Nitashangaa kama TTCL, ATCL, Posta, TANESCO, NIC zitaachwa

BLACK MOVEMENT

JF-Expert Member
Mar 11, 2020
2,704
6,501
Kwa kifupi Mashirika yote ya umma yanayofanya Biashara yanapaswa kupigwa bei, tubakie na mashiria kama TANAPA basi.

Kama Bandari inakodishwa then TTCL, ATCL, wakina TANESCO wanaachwa basi kuna shida au kuna walakini, mashirika ypte ya umma yaingie sokoni na Serikali inachana na Biashara.

Hakuna ufanisi kwenye serikali kufanya Biashara, mashirika ya umma ni taasisi za wakubwa kwenda kuchota pesa.

Ikiwezekana hata kama kuna baadhi ya Vyuo vya kuuzwa viuzwe ilimuladi kama kuuzwa kwao kutaleta ufanisi mkubwa sana.

Karine hii Serikali kuwa na mashirika ya biashara mara mashirika ya kuchimba madini ni ujinga.
 
Hata huko TANAPA ni wizi mtupu, serikali iwachane kabisa na biashara zote.

Mashirika yote ya umma yabinafsishwe, serikali ibaki kuwa mbia tu.
 
Back
Top Bottom