Setfree
JF-Expert Member
- Dec 25, 2024
- 5,699
- 7,418
"We shetani, nakuambia bila kupepesa macho, na kila mtu asikie. Wewe ulikuwa malaika mbinguni; uliumbwa ukiwa mzuri na mwenye utukufu. Ukaanza kujiona bora zaidi ya Muumba wako. Ukadhani unaweza kukaa kwenye kiti cha Mungu. Ona kilichokupata. Ulitupwa chini kama takataka! Kiburi chako kilikuangusha, upumbavu wako ulikufanya kuwa wa hovyo.
Wewe ni wa ajabu sana. Una umri mkubwa, lakini huna hekima. Yote unayofanya ni marudio tu ya hila za zamani. Huna jipya!
Yesu alipokuja duniani, ulijiona umeshinda ulipompeleka msalabani, kumbe ulikuwa unajimaliza mwenyewe. Kwa kifo chake na kufufuka kwake, Yesu alikupiga "knock out" na kuzivunja kazi zako zote. Kuanzia siku ile, ikajulikana wazi kuwa wewe si chochote, si lolote.
Unajivuna eti wewe ni simba angurumaye. Lakini ukweli ni kwamba wewe ni simba mwenye meno ya karatasi! Unajua kuunguruma sana, lakini huna meno ya kung’ata. Umejaa kelele tupu. Unawatisha tu wasiomjua Mungu: walevi, wazinzi, waongo na wenye dhambi kama wewe. Lakini sisi tuliookoka tunakutazama na kukucheka.
Kila siku unazunguka huku na kule ukitafuta mtu wa kummeza. Kumbuka siku ile, uliwatuma majambazi wanimalize barabarani. Walikuja kwa njia moja, nikawapiga "fire" kwa Jina la Yesu, wakatawanyika kwa njia saba.
Ukatuma tena wachawi usiku, eti waniangamize. Kwa Jina la Yesu niliwapiga kipigo cha mbwa koko! Wakachoropoka mbio kama paka aliyefukuzwa jikoni kwa kutaka kuiba nyama.
Aibu yako shetani! Hata mtoto mdogo akitaja jina la Yesu, unatetemeka!
Na sasa nakukumbusha hatima yako, kila mtu asikie. Your days are numbered. Mwisho wako tayari umeandikwa: ni kutupwa katika ziwa la moto. Utakaa humo daima na kupata mateso yasiyoisha.
I dare to talk openly: sikuogopi shetani. Yesu alinipa mamlaka ya kuzikanyaga nguvu zako za giza. Nakukemea, kwa Jina la Yesu Kristo, toka hapa. Natangaza mbele ya kila mmoja kuwa umeshindwa. Wewe ni wa hovyo, nimekuaibisha leo. Nimekuzodoa!"
Wewe ni wa ajabu sana. Una umri mkubwa, lakini huna hekima. Yote unayofanya ni marudio tu ya hila za zamani. Huna jipya!
Yesu alipokuja duniani, ulijiona umeshinda ulipompeleka msalabani, kumbe ulikuwa unajimaliza mwenyewe. Kwa kifo chake na kufufuka kwake, Yesu alikupiga "knock out" na kuzivunja kazi zako zote. Kuanzia siku ile, ikajulikana wazi kuwa wewe si chochote, si lolote.
Unajivuna eti wewe ni simba angurumaye. Lakini ukweli ni kwamba wewe ni simba mwenye meno ya karatasi! Unajua kuunguruma sana, lakini huna meno ya kung’ata. Umejaa kelele tupu. Unawatisha tu wasiomjua Mungu: walevi, wazinzi, waongo na wenye dhambi kama wewe. Lakini sisi tuliookoka tunakutazama na kukucheka.
Kila siku unazunguka huku na kule ukitafuta mtu wa kummeza. Kumbuka siku ile, uliwatuma majambazi wanimalize barabarani. Walikuja kwa njia moja, nikawapiga "fire" kwa Jina la Yesu, wakatawanyika kwa njia saba.
Ukatuma tena wachawi usiku, eti waniangamize. Kwa Jina la Yesu niliwapiga kipigo cha mbwa koko! Wakachoropoka mbio kama paka aliyefukuzwa jikoni kwa kutaka kuiba nyama.
Aibu yako shetani! Hata mtoto mdogo akitaja jina la Yesu, unatetemeka!
Na sasa nakukumbusha hatima yako, kila mtu asikie. Your days are numbered. Mwisho wako tayari umeandikwa: ni kutupwa katika ziwa la moto. Utakaa humo daima na kupata mateso yasiyoisha.
I dare to talk openly: sikuogopi shetani. Yesu alinipa mamlaka ya kuzikanyaga nguvu zako za giza. Nakukemea, kwa Jina la Yesu Kristo, toka hapa. Natangaza mbele ya kila mmoja kuwa umeshindwa. Wewe ni wa hovyo, nimekuaibisha leo. Nimekuzodoa!"