hapo ndipo ulipokosea, wasambaa ni mchanganiko wa makabila mbali mbali waliosambaa katika milima ya usambara baada ya kuhama sehemu zao na kwenda usambaani kwenye ardhi yenye rutuba,
mwanzoni kabisa kabla ya milima ya usambara kuvamiwa na binadam, kulikuwa na msitu mkubwa uliosheheni kila aina ya wanyama na ndege wa kila namna, walikuwepo simba, tembo na wanyama wengine wengi sana,
wambugu ni kabila la kwanza kuhamia milima ya usambara wakitokea arusha ambako walipigana na jamii nyingine ya wamasai, wambugu walipofika moshi na mifugo yao walifukuzwa na walipofika upareni walifukuzwa na wapare ndipo walipohamia milima ya usambara, makabila mengine yaliofika lushoto ni wazigua, wabondei, wapare na wakenya toka taita ndo maana kuna wasambaa wanatumia jina la ukoo WATAITA, Kimweri alitokea handeni na akaja kuwa mtawala wa maeneo yote ya lushoto Enzi hizo japo kiukweli kimweri si wakwanza kufika lushoto, wasambaa wanaojiita WAKILINDI (mimi mmojawapo) tumetokana na kizazi cha chief Kimweri, ambapo asili ya jina wakilindi ni kwamba baba yake kimweri ana asili ya bara asia japo yeye alizaliwa na mama mwafrika mzigua ndo maana wakilindi ni watu weupe sana coz ni machotara wenye asili ya kiarabu.
CC.
Elli ,
MANI ,
Paloma ,
mshana jr