mtu ammeze. Nanyi mpingeni huyo, mkiwa thabiti katika imani...
 
Kama shetani ni rafiki yako, kamwambie aje hapa aone nilivyomzodoa kwa kishindo, asilete ujuaji.
Hujanelewa, wewe unadhani naongea kwa kupigia debe, hapana maana yangu ni kuwa tunachanganywa sana na Majini
Watu wanafahamu majini, Mizimu, Wachawi ni Shetani mwenyewe
Tizama namna gani kila kona ina vilinge na makanisa ya kupambana na Wachawi
Hawa wachawi sio Shetani mwenyewe, hawa ni watu kama sisi lakini wanavaa ubaya na mchana wanakuwa watu kama kawaida na tunaishi nao mitaani
 
"We shetani, nakuambia bila kupepesa macho, na kila mtu asikie. Wewe ulikuwa malaika mbinguni; uliumbwa ukiwa mzuri na mwenye utukufu. Ukaanza kujiona bora zaidi ya Muumba wako. Ukadhani unaweza kukaa kwenye kiti cha Mungu. Ona kilichokupata. Ulitupwa chini kama takataka! Kiburi chako kilikuangusha, upumbavu wako ulikufanya kuwa wa hovyo.

Wewe ni wa ajabu sana. Una umri mkubwa, lakini huna hekima. Yote unayofanya ni marudio tu ya hila za zamani. Huna jipya!

Yesu alipokuja duniani, ulijiona umeshinda ulipompeleka msalabani, kumbe ulikuwa unajimaliza mwenyewe. Kwa kifo chake na kufufuka kwake, Yesu alikupiga "knock out" na kuzivunja kazi zako zote. Kuanzia siku ile, ikajulikana wazi kuwa wewe si chochote, si lolote.

Unajivuna eti wewe ni simba angurumaye. Lakini ukweli ni kwamba wewe ni simba mwenye meno ya karatasi! Unajua kuunguruma sana, lakini huna meno ya kung’ata. Umejaa kelele tupu. Unawatisha tu wasiomjua Mungu: walevi, wazinzi, waongo na wenye dhambi kama wewe. Lakini sisi tuliookoka tunakutazama na kukucheka.

Kila siku unazunguka huku na kule ukitafuta mtu wa kummeza. Kumbuka siku ile, uliwatuma majambazi wanimalize barabarani. Walikuja kwa njia moja, nikawapiga "fire" kwa Jina la Yesu, wakatawanyika kwa njia saba.

Ukatuma tena wachawi usiku, eti waniangamize. Kwa Jina la Yesu niliwapiga kipigo cha mbwa koko! Wakachoropoka mbio kama paka aliyefukuzwa jikoni kwa kutaka kuiba nyama.

Aibu yako shetani! Hata mtoto mdogo akitaja jina la Yesu, unatetemeka!

Na sasa nakukumbusha hatima yako, kila mtu asikie. Your days are numbered. Mwisho wako tayari umeandikwa: ni kutupwa katika ziwa la moto. Utakaa humo daima na kupata mateso yasiyoisha.

I dare to talk openly: sikuogopi shetani. Yesu alinipa mamlaka ya kuzikanyaga nguvu zako za giza. Kwa Jina la Yesu, nakupinga sasa, nakukemea, natangaza mbele ya kila mmoja kuwa umeshindwa. Wewe ni wa hovyo, nimekuaibisha leo. Nimekuzodoa!

Kwa jina la Yesu Kristo, toka hapa, ondoka!"
Hakuna malaika aliekua shetani
 
Yani tunakuelewa
Hatuzungumzi kwa kusifia bali kutaka kuonesha kuwa tutizame tumepishanaje na vitu kuanzia umri ndipo tunyooshe kidole

Swala ni kwamba Shetani hafwati watu kwasababu hatuna cha kumshawishi wanaotufwata ni Mizimu, Vibwengo, Wachawi na Mizimu
Na hawa wana tabia ya kujifanya ni Shetani kwahiyo wanatuchanganya ila uhalisia ni kuwa sionShetani

Shetani hana muda wa kupoteza kufwata watu kwasababu hatuna cha kumshawishi sana sana ataenda kuzungumza na Malaika
Kama hayo umeambiwa na shetani, basi amekudanganya kisawasawa. Shetani ni muongo (Yohana 8:44)
 
Wewe unaongea bila ushahidi wowote. Ushahidi huu hapa unaoonesha kuwa shetani anawafuata watu lakini tumepewa mamlaka ya kumpinga.
1 Pet 5:8
Mwe na kiasi na kukesha; kwa kuwa mshitaki wenu Ibilisi, kama simba angurumaye, huzunguka-zunguka, akitafuta mtu ammeze. Nanyi mpingeni huyo, mkiwa thabiti katika imani...
Hapa iko hivi, wanaokuja kila siku hata ukiuliza Wachungaji watakwambia wanawaona Wachawi, Mizimu na Majini hawajawahi kusema walimuona Shetani
Majini wamejaa mitaani na ndio wanaotutesa, uliza hata Mashehe watakwambia
Tafuta Mashehe wakwambie ukweli wa haya mambo
Kama sio Majini basi ni Wachawi au Mizimu
Shetani hana muda wa kufwata watu kwasababu anaamini sisi ni wadogo sana hatuna tunachomshawishi

Maandiko yanasema hivyo lakini yeye hafwati watu yalikuwa kama tahadhari
Ni sawa na wewe upewe mwavuli wa kujikinga na mvua lakini baada ya kupokea usione mvua ukaona rasha rasha ambazo ndio Wachawi, Mizimu, Vibwengo na Majini Setfree
 
Hawa wachawi sio Shetani mwenyewe, hawa ni watu kama sisi lakini wanavaa ubaya na mchana wanakuwa watu kama kawaida na tunaishi nao mitaani
We hata wachawi huwaelewi. Hakuna mtu wa kawaida anayeweza kuwa mchawi, akaloga, au akaingia ndani ya nyumba ya mtu wakati milango imefungwa, bila kutumiwa na mapepo au na shetani mwenyewe.

Halafu unapoongea, ongea kwa kuweka ushahidi. Unanukuu kutoka wapi hayo unayosema? Kama shetani alikuambia hayo, nimeishakuambia AMEKUDANGANYA, shtuka, lengo lake ni kukupeleka jehanam
 
Hapa iko hivi, wanaokuja kila siku hata ukiuliza Wachungaji watakwambia wanawaona Wachawi, Mizimu na Majini hawajawahi kusema walimuona Shetani
Majini wamejaa mitaani na ndio wanaotutesa, uliza hata Mashehe watakwambia
Tafuta Mashehe wakwambie ukweli wa haya mambo
Kama sio Majini basi ni Wachawi au Mizimu
Shetani hana muda wa kufwata watu kwasababu anaamini sisi ni wadogo sana hatuna tunachomshawishi

Maandiko yanasema hivyo lakini yeye hafwati watu yalikuwa kama tahadhari
Ni sawa na wewe upewe mwavuli wa kujikonga na mvua lakini baada ya kupokea usione mvua Setfree
Unauliza mashehe wa nini wakati kila kitu kiko wazi katika Biblia? Soma hayo maandiko niliyokupa uyatafakari. Na ukiendelea kumtetea shetani ndio utanifanya niongeze gia ya kumzodoa
 
Kama hayo umeambiwa na shetani, basi amekudanganya kisawasawa. Shetani ni muongo (Yohana 8:44)
Wala sijatumwa, kilichopo ni kuwa watu wanadhani Wachawi, Mizimu, Vibwengo, Majini ni yeye
Ndio maana mtu atakwambia alimuona Shetani kumbe alikuwa Jini, au Mzimu au Mchawi
Mashehe wan ujuzi mkubwa na elimu hii wanafahamu Majini ndio wanaosumbua na watu tunaamini ni Shetani mwenyewe Setfree
 
Wewe kumbe huijui historia ya shetani. Shetani alikuwa malaika mkuu mbinguni, wakati huo alikuwa akiitwa Lucifer. Huyo ndiye aliyeongoza uasi mbinguni kwa kushirikiana na theluthi moja ya malaika waliokuwa chini yake. Alivyotupwa chini hao malaika wadogo wakatupwa pamoja naye. Hao ndio wanaojulikana kama mapepo, na wengine wanawaita majini au vibwengo. Wote wanafanya uovu kwa pamoja na hukumu yao wote imeishatolewa.

Acha kumsifia shetani. Ukiendelea kumsifia na kushirikiana naye utatupwa motoni pamoja naye.
Nini tofauti ya Lucifer na wale malaika waliowatamani wanadamu na kuzaa nao(Watchers)?

Kitu kilichoweza kupambana na Mungu na Malaika zake bila kushindwa ndio mkiweze kwa maneno tu?

Kitu ambacho ndio Lighter bringer, Morning star ndio kishindwe kwa kukisema au kukikemea wewe Mwanadamu?

Kitu ambacho kinatawala kuzimu na Dunia ndio kikuogope wewe?

Tuache maigizo 😂😂😂😂😂😂😂
 
We hata wachawi huwaelewi. Hakuna mtu wa kawaida anayeweza kuwa mchawi, akaloga, au akaingia ndani ya nyumba ya mtu wakati milango imefungwa, bila kutumiwa na mapepo au na shetani mwenyewe.

Halafu unapoongea, ongea kwa kuweka ushahidi. Unanukuu kutoka wapi hayo unayosema? Kama shetani alikuambia hayo, nimeishakuambia AMEKUDANGANYA, shtuka, lengo lake ni kukupeleka jehanam
Hapana mimi nina elimu ya Majini niliyopewa na Mashehe, hii ni elimu ya kawaida na imelenga Majini
Sasa hawa sio Shetani mwenyewe
Huwa wana tabia ya kutumia jina lake
Pia wanawapa watu nguvu za kuloga lakini sio Shetani mwenyewe
N wanatibika kwa visomo na maombi unayozungumzia wewe

Shetani yeye hafwati watu anaamini hatuna ushawishi
Kam hafuati watu tunapigana nae kivipi kwasababu ni sawa na kupigana na hewa

Ndugu yangu majini ndio kero na ukiweza kuwatofautisha utafahamu nayozungumza

Tafuta Shehe akusaidie kukutofautishia Setfree
 
Nini tofauti ya Lucifer na wale malaika waliowatamani wanadamu na kuzaa nao(Watchers)?

Kitu kilichoweza kupambana na Mungu na Malaika zake bila kushindwa ndio mkiweze kwa maneno tu?

Kitu ambacho ndio Lighter bringer, Morning star ndio kishindwe kwa kukisema au kukikemea wewe Mwanadamu?

Kitu ambacho kinatawala kuzimu na Dunia ndio kikuogope wewe?

Tuache maigizo 😂😂😂😂😂😂😂
Unajua kinachomtesa ni kushindwa kutofautisha kati ya Wachawi, Mizimu, Vibwengo na Majini
Watu wengi wanaamini Majini ndio Shetani mwenyewe
Lakini hawa wanatafuta ugali wao na vyeo vyao na wanapokutana na watu wanakiulizwa wao ni nani wanadanganya Shetani ili waogopwe
Lakini ukweli wanakuwa majini na wana Majina yao

Mizimu nayo ina tabia ya kudanganya watu kuwa ndio Shetani

Lakini kuna Wachawi pia ambao ni watu wa kawaida tunaoishi nao mitaani kila siku

Kwahiyo nawez kukabwa na jirani yangu mchawi nikadhani ni Shetani na nikamweza kwa maombi

Lakini Shetani yeye kwanza kabisa kwa Cheo chake hakimshawishi kutufuatilia anaamini sisi si kitu

Labda mitume ndio walifanikiwa kusogelewa nae
Kikubwa ni madaraja, hata mimi leo nikwambie raisi wa Tanzania alinifwata kwanza haingii akilini

Lakini raisi wa Tanzania kumtembelea wa Kenya ni jambo la kawaida kabisa Setfree
 
Unauliza mashehe wa nini wakati kila kitu kiko wazi katika Biblia? Soma hayo maandiko niliyokupa uyatafakari. Na ukiendelea kumtetea shetani ndio utanifanya niongeze gia ya kumzodoa
Wewe unaaminije? Inawezekana sijakusikiliza kwa makini Setfree
 
Hapana mimi nina elimu ya Majini niliyopewa na Mashehe, hii ni elimu ya kawaida na imelenga Majini
Sasa hawa sio Shetani mwenyewe
Huwa wana tabia ya kutumia jina lake
Pia wanawapa watu nguvu za kuloga lakini sio Shetani mwenyewe
N wanatibika kwa visomo na maombi unayozungumzia wewe

Shetani yeye hafwati watu anaamini hatuna ushawishi
Kam hafuati watu tunapigana nae kivipi kwasababu ni sawa na kupigana na hewa

Ndugu yangu majini ndio kero na ukiweza kuwatofautisha utafahamu nayozungumza

Tafuta Shehe akusaidie kukutofautishia Setfree
Umedanganyika. Mapepo na majini yanafukuzwa kwa Jina la Yesu tu. Jina la Yesu liko juu ya jina la shetani na mapepo na wachawi. Ukiokoka na kulitumia Jina la Yesu, shetani hafurukuti. Shetani ni muongo. Nimeishakutajia andiko lile kwamba Ibilisi ndiye anayezungukazunguka akitafuta mtu wa kummeza. Ila kwakuwa hapendi ajulikane ndo anakuambia uongo huo kwamba yeye hafuati mtu. Mada hii ikusaidie kumfahamu shetani na uongo wake na jinsi ambavyo HANA nguvu mbele ya watoto wa Mungu.
 
Wewe unaaminije? Inawezekana sijakusikiliza kwa makini Setfree
Naamini kama "CV" hii ya shetani ilivyoainisha
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom