Niulize chochote kuhusu vipimo vya Maabara za Afya

Niulize chochote kuhusu vipimo vya Maabara za Afya

hapana mkuu, MRDt inaripotiwa katika mfumo wa POSITIVE na NEGATIVE...
Mi nakijua hiki, kina C, 1 & 2 ambapo kuna baadhi ya maeneo mtu anaweza akapimwa na vikaja vimistari vyote vitatu


images (1).jpg
 
mkuu naomba nikukosoe hapo sio "dhana" bali ni technique ya kureport majibu...
Imekaa poa mkuu... kama sijakuelewa vibaya ni kwamba namba ikiwa kubwa inamaanisha kuwaugonjwa ni severe ila nimewahi kukuona mtu wa malaria 3 akiwa hoi ilhali mwenye 200 ni mtu aliyeenda kufanya check up baada ya kujihisi mchovu mchovu.

Je, hii ni kutokana na kinga za mwili wa mtu husika au kuna kigezo tofauti?
 
Tukienda kupima malaria vipimo unatakiwa utamkiwe kwa mdomo au uandikiwe kwenye karatasi? maana kuna sehemu majuzi nimeenda kupima majibu nimeambiwa tu kwa mdomo kuwa nina malaria sina typhoid,hii n sawa utoaji wa majibu kwa namna hii kwa mgonjwa?
 
huwa maabara mkipima ukimwi mnatumia kipimo gani? nimesikia mahali mnatumia kama hivi hivi tunavyouziwa wananchi tuji pime wenyewe? kuna ukweli ktk hilo
hua tunatumia

1. rapid test ambazo kuna SD bioline na Unigold.. Unigold ndio standard na best( confirmatory test).. kwenye pharmacy hua zinakuepo ila ni magendo.
2. Elisa,
3. PCR.. hiki ndo kinachopima na viral load pia.
 
Ok, malaria mbaya/hatari ni ipi sasa kwa maana ya ukubwa wa namba ni ile ya 1,2,3.., au ile inayoanzia 100+?
hakuna malaria nzuri mkuu, zote ni mbaya na kadri idadi inavyokua kubwa ndio ukubwa wa ugonjwa unazidi kua kubwa

NB: Hakuna malaria 1, 2 3 wala 4.. kuna sehemu huko juu nmeelezea mkuu
 
Imekaa poa mkuu... kama sijakuelewa vibaya ni kwamba namba ikiwa kubwa inamaanisha kuwaugonjwa ni severe ila nimewahi kukuona mtu wa malaria 3 akiwa hoi ilhali mwenye 200 ni mtu aliyeenda kufanya check up baada ya kujihisi mchovu mchovu

Je hii ni kutokana na kinga za mwili wa mtu husika au kuna kigezo tofauti?
mkuu mtu ukiumwa malaria kiasi ukawa hoi huwezi kua na malaria 3. .am soo sure katika hili, labda uliingizwa chaka kidogo au umejichanganya sehemu.

Pia unaweza ukakuta mtu yes yeye ansjihisi vibaya tu ila sio kuzidiwa na ukampima malaria ukakuta anayo kubwa kuliko mtu mwingine ambae yupo hoi, wanaume wengi hua inakua hivi.. kwasababu ya immunity,life style, jinsia, umri pia
 
hapana si illegal,iweje vya mimba viwe legal hv vingine viwe illegal? ukipata muda wewe kajinunulie zako
cha mimba ni vyepesi kukitumia na vile vilikua designed kwa matumizi ya nyumbani mkuu.

ila hvi vya ukimwi hua kuna errors ambazo zinapelekea kupata false results, imagine ulikosea sehemu majibu yamekuja unaona kimstari kua una virusi vya Ukimwi hali ya kua huna kama bado una moyo mwepesi si utajiweka kitanzi!? wakati kuna makosa yalitokea!?.. usipende kujipima mkuu
 
Tukienda kupima malaria vipimo unatakiwa utamkiwe kwa mdomo au uandikiwe kwenye karatasi? maana kuna sehemu majuzi nimeenda kupima majibu nimeambiwa tu kwa mdomo kuwa nina malaria sina typhoid,hii n sawa utoaji wa majibu kwa namna hii kwa mgonjwa?
kabla hujachukuliwa sampuli, unatakiwa usomewe vipimo vyako na kuelezewa process ambayo itafatwa wakati unachukuliwa kipimo husika, na majibu inategemea na mfumo wa sehemu husika yawezekana wanatumia mfumo wa computer (Information System) ambayo mtaalam akimaliza kukupima anatuma majibu kupitia mfumo kwa daktari na daktari anakusomea kwa mdomo.. ila pia unaweza kuomba "hardcopy" ya majibu yako, ni haki yako.
 
hakuna malaria nzuri mkuu, zote ni mbaya na kadri idadi inavyokua kubwa ndio ukubwa wa ugonjwa unazidi kua kubwa

NB: Hakuna malaria 1, 2 3 wala 4.. kuna sehemu huko juu nmeelezea mkuu
Mkuu samahani
Nishawahi kusikia mtu anaambiwa ana malaria ringi 1,2,3....
Hii ipoje?
 
Mkuu samahani
Nishawahi kusikia mtu anaambiwa ana malaria ringi 1,2,3....
Hii ipoje?
kiutaalam hapo kuna shida ya incompetence kwa mtaalam husika ndio maana serikali inahamasisha matumizi ya mrdt ili kuepuka na kupunguza vitu kama hivyo.
 
kiutaalam hapo kuna shida ya incompetence kwa mtaalam husika ndio maana serikali inahamasisha matumizi ya mrdt ili kuepuka na kupunguza vitu kama hivyo.
Naam shukrani sana kwa kuendelea kutujibu maswali yetu na kututoa tongotongo machoni mwetu Mungu akubariki kwa hilo.

Swali langu linahusu upimaji wa mbegu za kiume, sijajua upimaji wake upoje ila kuna uzi nilisoma humu watu wakawa wanabishana kuwa kuna waliosema zile mbegu zinazopimwa as sample zinatakiwa zipatikane kwa njia ya masturbation wengine walisema zipatikane kwa njia ya sex with your partner.

Sikujua kundi lipi walikuwa sahihi na kwanini.. Karibu mkuu
 
Naam shukrani sana kwa kuendelea kutujibu maswali yetu na kututoa tongotongo machoni mwetu Mungu akubariki kwa hilo...
wote wako sahihi mkuu, vyovyote vile ila cha msingi mbegu zipatikane.

ila bao la masturbation ni bora zaidi kwasababu, ni vyepesi kuzikusanya mbegu zote kwa pamoja unlike la sex unaweza kumwagia ndani kidogo.. ila kama unaweza sex na ukalitoa(kumwagia) nje bao lote basi ni safi.

By the way mi naona katika sex uwezo wa kumwagia nje ni kipaji, binafsi sina teh teh! ..ndo mana nashauri la masturbation.
 
Back
Top Bottom