Njoo tujuzane ujuzi wa kutafuta sattelite za chaneli bila kubahatisha

elimu bila nyenzo bado haijakamilika... ngoja nitafute kwanza vifaa nikianzia na hizo receiver, lnb nk.
Itapendeza sana ndugu. Vifaa vipo kibao tu madukani.
  1. Nunua dish la ft 6 au ft 8 kwa ajili ya C band, mengi yanauzwa kati ya 200,000 mpaka 300,000 kutegemea uimara wake. Lkn pia unaweza kupata kutoka kwa mafundi wenzako
  2. Nunua dish la ft 3 kwa ajili ya kujifunzia kufunga chanels za KU band
  3. Nunua satellite finder, aidha analog ama digital. Analog kwa Kariakoo zinauzwa kati ya 30,000 na 40,000 na digital zinaenda hadi 350,000 (MPEG 4)
  4. Nunua seti ya spana na bisibisi
  5. Nunua waya wa coaxial (75 Ohm).
 
Itapendeza sana ndugu. Vifaa vipo kibao tu madukani.
  1. Nunua dish la ft 6 au ft 8 kwa ajili ya C band, mengi yanauzwa kati ya 200,000 mpaka 300,000 kutegemea uimara wake. Lkn pia unaweza kupata kutoka kwa mafundi wenzako
  2. Nunua dish la ft 3 kwa ajili ya kujifunzia kufunga chanels za KU band
  3. Nunua satellite finder, aidha analog ama digital. Analog kwa Kariakoo zinauzwa kati ya 30,000 na 40,000 na digital zinaenda hadi 350,000 (MPEG 4)
  4. Nunua seti ya spana na bisibisi
  5. Nunua waya wa coaxial (75 Ohm).
asante mkuu ila labda nikuweke wazi mimi sio fundi sema ni vile nimekuwa interested na haya mavitu toka utotoni naomba usinichoke nitakuwa nakuuliza pale ninapokwama
 
Inawezekana kabisa, ila sio 'BURE'. Nunua receiver yenye uwezo wa kufungua channels zilizofungwa kwa powervu, kama vile Freesat, Gsky, Hometech ama Qsat Q26 na matoleo ya mbele yake. Baada ya hapo nunua dish la ft 6 ama ft 8, unakua umemaliza kazi. Tafuta fundi, akufungie satellite ya NSS 12 iliyo nyuzi 57E (ppana Sports 24, inayorusha EPL) ama Intelsat 20 iliyo nyuzi 68E (pana channels za Sony zinarusha pia EPL). Hapo utapata mpira wa EPL
Uelekeo wa dish n wap
 
Habari za majukumu Wakuu
MM mwenzenu sina ufundi sana na hii Kitu ila nna uelewa nusu tuu.
Kwa mda nilikua natumia Cable za hapa Maneo Ya Nyumbani kwetu, Ila Now Nmeamua Kuachana nazo. Sababu ya Gharama na sababu nyingine za kwality ya Picha.

Kutokana na Upatikanaji wa receivers kwa eneo nililopo nmefanikiwa kupata Tiger Link I555 (najua si nzuri sana), lakini ina Bypas powerVU Encryption . Nme update software... Mara Ya kwanza Niliweka Degrees 38e Nikawa napata Chanel za Pakistan (PTV) . ila now Nmehamisha Mpaka 57e Degrees Napata sports 24 na baadhi ya Chanel za BBC. Ila Bado Kwangu Ni Tatizo maana Maana Napendelea footbal na Basketball, Ila Sports 24 wanaonyesha basketball mara chache sana, na football wanaonyesha epl tuu.

nlikua naomba ushauri
1. nifanye kipi nipate chanel znazoonyesha basket na pia football nipate...
2. ujuzi wa kuweka double lnb.. maana kwa degrees 64e nlikua napata Amerixca forces betwork wanaonyesha basket ila nikawa na kosa basket.. nmeskia kwa usawa nlio weka now naweza weka lnb nyingine ikawa 64e ila nikijaribu sipati kitu
3. Je nahitaj dish la ukubwa gani nipate sony six ... maana ile inakosa epl tuu ila ina basket, laliga, na serie A

Thanks in Advance
 
nlikua naomba ushauri
1. nifanye kipi nipate chanel znazoonyesha basket na pia football nipate...
Uko katika njia sahihi, ingawa uko half way. Tafuta dishi la futi nane, la wavu ama bati, whatever. Katika mfumo huo huo uliofunga NSS 12 @57E, pandishia lnb nyingine ya C band juu ya hio NSS 12 ili upate channels za local pamoja na AFN sports pale 64.2E.

2. ujuzi wa kuweka double lnb.. maana kwa degrees 64e nlikua napata Amerixca forces betwork wanaonyesha basket ila nikawa na kosa basket.. nmeskia kwa usawa nlio weka now naweza weka lnb nyingine ikawa 64e ila nikijaribu sipati kitu
Kuna utundu flani unahitajika ili kupandanisha Lnb zaidi ya moja. Sidhani kama nikukielekeza hapa utanielewa kirahisi, ila inawezekana ukiangalia picha za muundo wake. Nitaweka picha hapa

3. Je nahitaj dish la ukubwa gani nipate sony six ... maana ile inakosa epl tuu ila ina basket, laliga, na serie A
Kama nilvyoandika hapo juu, dish la kuaminika lianzie futi nane na kuendelea
 
Habari za majukumu Wakuu
MM mwenzenu sina ufundi sana na hii Kitu ila nna uelewa nusu tuu.
Kwa mda nilikua natumia Cable za hapa Maneo Ya Nyumbani kwetu, Ila Now Nmeamua Kuachana nazo. Sababu ya Gharama na sababu nyingine za kwality ya Picha.

Kutokana na Upatikanaji wa receivers kwa eneo nililopo nmefanikiwa kupata Tiger Link I555 (najua si nzuri sana), lakini ina Bypas powerVU Encryption . Nme update software... Mara Ya kwanza Niliweka Degrees 38e Nikawa napata Chanel za Pakistan (PTV) . ila now Nmehamisha Mpaka 57e Degrees Napata sports 24 na baadhi ya Chanel za BBC. Ila Bado Kwangu Ni Tatizo maana Maana Napendelea footbal na Basketball, Ila Sports 24 wanaonyesha basketball mara chache sana, na football wanaonyesha epl tuu.

nlikua naomba ushauri
1. nifanye kipi nipate chanel znazoonyesha basket na pia football nipate...
2. ujuzi wa kuweka double lnb.. maana kwa degrees 64e nlikua napata Amerixca forces betwork wanaonyesha basket ila nikawa na kosa basket.. nmeskia kwa usawa nlio weka now naweza weka lnb nyingine ikawa 64e ila nikijaribu sipati kitu
3. Je nahitaj dish la ukubwa gani nipate sony six ... maana ile inakosa epl tuu ila ina basket, laliga, na serie A

Thanks in Advance
20170118_222631.jpg
20170118_222646.jpg
20170118_222625.jpg

Kwa muujibu wa picha hii, hapo base Lnb ni Intelsat 20 @ 68.5°E (Sony pics, Discovery na Animal Planet). Chini yake ni Intelsat 906 @ 64.2°E, (local channels na AFN) na chini kabisa ni NSS 12 @57°E (sports 24, Skynews na BBC).
 
Uko katika njia sahihi, ingawa uko half way. Tafuta dishi la futi nane, la wavu ama bati, whatever. Katika mfumo huo huo uliofunga NSS 12 @57E, pandishia lnb nyingine ya C band juu ya hio NSS 12 ili upate channels za local pamoja na AFN sports pale 64.2E.


Kuna utundu flani unahitajika ili kupandanisha Lnb zaidi ya moja. Sidhani kama nikukielekeza hapa utanielewa kirahisi, ila inawezekana ukiangalia picha za muundo wake. Nitaweka picha hapa


Kama nilvyoandika hapo juu, dish la kuaminika lianzie futi nane na kuendelea
Asante Mkuu... Nina Dish La Bati Futi 6... Mayb nitafute futi 8 ili nifanyie kaz hyo kitu
 
Asante Mkuu... Nina Dish La Bati Futi 6... Mayb nitafute futi 8 ili nifanyie kaz hyo kitu
Yap. Ila hata futi 6 linaweza, ingawa kwa kupandanisha LNB la futi nane ama zaidi lingefaa zaidi kwa kazi hii. Anza mdogo mdogo, utafika tu!
 
Kuna mambo mengi ya kuzingatia wakati wa kuelekeza dish kwenye satellite, ukiyafuata dakika 10 nyingi unakua umemaliza, mafundi wetu wengi wanafanya kubahatisha kuzungusha dish hadi kuipata satellite. Ngoja nieleze kwa uzoefu wangu nilionao, unaweza tafuta satellite yoyote ile na kwa muda mfupu kama ukifuata taratibu hizi
  1. Pata footprint(Eneo lote ambalo mawimbi ya satellite husika yanafika) ya satellite. Kuna Website nyingi na tools zinazowezesha hili kwa mfano kwa kutumia Satbeams - World Of Satellites at your fingertips chagua satellite unayoitaka na utaona footprint yake na taarifa zaidi kama inavyoonekata kenye hii picha
    satellite-png.387957
Hapo ni kwa dar es salaam satellite ya Eutelsat 36B ipo nyuzi 36 mashariki (DSTV wanaporusha matangazo). Pia utaona ukubwa wa dishi linalotakiwa ili kupata signal, mfano hapo ni kuanzia 80cm unaipata vizuri tu. mkono wa kushoto kuna taarifa zaidi muhimu. hizi ni elevation angle 80.8 (hii ni kiasi gani dishi linatakiwa linyanyuke), True azimuth 334.2 (ni uelekeo wa dish) na lnb skew 25.6 (Uelekeo wa lnb). Hivyo vitu vi 4 nilivyobold ndiyo muhimu uvijue ukitaka kutafuta satellite yoyote ile.

2. Hatua inayofuata ni kufunga dish pole (ule mlingoti wa kuwekea dishi lenyewe). Hakikisha ile mlingoti umesima wima kwa nyuzi 90 (Ni muhimu sana hili) unaweza pima kwa kutumia kipima pembe au pima maji. Angalia hii picha
hqdefault-jpg.387977


3. Baada ya hapo ni kuweka dish lako sasa kwa kufuata vipimo ulivyopata hapo juu (Elevation, azimuth na lnb skew). Kuweka elevation angle 80.8 tumia alama zilizowekwa kwenye dishi mfano angalia picha hii hapo kuna kuanzia 0 hadi 90. elevation angle hutofautiana kutokana na satellite unayouitafuta, kwa mfano kwa hiyo ya dstv ni 80.8 na Eutelsat 7 (azam wanaporusha matangazo) ni 51.6 hivyo utakweka hapo kwenya hizo alama za dishi. kama dishi lako halina alama hizo unaweza kutumia kipima pembe kama hicho kenye picha hapo juu.
images-png.387978

adjustment-jpg.387981


4. Hatua inayofuata ni kuweka azmuth angle (uelekeo wa dishi kwa kuzungusha kulia au kushoto ukiwa nyuma ya dishi). Kifaa ninachotumika ni compass (dira), hichi kipo hata kwenye smartphone na uelekeze kwenye nyuzi 334.2

5. Katika hatua hii ni kuweka uelekeo wa lnb (Lnb skew angle) ukiangalia pale unapoweka lnb kuna alma pia za kuweka, angalia mfano kwenye picha hii
lnbf-skewing-angle-check-jpg.387986


Ukifuata hatua hizi 5 unapata satellite yoyote unayouitaka ndani ya muda mfupi sana dakika 10 nyingi siyo kubahatisha tu vitu vinaenda kwa vipimo kila kitu kipo kutokana na satellite unayoitaka. satellite zingine signal yake ni weak mfano Nilesat ukisema utafute kwa kuzungusha tu dish kwa kubahatisha unaweza kumaliza siku nzima hujaipata ila ukifuata vipimo vyake unaipata haraka sana.

Unaweza uelewa zaidi kwa kuangalia video hii youtube

View attachment 387957 View attachment 387977 View attachment 387978 View attachment 387981 View attachment 387986

Umeniongezea madini....asante na uba
Kuna mambo mengi ya kuzingatia wakati wa kuelekeza dish kwenye satellite, ukiyafuata dakika 10 nyingi unakua umemaliza, mafundi wetu wengi wanafanya kubahatisha kuzungusha dish hadi kuipata satellite. Ngoja nieleze kwa uzoefu wangu nilionao, unaweza tafuta satellite yoyote ile na kwa muda mfupu kama ukifuata taratibu hizi
  1. Pata footprint(Eneo lote ambalo mawimbi ya satellite husika yanafika) ya satellite. Kuna Website nyingi na tools zinazowezesha hili kwa mfano kwa kutumia Satbeams - World Of Satellites at your fingertips chagua satellite unayoitaka na utaona footprint yake na taarifa zaidi kama inavyoonekata kenye hii picha
    satellite-png.387957
Hapo ni kwa dar es salaam satellite ya Eutelsat 36B ipo nyuzi 36 mashariki (DSTV wanaporusha matangazo). Pia utaona ukubwa wa dishi linalotakiwa ili kupata signal, mfano hapo ni kuanzia 80cm unaipata vizuri tu. mkono wa kushoto kuna taarifa zaidi muhimu. hizi ni elevation angle 80.8 (hii ni kiasi gani dishi linatakiwa linyanyuke), True azimuth 334.2 (ni uelekeo wa dish) na lnb skew 25.6 (Uelekeo wa lnb). Hivyo vitu vi 4 nilivyobold ndiyo muhimu uvijue ukitaka kutafuta satellite yoyote ile.

2. Hatua inayofuata ni kufunga dish pole (ule mlingoti wa kuwekea dishi lenyewe). Hakikisha ile mlingoti umesima wima kwa nyuzi 90 (Ni muhimu sana hili) unaweza pima kwa kutumia kipima pembe au pima maji. Angalia hii picha
hqdefault-jpg.387977


3. Baada ya hapo ni kuweka dish lako sasa kwa kufuata vipimo ulivyopata hapo juu (Elevation, azimuth na lnb skew). Kuweka elevation angle 80.8 tumia alama zilizowekwa kwenye dishi mfano angalia picha hii hapo kuna kuanzia 0 hadi 90. elevation angle hutofautiana kutokana na satellite unayouitafuta, kwa mfano kwa hiyo ya dstv ni 80.8 na Eutelsat 7 (azam wanaporusha matangazo) ni 51.6 hivyo utakweka hapo kwenya hizo alama za dishi. kama dishi lako halina alama hizo unaweza kutumia kipima pembe kama hicho kenye picha hapo juu.
images-png.387978

adjustment-jpg.387981


4. Hatua inayofuata ni kuweka azmuth angle (uelekeo wa dishi kwa kuzungusha kulia au kushoto ukiwa nyuma ya dishi). Kifaa ninachotumika ni compass (dira), hichi kipo hata kwenye smartphone na uelekeze kwenye nyuzi 334.2

5. Katika hatua hii ni kuweka uelekeo wa lnb (Lnb skew angle) ukiangalia pale unapoweka lnb kuna alma pia za kuweka, angalia mfano kwenye picha hii
lnbf-skewing-angle-check-jpg.387986


Ukifuata hatua hizi 5 unapata satellite yoyote unayouitaka ndani ya muda mfupi sana dakika 10 nyingi siyo kubahatisha tu vitu vinaenda kwa vipimo kila kitu kipo kutokana na satellite unayoitaka. satellite zingine signal yake ni weak mfano Nilesat ukisema utafute kwa kuzungusha tu dish kwa kubahatisha unaweza kumaliza siku nzima hujaipata ila ukifuata vipimo vyake unaipata haraka sana.

Unaweza uelewa zaidi kwa kuangalia video hii youtube

View attachment 387957 View attachment 387977 View attachment 387978 View attachment 387981 View attachment 387986

Asante mkuu...umeniongezea madini kwa kiasi kikubwa Mungu akubariki.
 
Katika satellite nawezaje tambua kama transponder ipi iko powerful ambayo naweza tafutia angle napoangalia katika mtandao kama Lyngsat????
 
Napiga kazi kwa dakika chache sana kwa Satellite finder pia ina satellite guide
 

Attachments

  • satlink.jpg
    satlink.jpg
    118.2 KB · Views: 168
  • safinder.jpg
    safinder.jpg
    147.2 KB · Views: 158

Similar Discussions

Back
Top Bottom