Niulizeni kuhusu mkoa wa Pwani

Niulizeni kuhusu mkoa wa Pwani

Hivi yale maeneo ya Vikindu, Vihanze na Malogolo mtayapima lini maana eneo kama Malogolo ilisemekana Manispaa ya Temeke ni la kwake

Mpango mkakati uko katika hatua za kuridhisha.Maeneo yote hayo yako mkoa wa Pwani na yatapimwa. Vuta subira
 
hongereni kwa kutoa Rais toka mkoa wenu...nitajie makabila yanayopatikana mkoani kwako?

Wazaramo,Wakwere,Washirazi na Wandengereko ndio makabila makuu na ndio wenyeji.Lakini,mkoa wa Pwani una mkusanyiko wa makabila yote ya Tanzania kama ilivyo mikoa mingine
 
Kwani wakazi zaidi ya asilimia hamsini wanalima mazao ambayo hayahitaji huduma kama palizi za mara kwa mara ?
Kwanini wakazi wengi wa Pwani wana mboyoyo= maneno mengi ?

Mazao yalimwao Pwani yametokana na hali ya hewa iliyopo katika mkoa huo. Panalimwa mpunga,mihogo,viazi vitamu,mbaazi na kadhalika. Kuhusu maneno mengi,hii inatokana na kasi ya kilahaja iliyopo katika mkoa wa Pwani.Kumbuka kuwa,lugha ya Kiswahili ilianzia sehemu za Pwani
 
Kwa nini wakazi wa Pwani wanapenda na kuendekeza ngono zembe na kuwa idadi kubwa ya waathirika wa magonjwa ya zinaa na UKIMWI?

Suala la ngono zembe si suala la mkoa wa Pwani pekee. Ni la kinchi na ndiyo maana kuna kampeni ya kupambana na hali hiyo. Si kweli kuwa mkoa wa Pwani una idadi kubwa ya waathirika wa UKIMWI.Pwani haipo hata tano bora za kinchi katika suala hilo
 
Kwanini wachaga na wakinga wamewaamisha mjini Kariakoo na bado wanawafuata na kuwaamisha huko bagamoyo, Mkuranga, Masaki, Mwaneromango, Soga, Rufiji, Chamazi n.k. Hamuoni kwamba mtakosa sehemu kabisa za kuishi?

Wapo pia Wazaramo,Wakwere na Washirazi waliowahamisha Wachaga na Wakinga huko kwao.Nchi hii ni yetu sote.Kila mmoja anaweza kuishi atakapo na atakavyo ilimradi asivunje sheria
 
Nikweli Habib Mchange aliuza jimbo la Kibaha 2010?Unapafahamu home kwao/kwake?

Habari hizo zipo lakini sina uthibitisho wake. Inadaiwa kuwa aliuza Jimbo la Kibaha Mjini kwa Mbunge wa sasa Silvestry Koka. Zimeenea kuanzia Mailimoja hadi Visiga;Mwanalugali hadi Simbani. Kuanzia Tumbi hadi Mwanabwito;Mwanabwito hadi Msufini.Lakini,lisemwalo lipo na kama halipo laja. Kuhusu jumbani kwa Mchange ndani ya Wilaya ya Kibaha,mimi sipajui. Mchange si mzaliwa wala aliyekulia mkoa wa Pwani. Alishindwa kuonyesha kwao alipotakiwa kufanya hivyo mwaka 2010.
 
Nitafarijika kujibu maswali yenu. Nitawaeleza kuhusu Kibaha, Bagamoyo,Kisarawe,Mkuranga,Rufiji na Mafia

Karibuni kwa maswali

Napenda kufahamu kuhusu kisiwa cha Mafia.
Please tujuze zaidi kina idadi ya watu wangapi na je, kuna visiwa vingine ndani ya kisiwa hicho cha Mafia?
Inasemekana kuna maeneo ambayo wanawake hawaruhusiwi kutembelea katika kisiwa hicho, je ni kweli?
Nasubiri kujuzwa
 
Napenda kufahamu kuhusu kisiwa cha Mafia.
Please tujuze zaidi kina idadi ya watu wangapi na je, kuna visiwa vingine ndani ya kisiwa hicho cha Mafia?
Inasemekana kuna maeneo ambayo wanawake hawaruhusiwi kutembelea katika kisiwa hicho, je ni kweli?
Nasubiri kujuzwa

Mkuu,kadiri nijuavyo,hakuna visiwa vingine ndani ya kisiwa cha Mafia.Kisiwa cha Mafia kinaunda wilaya mojawapo ya wilaya sita za Mkoa wa Pwani.Mafia pia ni Jimbo la Uchaguzi ambalo lina kata saba: Baleni,Jibondo,Kanga,Kilindoni,Kirongwe,Kiegeani na Mibulani. Si kweli kuwa kuna maeneo wanawake wanakatazwa kutembea katika Kisiwa/Wilaya ya Mafia. Idadi ya wakazi wa Mafia ni zaidi elfu sabini.
 
Hakuna uhusiano wowote mkuu.Uvivu ni hulka ya mtu.Aweza kuwa wa Pwani au kwingineko
swali la nyongeza
kunauwezekano wakupata eneo kuanzia ruvu lenye ukubwa wa sq metre 40000 kwa ajili ya ujenzi wa bandari kavu?
kama swali litakuwa gumu naomba unisaidi adress ya chamber of commerce mkoa wa pwani kwa ajili ya ufafanuzi zaidi
 
swali la nyongeza
kunauwezekano wakupata eneo kuanzia ruvu lenye ukubwa wa sq metre 40000 kwa ajili ya ujenzi wa bandari kavu?
kama swali litakuwa gumu naomba unisaidi adress ya chamber of commerce mkoa wa pwani kwa ajili ya ufafanuzi zaidi

Nahitaji muda wa kutafiti Mkuu juu ya suala hili
 
Mkuu,kadiri nijuavyo,hakuna visiwa vingine ndani ya kisiwa cha Mafia.Kisiwa cha Mafia kinaunda wilaya mojawapo ya wilaya sita za Mkoa wa Pwani.Mafia pia ni Jimbo la Uchaguzi ambalo lina kata saba: Baleni,Jibondo,Kanga,Kilindoni,Kirongwe,Kiegeani na Mibulani. Si kweli kuwa kuna maeneo wanawake wanakatazwa kutembea katika Kisiwa/Wilaya ya Mafia. Idadi ya wakazi wa Mafia ni zaidi elfu sabini.

Na je kuna visiwa vingapi jirani na visiwa vya mafia au ndani ya Mafia?
 
Jinsi upepo unavovuma Kibaha Mjini, Dogo Habib Mchange na chama chake cha ACT anaweza shinda ubunge mwaka 2015?
 
Jinsi upepo unavovuma Kibaha Mjini, Dogo Habib Mchange na chama chake cha ACT anaweza shinda ubunge mwaka 2015?

Sioni hata dalili ya Mchange hata kupata wasikilizaji. Hatahivyo,bado simuoni Mgombea mwenye nguvu wa CHADEMA ingawa CCM imechokwa na wananchi wanajiandaa kuikataa.
 
Last edited by a moderator:
kwann mkoa wenu unaongoza kwa umasikini pamoja na miundo mbinu ya barabara kuwepo...ardhi ya kutosha na bahari.
 
Nahitaji muda wa kutafiti Mkuu juu ya suala hili
noted.
ila naomba nikuulize swali la ufahamu, hivi kibaha education centre ilijengwa mwaka gani? je ulikuwa ni msaada kutoka nchi fulani ya ulaya? maana kuna raia mmoja wa kigeni alikuwa anatamba kuwa wao ndio walijenga sio nyerere!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom