Njoo tukumbushane ulivyoibiwa simu au kompyuta

Njoo tukumbushane ulivyoibiwa simu au kompyuta

Jumong S

JF-Expert Member
Joined
Jul 3, 2013
Posts
7,427
Reaction score
10,749
Nilitembelea maonesho ya Nane nane last year Arusha. Watu walikuwa wengi kiasi. Nilipofika karibu na banda la Veta walikuja mbele yangu wadada watatu. Walivalia kawaida kidogo. Suruali za wawili hazikuvutia sana kuwaangalia na mmoja alivaa suti kama za mke wa mchungaji.

Yule mwenye suti aliniomba nimuelekeze lilipo banda la Mosanto. Sikua napajua ila nikamwambia akamuulize mlinzi aliyekuwa jirani. Wakati namuelekeza mlinzi alipo na akaridhika nilianza kuondoka. Nilichogundua wale wenzake wawili walikuwa washaondoka. Nikarudia kumwangalia niliyekuwa namuelekeza naye alikuwa keshapotea. Sikujali. Niliendelea na mizunguko. Nikahisi nywele zinanisisimka. Nilipogusa mfuko wangu wa suruali niligundua Samsung yangu haipo na kisimu changu kidogo cha Nokia pia. Nilianza kurudi kuwatafuta sikuwaona. Nikawa nimelizwa tena na wadada!!

Nitarudi kueleza nilivyolizwa PC yangu ya 950E.

Je, wewe uliibiwaje? Tutumie njia gani kujilinda na kuibiwa vifaa hivi vidogo ila ghali sana?

Karibu!
 
Nilibiwa Laptop Bulls Park!Tarehe 12/04/2018
Jamaa wanafanya timing Unaposhukia anakuwa upande wa pili ,kwakuwa nilikuwa alone haikuwa kazi kwake wkt nafungua mlango nae akawa anafungua wa Pili then napofunga wangu kumbe yeye anauacha wazi ukienda kaa ndio unapopigwa
 
NILIVYOPOTEZA SIMU NA LAPTOP.
Ilikua tarehe 5 mwezi wa 6 2017 narudi geto saa 6 hivii mitaa ya Fuoni Zanzibar nafungua mlango nakuta vitu viko hovyo hovyo. Vitabu,Nguo,Cds zilikua kwenye kabati. Vyote vimemwagwa hadi shuka imetanduliwa kitandani. Nikawa nafikiri nini kimetokea. Whaaaaaat nikakumbuka Laptop Toshiba yangu na Simu yangu ya Samsung Galaxy S4 GT-19500. Nilikua nikiondoka navifungia ndani ya begi la nguo. Siku hiyo na simu niliacha nikatembea na sim ndogo ya HTC.

Kufungya begi hakuna kituu. Laptop ndio nilikua nina mwaka 1 nimeinunua bado mupyaaa kabisa. Simu nilikua nina mwaka na miezi kadhaa ninayo. Ukweli nililia sana sanaa hata sikulala kabisaa.

Waliiba Pasi ya umeme na Hearter pia.
Kama waliuza kwa bei za kueleweka hawakukosa Millioni hivi.

Toka siku hiyo nilipachukia Zenji kabisaa
 
NILIVYOPOTEZA SIMU NA LAPTOP.
Ilikua tarehe 5 mwezi wa 6 2017 narudi geto saa 6 hivii mitaa ya Fuoni Zanzibar nafungua mlango nakuta vitu viko hovyo hovyo. Vitabu,Nguo,Cds zilikua kwenye kabati. Vyote vimemwagwa hadi shuka imetanduliwa kitandani. Nikawa nafikiri nini kimetokea. Whaaaaaat nikakumbuka Laptop Toshiba yangu na Simu yangu ya Samsung Galaxy S4 GT-19500. Nilikua nikiondoka navifungia ndani ya begi la nguo. Siku hiyo na simu niliacha nikatembea na sim ndogo ya HTC.

Kufungya begi hakuna kituu. Laptop ndio nilikua nina mwaka 1 nimeinunua bado mupyaaa kabisa. Simu nilikua nina mwaka na miezi kadhaa ninayo. Ukweli nililia sana sanaa hata sikulala kabisaa.

Waliiba Pasi ya umeme na Hearter pia.
Kama waliuza kwa bei za kueleweka hawakukosa Millioni hivi.

Toka siku hiyo nilipachukia Zenji kabisaa
Wezi wanaboa sana. Hawa watakuwa walikusoma mapema.
 
Nilibiwa Laptop Bulls Park!Tarehe 12/04/2018
Jamaa wanafanya timing Unaposhukia anakuwa upande wa pili ,kwakuwa nilikuwa alone haikuwa kazi kwake wkt nafungua mlango nae akawa anafungua wa Pili then napofunga wangu kumbe yeye anauacha wazi ukienda kaa ndio unapopigwa
Hii mpya. Hapo ni kuhakiki kabla hujaliacha gari kama milango ipo locked na hakuna mtu uliyemfungia ndani.
 
Nilipumbazwaa kwa watu wanaojidai wanauza madini Kuja kushtukaa Sina kituu waliniibia simuu kipindi hicho simu Mali sanaaa.... toka siku hiyoo sitaki kuona MTU ananifata anauza kitu cha aina yoyote barabarani Kama madini...sijui simuu
 
Kuna mtu aliniomba laptop yangu acheki muvi nikampa kesho ananipigia ananiambia njoo home kuna ishu imetokea.

Nikafika ananiambia asubuhi leo nimeacha laptop kitandani nilikua nafagia nje nimerudi ndani laptop haipo. Nikabaki nimeduwaa tu pale akili inaniwazisha vilivyomo mle ndani...
Proposal
Research
Articles
Software za vyeti
Back up ya smartphone nilizowahi kutumia.
Back up ya contacts.
Picha.

Halafu kumdai siwezi.
 
ukipata ajari tuu ukishuka shangaa uliyemgonga watu wengine wanakimbia vitu vilivyo kwenye gari
 
NILIVYOPOTEZA SIMU NA LAPTOP.
Ilikua tarehe 5 mwezi wa 6 2017 narudi geto saa 6 hivii mitaa ya Fuoni Zanzibar nafungua mlango nakuta vitu viko hovyo hovyo. Vitabu,Nguo,Cds zilikua kwenye kabati. Vyote vimemwagwa hadi shuka imetanduliwa kitandani. Nikawa nafikiri nini kimetokea. Whaaaaaat nikakumbuka Laptop Toshiba yangu na Simu yangu ya Samsung Galaxy S4 GT-19500. Nilikua nikiondoka navifungia ndani ya begi la nguo. Siku hiyo na simu niliacha nikatembea na sim ndogo ya HTC.

Kufungya begi hakuna kituu. Laptop ndio nilikua nina mwaka 1 nimeinunua bado mupyaaa kabisa. Simu nilikua nina mwaka na miezi kadhaa ninayo. Ukweli nililia sana sanaa hata sikulala kabisaa.

Waliiba Pasi ya umeme na Hearter pia.
Kama waliuza kwa bei za kueleweka hawakukosa Millioni hivi.

Toka siku hiyo nilipachukia Zenji kabisaa
Habari za tunguu mkuu
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom