Niulize chochote kuhusu Subwoofer na Sounds system

kelphin

JF-Expert Member
Dec 24, 2019
9,126
14,497
Ikiwa inakusumbua,ikiwa unataka kufahamu chochote kinachokutatiza.

Karibu
images.jpg


Nieleze kidogo kuhusu subwoofer
Je, unataka kununua, basi zingatia haya.

Zipo za aina mbili old model na digital. Siyo majina hapana ,yaani inaweza kua rising,seapiano,codjec,aborder au vyovyote Ila itakua digital au old model.

Hizo digital ni Aina ya subwoofer ambayo inamuundo wakisasa ,mala nyingi utakuta Ina (nob) kivingilisho Cha sauti kimoja tu.

Ila kinafanya multipurpose, ukibonyeza hyo hiyo nob unaweza ongeza sauti ,kuongeza bass, na mid.
kifupi mambo yote ni in one button.

Faida yake ni kuwa, aina ya power supply yake Ni ilitaka ifanane na ya home theater(Ila haijawahi[emoji2inakua na umeme mnyoofu kidogo.

Zinakua na music mkubwa na mdundo zaidi ni digital,yaani yakisasa,
lakini pia display yake ni LCD haitumii umeme mwingi.

Je utaijuaje?
Nob ya kuongezea sauti ni moja tu na zaidi utakuta button za menu na input inategemeana). Ukiigeuza nyuma ina kiplastic kidogo kilichozungushwa nati, yaani ikiwa italeta shida fundi huku nyuma hafungui mfuniko wote wa nyuma, hufungua ki plastic tu hapo nyuma ndio kimebeba card zoote na subwoofer.

Hasara zake
  1. Ikitokea imeharibu card yake hauwez kubadilisha ,sababu ndani Ina circuit Kama ya phone mafundi weeengi hawana(hatuna) technology yakuitengeneza kwahyo unaenda dukani unanunua Tena kard na si chini ya 40000.
  2. Ila ukifika unaipachika tu huangaiki.
  3. Inahitaji utulie ili uioperate maana inatumia single nob.
  4. Speaker yake ya bass huwekwa ohms ndogo ili idunde sana kwahiyo usipende kuweka sauti kubwa Sana kwa muda mrefu.

Aina ya pili ndio zile old model
Hizo zinaitwa dunda udundavyo ni nzuri kwenye uzuri wake. Yenyewe ukiingalia utakuta Ina nob yaani vile vyakuongezea sauti zaidi ya kimoja. Yaani cha master volume, bass, tweeter na mic, na ukivizungusha vinafika mwisho.

Yenyewe ndani power supply yake ni ya kawaida, inatumia mtransformer wake na diodes za kawaida. kisha umeme huingia kwenye capacitor ndio unaanza kusambazwa ndani. Yaweza kuwa Seapiano, Codjec Aborder au vyovyote. Ukiigeuza nyuma mfuniko wote unafunguka wa nyuma.

Faida yake
  1. ikizingua unaiweza kuirekebisha kiurahisi tu
  2. Zinavumilia sana
  3. Hata muziki upo pia
  4. Rahisi kuitumia
Hasara zake
  1. Display yake ni VFD kama ni seapiano hapa mbele inakioo,inavyoimba Kuna vitu vinacheza cheza kwenye kioo(hii ni kwa baadhi ya subwoofer)
  2. Muonekano wake ni wakizamani ikilinganishwa na hizi mpya

Soma hi pia
Ndani ya subwoofer panya hupenda kuishi humo, huzaliana na kuleta hitilafu kwa kukata nyaya na kula speaker.
Waya wa speaker una chumvi chumvi hivyo akiingia hauachi.

Simple way jinsi ya kudhibiti
Pale kwenye tobo kuna ki corn cha duara huwa wanakipachika unaweza kukitoa kwa kufuata mpangilio ufuatao:

  1. Chukua maji ya moto kidogo na kitambaa, kichovye kitambaa kwenye maji kisha kikande kuzunguka mduara kwa dakika tano.
  2. Kisha chukua kisu, tumia ncha yake kuingiza pembezoni mwa mduara bila kuikwajua. Huku ukiinua kidogo kidogo kuzunguka corn nzima,ukisha kitoa kitoboe vitundu vidogo kukizunguka upande wa ndani(sio Huku uliko Kanda kwa maji).
  3. Ukisha kitoa chukua waya mgumu usuke upande wa ndani kuzunguka uwazi wa duara wote mule ulimotoboa, kisuke hakikisha unaacha vyumba vidogovidogo kiasi kwamba kinaweza kupita kidore kidogo tu.
  4. Paka gundi upande wa ndani, huku ulikokua unakanda na maji kisha kibandike tena kama kilivyokuwa.

NB: Hii ni kwazile subwoofer kama pichani hapo juu, ambazo hutolea upepo pembeni kwenye kiduara. Wale zinazotolea mbele chini ni habari nyingine.

***
Kiasi chake mtanielewaView attachment 1560194View attachment 1560195

Some updates,
Je, music system yako haina bluetooth na unataka kuongezea? Easy sana na inawezekana pia, kwa mafundi ninaweza kuwaelekeza.

Lakini pia music system yako ulipenda itoe mp5, yaani picture, video inawezekana pia.
Hususani wale wenye TV za kizamani yaani unachomeka flash disk yako kwenye subwoofer, unapata mdundo alafu kuna cable itatoka kwenye subwoofer hadi kwenye TV yako.

Stay here.
More good things are here.
Welcome.

View attachment 1921368
View attachment 1921369
 
Sauti tunayoiskia inatokeaje?
Ndani ya hiyo subwoofer Kuna circuit(card, ramani) ya amplifier (hapa ndipo sauti inakuzwa) sauti hiyo inakua imetokea kwenye mp3 player (Ile sehemu unayochomekaga frash). Sauti hiyo huwa Ni ndogo Sana(signal) mfano wa music wa earphones, Kisha hupita kwenye operation amplifier au wengine huita op amp
Op amp kazi yake Ni kutengeneza sauti kwenye frequency tofauti.

Ndio maana unasikia mdundo na sauti nyembamba kwenye speaker ndogo za pembini. Kisha opamp hupeleka signal kwenye amplifier ndio wewe unasikia huo miziki.

Ikiwa opamp itazingua au haitakuepo Basi hata hyo bass itaimba kawaida haitadunda hivyo
 
Oy mtaalam kuna mdau ananishauri nichukue hii PANASONIC vipi Kwa ujuzi wako hii ni home thietre au!? Na kimziki inapiga vizuri!!?View attachment 2624910

Kila redio ni kubwa
Inategemeana tu na ukubwa wa nyumba yako
Ndio maana mala nyingi hua nashauri mtu anunue kitu kwa kukiona na kusikiliza.
Kwa ila kwa muonekano wake inapiga mziki wa kusikiliza i mean wa kawaida.
 
Naomba tofauti kati ya home theater na subwoofer


Ukiacha ile tofauti ya kuwa subwoofer ni uswazi na home theater ni ushuani
Vyote Ni vifaa vya kielectronic
Vyote vinakuza nguvu ya sauti
Lakini utofauti wake Ni hu Ili hiyo subwoofer iwake iwe on. Inahitaji umeme Kama home theater.
Umeme ukishaingia kwenye subwoofer unaenda kwenye transformer .....unapunguzwa Kisha unaenda kugeuzwa kua DC ( vifaa vya electronics vingi vinatumia DC,umeme wa nyumbani Ni ac) hi (inaitwa power supply).

Baada ya hapo unaanza kutembea kwenye circuit za hyo subwoofer. Lakin kwenye home theater Ni tofauti
Power supply yake Ni tofauti yaani inatoa umeme wenye current standard na Haina gaps yaani current Ina Tembea smoothly hata umeme ukicheza (uliwahi ona taa zinafifia hasa jioni)power supply zake zinaditect Kisha zinaunyoosha

Pili Ni kwenye sauti
Ikumbukwe kitu muhimu Ni kua zote Zina amplifier ndani yaan subwoofer na home theater
Ila home theater hua Kuna integrated circuit (ic) ambazo hua wanaziprogram kwenye computer zinatengeneza sauti kusikika vile kabla yakuingia kwenye amplifier
 
Wakuu nina sony rt3 soundbar.Nime notice sauti ikizid 30 basi redio inapunguza mdundo. Shida inaweza kuwa nini?

Hakuna shida...,
Chukua hi..
Unapoongeza sauti inamaana unaruhusu umeme mwingi kwenye speaker
Kadri unavyojaza sauti basi kiwango kile kinachotoka kwenye transformers kinatawanyika kwenye amplify channel zako
“Ili kisitokee hicho ilibidi unapoongeza sauti basi na transfoma yako iongeze kiwango cha umeme”(hi nimeongea kifundi)
Hivyo mkuu hiyo ni kawaida.
 
Isaya

Kipimo cha sounds system bora ni usikivu wa mziki
Arrangement(muonekano,design ) na ubora wa material zake walizotumia kuu tengeneza nkiwa na maana kwenye circuits na box design (metals au wood)
Frequency ni mawimbi tofauti ya USIKIVU WA MZIKI
Kuna frequency za tweeter (sauti kari nyembamba, mid yaani ya kati.. na bass yaan low frequency ambazo ni mziki mzito)
Decibel (dB) ni kipmo cha kupima ukubwa wa usikivu wa mzikii
Speaker zinapotoa mziki mziki huo utasikika parefu ikiwa utaongeza sauti
Unapoongeza sauti unaongeza db za kusikika parefu zaidi
Ila kitu chakuelewa ni kua hapa sijaongelea device inayotoa mziki
Simaanishi mziki wa club au wap
Note hi inawezekana kua subwoofer-HT au PA system
Cha kuelewana ni kua ukubwa wa kuongeza sauti na sio aina ya kifaa kinachotoa mziki

Power ni watts ,output power ni output watts za amplifier yako
Yaani ukubwa wa amplifier yako
Kuhusu masikio kuuma naweza kusema yategemeana na tetting za mziki wako tu
Wakati mwingine bass husababisha maumivu ya kichwa

Kuhusu ubora wa usikivu wa mziki kwenye sonny,jbl au HT kiujumla

Hi ni kwasababu ya well tuning ya system ya hizi sounds mthus wanaziuza hela ndefu
Wakati mwingine ni imani pia

Ambapo hujaelewa ntakuelewesha niambie
Nimekuelewa mkuu, ila kwenye imani sio kweli hiz brand kubwa zinafanya kaz unajua kuna muda unaweza skiliza wimbo kifaa chako ukienda kuskiliza kwakutumia brand nyingine usikivu unabadilika test tofaut
 
Mkuu ninasab woofer hapa aina ya ABORDER. Sasa hivi majuzi ilikwama ghafla ikawa inapiga tweeter peke yake. Bass na main speaker vilikata Kabisa. SASA kuna fundi hapa nilimpelekea... Cha ajabu Maneno yamekuwa mengi mara tusuke kipande kusaport bass, mara tununue power IC. Nikampa Pesa ya vifaa ila redio imemshinda karidisha mfumo wa bass ila rediooo inatoa kikohozi moja kwamoja. Kimsingi inanilazimu kufungua sauti ya juu ilikupunguza hizo zoisy. Embu msaada wako kuhusu hili..................
Aboder nyingi zinatumia TIP transistor ila circuit yake hua ni half powered
Inaweza kumuwia vigum kidogo kuitengeneza sababu huku chin hua wanatumia smd transistor
Alikua sawa kusema atengeneze ki amp kidogo cha bass ila huenda kashindwa ku attach ifanye kazi
Upo mkoa gani?
 
Ahsante sana Kelphin, nyongeza kwa matokeo mazuri ya soundbar nzuri ianzie watts ngap.?

Watts inapimwa kama uwezo wa redio kupiga mziki mkubwa bila ya kua na kelele yoyote
Hivyo tuseme watts nyingi inakua powerful zaidi kwa ukubwa wa muziki kuzidi zenye watts ndogo
Hasara ya sound system zenye watts nyingi ni kua zinakula umeme zaidi kuzidi zenye watts chache
Lakini pia ghalama inakua kubwa pia kuzidi zenye watts chache.
Hivyo zote ni nzuri ila ikiwa utataka mziki mkubwa ndio uone za kuanzia watts 300+
Ila kwa uzuri wa usikivu wa muziki zote ni bora
 
Kwanini haya makitu hayatengenezeki, yaani likipona linapungua ubora, na linarudi kutoka kwa fundi na masharti kibao ya kulitumia.

Na ukilitumia baada ya kipindi kifupi tu linazimika jumla. Nilinunua kama matatu hivi mpaka nilipohamia kwenye hometheatre nikasahau majanga mbali mbali.
 
Back
Top Bottom