Njoo tujuzane ujuzi wa kutafuta sattelite za chaneli bila kubahatisha

Kuna mambo mengi ya kuzingatia wakati wa kuelekeza dish kwenye satellite, ukiyafuata dakika 10 nyingi unakua umemaliza, mafundi wetu wengi wanafanya kubahatisha kuzungusha dish hadi kuipata satellite. Ngoja nieleze kwa uzoefu wangu nilionao, unaweza tafuta satellite yoyote ile na kwa muda mfupu kama ukifuata taratibu hizi
  1. Pata footprint(Eneo lote ambalo mawimbi ya satellite husika yanafika) ya satellite. Kuna Website nyingi na tools zinazowezesha hili kwa mfano kwa kutumia Satbeams - World Of Satellites at your fingertips chagua satellite unayoitaka na utaona footprint yake na taarifa zaidi kama inavyoonekata kenye hii picha
    satellite-png.387957
Hapo ni kwa dar es salaam satellite ya Eutelsat 36B ipo nyuzi 36 mashariki (DSTV wanaporusha matangazo). Pia utaona ukubwa wa dishi linalotakiwa ili kupata signal, mfano hapo ni kuanzia 80cm unaipata vizuri tu. mkono wa kushoto kuna taarifa zaidi muhimu. hizi ni elevation angle 80.8 (hii ni kiasi gani dishi linatakiwa linyanyuke), True azimuth 334.2 (ni uelekeo wa dish) na lnb skew 25.6 (Uelekeo wa lnb). Hivyo vitu vi 4 nilivyobold ndiyo muhimu uvijue ukitaka kutafuta satellite yoyote ile.

2. Hatua inayofuata ni kufunga dish pole (ule mlingoti wa kuwekea dishi lenyewe). Hakikisha ile mlingoti umesima wima kwa nyuzi 90 (Ni muhimu sana hili) unaweza pima kwa kutumia kipima pembe au pima maji. Angalia hii picha
hqdefault-jpg.387977


3. Baada ya hapo ni kuweka dish lako sasa kwa kufuata vipimo ulivyopata hapo juu (Elevation, azimuth na lnb skew). Kuweka elevation angle 80.8 tumia alama zilizowekwa kwenye dishi mfano angalia picha hii hapo kuna kuanzia 0 hadi 90. elevation angle hutofautiana kutokana na satellite unayouitafuta, kwa mfano kwa hiyo ya dstv ni 80.8 na Eutelsat 7 (azam wanaporusha matangazo) ni 51.6 hivyo utakweka hapo kwenya hizo alama za dishi. kama dishi lako halina alama hizo unaweza kutumia kipima pembe kama hicho kenye picha hapo juu.
images-png.387978

adjustment-jpg.387981


4. Hatua inayofuata ni kuweka azmuth angle (uelekeo wa dishi kwa kuzungusha kulia au kushoto ukiwa nyuma ya dishi). Kifaa ninachotumika ni compass (dira), hichi kipo hata kwenye smartphone na uelekeze kwenye nyuzi 334.2

5. Katika hatua hii ni kuweka uelekeo wa lnb (Lnb skew angle) ukiangalia pale unapoweka lnb kuna alma pia za kuweka, angalia mfano kwenye picha hii
lnbf-skewing-angle-check-jpg.387986


Ukifuata hatua hizi 5 unapata satellite yoyote unayouitaka ndani ya muda mfupi sana dakika 10 nyingi siyo kubahatisha tu vitu vinaenda kwa vipimo kila kitu kipo kutokana na satellite unayoitaka. satellite zingine signal yake ni weak mfano Nilesat ukisema utafute kwa kuzungusha tu dish kwa kubahatisha unaweza kumaliza siku nzima hujaipata ila ukifuata vipimo vyake unaipata haraka sana.

Unaweza uelewa zaidi kwa kuangalia video hii youtube

View attachment 387957 View attachment 387977 View attachment 387978 View attachment 387981 View attachment 387986

safi xana mkuu
 
  • Thanks
Reactions: M12
Mi nataka niangalie mpira wa Epl bila kupitia dstv maana wanachosha na malipo hewa
 
Wakuu mi nipo nje ya maada kidgo naombeni msaada, vipi niki badilisha kadi za ving'amuzi nikatoa kadi kwenye king'amuzi A nikaweka kwenye king'amuzi B, ila cha aina moja (lets say vyote ni azam) vipi itafanya kazi?
 
Mi nataka niangalie mpira wa Epl bila kupitia dstv maana wanachosha na malipo hewa
Inawezekana kabisa, ila sio 'BURE'. Nunua receiver yenye uwezo wa kufungua channels zilizofungwa kwa powervu, kama vile Freesat, Gsky, Hometech ama Qsat Q26 na matoleo ya mbele yake. Baada ya hapo nunua dish la ft 6 ama ft 8, unakua umemaliza kazi. Tafuta fundi, akufungie satellite ya NSS 12 iliyo nyuzi 57E (ppana Sports 24, inayorusha EPL) ama Intelsat 20 iliyo nyuzi 68E (pana channels za Sony zinarusha pia EPL). Hapo utapata mpira wa EPL
 
Wakuu mi nipo nje ya maada kidgo naombeni msaada, vipi niki badilisha kadi za ving'amuzi nikatoa kadi kwenye king'amuzi A nikaweka kwenye king'amuzi B, ila cha aina moja (lets say vyote ni azam) vipi itafanya kazi?
jibu ni HAPANA. Kila king'amuzi kinasajiliwa na kadi yake wakati wa usajili. Haiwezekani kutumia kadi ya king'amuzi A kwa king'amuzi B.
 
Hapo ukiwa mtafiti utagundua kuwa kumebe kadiri unapozungusha dishi kulia (ukiwa nyuma ya dishi) ndivyo nyuzi zinavyozidi kupanda na kadri unaporudisha dish kushoto (ukiwa nyuma ya dishi) ndivyo nyuzi zinavyozidi kupungua ,
Ila cha muhimu unapotafuta signal ya satelite yoyote usitegemee uone mafanikio kwa haraka haraka inakubidi usome level ya msitari mwekundu ndo upate uhakika kuwa unachokitafuta utakipata muda sio mrefu ,
Kwa mfano unatafuta satelite ya Intelsat 10 unatakiwa kuvizia mida ya jioni jua linapotaka kuzama lengesha lnb ya kwenye dish iangaliane sambamba na jua halafu anza kuzungusha kurudi kushoto itafika sehemu mritari wa level au strength utakataa kupanda zaidi ya 80% au 81% uzilazimishe anza kupandisha na kushusha im sure lazima msitari wa quality utaonekana tu ,

ANGALIZO.
=>HAKIKISHA LNB UMEIFUNGA IMELENGA KATIKATI YA DISH ,
=>MAHALA ULIPOPWEKA DISH KWA MBELE KUSIWE NA VIZUIZI VINAVYOPUNGUZA AU KUKATA SIGNAL (MITI, UKUTA )
=>HAKIKISHA SEHEMU YA ARDHI UNAYOTAKA KUWEKA DISH IPO SAWIA ,

Bahati njema!
Kaka unawezaje kuweka package ya continental kwenye azm naomba utupe mwongoz?
 
Kunasehemu nilipita nikakuta recevr ya azam Ina onesha chnl za continental bure
Hili linawezekana kwa receiver yeyote ile ila pindi tu continental wanapokuwa FTA

Ni kwa muda mrefu walikuwa hawajafunga channel zao

Kuhusu receiver za azam:
- Ni matoleo yale ya mwanzo, ndio ulikuwa unaweza add sat./ frequency na kupata package za FTA kama ulivyotolea mfano wa continental.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom