Nitarudi tena Marangu

Nitarudi tena Marangu

Bora iseme wewe chasaka wakiongea wengine humu hawakawii kusema mwamba ngoma karibu sana marangu hakukupeleka kinuka mori mkuu.
 
Karibu Mkuu Marangu...Mimi ni mwenyeji kule Sembeti....Ukifika hapo Marangu Mtoni unakunja kushoto unakutana na Sembeti......

Hahahaa acha uongo bana kwenda kwenu mtoni unafata nini yaani unataka kwenda kkoo unaenda zungukia posta?.
 
Uje na huku kwetu machame utusalimie kuna majumba pia ya ajabu
 
Habarini za saa hizi.Kuna jambo ambalo nimeona nishee na wanajamii kuhusu Marangu.Mimi mzaliwa wa Dar es salaam ingawa kwa kabila ni msukuma.Tangu nimezaliwa nilikuwa sijawahi kwenda mikoa ya kaskazini.Kuna mshkaji wangu mmoja tulikuwa tunasoma nae pale Mlimani ni Mchaga toka Marangu.Kijiji anachotoka kinaitwa Rauya yaani kama Jina langu.Mara kwa mara alikuwa akiniambia kuna kijiji kinaitwa Rauya na mara nyingi alikuwa akinitania kwa kuniita Mangi.Nilikuwa nachukia sana coz nilikuwa sifagilii sana kabila la wachaga.Ila siku zilivyoendelea kusonga nilimzoea na tukawa marafiki wakubwa haswa.

Sasa juzi kati mzimu wa sikuku za xmass na mwaka mpya alinialika niende Marangu nikakione hicho kijiji cha Rauya.Nilikubali bila hiyana.Mama yanguu.Nilipofika sikuamini kama ni kijijini.Kulaleki wachaga ni Nyoko.Hiyo mijumba iliyofunikwa katikati ya migomba ilinifanya nitoe macho kama mjusi aliyebanwa na lango kuu la magereza.Yaani ni masinagogi ya kifahari haswa.Mijumba ya thamani kubwa imezungukwa na migomba.Mi nilijua naenda kijijini nitakuta nyumba za mbavu za mbwa kumbe ni kinyume chake.Wazazi wake walinipokea kwa moyo mkunjufu na wa upendo.Nilikuwa nimepanga kukaa siku tatu lakini nikajikuta nakaa wiki na ushee.Mazingira ya kijani kibichi yalinivutia sana.Mito mikubwa yenye maporomoko ndo usiseme.Alinipeleka mahali panaitwa Marangu mtoni.Hapo kuna kila huduma zinazopatikana mjini.Pub na restaurant za maana kama vile niko samakisamaki Dar.

Kwa mara ya kwanza nilikunywa mbege(Nilikuwa naidharaugi sana)Ila nilipoionja nilijua ni kwanini wachaga wanaisifiaga sana.Mbuzi na ng'ombe zilikuwa zinachinjwa kama vile hakuna kesho.Watoto warembo wakichaga ndani ya magari ya kifahari ndo usiseme.Usafiri wa kila aina hadi tax za maana.Basi jamaa akanipeleka kwa mshikaji mmoja wa mwenge Dar na yeye ni mchaga wa Marangu ingawa ni kijiji kingine.Huwa anafanya kazi za kuchomelea.Nilipofika kwake kidogo nilie baada ya kushangaa sana.Huo mjumba alioujenga ni balaa.Kidogo niseme niko msasani Dar.Mimi nilikuwa namdharau anavyoangaika na mavyuma kumbe jamaa ana jumba la mamilioni huko kiliji.Du!Naweza nikaeleza mengi ila kwa kifupi hawa watu wako juu.Na nitarudi tena Marangu Rauya.

Mkuu Rauyah kama wewe ni me mwombe Mungu akutanishe na ke wa uchagani, hakika hutajutia!!!! Baada ya kusoma pande hizo miaka ile niliona maendeleo sana japo siku hizi ni balaa mpaka magorofa ya mamilioni yapo na huduma zote nikaweka nia "ni lazima nimpate wa ubavu". Hakika sijutii,natamani pale kijijini kwetu waoe hata wachaga kumi hivi.
 
Habarini za saa hizi.Kuna jambo ambalo nimeona nishee na wanajamii kuhusu Marangu.Mimi mzaliwa wa Dar es salaam ingawa kwa kabila ni msukuma.Tangu nimezaliwa nilikuwa sijawahi kwenda mikoa ya kaskazini.Kuna mshkaji wangu mmoja tulikuwa tunasoma nae pale Mlimani ni Mchaga toka Marangu.Kijiji anachotoka kinaitwa Rauya yaani kama Jina langu.Mara kwa mara alikuwa akiniambia kuna kijiji kinaitwa Rauya na mara nyingi alikuwa akinitania kwa kuniita Mangi.Nilikuwa nachukia sana coz nilikuwa sifagilii sana kabila la wachaga.Ila siku zilivyoendelea kusonga nilimzoea na tukawa marafiki wakubwa haswa.

Sasa juzi kati mzimu wa sikuku za xmass na mwaka mpya alinialika niende Marangu nikakione hicho kijiji cha Rauya.Nilikubali bila hiyana.Mama yanguu.Nilipofika sikuamini kama ni kijijini.Kulaleki wachaga ni Nyoko.Hiyo mijumba iliyofunikwa katikati ya migomba ilinifanya nitoe macho kama mjusi aliyebanwa na lango kuu la magereza.Yaani ni masinagogi ya kifahari haswa.Mijumba ya thamani kubwa imezungukwa na migomba.Mi nilijua naenda kijijini nitakuta nyumba za mbavu za mbwa kumbe ni kinyume chake.Wazazi wake walinipokea kwa moyo mkunjufu na wa upendo.Nilikuwa nimepanga kukaa siku tatu lakini nikajikuta nakaa wiki na ushee.Mazingira ya kijani kibichi yalinivutia sana.Mito mikubwa yenye maporomoko ndo usiseme.Alinipeleka mahali panaitwa Marangu mtoni.Hapo kuna kila huduma zinazopatikana mjini.Pub na restaurant za maana kama vile niko samakisamaki Dar.

Kwa mara ya kwanza nilikunywa mbege(Nilikuwa naidharaugi sana)Ila nilipoionja nilijua ni kwanini wachaga wanaisifiaga sana.Mbuzi na ng'ombe zilikuwa zinachinjwa kama vile hakuna kesho.Watoto warembo wakichaga ndani ya magari ya kifahari ndo usiseme.Usafiri wa kila aina hadi tax za maana.Basi jamaa akanipeleka kwa mshikaji mmoja wa mwenge Dar na yeye ni mchaga wa Marangu ingawa ni kijiji kingine.Huwa anafanya kazi za kuchomelea.Nilipofika kwake kidogo nilie baada ya kushangaa sana.Huo mjumba alioujenga ni balaa.Kidogo niseme niko msasani Dar.Mimi nilikuwa namdharau anavyoangaika na mavyuma kumbe jamaa ana jumba la mamilioni huko kiliji.Du!Naweza nikaeleza mengi ila kwa kifupi hawa watu wako juu.Na nitarudi tena Marangu Rauya.

Umeonaaee!! ndio maana hawapendwi kisa wana akili!
 
Habarini za saa hizi.Kuna jambo ambalo nimeona nishee na wanajamii kuhusu Marangu.Mimi mzaliwa wa Dar es salaam ingawa kwa kabila ni msukuma.Tangu nimezaliwa nilikuwa sijawahi kwenda mikoa ya kaskazini.Kuna mshkaji wangu mmoja tulikuwa tunasoma nae pale Mlimani ni Mchaga toka Marangu.Kijiji anachotoka kinaitwa Rauya yaani kama Jina langu.Mara kwa mara alikuwa akiniambia kuna kijiji kinaitwa Rauya na mara nyingi alikuwa akinitania kwa kuniita Mangi.Nilikuwa nachukia sana coz nilikuwa sifagilii sana kabila la wachaga.Ila siku zilivyoendelea kusonga nilimzoea na tukawa marafiki wakubwa haswa.

Sasa juzi kati mzimu wa sikuku za xmass na mwaka mpya alinialika niende Marangu nikakione hicho kijiji cha Rauya.Nilikubali bila hiyana.Mama yanguu.Nilipofika sikuamini kama ni kijijini.Kulaleki wachaga ni Nyoko.Hiyo mijumba iliyofunikwa katikati ya migomba ilinifanya nitoe macho kama mjusi aliyebanwa na lango kuu la magereza.Yaani ni masinagogi ya kifahari haswa.Mijumba ya thamani kubwa imezungukwa na migomba.Mi nilijua naenda kijijini nitakuta nyumba za mbavu za mbwa kumbe ni kinyume chake.Wazazi wake walinipokea kwa moyo mkunjufu na wa upendo.Nilikuwa nimepanga kukaa siku tatu lakini nikajikuta nakaa wiki na ushee.Mazingira ya kijani kibichi yalinivutia sana.Mito mikubwa yenye maporomoko ndo usiseme.Alinipeleka mahali panaitwa Marangu mtoni.Hapo kuna kila huduma zinazopatikana mjini.Pub na restaurant za maana kama vile niko samakisamaki Dar.

Kwa mara ya kwanza nilikunywa mbege(Nilikuwa naidharaugi sana)Ila nilipoionja nilijua ni kwanini wachaga wanaisifiaga sana.Mbuzi na ng'ombe zilikuwa zinachinjwa kama vile hakuna kesho.Watoto warembo wakichaga ndani ya magari ya kifahari ndo usiseme.Usafiri wa kila aina hadi tax za maana.Basi jamaa akanipeleka kwa mshikaji mmoja wa mwenge Dar na yeye ni mchaga wa Marangu ingawa ni kijiji kingine.Huwa anafanya kazi za kuchomelea.Nilipofika kwake kidogo nilie baada ya kushangaa sana.Huo mjumba alioujenga ni balaa.Kidogo niseme niko msasani Dar.Mimi nilikuwa namdharau anavyoangaika na mavyuma kumbe jamaa ana jumba la mamilioni huko kiliji.Du!Naweza nikaeleza mengi ila kwa kifupi hawa watu wako juu.Na nitarudi tena Marangu Rauya.

Kwa maelezo yako wewe ni Mmarangu, naona umetak upazungumzie kijijini kwenu.

Sishangai sana kwa kuwa Wamarangu na misifa hawajambo.
Siku ingine uwaulize wakuoneshe pia kwa yule mzee aliyekuwa akiwalawiti mabinti zake kule Marangu
 
Kwa maelezo yako wewe ni Mmarangu, naona umetak upazungumzie kijijini kwenu.

Sishangai sana kwa kuwa Wamarangu na misifa hawajambo.
Siku ingine uwaulize wakuoneshe pia kwa yule mzee aliyekuwa akiwalawiti mabinti zake kule Marangu

chuki binafsi
 
Karibu tena Marangu, nafurahi kwamba kuna jambo umejifunza... kuna watu wanafikiri maendeleo yanakuja kwa kucheza bao na zunna!!! nikipita mitaa ya mtogole, tandika, magomeni au kinondoni hua nasikitika sana.. halafu hao hao ndio wa kwanza kulalamika
 
Kule ndivyo kulivyo;
Na ujue maeneo ya Rauyah yalikuja kuendelea majuzi kati baada ya vijana wao kupata pesa;
Ukweli ukitaka kujua maendeleo ya marangu nenda maeneo ya mamba ukajionee
hayo majumba huko migombani.
 
Last edited by a moderator:
Ni sawa kuwa na majumba mazuri kijijini na pia ni vizuri kurudi nyumbani kwani ni motisha kwa wale waliosalia kule kujituma zaidi kutokana na mafanikio ya ndugu na jamaa zao. Ila hakuna 'economic justification' ya kujenga mjengo wa mamilioni halafu unakwenda kukaa huko wakati wa sikukuu tu. Kwa mtu aliyejenga mjengo akiwa na umri wa miaka 30-40, by the time anastaafu au amefikia umri wa miaka 65-70 mjengo huo utakuwa umepungua thamani kwa kiasi kikubwa na ni lazima ufanyiwe renovation kubwa. Wachaga badilikeni. Mngesaidia watu wenu zaidi kwa kuwekeza kwenye viwanda vidogo vidogo (hata kwa kushikisha mitaji ambayo mnayo) kama vile viwanda vya kusindika maziwa, kutengeneza viatu, n.k. Ukienda maeneo hata hayo ya Marangu sasa hivi kuna vijana wengi waliosalia kule wameishia kunywa viruba na gongo. Nimeshakuwa Moshi maeneo mbalimbali hadi huko Marangu, na hili ni tatizo kubwa kwa sasa. Ajira kubwa kule kwa sasa kwa vijana kama yalivyo maeneo mengine ni pikipiki. Najua, hata Mengi angeamua kuwekeza kwenye usindikaji wa maziwa pale Kilimanjaro na Arusha kwa mfano, kungekuwa na mabadiliko ya haraka kuliko hizi tambo za wakati wa sikukuu wakati kuna maskini wa kutupwa huko.
 
Kweli wachagga wanajali sana kwao ndio maana kila mwisho wa mwaka hurudi kwao. Watu wa baadhi ya maeneo hapa Tanganyika wakisha toka kwao na kufika Dar ndio basi tena hawarudi kwao wengine hata wakifa hawarudishwi kwao kwasababu hawakuweka mazingira mazuri wakati wakiwa hai ndio maana ukikaa hapa kimara utaona kosta nyingi zilizobeba maiti ni za kuelekea Moshi na Arusha na hii si kwamba watu wa maeneo mengine hawafi bali wengine hushia kuzikwa Dar kwakuwa kwao walishahama. Ingekuwa jambo la kufurahisha pia inapofika mwishoni mwa mwaka Dar inakuwa haina watu labda wazaramo lakini wengine wote wa kusini, kati, magharibi, kusini nyanda za juu, kanda ya ziwa na kwingineko nao wanarudi kwao kufanya maendeleo na kupanga mikakati ya familia. Kweli wachagga watoa somo zuri sana la kujali nyumbani.
 
Sisi Wachaga Hutunaga Maneno Mengi Sisi Ni Kazi Tu. Mapenz Tumewaachia Watu Wa pwani

Mabingwa wa kujiuwa sababu ya mapenzi..............huwa pia nasikia wazee wa kichaga huzaa na wake za vijana wao........hivyo ukimuachia mzee demu anamaliza!!!!!
 
siku nyingine panda kidogo ufike kotela na kokirie na komakundi kidogo uone mambo na pia fika kimbogho na kiria na mkolowonyi utembee kidogo uone mazingira mkuu Rauyah
 
Last edited by a moderator:
Ha ha ha..ndugu nilivutiwa sana.Kuna biashara nimepania kufanya maeneo ya Marangu mtoni.Mambo ya kikaa sawa nitawajulisha ni biashara gani.
Arushaone ushamuona huyu jamaa eeeh anataka apate wenyeji kabisa na inawezekana "biashara" hiyo ashaona mtoto mzuri wa marangu anataka aweke makazi kabisa Mentor, kiwatengu, Asprin, Rejao, ndo hivyo msukuma kashafika bei watoto wa marangu anataka ajenge kibanda kabisa
 
Last edited by a moderator:
Karibu Mkuu Marangu...Mimi ni mwenyeji kule Sembeti....Ukifika hapo Marangu Mtoni unakunja kushoto unakutana na Sembeti......
Mkuu hiyo ni sembeti nyingine au? mimi ninafahamu sembeti ya kupitia mahali wanaita barabara ya kilema au kwa Anaseli. Marangu mtoni ukielekea kushoto unaenda kilema, si ndio?
 
Back
Top Bottom