Njoo tukumbushane ulivyoibiwa simu au kompyuta

Njoo tukumbushane ulivyoibiwa simu au kompyuta

Niluibiwa tecno yangu na mshkaji tena jirani yangu, alichonga mchongo na mtu aje kuniliza geto kwangu. Kisa kwa mwenye nyumba kuna denti wa form 2 anamzimia, ambaye kamtema. Sasa denti akawa anapapatika kwangu, mimi sina muda naye naogopa jela.

Jamaa wakamjaza upepo kuwa mtoto nimekula, ndiyo akaamua kunikomoa kisa kapigwa chaga
 
Wale wez wa Mabibo hostel sijui walikuwa wanaibaje kwakeli!sie BlocK C kwenye floor ya 3 room 3 watu waliiibiwa laptop na hazikupatikana mpaka leo
Yaan sisi tulikua Block A floor ya 4 , tuliibiwa simu zote, waliacha vinokia tochi tu ,na mlango ulikua umefungwa sijui walipitia dirishani aisee mpk Leo huwa sielewi waliibaje
 
Yaan sisi tulikua Block A floor ya 4 , tuliibiwa simu zote, waliacha vinokia tochi tu ,na mlango ulikua umefungwa sijui walipitia dirishani aisee mpk Leo huwa sielewi waliibaje
Hamjawahi kuchoma hata wezi 6 ili wengine wajifunze kupaogopa?
 
Hawa watu nahisi kama wanatumia dawa hv. Nilikuwa maeneo ya ilala boma ghafla nikiwa napita kwenye uchochoro wa mabanda ya Nguo akatokea jamaa kwa mbele ameshika jinsi anakuwa kama anaikagua hv. Ile kumsogelea ili nimuambie anipishe nipite akajifanya hajaniskia akanikanyaga mguun
Zile purukushani za kumwambia unanikanyaga na kumtaka anipishe kumbe kuna mwenzake kashazama mfukoni akapita na katecno kangu.
 
2008 niliibiwa Camera mtaa wa Swahili na Mchikichi, gari inkuja, kuna mtu akaweka mguu nikamkanyaga, akanitikisa, nikaomba msamaha akanisamehe mfukoni sina kitu. Mungu mkubwa nilirudi lile eneo nikamkuta kasimama na Kamera nikaichukua.


Simu nimeibiwa Mbezi Mwisho nashangaa wale wapuuzi wanaouza dawa za nyoka
 
Hamjawahi kuchoma hata wezi 6 ili wengine wajifunze kupaogopa?
hahaa, walishawahi kumkamata mmoja wakamdunda sana , mpk Auxiliary police officers wamefika yuko hoi ,naskia alifia hospital, ila wezi wanaboa jamani , kuna siku nilikua kariakoo kuna mwizi anafukuzwa huko katoka speed wanaomkimbiza wako nyuma wanapiga kelele mwizii, duuh kuna watu walikua madukani kwao ile kuskia tu wakamkamata na mitama juu kama kawaibia wao wakampiga mpk wanafika waliokua wanamkimbiza yuko hoi, aisee nikamuonea huruma tena watu wamechoka kuibiwa wallahi.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom