Nitarudi tena Marangu

Nitarudi tena Marangu

Samahanini sana akina Mangi sikujua kama inakuwaga siri.Ila ndo hivyo tena nimesha mwaga mchele kwenye kuku wengi.

Samahani bila sale na ndoo ya mbegee!!? Wewe namna gani aisee makosa yanatozwa eti.
 
Bora iseme wewe chasaka wakiongea wengine humu hawakawii kusema mwamba ngoma karibu sana marangu hakukupeleka kinuka mori mkuu.

nakuambia angeenda kinuka mori huyu angeandika kitabu cha historia..au angeenda kwenye mihoteli ya kitalii kama Kilimanjaro Mountain Resort au angempeleka maeneo ya kinapa ajionee mihoteli asingerud huyu...lol
 
Mshiki unaonaje ukinipeleka huko kote....:dance:

nakuambia angeenda kinuka mori huyu angeandika kitabu cha historia..au angeenda kwenye mihoteli ya kitalii kama Kilimanjaro Mountain Resort au angempeleka maeneo ya kinapa ajionee mihoteli asingerud huyu...lol
 
Wasinenepe kichwa kwa masifa. Mbaona wengi waliochangia ni wa hukohuko. Tena mmojawao ana jina la Rauya, wengine naanglia kamusi yakichagga? au kajiunga leo JF?
 
mara nyingine mpeleke kwanza usukumani kabla wewe hujarudi huko marangu, usisahau hilo
 
Kuna Rauya mbili: Rauya ya Marangu na Rauya ya Mamba. Wewe ulikuwa Rauya ipi na yenye maporomoko ya maji kama siyo muongo kama yule waziri wa TANESCO?
kama hujui kitu nyamaza mkuu maana ulichoandika kinakufunga mwenyewe .ina maaana kama alikuwa rauya ya marangu alikwenda marangu mtoni kuona maporomoko ya kinukamori wewe
 
sijuim kwann sion kitufe cha like
BTW karibu tena unywe kiburu, kitalolo, kisusio, kitawa, ng'ande., ngararimo, mtori, machalari, vibere, vikwa, viiye, nyany' et al
cc Arushaone, Asprin Smile, Lily Flower et al
 
Last edited by a moderator:
Mkuu hiyo ni sembeti nyingine au? mimi ninafahamu sembeti ya kupitia mahali wanaita barabara ya kilema au kwa Anaseli. Marangu mtoni ukielekea kushoto unaenda kilema, si ndio?
wewe unatokea kijiji kipi??

manake nakufananisha na wa kimaroroni vile................
 
Habarini za saa hizi.Kuna jambo ambalo nimeona nishee na wanajamii kuhusu Marangu.Mimi mzaliwa wa Dar es salaam ingawa kwa kabila ni msukuma.Tangu nimezaliwa nilikuwa sijawahi kwenda mikoa ya kaskazini.Kuna mshkaji wangu mmoja tulikuwa tunasoma nae pale Mlimani ni Mchaga toka Marangu.Kijiji anachotoka kinaitwa Rauya yaani kama Jina langu.Mara kwa mara alikuwa akiniambia kuna kijiji kinaitwa Rauya na mara nyingi alikuwa akinitania kwa kuniita Mangi.Nilikuwa nachukia sana coz nilikuwa sifagilii sana kabila la wachaga.Ila siku zilivyoendelea kusonga nilimzoea na tukawa marafiki wakubwa haswa.

Sasa juzi kati mzimu wa sikuku za xmass na mwaka mpya alinialika niende Marangu nikakione hicho kijiji cha Rauya.Nilikubali bila hiyana.Mama yanguu.Nilipofika sikuamini kama ni kijijini.Kulaleki wachaga ni Nyoko.Hiyo mijumba iliyofunikwa katikati ya migomba ilinifanya nitoe macho kama mjusi aliyebanwa na lango kuu la magereza.Yaani ni masinagogi ya kifahari haswa.Mijumba ya thamani kubwa imezungukwa na migomba.Mi nilijua naenda kijijini nitakuta nyumba za mbavu za mbwa kumbe ni kinyume chake.Wazazi wake walinipokea kwa moyo mkunjufu na wa upendo.Nilikuwa nimepanga kukaa siku tatu lakini nikajikuta nakaa wiki na ushee.Mazingira ya kijani kibichi yalinivutia sana.Mito mikubwa yenye maporomoko ndo usiseme.Alinipeleka mahali panaitwa Marangu mtoni.Hapo kuna kila huduma zinazopatikana mjini.Pub na restaurant za maana kama vile niko samakisamaki Dar.

Kwa mara ya kwanza nilikunywa mbege(Nilikuwa naidharaugi sana)Ila nilipoionja nilijua ni kwanini wachaga wanaisifiaga sana.Mbuzi na ng'ombe zilikuwa zinachinjwa kama vile hakuna kesho.Watoto warembo wakichaga ndani ya magari ya kifahari ndo usiseme.Usafiri wa kila aina hadi tax za maana.Basi jamaa akanipeleka kwa mshikaji mmoja wa mwenge Dar na yeye ni mchaga wa Marangu ingawa ni kijiji kingine.Huwa anafanya kazi za kuchomelea.Nilipofika kwake kidogo nilie baada ya kushangaa sana.Huo mjumba alioujenga ni balaa.Kidogo niseme niko msasani Dar.Mimi nilikuwa namdharau anavyoangaika na mavyuma kumbe jamaa ana jumba la mamilioni huko kiliji.Du!Naweza nikaeleza mengi ila kwa kifupi hawa watu wako juu.Na nitarudi tena Marangu Rauya.

Karibu tena jamani,ndo asili yetu siye wachaga kutengeneza nyumbani kwanza,na ndo heshima yetu,hapana chezea mchaga weye.
 
Tatizo wanajenga hayo majumba halafu hawakai ni mpaka siku ya xmas sasa ya kazi gani hayo..na umri wa juu wa mtanzania ni miaka 55 tuu...wanawajengea mapanya na mabuibui tuu..mie sifagilii hiko kitu banaa..maisha ni kule unakoishi sio !!sio Dar umepanga chumba unachomelea vyuma, huko marangu una sinagogi na hauishi what the f.u*&^&...

Kweli unamauzauza kama jina lako lilivyo,kule ndo nyumbani,elewa ivyo,kwingine tunapita tu tukitafuta maisha,ila tunarudi paleee kijijini marangu kwenye chimbuko,kwa baba na mama zetu,babu na bibi zetu,kwetu,kwa ndugu zetu (kwenye shina letu) huku mjini ni watafutaji tu.na mwisho wa siku hata tukifa tunarudishwa paaaaaaleeee.put in your mind,tafuta pesa,peleka maendeleo nyumbani,hayo mengine ya ziada mjini.
 
Kisusio, Next time ukifika maeneo ya Marangu Hotel nitafute nikuonjeshe Kiburu, Kitawa, Machalari, Shiro, Ng'ande, Mtori, Ndafu na Ngararimo.

umenikumbusha mbali sana mi ni mpenzi wa hivyo vyakula nimevimiss kweli pasaka itabidi niende, umesahau ndizi za kuchoma kwa maziwa ya mtindi au parachichi
 
Kwa maelezo yako wewe ni Mmarangu, naona umetak upazungumzie kijijini kwenu.

Sishangai sana kwa kuwa Wamarangu na misifa hawajambo.
Siku ingine uwaulize wakuoneshe pia kwa yule mzee aliyekuwa akiwalawiti mabinti zake kule Marangu

Ha ha ha..nimeshakuwa tena Mmarangu.Thanks anyway.
 
Kwa wachaga wezangu wale tuliopo mijini zamani tulieshemika kwa elimu na ndiyo iliyotupa eshima mpaka sasa lakini tukumbuke wakati hule kaka zetu walisomesho na kahawa ambayo sasa akuna lakini kuna wadogo zetu wameshidwa kwnda shule kwasababu kahawa akuna tena kwanini tusifanye arambee ya kusaidiye watoto hawo najuwa kabisa wachaga tuko kila mahali na tu uwezo wakusaidia wadogo zetu ili mkoa wetu uendelea kuwa na heshima
 
Back
Top Bottom